Yeremia 4 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 4:1-31

14:1 Yoe 2:12; Ezr 8:5; 2Fal 7:13; 21:4; Kum 4:30; Hos 12:6; Yer 16:18; 35:15“Ikiwa utataka kurudi, ee Israeli,

nirudie mimi,”

asema Bwana.

“Ikiwa utaondoa sanamu zako za kuchukiza mbele ya macho yangu

na usiendelee kutangatanga,

24:2 Kum 10:20; Hes 14:21; Gal 3:8; Hos 4:15; Mwa 12:2; Isa 19:18; 65:16; Yer 12:16ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa,

‘Kwa hakika kama vile Bwana aishivyo,’

ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye

na katika yeye watajitukuza.”

34:3 Hos 10:12; Mk 4:18Hili ndilo asemalo Bwana kwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu:

“Vunjeni mabonge kwenye mashamba yenu,

wala msipande katikati ya miiba.

44:4 Law 26:41; Rum 2:28-29; Sef 2:2; Amo 5:6; Ay 41:21; Kut 32:22; Yer 8:14; Yos 10:20; Yer 5:20; Hes 10:2-7; Ay 39:24Jitahirini katika Bwana,

tahirini mioyo yenu,

enyi wanaume wa Yuda

na watu wa Yerusalemu,

la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu

na kuwaka kama moto

kwa sababu ya uovu mliotenda,

ikiwaka pasipo wa kuizima.

Maafa Kutoka Kaskazini

5“Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema:

‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’

Piga kelele na kusema:

‘Kusanyikeni pamoja!

Tukimbilie katika miji yenye maboma!’

64:6 Yer 1:13-15; Isa 14:31; Za 74:4; Isa 31:9; Yer 50:2; 11:11; 18:11Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni!

Kimbilieni usalama pasipo kuchelewa!

Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini,

maangamizi ya kutisha.”

74:7 Dan 7:4; Eze 12:20; Yer 2:15; Isa 6:11; Yer 25:38; Hos 5:14; Nah 2:12; Yer 6:26Simba ametoka nje ya pango lake,

mharabu wa mataifa amejipanga.

Ametoka mahali pake

ili aangamize nchi yenu.

Miji yenu itakuwa magofu

pasipo mtu wa kuishi humo.

84:8 1Fal 21:27; Yer 30:24; Isa 22:12; 3:24; Yer 6:26; Eze 7:18; Yer 7:29; 9:20Hivyo vaeni nguo za magunia,

ombolezeni na kulia kwa huzuni,

kwa kuwa hasira kali ya Bwana

haijaondolewa kwetu.

9“Katika siku ile,” asema Bwana

“mfalme na maafisa watakata tamaa,

makuhani watafadhaika,

na manabii watashangazwa mno.”

104:10 Eze 14:9; Kut 5:23; 2The 2:11; Isa 63:17; Yer 6:14; 8:11; Eze 13:10; Mik 3:5Ndipo niliposema, “Aa, Bwana Mwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye koo zetu!”

114:11 Mwa 41:6; Hos 13:15; Eze 17:10; Law 26:33; Ay 1:19Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa, 124:12 Isa 64:6; Yer 1:16upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”

134:13 Isa 5:28; 2Sam 22:10; Eze 26:10; Kum 28:49; Mao 4:19; Isa 66:15Tazama! Anakuja kama mawingu,

magari yake yanakuja kama upepo wa kisulisuli,

farasi wake wana mbio kuliko tai.

Ole wetu! Tunaangamia!

144:14 Rut 3; 3; Yak 4:8; Za 51:2; Isa 45:22; Za 6:3Ee Yerusalemu, usafishe uovu kutoka moyoni mwako na uokolewe.

Utaendelea kuficha mawazo mapotovu mpaka lini?

154:15 Yer 8:16; Mwa 30:6; Yer 31:6Sauti inatangaza kutoka Dani,

ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.

16“Waambie mataifa jambo hili,

piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu:

‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali,

likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.

174:17 2Fal 25:1-4; 1Sam 12:15; Yer 5:23Wamemzunguka kama watu walindao shamba,

kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’ ”

asema Bwana.

184:18 Za 107:17; Ay 20:6-11; Yer 2:17-19; Isa 1:28; Yer 5:25“Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe

yameleta haya juu yako.

Hii ndiyo adhabu yako.

Tazama jinsi ilivyo chungu!

Tazama jinsi inavyochoma moyo!”

194:19 Isa 16:11; Mao 1:20; Hes 10:9; Yer 20:9; Sef 1:16; Isa 22:4; Yer 6:24Ee mtima wangu, mtima wangu!

Ninagaagaa kwa maumivu.

Ee maumivu makuu ya moyo wangu!

Moyo wangu umefadhaika ndani yangu,

siwezi kunyamaza.

Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta,

nimesikia kelele ya vita.

204:20 Kum 31:17; Za 42:7; Hes 24:5; Mao 2:4; Yer 10:20Maafa baada ya maafa,

nchi yote imekuwa magofu.

Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa,

makazi yangu kwa muda mfupi.

214:21 Hes 2:2; Isa 18:3; Yos 6:20; Hos 5:8Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita

na kusikia sauti za tarumbeta?

224:22 1Kor 14:20; Yer 5:21; 13:23; Za 36:3; Rum 16:19; Yer 5:21; 10:8; Za 14:4“Watu wangu ni wapumbavu,

hawanijui mimi.

Ni watoto wasio na akili,

hawana ufahamu.

Ni hodari kutenda mabaya,

hawajui kutenda yaliyo mema.”

234:23 Ay 9:7; 30:26; Isa 5:30; 59:9; Mao 3:2Niliitazama dunia,

nayo haikuwa na umbo tena ni tupu;

niliziangalia mbingu,

mianga ilikuwa imetoweka.

244:24 Eze 38:20; Ay 9:6; Isa 5:25; Kut 19:18Niliitazama milima, nayo ilikuwa ikitetemeka,

vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.

254:25 Hos 4:3; Sef 1:3; Yer 7:20Nilitazama, wala watu hawakuwepo;

kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.

26Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri imekuwa jangwa,

miji yake yote ilikuwa magofu

mbele za Bwana,

mbele ya hasira yake kali.

274:27 Amo 9:8; Yer 5:10; 12:12; Eze 20:17; Yer 46:28Hivi ndivyo Bwana asemavyo:

“Nchi yote itaharibiwa,

ingawa sitaiangamiza kabisa.

284:28 Yer 14:2; Hos 4:3; Hes 23:19; Isa 5:30; Yer 30:24; 23:20; 12:4-11Kwa hiyo dunia itaomboleza

na mbingu zilizo juu zitakuwa giza,

kwa sababu nimesema nami sitarudi nyuma,

nimeamua na wala sitageuka.”

294:29 Yer 8:16; Isa 6:12; 2Fal 25:4; Yer 6:23; 1Sam 26:20; Kut 33:22Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde

kila mji unakimbia.

Baadhi wanakimbilia vichakani,

baadhi wanapanda juu ya miamba.

Miji yote imeachwa,

hakuna aishiye ndani yake.

304:30 Isa 10:3-4; Eze 16:11; 23:40; 2Fal 9:30; Ay 19:14; Eze 23:9; Za 35:4Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa?

Kwa nini unajivika vazi jekundu

na kuvaa vito vya dhahabu?

Kwa nini unapaka macho yako rangi?

Unajipamba bure.

Wapenzi wako wanakudharau,

wanautafuta uhai wako.

314:31 Mwa 3:16; Mik 4:10; Isa 42:14; Mao 1:17; Yer 6:24; 13:21; 22:23; Za 9:14; Isa 42:14; Kum 32:25; Mao 2:21Nasikia kilio kama cha mwanamke

katika utungu wa kuzaa,

kilio cha uchungu kama cha anayemzaa

mtoto wake wa kwanza:

kilio cha Binti Sayuni akitweta ili aweze kupumua,

akiinua mikono yake, akisema,

“Ole wangu! Ninazimia;

maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Jeremías 4:1-31

1«Israel, si piensas volver,

vuélvete a mí

—afirma el Señor—.

Si quitas de mi vista tus ídolos abominables

y no te alejas de mí,

2si con fidelidad, justicia y rectitud

juras: “Por la vida del Señor”,

entonces “en él serán benditas las naciones,

y en él se gloriarán”».

3Así dice el Señor

a los habitantes de Judá y de Jerusalén:

«Abrid surcos en terrenos no labrados,

y no sembréis entre espinos.

4Habitantes de Judá y de Jerusalén,

marcad vuestro corazón con la señal del pacto:

circuncidaos para honrar al Señor,

no sea que por la maldad de vuestras obras

mi furor se encienda como el fuego

y arda sin que nadie pueda apagarlo.

La amenaza del norte

5»¡Anunciadlo en Judá,

proclamadlo en Jerusalén!

¡Tocad la trompeta por todo el país!

Gritad en voz alta:

“¡Reuníos y entremos

en las ciudades fortificadas!”

6Señalad a Sión con la bandera;

¡Buscad refugio, no os detengáis!

Porque yo traigo del norte

calamidad y gran destrucción.

7Un león ha salido del matorral,

un destructor de naciones se ha puesto en marcha;

ha salido de su lugar de origen

para desolar tu tierra;

tus ciudades quedarán en ruinas

y totalmente despobladas.

8Por esto, vestíos de luto,

lamentaos y gemid,

porque la ardiente ira del Señor

no se ha apartado de nosotros.

9»En aquel día desfallecerá

el corazón del rey y de los jefes;

los sacerdotes se llenarán de pánico

y los profetas quedarán atónitos»,

afirma el Señor.

10Yo dije: «¡Ah, Señor mi Dios,

cómo has engañado a este pueblo y a Jerusalén!

Dijiste: “Tendrán paz”,

pero tienen la espada en el cuello».

11En aquel tiempo se les dirá

a este pueblo y a Jerusalén:

«Desde las estériles lomas del desierto

sopla un viento abrasador

en dirección a la capital de mi pueblo.

No es el viento que sirve para aventar

ni para limpiar el trigo;

12el viento que haré venir

es demasiado fuerte para eso,

porque yo mismo

dictaré sentencia contra ellos».

13¡Miradlo avanzar como las nubes!

¡Sus carros de guerra parecen un huracán!

¡Sus caballos son más veloces que las águilas!

¡Ay de nosotros! ¡Estamos perdidos!

14Jerusalén, limpia de maldad tu corazón

para que seas salvada.

¿Hasta cuándo hallarán lugar en ti

los pensamientos perversos?

15Una voz anuncia desgracia

desde Dan y desde las colinas de Efraín.

16«Advertid a las naciones,

proclamadlo contra Jerusalén:

“De lejanas tierras vienen sitiadores

lanzando gritos de guerra

contra las ciudades de Judá”.

17La rodean como quien cuida un campo,

porque ella se rebeló contra mí

—afirma el Señor—.

18Tu conducta y tus acciones

te han causado todo esto.

Esta es tu desgracia. ¡Qué amarga es!

¡Cómo te ha calado en el propio corazón!»

19¡Qué angustia, qué angustia!

¡Me retuerzo de dolor!

Mi corazón se agita. ¡Ay, corazón mío!

¡No puedo callarme!

Puedo escuchar el toque de trompeta

y el grito de guerra.

20Un desastre llama a otro desastre;

todo el país está devastado.

De repente fueron destruidos

los pabellones y las tiendas donde habito.

21¿Hasta cuándo tendré que ver la bandera

y escuchar el toque de la trompeta?

22«Mi pueblo es necio,

no me conoce;

son hijos insensatos

que no tienen entendimiento.

Son hábiles para hacer el mal;

no saben hacer el bien».

23Miré a la tierra, y era un caos total;

miré a los cielos, y todo era tinieblas.

24Miré a las montañas, y estaban temblando;

¡se sacudían todas las colinas!

25Miré, y no quedaba nadie;

habían huido todas las aves del cielo.

26Miré, y la tierra fértil era un desierto;

yacían en ruinas todas las ciudades,

por la acción del Señor,

por causa de su ardiente ira.

27Así dice el Señor:

«Todo el país quedará desolado,

pero no lo destruiré por completo.

28Por eso el país estará de luto,

y los altos cielos se oscurecerán,

pues ya lo dije, y no me retractaré;

lo he decidido, y no me volveré atrás».

29Ante el ruido de arqueros y jinetes

huye toda la ciudad.

Algunos se meten en los matorrales,

otros trepan por los peñascos.

Toda la ciudad queda abandonada;

¡no queda un solo habitante!

30¿Qué piensas hacer, ciudad devastada?

¿Para qué te vistes de púrpura?

¿Para qué te pones joyas de oro?

¿Para qué te maquillas los ojos?

En vano te embelleces,

pues tus amantes te desprecian;

solo buscan tu muerte.

31Oigo gritos como de parturienta,

gemidos como de primeriza.

Son los gemidos de la bella Sión,

que respira con dificultad;

que extiende los brazos y dice:

«¡Ay de mí, que desfallezco!

¡Estoy en manos de asesinos!»