Yeremia 46 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 46:1-28

Ujumbe Kuhusu Misri

146:1 Yer 25:15-38; 1:10Hili ni neno la Bwana lililomjia nabii Yeremia kuhusu mataifa:

246:2 2Fal 23:29; 2Nya 35:20; Mwa 2:14Kuhusu Misri:

Huu ni ujumbe dhidi ya jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililoshindwa huko Karkemishi kwenye Mto Frati na Nebukadneza mfalme wa Babeli, katika mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda:

346:3 Isa 21:5; Yer 51:11-12; Isa 8:9-10; Yoe 3:9-10“Wekeni tayari ngao zenu, kubwa na ndogo,

mtoke kwa ajili ya vita!

446:4 Eze 21:9-11; 2Nya 26:14; Neh 4:16; 1Sam 17:5, 38Fungieni farasi lijamu,

pandeni farasi!

Shikeni nafasi zenu

mkiwa mmevaa chapeo!

Isugueni mikuki yenu,

vaeni dirii vifuani!

546:5 Yer 48:44; Za 31:13; Yer 49:29; Ufu 6:15-17Je, ninaona nini?

Wametiwa hofu,

wanarudi nyuma,

askari wao wameshindwa.

Wanakimbia kwa haraka

pasipo kutazama nyuma,

tena kuna hofu kuu kila upande,”

asema Bwana.

646:6 Isa 30:16; Za 20:8; Dan 11:19; Mwa 2:14; 15:18Walio wepesi na wenye mbio hawawezi kukimbia,

wala wenye nguvu hawawezi kutoroka.

Kaskazini, kando ya Mto Frati,

wanajikwaa na kuanguka.

746:7 Dan 11:22; Yer 47:2“Ni nani huyu ajiinuaye kama Mto Naili,

kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi?

846:8 Dan 11:10; Eze 29:3, 9; 30:12; Amo 8:8Misri hujiinua kama Mto Naili,

kama mito yenye maji yanayofanya mawimbi.

Husema, ‘Nitainuka na kufunika dunia,

nitaiangamiza miji na watu wake.’

946:9 Mwa 10:6; Yer 47:3; Isa 66:19; Eze 26:10Songeni mbele, enyi farasi!

Endesheni kwa ukali, enyi magari ya farasi,

Endeleeni mbele, enyi mashujaa:

watu wa Kushi46:9 Kushi ni Naili ya Juu; sasa ni Sudan. na Putu46:9 Putu sasa ni Libya. wachukuao ngao,

watu wa Ludi46:9 Nchi iliyo Afrika ya Kaskazini, magharibi ya Mto Naili; sasa ni Libya. wavutao upinde.

1046:10 Eze 32:10; Mao 1:15; Hes 31:3; 2Fal 23:29-30; Law 3:9; Isa 34:6Lakini ile siku ni ya Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote,

siku ya kulipiza kisasi,

kisasi juu ya adui zake.

Upanga utakula hata utakapotosheka,

hadi utakapozima kiu yake kwa damu.

Kwa maana Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, atatoa dhabihu

kwenye nchi ya kaskazini, kando ya Mto Frati.

1146:11 Yer 8:22; Mwa 37:35; 2Fal 19:21; Isa 47:1; Yer 30:13“Panda hadi Gileadi ukapate zeri,

ee Bikira Binti wa Misri.

Lakini umetumia dawa nyingi bila mafanikio;

huwezi kupona.

1246:12 Isa 19:4; Nah 3:8-10Mataifa yatasikia juu ya aibu yako,

kilio chako kitaijaza dunia.

Shujaa mmoja atajikwaa juu ya mwingine,

nao wataanguka chini pamoja.”

1346:13 Yer 43:10; Isa 19:1; Yer 27:7; Eze 32:11Huu ndio ujumbe Bwana aliomwambia nabii Yeremia kuhusu kuja kwa Nebukadneza mfalme wa Babeli ili kuishambulia Misri:

1446:14 Yer 43:8; Isa 19:13; 2Sam 2:26; Kum 32:42; Yer 24:8“Tangaza hili katika Misri, nawe ulihubiri katika Migdoli,

hubiri pia katika Memfisi46:14 Memfisi kwa Kiebrania ni Nofu. na Tahpanhesi:46:14 Ni mji katika Misri.

‘Shikeni nafasi zenu na mwe tayari,

kwa kuwa upanga unawala wale wanaokuzunguka.’

1546:15 Yos 23:5; Isa 66:15-16Kwa nini mashujaa wako wamesombwa

na kupelekwa mbali?

Hawawezi kusimama, kwa maana Bwana

atawasukuma awaangushe chini.

1646:16 Law 26:37; Isa 13:14; Yer 25:38Watajikwaa mara kwa mara,

wataangukiana wao kwa wao.

Watasema, ‘Amka, turudi

kwa watu wetu na nchi yetu,

mbali na upanga wa mtesi.’

1746:17 Isa 19:11-16; 1Fal 20:10-11Huko watatangaza,

‘Farao mfalme wa Misri ni makelele tu,

amekosa wasaa wake.’

1846:18 Yer 48:15; Yos 19:22; 1Fal 18:42“Kwa hakika kama niishivyo,” asema Mfalme,

ambaye jina lake ni Bwana Mwenye Nguvu Zote,

“mmoja atakuja ambaye ni kama Tabori miongoni mwa milima,

kama Karmeli kando ya bahari.

1946:19 Yer 48:18; Isa 20:4; 19:13; Eze 29:10-12; 35:7Funga mizigo yako kwenda uhamishoni,

wewe ukaaye Misri,

kwa kuwa Memfisi utaangamizwa

na kuwa magofu pasipo mkazi.

2046:20 Isa 14:31; Hos 10:11; Yer 47:2“Misri ni mtamba mzuri,

lakini kipanga anakuja dhidi yake kutoka kaskazini.

2146:21 2Fal 7:6; Ay 20:24; Za 18:18; Yer 18:17; Lk 15:27; Ay 18:20; Za 37:13Askari wake waliokodiwa katika safu zake

wako kama ndama walionenepeshwa.

Wao pia watageuka na kukimbia pamoja,

hawataweza kuhimili vita,

kwa maana siku ya msiba inakuja juu yao,

wakati wao wa kuadhibiwa.

2246:22 Za 74:5Misri atatoa sauti kama ya nyoka anayekimbia

kadiri adui anavyowasogelea na majeshi,

watakuja dhidi yake wakiwa na mashoka,

kama watu wakatao miti.

2346:23 Isa 29:4; Amo 7:12; Za 74:5; Kum 28:42Wataufyeka msitu wake,”

asema Bwana,

“hata kama umesongamana kiasi gani.

Ni wengi kuliko nzige,

hawawezi kuhesabika.

2446:24 2Fal 24:7; Yer 1:15Binti wa Misri ataaibishwa,

atatiwa mikononi mwa watu wa kaskazini.”

2546:25 Eze 30:14; Nah 3:4; Yer 43:12; Isa 20:6; Eze 30:22; 2Fal 24:7Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asema: “Nakaribia kuleta adhabu juu ya Amoni mungu wa Thebesi,46:25 Thebesi kwa Kiebrania ni No (au No-Amoni), mji katika Misri. na juu ya Farao, Misri na miungu yake, na wafalme wake, pamoja na wale wanaomtegemea Farao. 2646:26 Yer 44:30; Isa 19:4; Eze 32:11; 29:11-16Nitawatia mikononi mwa wale wanaotafuta uhai wao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babeli na maafisa wake. Hatimaye, hata hivyo, Misri itakaliwa kama nyakati zilizopita,” asema Bwana.

2746:27 Yer 29:14; Isa 41:13; Yer 51:46; Isa 11:11; 43:5; 41:8; Yer 50:19“Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu,

usifadhaike, ee Israeli.

Hakika nitakuokoa kutoka nchi za mbali,

uzao wako kutoka nchi ya uhamisho wao.

Yakobo atakuwa tena na amani na salama,

wala hakuna hata mmoja atakayewatia hofu.

2846:28 Kut 14:22; Hes 14:9; Yer 4:27; Isa 8:9-10Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu,

kwa maana mimi niko pamoja nawe,”

asema Bwana.

“Ingawa nitayaangamiza kabisa mataifa yote

ambayo miongoni mwake nimekutawanya,

sitakuangamiza wewe kabisa.

Nitakurudi, lakini kwa haki tu,

wala sitakuacha kabisa bila kukuadhibu.”

New International Reader’s Version

Jeremiah 46:1-28

A Message About Egypt

1A message from the Lord came to Jeremiah the prophet. It was about the nations.

2Here is what the Lord says about Egypt.

Here is his message against the army of Pharaoh Necho. He was king of Egypt. Nebuchadnezzar, the king of Babylon, won the battle over Necho’s army. That happened at Carchemish on the Euphrates River. It was in the fourth year that Jehoiakim was king of Judah. He was the son of Josiah. The message says,

3“Egyptians, prepare your shields!

Prepare large and small shields alike!

March out for battle!

4Get the horses and chariots ready to ride!

Take up your battle positions!

Put on your helmets!

Shine up your spears!

Put on your armor!

5What do I see?

The Egyptians are terrified.

They are pulling back.

Their soldiers are losing.

They run away as fast as they can.

They do not look back.

There is terror on every side,” announces the Lord.

6“Those who run fast can’t get away.

Those who are strong can’t escape.

In the north by the Euphrates River

they trip and fall.

7“Who is this that rises like the Nile River?

Who rises like rivers of rushing waters?

8Egypt rises like the Nile River.

It rises like rivers of rushing waters.

Egypt says, ‘I will rise and cover the earth.

I’ll destroy cities and their people.’

9Charge, you horses!

Drive fast, you chariot drivers!

March on, you soldiers!

March on, you men of Cush and Put who carry shields.

March on, you men of Lydia who shoot arrows.

10But that day belongs to me.

I am the Lord who rules over all.

It is a day for me to pay back my enemies.

My sword will eat until it is satisfied.

It will drink until it is not thirsty for blood anymore.

I am the Lord. I am the Lord who rules over all.

I will offer a sacrifice.

I will offer it in the land of the north

by the Euphrates River.

11“People of Egypt,

go up to Gilead and get some healing lotion.

You may try many medicines, but you will not be healed.

There isn’t any healing for you.

12The nations will hear about your shame.

Your cries of pain will fill the earth.

One soldier will trip over another.

Both of them will fall down together.”

13Nebuchadnezzar, the king of Babylon, was coming to attack Egypt. Here is the message the Lord spoke to Jeremiah the prophet about it. He said,

14“Egyptians, here is what I want you to announce in your land.

Announce it in the city of Migdol.

Also announce it in Memphis and Tahpanhes.

Say, ‘Take up your battle positions! Get ready!

The sword eats up those around you.’

15Why are your soldiers lying on the ground?

They can’t stand, because I bring them down.

16They will trip again and again.

They will fall over one another.

They will say, ‘Get up. Let’s go back home.

Let’s return to our own people and our own lands.

Let’s get away from the swords

that will bring us great harm.’

17The Egyptian soldiers will cry out,

‘Pharaoh, our king, is only a loud noise.

He has missed his chance to win the battle.’

18“I am the King.

My name is the Lord Who Rules Over All.

Someone will come who is like Mount Tabor among the mountains.

He is like Mount Carmel by the Mediterranean Sea.

And that is just as sure as I am alive,”

announces the King.

19“So pack your belongings, you who live in Egypt.

You will be taken away from your land.

Memphis will be completely destroyed.

Its buildings will be broken down.

No one will live there.

20“Egypt is like a beautiful young cow.

But Nebuchadnezzar is coming against her from the north.

He will bite her like a fly.

21Hired soldiers are in Egypt’s army.

They are like fat calves.

All of them will turn and run away.

They will not hold their positions.

The day of trouble is coming on them.

The time for them to be punished is near.

22The Egyptians will hiss like a snake that is trying to get away.

A powerful army will advance against them.

Their enemies will come against them with axes.

They will be like those who cut down trees.

23Egypt is like a thick forest.

But they will chop it down,” announces the Lord.

“There are more of their enemies than there are locusts.

In fact, they can’t even be counted.

24The nation of Egypt will be put to shame.

It will be handed over to the people of the north.”

25The Lord who rules over all is the God of Israel. He says, “I am about to punish Amon, the god of Thebes. I will also punish Pharaoh. I will punish Egypt and its gods and kings. And I will punish those who depend on Pharaoh. 26I will hand them over to those who want to kill them. I will give them to Nebuchadnezzar, the king of Babylon, and his officers. But later, many people will live in Egypt again as in times past,” announces the Lord.

27“People of Jacob, do not be afraid.

You are my servant.

Israel, do not be terrified.

I will bring you safely out of a place far away.

I will bring your children back

from the land where they were taken.

Your people will have peace and security again.

And no one will make them afraid.

28People of Jacob, do not be afraid.

You are my servant.

I am with you,”

announces the Lord.

“I will completely destroy all the nations

among which I scatter you.

But I will not completely destroy you.

I will correct you. But I will be fair.

I will not let you go without any punishment.”