Yeremia 24 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Yeremia 24:1-10

Vikapu Viwili Vya Tini

124:1 2Fal 24:16; 2Nya 36:9; Kut 23:19; Kum 26:2; Amo 8:1-2Baada ya Yekonia24:1 Yekonia au Konia ni jina jingine la Yehoyakini. mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na maafisa, mafundi stadi na wahunzi wa Yuda, kuchukuliwa kutoka Yerusalemu kwenda Babeli na Nebukadneza mfalme wa Babeli kwenda uhamishoni huko Babeli, Bwana akanionyesha vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya Hekalu la Bwana. 224:2 Wim 2:13; Isa 5:4Kikapu kimoja kilikuwa na tini nzuri sana, kama zile za mavuno ya kwanza. Kikapu cha pili kilikuwa na tini dhaifu sana, mbovu mno zisizofaa kuliwa.

324:3 Yer 1:11; Amo 8:1-2Kisha Bwana akaniuliza, “Je, Yeremia, unaona nini?”

Nikamjibu, “Ninaona tini zile zilizo nzuri ni nzuri sana, lakini zilizo dhaifu ni mbovu mno zisizofaa kuliwa.”

4Kisha neno la Bwana likanijia: 524:5 Yer 29:4, 20“Hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Kama zilivyo hizi tini nzuri, ndivyo ninavyowaona kuwa bora watu wa uhamisho kutoka Yuda, niliowaondoa kutoka mahali hapa kwenda katika nchi ya Wakaldayo. 624:6 Kum 30:3; Eze 11:17; Yer 42:10; 30:9; Amo 9:14-15Macho yangu yatakuwa juu yao kwa ajili ya kuwapatia mema, nami nitawarudisha tena katika nchi hii. Nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawangʼoa, 724:7 Law 26:12; Ebr 8:10; Yer 32:40; 2Nya 6:37; Eze 11:19; Isa 11:9; 51:18; Zek 2:11nitawapa moyo wa kunifahamu mimi, kwamba mimi ndimi Bwana. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao, kwa maana watanirudia kwa moyo wao wote.

824:8 Yer 29:17; 39:6-9; 44:26; 46:14; 32:4-5; 44:30“ ‘Lakini kama zilivyo zile tini dhaifu, ambazo ni mbovu mno zisizofaa kuliwa,’ asema Bwana, ‘ndivyo nitakavyomtendea Sedekia mfalme wa Yuda, maafisa wake na mabaki wengine kutoka Yerusalemu, wawe wamebaki katika nchi hii, au wanaishi Misri. 924:9 Yer 25:18; 34:17; Kum 28:25; 2Fal 22:19; Yer 29:18; Dan 9:7; Yer 15:4Nitawafanya kuwa chukizo kabisa na kitu cha kulaumiwa katika mataifa yote ya dunia, watakuwa aibu na kitu cha kudharauliwa, chombo cha dhihaka na kulaaniwa, popote nitakapowafukuzia. 1024:10 Isa 51:19; Ufu 6:8; Yer 27:8; 9:16; 15:2; Kum 28:21Nitautuma upanga, njaa na tauni dhidi yao hadi wawe wameangamia kutoka nchi niliyowapa wao na baba zao.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

耶利米書 24:1-10

兩筐無花果的比喻

1巴比倫尼布甲尼撒耶路撒冷猶大約雅敬的兒子耶哥尼雅猶大的官員、技工和工匠擄到巴比倫以後,耶和華使我看見兩筐無花果放在祂的殿前。 2一筐無花果極好,好像初熟的果子;另一筐則壞得不能吃。 3耶和華問我:「耶利米啊,你看見什麼?」我回答說:「無花果。好的好極了,壞的壞得不能吃。」

4耶和華便對我說: 5以色列的上帝耶和華這樣說,『那些從這裡被擄到迦勒底猶大人在我眼中是好無花果。 6我要眷顧他們,帶他們回到這裡。我要使他們興起,不再毀滅他們;我要栽培他們,不再剷除他們; 7我要賜給他們一顆心,使他們認識我是耶和華。他們要做我的子民,我要做他們的上帝,因為他們必全心全意地歸向我。』 8至於那些壞得不能吃的無花果,耶和華這樣說,『猶大西底迦及其官員,以及留在耶路撒冷埃及的人在我眼中就像壞得不能吃的無花果。我必丟棄他們, 9使他們的遭遇令天下萬國驚懼。在我流放他們去的地方,他們必受凌辱、嘲笑、譏諷和咒詛。 10我要使戰爭、饑荒和瘟疫臨到他們,直到他們在我賜給他們和他們祖先的土地上滅亡。』」