Yeremia 33 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 33:1-26

Ahadi Ya Kurudishwa

133:1 Yer 32:2; 37:21; 38:28; Za 88:8; Yer 13:3Wakati Yeremia alipokuwa angali amefungwa kwenye ua wa walinzi, neno la Bwana lilimjia mara ya pili kusema: 233:2 Yer 10:16; Za 136:6; Kut 3:15; 15:3“Hili ndilo Bwana asemalo, yeye aliyeumba dunia, Bwana aliyeifanya na kuithibitisha, Bwana ndilo jina lake: 333:3 Mwa 18:17; Yer 29:12; Isa 55:6; Ay 28:11‘Niite nami nitakuitika na kukuambia mambo makuu na yasiyochunguzika, usiyoyajua.’ 433:4 2Fal 25:1; Eze 4:2; 26:8; Hab 1:10; Yer 32:24Kwa maana hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo kuhusu nyumba katika mji huu na majumba ya kifalme ya Yuda yaliyobomolewa ili yatumiwe dhidi ya kule kuzungukwa na jeshi na upanga 533:5 Yer 21:4-7; Kum 31:17; Isa 8:17katika kupigana na Wakaldayo: ‘Zitajazwa na maiti za watu nitakaowachinja katika hasira na ghadhabu yangu. Nitauficha uso wangu kwa sababu ya maovu yake yote.

633:6 Kum 32:39; Isa 30:26; 9:6“ ‘Hata hivyo, nitauletea afya na uponyaji, nitawaponya watu wangu na kuwafanya wafurahie amani tele na salama. 733:7 Yer 32:44; Eze 39:25; Amo 9:14; Isa 1:26; Yer 24:6; 30:3Nitawarudisha Yuda na Israeli kutoka nchi ya kutekwa kwao, na kuwajenga tena kama walivyokuwa hapo awali. 833:8 Law 16:30; Ebr 9:13-14; 2Sam 24:14; Mik 7:18; Yer 31:34Nitawatakasa dhambi zote walizofanya dhidi yangu, na nitawasamehe dhambi zote za uasi dhidi yangu. 933:9 Isa 60:18; Yer 13:11; Isa 64:2; Yer 3:17; 1Yn 1:7-9; Isa 55:13Kisha mji huu utaniletea utukufu, furaha, sifa na heshima mbele ya mataifa yote ya dunia yatakayosikia mambo yote mazuri ninayoufanyia. Nao watashangaa na kutetemeka kwa ajili ya wingi wa mafanikio na amani nitakayoupatia.’

1033:10 Yer 32:43; 9:11“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Mnasema kuhusu mahali hapa kwamba, “Ni mahali palipoachwa ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama.” Lakini katika miji ya Yuda na barabara za Yerusalemu ambazo zimeachwa, ambazo hazikaliwi na wanadamu wala wanyama, huko kutasikika kwa mara nyingine 1133:11 Za 51:8; 24:8; Law 7:12; 2Nya 5:13; Za 25:8; 100:4-5; 14:7sauti za shangwe na furaha, sauti za bibi na bwana arusi, na sauti za wale waletao sadaka za shukrani katika nyumba ya Bwana, wakisema,

“ ‘ “Mshukuruni Bwana Mwenye Nguvu Zote,

kwa maana Bwana ni mwema;

upendo wake wadumu milele.”

Kwa kuwa nitairudishia nchi baraka kama zilivyokuwa hapo awali,’ asema Bwana.

1233:12 Yer 32:43; Isa 65:10; Eze 34:11-15“Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Mahali hapa, ambapo ni ukiwa, pasipo na wanadamu wala wanyama: katika miji yake, patakuwepo tena malisho kwa ajili ya wachungaji kupumzisha makundi yao ya kondoo. 1333:13 Yer 32:43; Isa 65:10; Eze 34:11-15Katika miji ya nchi ya vilima, ya vilima vya magharibi na ya Negebu, katika nchi ya Benyamini, katika vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu na katika miji ya Yuda, makundi ya kondoo yatapita tena chini ya mkono wa yeye ayahesabuye,’ asema Bwana.

1433:14 Kum 28:1-14; Yos 23:15; Yer 29:10“ ‘Siku zinakuja,’ asema Bwana, ‘wakati nitakapotimiza ahadi yangu ya rehema niliyoifanya kwa nyumba ya Israeli na kwa nyumba ya Yuda.

1533:15 Isa 4:2; Za 72:2; Isa 11:1; 2Sam 7:12“ ‘Katika siku hizo na wakati huo

nitalifanya Tawi la haki lichipuke kutoka ukoo wa Daudi,

naye atafanya lile lililo haki na sawa

katika nchi.

1633:16 Isa 45:17; 1Kor 1:30; Zek 8:3, 16; Sef 3:13; Eze 48:35; Yer 3:17; Isa 59:14; Yer 32:37Katika siku hizo, Yuda ataokolewa

na Yerusalemu ataishi salama.

Hili ndilo jina atakaloitwa:

Bwana Haki Yetu.’

1733:17 2Sam 7:13; 2Nya 7:18; Za 89:29-37Kwa maana hili ndilo asemalo Bwana: ‘Daudi kamwe hatakosa mtu wa kukalia kiti cha enzi cha nyumba ya Israeli, 1833:18 Kum 18:1; Ebr 13:15; Hes 25:11-13; Ebr 7:17-22wala hata makuhani, ambao ni Walawi, kamwe hawatakosa mtu wa kusimama mbele zangu daima ili kutoa sadaka za kuteketezwa, ili kuteketeza sadaka ya nafaka na kutoa dhabihu.’ ”

19Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema: 2033:20 Za 89:36; Mwa 8:22; Isa 54:9; Mwa 1:14“Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Ikiwa mtaweza kuvunja agano langu kuhusu usiku na mchana, ili usiku na mchana visiwepo kwa nyakati zake, 2133:21 Za 89:34; 2Sam 7:13-18; 2Nya 7:18basi agano langu na Daudi mtumishi wangu, na agano langu na Walawi ambao ni makuhani wanaohudumu mbele zangu, linaweza kuvunjwa, na Daudi hatakuwa tena na mzao wa kutawala katika kiti chake cha enzi. 2233:22 Mwa 15:5; Hos 1:10; Mwa 13:16; Yer 30:19; Mwa 12:2Nitawafanya wazao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi wanaohudumu mbele zangu wengi, wasioweza kuhesabika kama nyota za angani, tena wasiopimika kama mchanga wa ufuoni mwa bahari.’ ”

23Neno la Bwana likamjia Yeremia kusema: 2433:24 Eze 37:22; Neh 4:4; Yer 30:17; Eze 36:20“Je, hujasikia kwamba watu hawa wanasema, ‘Bwana amezikataa zile falme mbili alizozichagua?’ Kwa hiyo wamewadharau watu wangu, na hawawaoni tena kama taifa. 2533:25 Mwa 1:18; Yer 31:35-36; Za 74:16-17; 148:6Hili ndilo asemalo Bwana: ‘Kama sijathibitisha agano langu na usiku na mchana, na kuziweka wakfu sheria za mbingu na nchi, 2633:26 Law 26:44; Yer 31:37; Isa 14:1; Zek 10:6; Za 14:7; Yer 30:18basi nitawakataa wazao wa Yakobo na Daudi mtumishi wangu, na sitachagua mmoja wa wanawe kutawala juu ya wazao wa Abrahamu, Isaki na Yakobo. Kwa maana nitawarudisha kutoka nchi ya kutekwa kwao na kuwaonea huruma.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米書 33:1-26

應許以色列人必復興

1耶利米被囚禁在護衛兵院子裡的時候,耶和華第二次對他說: 2「耶和華創造大地,使其成形、根基穩固,祂名叫耶和華。祂說, 3『你呼求我,我就回應你,並且把你不知道的偉大、奧妙之事告訴你。 4以色列的上帝耶和華說,耶路撒冷城中的房屋和王宮被拆毀,用來修建防衛工事, 5城中的人與迦勒底人爭戰只會使自己的房屋堆滿死屍,因為我要在憤怒中毀滅他們。他們作惡多端,我必掩面不理這城。 6但有一天,我必使這城復興,醫治她的創傷,使她繁榮昌盛。 7我要使被擄的猶大人和以色列人回到故土,重建家園。 8我要除去他們的一切罪惡,赦免他們的一切罪過。 9這城要使我在天下萬國面前得到尊崇、頌讚和榮耀。萬民聽見我使這城繁榮昌盛,都恐懼戰慄。』」

10耶和華說:「你們說猶大的城邑和耶路撒冷的街道一片荒涼、人畜絕跡, 11但這些地方必傳出歡樂聲、新郎新娘的歡笑聲和在耶和華殿中獻感恩祭者的歌唱聲,

『要感謝萬軍之耶和華,

因為耶和華是美善的,

祂的慈愛永遠長存』。

因為我必使被擄的人回到故土,重建家園。這是耶和華說的。」

12萬軍之耶和華說:「在這一片荒涼、人畜絕跡的地方,在它所有城邑的周圍必再有供牧人放羊的草場。 13在山區、丘陵和南地的城邑,以及便雅憫耶路撒冷周圍和猶大的城邑必有人清點羊群。這是耶和華說的。」 14耶和華說:「看啊,時候將到,我要實現我給以色列人和猶大人的美好應許。 15那時,我要使大衛公義的苗裔興起,他要在地上秉公行義。 16那時,猶大必得到拯救,耶路撒冷必安享太平並被稱為『耶和華是我們的義』。 17因為耶和華說,『我應許大衛的後裔必永遠統治以色列18做祭司的利未人必永遠在我面前獻燔祭、素祭等祭物。』」

19耶和華對耶利米說: 20「這是耶和華說的,『除非你們能廢除我與白晝黑夜所立的約,叫白晝黑夜不再按時更替, 21才能廢除我與我僕人大衛所立的約,使他的王位後繼無人,也才能廢除我與事奉我的利未祭司所立的約。 22我要使我僕人大衛的後裔和事奉我的利未人像天上的星和海邊的沙一樣不可勝數。』」

23耶和華對耶利米說: 24「你聽見了嗎?人們說,『耶和華已經棄絕了祂所揀選的以色列猶大兩個國家。』他們藐視我的子民,視他們為亡國之民。 25然而,耶和華說,『正如我決不廢棄我所定的晝夜交替和天地運行之律, 26我也決不棄絕雅各的後裔,不棄絕我僕人大衛的後裔。我必讓大衛的後裔做王統治亞伯拉罕以撒雅各的子孫,因為我必使被擄的人回到故土,恩待他們。』」