Wimbo 1 – NEN & NASV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Wimbo 1:1-17

11:1 1Fal 4:32; Za 45Wimbo ulio bora wa Solomoni.

Shairi La Kwanza

Mpendwa

21:2 Wim 8:6; Mwa 14:18; Amu 9:13; Wim 4:10Unibusu kwa busu la kinywa chako,

kwa maana upendo wako unafurahisha kuliko divai.

31:3 Es 2:12; Za 45:8-14; Mhu 7:1Manukato yako yananukia vizuri,

jina lako ni kama manukato yaliyomiminwa.

Ndiyo sababu wanawali wanakupenda!

41:4 Yer 31:3; Flp 3:12; Wim 2:3Nichukue twende nawe, na tufanye haraka!

Mfalme na anilete ndani ya vyumba vyake.

Marafiki

Tunakushangilia na kukufurahia,

tutasifu upendo wako zaidi kuliko divai.

Mpendwa

Tazama jinsi ilivyo bora wakupende!

51:5 Wim 2:14; 2:7; 5:16; 4:3; Mwa 25:13Mimi ni mweusi, lakini napendeza,

enyi binti za Yerusalemu,

mweusi kama mahema ya Kedari,

kama mapazia ya hema la Solomoni.

61:6 Za 69:8; Wim 7:12; 8:12; 2:15Usinikazie macho kwa sababu mimi ni mweusi,

kwa sababu nimefanywa mweusi na jua.

Wana wa mama yangu walinikasirikia

na kunifanya niwe mtunza mashamba ya mizabibu.

Shamba langu mwenyewe la mizabibu nimeliacha.

71:7 Wim 3:1-4; Isa 13:20; Mwa 24:65Niambie, wewe ambaye ninakupenda,

unalisha wapi kundi lako la kondoo

na ni wapi unapowapumzisha kondoo wako adhuhuri.

Kwa nini niwe kama mwanamke aliyefunikwa shela

karibu na makundi ya rafiki zako?

Marafiki

81:8 Wim 5:9; 6:1Kama hujui, ewe mwanamke mzuri kuliko wote,

fuata nyayo za kondoo,

na kulisha wana-mbuzi wako

karibu na hema za wachungaji.

Mpenzi

91:9 Wim 2:2; 2Nya 1:16-17Mpenzi wangu, ninakufananisha na farasi jike

aliyefungwa katika mojawapo ya magari ya vita ya Farao.

101:10 Eze 16:11; Isa 61:10; Wim 5:13Mashavu yako yanapendeza yakiwa na vipuli,

shingo yako ikiwa na mikufu ya vito.

11Tutakufanyia vipuli vya dhahabu,

vyenye kupambwa kwa fedha.

Mpendwa

121:12 Wim 4:11-14Wakati mfalme alipokuwa mezani pake,

manukato yangu yalisambaza harufu yake nzuri.

131:13 Mwa 37:25Mpenzi wangu kwangu mimi ni kifuko cha manemane

kati ya matiti yangu.

141:14 Wim 4:13; 1Sam 23:291:14 2Nya 20:2; Wim 2:3; 5:8Mpenzi wangu kwangu mimi ni kama kishada cha maua ya mhina

kutoka mashamba ya mizabibu ya En-Gedi.

Mpenzi

151:15 Wim 4:7; 7:6; Za 74:19; Yer 48:28Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu!

Tazama jinsi ulivyo mzuri!

Macho yako ni kama ya hua.

Mpendwa

16Tazama jinsi ulivyo mzuri, mpenzi wangu!

Ee, tazama jinsi unavyopendeza!

Na kitanda chetu ni cha majani mazuri.

Mpenzi

171:17 1Fal 6:9Nguzo za nyumba yetu ni mierezi,

na mapao yetu ni miberoshi.

New Amharic Standard Version

ማሕልየ መሓልይ 1:1-17

1ከመዝሙር ሁሉ የሚበልጥ የሰሎሞን መዝሙር።

ሙሽራዪቱ

2በከንፈሩ መሳም ይሳመኝ

ፍቅርህ ከወይን ጠጅ ይልቅ ደስ ያሰኛልና።

3የሽቱህ መዐዛ ደስ ያሰኛል፤

ስምህ እንደሚፈስስ ሽቱ ነው፤

ታዲያ ቈነጃጅት ቢወድዱህ ምን ያስደንቃል!

4ይዘኸኝ ሂድ፤ እንፍጠን፤

ንጉሡ ወደ ዕልፍኞቹ አምጥቶኛል።

ባልንጀሮቿ

በአንተ1፥4 በዕብራይስጥ ነጠላ ተባዕታይ ነው። ደስ ይለናል፤ ሐሤትም እናደርጋለን፤

ከወይን ጠጅ ይልቅ ፍቅርህን እንወድሳለን።

ሙሽራዪቱ

አንተን እንደዚህ ማፍቀራቸው ትክክል ነው።

5እናንት የኢየሩሳሌም ቈነጃጅት ሆይ፤

እኔ ጥቍር ነኝ፤ ይሁን እንጂ ውብ ነኝ፤

ጥቍረቴ እንደ ቄዳር ድንኳኖች፣

እንደ ሰሎሞን1፥5 ወይም ሳልማ ቤተ መንግሥት መጋረጃዎችም ነው።

6ጥቍር ስለሆንሁ ትኵር ብላችሁ አትዩኝ፤

መልኬን ያጠቈረው ፀሓይ ነውና፤

የእናቴ ልጆች ወንድሞቼ ተቈጡኝ፤

የወይን ተክል ቦታዎችም ጠባቂ አደረጉኝ፤

የራሴን የወይን ተክል ቦታ ተውሁት።

7ውዴ ሆይ፤ መንጋህን የት እንደምታሰማራ፣

በቀትርም የት እንደምትመስጋቸው

እባክህ ንገረኝ፤

በወዳጆችህ መንጎች ኋላ፣

ፊቷን ሸፍና እንደምትቅበዘበዝ ሴት ለምን ልሁን?

ባልንጀሮቿ

8አንቺ ከሴቶች ሁሉ ይበልጥ የተዋብሽ ሆይ፤ የማታውቂ ከሆነ፣

የበጎቹን ዱካ ተከተዪ፤

የፍየል ግልገሎችሽንም፣

በእረኞቹ ድንኳን አጠገብ አሰማሪ።

ሙሽራው

9ውዴ ሆይ፤ የፈርዖንን ሠረገሎች ከሚስቡ ፈረሶች መካከል፣

በአንዲቱ ባዝራ መሰልሁሽ።

10ጕንጮችሽ በጕትቻ፣

ዐንገትሽም በዕንቍ ሐብል አጊጠዋል።

11እኛም ባለ ብር ፈርጥ፣

የወርቅ ጕትቻ እናሠራልሻለን።

ሙሽራዪቱ

12ንጉሡ ማእዱ ላይ ሳለ፣

ሽቱዬ መዐዛውን ናኘው።

13ውዴ ለእኔ በጡቶቼ መካከል እንዳረፈ፣

በመቋጠሪያ እንዳለ ከርቤ ነው።

14ውዴ ለእኔ ከዓይንጋዲ የወይን ተክል ቦታ

እንደ መጣ የሄና አበባ ዕቅፍ ነው።

ሙሽራው

15ውዴ ሆይ፤ እንዴት ውብ ነሽ!

እንዴትስ ያለሽ ቈንጆ ነሽ!

ዐይኖችሽም እንደ ርግብ ዐይኖች ናቸው።

ሙሽራዪቱ

16አንተ ውዴ ሆይ፤ እንዴት ውብ ነህ!

እንዴትስ ታምራለህ!

ዐልጋችንም እንደ ለምለም ሣር ነው።

ሙሽራው

17የቤታችን ተሸካሚዎች ዝግባዎች፣

የጣራችን ማዋቀሪያዎችም ጥዶች ናቸው።