Yeremia 31 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 31:1-40

Mahamisho Kurudi Kwa Shangwe

131:1 Law 26:12; Yer 30:22“Wakati huo, nitakuwa Mungu wa koo zote za Israeli nao watakuwa watu wangu,” asema Bwana.

231:2 Hes 14:20; Kut 33:14; Kum 12:9Hili ndilo asemalo Bwana:

“Watu watakaopona upanga

watapata upendeleo jangwani;

nitakuja niwape Israeli pumziko.”

331:3 Rum 11:28; Kum 4:37; Hos 11:4; Yn 6:44Bwana alitutokea wakati uliopita, akisema:

“Nimekupenda kwa upendo wa milele,

nimekuvuta kwa wema.

431:4 Yer 30:18-19; 2Fal 19:21; Mwa 31:27; Kut 15:20; Yer 30:19Nitakujenga tena nawe utajengeka upya,

ewe Bikira Israeli.

Utachukua tena matari yako

na kwenda kucheza na wenye furaha.

531:5 Yer 33:13; Oba 1:19; Isa 65:12; Amo 9:14; Kum 20:6; Yer 50:19; Isa 37:30Utapanda tena shamba la mizabibu

juu ya vilima vya Samaria,

wakulima watapanda

na kufurahia matunda yake.

631:6 Kum 33:19; Mik 4:2; Isa 52:8; 56:10; Yer 50:4-5Itakuja siku wakati walinzi watakapowapigia kelele

juu ya vilima vya Efraimu wakisema,

‘Njooni, twendeni juu Sayuni,

kwake Bwana Mungu wetu.’ ”

731:7 Kum 28:13; Isa 61:9; Za 14:7; 28:9; Isa 37:31; 12:6Hili ndilo asemalo Bwana:

“Mwimbieni Yakobo kwa furaha,

mpigieni kelele aliye mkuu wa mataifa.

Zifanyeni sifa zenu zisikike, nanyi mseme,

‘Ee Bwana, okoa watu wako,

mabaki ya Israeli.’

831:8 Yer 3:18; Mwa 33:13; Za 106:47; Isa 42:16; Eze 34:16; 34:12-14Tazama, nitawaleta kutoka nchi ya kaskazini

na kuwakusanya kutoka miisho ya dunia.

Miongoni mwao watakuwepo vipofu na viwete,

mama wajawazito na wenye utungu wa kuzaa.

Umati mkubwa wa watu utarudi.

931:9 Ezr 3:12; Za 126:5; Isa 63:13; Za 126:5; Isa 63:13; 40:4; 49:11; Kut 4:22; Hes 20:8Watakuja wakilia;

wataomba wakati ninawarudisha.

Nitawaongoza kando ya vijito vya maji

katika mapito yaliyo tambarare ambapo hawatajikwaa,

kwa sababu mimi ndimi baba wa Israeli,

naye Efraimu ni mzaliwa wangu wa kwanza.

1031:10 Isa 66:19; Kum 30:4; Isa 11:12; 40:11; Eze 34:12; Yer 25:22; Law 26:33“Sikieni neno la Bwana, enyi mataifa,

litangazeni katika nchi za pwani ya mbali:

‘Yeye aliyewatawanya Israeli atawakusanya

na atalichunga kundi lake la kondoo kama mchungaji.’

1131:11 Kut 6:6; Isa 44:23; Za 142:6; 9:16Kwa kuwa Bwana atamlipia fidia Yakobo

na kuwakomboa mkononi mwa walio na nguvu kuliko wao.

1231:12 Eze 40:2; Mik 4:1; Yoe 3:18; Hes 18:12; Hos 2:21-22; Wim 4:15; Yn 16:22; Isa 58:11; Wim 4:15; Isa 30:19Watakuja na kupiga kelele kwa furaha katika miinuko ya Sayuni;

watashangilia ukarimu wa Bwana:

nafaka, divai mpya na mafuta,

wana-kondoo wachanga

na ndama wa makundi ya ngʼombe nitakaowapa.

Watakuwa kama bustani iliyonyeshewa vizuri,

wala hawatahuzunika tena.

1331:13 Isa 61:3; Za 30:11; Isa 51:11Kisha wanawali watacheza na kufurahi,

vijana waume na wazee pia.

Nitageuza maombolezo yao kuwa furaha,

nitawapa faraja na furaha badala ya huzuni.

1431:14 Law 7:35-36; Za 36:8; Isa 30:23Nitawashibisha makuhani kwa wingi,

nao watu wangu watajazwa kwa ukarimu wangu,”

asema Bwana.

1531:15 Yos 18:25; Mwa 37:35; Yer 10:20; Mt 2:17-18; Ay 7:21Hili ndilo asemalo Bwana:

“Sauti imesikika huko Rama,

maombolezo na kilio kikubwa,

Raheli akiwalilia watoto wake

na anakataa kufarijiwa,

kwa sababu watoto wake hawako tena.”

1631:16 Za 30:5; Isa 25:8; Rut 2:12; Eze 11:17-18; 2Nya 15:7; Yer 30:3; Isa 30:19Hili ndilo asemalo Bwana:

“Izuie sauti yako kulia,

na macho yako yasitoe machozi,

kwa kuwa kazi yako itapata thawabu,”

asema Bwana.

“Watarudi kutoka nchi ya adui.

17Kwa hiyo kuna tumaini kwa siku zijazo,”

asema Bwana.

“Watoto wako watarudi nchi yao yenyewe.

1831:18 Ay 5:17; Hos 4:16; 10:11; Za 80:3-4; Mao 5:21; Yer 50:11“Hakika nimeyasikia maombolezo ya Efraimu:

‘Ulinirudi kama ndama mkaidi,

nami nimekubali kutii.

Unirudishe, nami nitarudi,

kwa sababu wewe ndiwe Bwana, Mungu wangu.

1931:19 Za 95:10; Eze 36:31; 21:12; Lk 18:13; Yer 8:4; Ezr 9:6; Za 25:7Baada ya kupotea, nilitubu;

baada ya kuelewa, nilijipiga kifua.

Niliaibika na kuona haya

kwa sababu niliibeba aibu ya ujana wangu.’

2031:20 Isa 44:21; Hos 4:4; Mik 7:18; 1Fal 3:26; Mao 3:33; Isa 55:7Je, Efraimu si mwanangu mpendwa,

mtoto ninayependezwa naye?

Ingawa mara kwa mara ninanena dhidi yake,

bado ninamkumbuka.

Kwa hiyo moyo wangu unamwonea shauku,

nina huruma kubwa kwa ajili yake,”

asema Bwana.

2131:21 Isa 35:8; Yer 50:5; Isa 52:11; Yer 3:12; Eze 21:19“Weka alama za barabara,

weka vibao vya kuelekeza.

Zingatia vyema njia kuu,

barabara ile unayoipita.

Rudi, ee Bikira Israeli,

rudi kwenye miji yako.

2231:22 Yer 2:23; Hos 4:16; Isa 43:19; Kum 32:10Utatangatanga hata lini,

ee binti usiye mwaminifu?

Bwana ameumba kitu kipya duniani:

mwanamke atamlinda mwanaume.”

2331:23 Yer 30:18; Isa 1:26; Zek 8:3; Mwa 28:3; Hes 6:24; Isa 2:2; Za 48:1Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo, “Nitakapowarudisha toka nchi ya kutekwa kwenu, watu walio katika nchi ya Yuda na miji yake kwa mara nyingine tena watatumia maneno haya: ‘Bwana akubariki, ee makao ya haki, ee mlima mtakatifu.’ 2431:24 Yer 33:12, 18; Zek 8:4-8; Yer 30:18Watu wataishi pamoja katika Yuda na miji yake yote, wakulima na wote wanaohamahama na mifugo yao. 2531:25 Yn 4:14; Isa 40:29Nitawaburudisha waliochoka na kuwatuliza walio na huzuni.”

26Kwa jambo hili niliamka na kuangalia pande zote. Usingizi wangu ulikuwa mtamu kwangu.

2731:27 Eze 36:9-11; Hos 2:23; Yer 16:14Bwana asema, “Siku zinakuja, nitakapoongeza idadi ya watu, na kuzidisha hesabu ya mifugo katika nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda. 2831:28 Yer 18:8; 44:27; Kum 30; 9; Amo 9:14; Ay 29:2; Eze 36:10-11; Yer 1:10Kama vile nilivyowaangalia ili kungʼoa na kubomoa, kuharibu, kuangamiza na kuleta maafa juu yao, vivyo hivyo nitawaangalia ili kujenga na kupanda,” asema Bwana. 2931:29 Mwa 9:25; Kum 24:16; Eze 18:2; Mao 5:7“Katika siku hizo, watu hawatasema tena,

“ ‘Baba wamekula zabibu chachu,

nayo meno ya watoto yakatiwa ganzi.’

3031:30 2Fal 14:6; Gal 6:7; Isa 3:11Badala yake, kila mmoja atakufa kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe; yeyote alaye zabibu chachu, meno yake mwenyewe yatatiwa ganzi.

3131:31 Kum 29:14; Ebr 8:8-12; Yer 33:14; Lk 22:20; Isa 42:6; 54:10; Ebr 10:16-17“Siku zinakuja,” asema Bwana,

“nitakapofanya agano jipya

na nyumba ya Israeli

na nyumba ya Yuda.

3231:32 Kut 24:8; Kum 5:3; 1:31; Yer 11:4; Isa 54:5Halitafanana na agano

nililofanya na baba zao

wakati nilipowashika mkono

kuwaongoza watoke Misri,

kwa sababu walivunja agano langu,

ijapokuwa nilikuwa mume kwao,”

asema Bwana.

3331:33 Kum 6:6; 2Kor 3:3; Yer 24:7; Ebr 10:16; Za 40:8; Kut 4:15“Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli

baada ya siku zile,” asema Bwana.

“Nitaweka sheria yangu katika nia zao,

na kuiandika mioyoni mwao.

Nitakuwa Mungu wao,

nao watakuwa watu wangu.

3431:34 1Yn 2:27; Yn 6:45; Isa 54:13; Za 85:2; Mik 7:19; Rum 11:27; Isa 11:9Mtu hatamfundisha tena jirani yake,

wala mtu kumfundisha ndugu yake akisema, ‘Mjue Bwana Mungu,’

kwa sababu wote watanijua mimi,

tangu aliye mdogo kabisa kwao, hadi aliye mkuu sana,”

asema Bwana.

“Kwa sababu nitasamehe uovu wao,

wala sitazikumbuka dhambi zao tena.”

3531:35 Za 136:7-9; Mwa 1; 16; Yer 10:16; Kut 14:21; Za 93:3Hili ndilo asemalo Bwana,

yeye aliyeweka jua

liwake mchana,

yeye anayeamuru mwezi na nyota

kungʼaa usiku,

yeye aichafuaye bahari

ili mawimbi yake yangurume;

Bwana Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake:

3631:36 Ay 38:33; Isa 54:9-10; Za 89:36-37; Yer 33:20-26“Ikiwa amri hizi zitaondoka machoni pangu,”

asema Bwana,

“ndipo wazao wa Israeli watakoma

kuwa taifa mbele yangu daima.”

3731:37 Ay 38:5; Yer 33:22, 24, 26; Rum 11:1-5Hili ndilo asemalo Bwana:

“Ikiwa mbingu zilizo juu zitaweza kupimika

na misingi ya dunia chini

ikaweza kuchunguzwa,

ndipo nitakapowakataa wazao wote wa Israeli

kwa sababu ya yote waliyoyatenda,”

asema Bwana.

3831:38 Yer 30:18; Neh 3:1; 2Nya 25:23; Zek 14:10; Yer 24:6; 2Fal 14:13“Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mji huu utajengwa upya kwa ajili yangu, kuanzia mnara wa Hananeli hadi Lango la Pembeni. 3931:39 1Fal 7:23Kamba ya kupimia itaanzia hapo kuendelea hadi kwenye kilima cha Garebu, na kisha kugeuka kuelekea Goa. 4031:40 Yer 2:23; 7:31-32; 1Sam 15:23; Yn 18:1; 2Fal 11:16; Yoe 3:17; Zek 14:21Bonde lote watupwapo maiti na majivu pia na matuta yote kutoka Bonde la Kidroni upande wa mashariki hadi pembe ya Lango la Farasi, itakuwa takatifu kwa Bwana. Kamwe mji huu hautangʼolewa tena wala kubomolewa.”

Korean Living Bible

예레미야 31:1-40

1여호와께서 말씀하신다. “그 때에 내가 이스라엘 모든 가족의 하나님이 되고 그들은 내 백성이 될 것이다.

2이스라엘 백성이 안식을 찾아갈 때에 광야에서 칼날을 피한 자들이 은혜를 얻었다.

3그때 나 여호와는 이스라엘 백성에게 나타나 ‘내가 영원한 사랑으로 너희를 사랑하였으므로 한결같은 사랑으로 너희를 인도하였다’ 하고 말하였다.

4이스라엘 백성아, 내가 다시 너희를 일으켜 세우겠다. 너희가 소고를 들고 즐겁게 춤출 것이다.

5너희가 다시 사마리아 산에 포도나무를 심을 것이며 그것을 심은 자가 그 과일을 먹을 것이다.

6에브라임 산에서 파수꾼들이 ‘자, 시온으로 올라가서 우리 하나님 여호와께 나아가자!’ 하고 외칠 날이 올 것이다.”

7여호와께서 다시 말씀하신다. “너희는 이스라엘을 위해 기쁨으로 노래하라. 세계에서 가장 위대한 나라를 위해 외쳐라. 너희는 이렇게 선포하며 찬양하라. ‘여호와께서 자기 백성을 구원하시고 남은 자를 다 구출하셨다.’

8보라, 내가 그들을 북쪽 땅에서 인도해 내고 그들을 땅 끝에서부터 모을 것이니 소경과 절뚝발이와 임신부와 해산할 여인들과 함께 그들이 큰 민족이 되어 돌아올 것이다.

9그들은 돌아올 때 기쁨의 눈물을 흘리며 기도할 것이요 나는 그들이 넘어지지 않도록 그들을 평탄한 시냇가의 길로 인도할 것이다. 이것은 내가 이스라엘의 아버지이며 에브라임은 나의 장남이기 때문이다.

10“모든 민족들아, 너희는 나 여호와의 말을 듣고 먼 해안 지역에 전파하라. ‘이스라엘 백성을 흩으신 자가 그들을 모으시고 목자가 자기 양떼를 지키듯이 그들을 지키실 것이다.’

11나 여호와가 이스라엘을 해방시키고 그들을 강한 자의 손에서 구할 것이다.

12그들은 돌아와 시온산에서 기쁨으로 노래할 것이며 나의 선물인 곡식과 새 포도주와 기름과 양떼와 소떼를 보고 기뻐할 것이다. 그들은 물을 댄 동산 같아서 다시는 걱정할 일이 없을 것이다.

13그때 처녀들이 춤을 추고 기뻐할 것이며 청년들과 노인들이 함께 즐거워할 것이다. 나는 그들의 슬픔이 변하여 기쁨이 되게 하고 그들을 위로하여 근심 대신 기쁨을 주겠다.

14내가 제사장들에게 풍성한 것으로 채우며 내 백성들을 나의 좋은 것으로 만족하게 할 것이다. 이것은 나 여호와의 말이다.”

15여호와께서 말씀하신다. “라마에서 한 소리가 들리니 슬퍼하고 통곡하는 소리이다. 라헬이 자식을 잃고 슬퍼하며 위로 받기를 거절하는구나.”

16여호와께서 다시 말씀하신다. “너는 울음을 그치고 눈물을 거두어라. 네 일이 보상받을 것이며 네 자식들이 원수의 땅에서 돌아올 것이다.

17너의 미래에 희망이 있을 것이니 그들이 고향 땅으로 돌아올 것이다. 이것은 나 여호와의 말이다.

18“나는 에브라임이 이렇게 탄식하는 소리를 들었다. ‘주께서 나를 징계하시므로 내가 길들지 않은 송아지처럼 징계를 받았습니다. 주는 나의 하나님 여호와이십니다. 나를 회복시키소서. 그러면 내가 돌아가겠습니다.

19나는 주를 떠난 후에 곧 뉘우쳤고 깨달은 후에는 가슴을 치며 슬퍼했습니다. 나는 젊었을 때 지은 죄로 창피해서 견딜 수 없었습니다.’

20“에브라임은 나의 사랑하는 아들이요 기뻐하는 자식이 아니냐? 내가 가끔 그를 꾸짖긴 하지만 나는 여전히 그를 기억하고 있다. 그러므로 내 마음이 그를 그리워하게 되니 내가 그를 불쌍히 여길 것이다. 이것은 나 여호와의 말이다.

21“처녀 이스라엘아, 너를 위해 도로 표지판을 세우고 안내판을 세워라. 그래서 네가 가는 길을 눈여겨 보았다가 돌아오너라. 네 성으로 돌아오너라.

22신실치 못한 딸아, 네가 언제까지 방황하겠느냐? 나 여호와가 이 땅에 새로운 일이 일어나게 할 것이니 31:22 또는 ‘여자가 남자를 안으리라’여자가 남자를 둘러싸고 보호하는 것과 같은 아주 색다른 일이다.”

23전능하신 여호와 이스라엘의 하나님이 말씀하신다. “내가 포로들을 다시 그들의 땅으로 돌아오게 할 때에 그들이 유다 땅과 그 모든 성에서 다시 이런 말을 쓸 것이다. ‘의의 처소여, 거룩한 산이여, 여호와께서 너를 축복하시기 원하노라.’

24“그리고 백성들이 유다와 그 모든 성에 함께 살 것이며 거기는 농부들과 양떼를 인도하는 목자들도 있을 것이다.

25내가 피곤한 자를 상쾌하게 하고 지쳐 있는 자를 만족하게 하겠다.”

26이때 나는 깨어나 단잠을 자고 난 것을 알게 되었다.

27여호와께서 말씀하신다. “보라, 내가 이스라엘과 유다 땅에 사람과 짐승의 수를 헤아릴 수 없이 많게 할 날이 올 것이다.

28내가 그들을 철저하게 뽑고 파괴하며 허물고 엎어 버리며 멸망시키고 재앙으로 쳤던 것처럼 앞으로는 철저하게 그들을 세우고 심을 것이다.

29그때 백성들은 ‘아버지가 신 포도를 먹었는데 아들의 이가 시다’ 는 말을 더 이상 하지 않을 것이다.

30그러므로 신 포도를 먹는 그 사람만 이가 시게 되는 것처럼 모든 사람은 자기 자신의 죄에 대해서만 책임을 지고 죽게 될 것이다.”

31여호와께서 말씀하신다. “내가 이스라엘 및 유다 백성과 새로운 계약을 맺을 날이 올 것이다.

32이 계약은 내가 그들의 조상들을 이집트에서 인도해 내던 때에 맺은 계약과 같지 않을 것이다. 나는 그들에게 남편처럼 되었으나 그들은 나와 맺은 계약을 어겼다.

33그러나 그 후에 내가 이스라엘 백성과 맺을 새로운 계약은 이렇다: 내가 나의 법을 그들 속에 새기고 그들의 마음에 기록할 것이다. 그리고 나는 그들의 하나님이 되고 그들은 내 백성이 될 것이다.

34그 때에는 아무도 자기 형제나 이웃에게 나를 알도록 가르칠 필요가 없을 것이다. 이것은 모든 사람이 다 나를 알게 될 것이기 때문이다. 내가 그들의 잘못을 용서하고 다시는 그들의 죄를 기억하지 않을 것이다. 이것은 나 여호와의 말이다.”

35낮에 빛을 내는 해를 주시고 달과 별들의 질서를 정하셔서 밤을 비추게 하시며 바다를 휘저어 성난 파도를 일으키시는 여호와, 그의 이름은 전능하신 여호와이시다.

36여호와께서 말씀하신다. “이런 자연 질서가 지속되는 한 이스라엘도 언제까지나 나라로서 존속할 것이다.

37하늘이 측량되고 땅의 기초가 탐지된다면 몰라도 그런 일이 있기 전에는 이스라엘 백성이 죄를 지었다는 이유로 내가 그들을 버리지 않을 것이다.”

38여호와께서 말씀하신다. “예루살렘은 북동쪽의 하나넬 망대에서부터 북서쪽의 모퉁이문까지 나 여호와의 성으로 건설될 것이다.

39그 경계선은 다시 모퉁이문에서부터 서쪽으로 가렙산에 곧게 이어지고 거기서 고아를 돌 것이다.

40그리고 죽은 사람의 시체나 재를 버리는 골짜기와 기드론 시내와 동쪽으로 말문에 이르는 모든 밭이 다 나 여호와의 성지가 되고 다시는 허물어지거나 파괴되는 일이 없을 것이다.”