Walawi 8 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Walawi 8:1-36

Kuwekwa Wakfu Kwa Aroni Na Wanawe

(Kutoka 29:1-37)

1Bwana akamwambia Mose, 28:2 Kut 28:1-4, 43; 30:10, 23-30; 39:27; 29:2-3; Law 1:5“Waletee Aroni na wanawe mavazi yao, mafuta ya upako, fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume wawili na kikapu chenye mikate iliyotengenezwa bila chachu. 38:3 Hes 8:9Kisha kusanya mkutano wote kwenye ingilio la Hema la Kukutania.” 4Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza, na mkutano ukakusanyika kwenye ingilio la Hema la Kukutania.

5Mose akaliambia kusanyiko, “Hili ndilo Bwana ameagiza lifanyike.” 68:6 Kut 29:4; 30:19; Mdo 22:16; Za 26:6; 1Kor 6:11; Isa 52:11; Eze 36:25; Efe 5:26; Ebr 9:9-14Kisha Mose akamleta Aroni na wanawe mbele, akawaosha kwa maji. 78:7 Kut 28:4Akamvika Aroni koti, akamfunga mshipi, akamvika joho na kumvalisha kisibau. Pia akafunga kisibau juu yake na kukifunga kiunoni mwake kwa mshipi wake uliosokotwa kwa ustadi. 88:8 Kut 25:7; 28:30; Hes 27:21; Kum 33:8; 1Sam 28:6; Neh 7:65Akaweka kifuko cha kifuani juu yake, na kuweka Urimu na Thumimu8:8 Urimu na Thumimu maana yake ni Nuru na Kweli; vifaa hivi viliwekwa kwenye kifuko cha juu cha kisibau cha kuhani mkuu ili kujua mapenzi ya Mungu kwenye mambo ya kutatanisha. kwenye hicho kifuko. 98:9 Kut 39:28; 28:2, 36; Law 21:10; Kut 29:6; Zek 3:5; 6:11Kisha akamvika Aroni kilemba kichwani pake, akaweka lile bamba la dhahabu, yaani ile taji takatifu, upande wa mbele wa kilemba, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

108:10 Kut 30:26; 26:1Ndipo Mose akachukua mafuta ya upako na kuipaka maskani na kila kitu kilichokuwamo ndani yake, kisha akaviweka wakfu. 118:11 Kut 30:29Akanyunyiza baadhi ya mafuta juu ya madhabahu mara saba, akaipaka madhabahu mafuta na vyombo vyake vyote pamoja na sinia na kinara chake, ili kuviweka wakfu. 128:12 Law 7:36; 21:10-12; Kut 30:30; 29:7; Za 133:2; Isa 61:2; 8:13; Kut 28:4; Law 21:10; Za 132:9; Isa 61:10Akamimina sehemu ya hayo mafuta ya upako kichwani mwa Aroni, akamtia mafuta ili kumweka wakfu. 13Kisha akawaleta wana wa Aroni mbele, akawavika makoti, akawafunga mishipi na kuwavika vilemba, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

148:14 Law 4:3, 15; Kut 30:10; 29:10; Za 51:19; Eze 43:19; Ebr 9:13-14Kisha akamtoa fahali kwa ajili ya sadaka ya dhambi, nao Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa chake. 158:15 Law 4:7, 18; Ebr 9:22; Eze 43:20Mose akamchinja yule fahali na akachukua sehemu ya hiyo damu, kisha kwa kidole chake akaitia kwenye pembe zote za madhabahu ili kutakasa madhabahu. Akaimwaga damu iliyobaki chini ya madhabahu. Kwa hiyo akayaweka wakfu ili kufanya upatanisho kwa ajili ya madhabahu. 168:16 Kut 29:13; Law 4:8; 8:17; 4:11-12; Kut 29:14Pia Mose akachukua mafuta yote yanayozunguka sehemu za ndani, mafuta yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, akayateketeza juu ya madhabahu. 17Lakini fahali, ikiwa pamoja na ngozi yake na nyama yake na sehemu zake za ndani na matumbo, akaiteketeza nje ya kambi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

188:18 Kut 29:15; 8:22; Law 4:15; Kut 29:19, 31; Law 7:37Kisha Mose akamleta kondoo dume kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa chake. 19Ndipo Mose akamchinja yule kondoo dume na kunyunyiza damu yake pande zote za madhabahu. 20Mose akamkata yule kondoo dume vipande vipande na kukiteketeza kichwa, vile vipande na yale mafuta. 21Kisha akamsafisha sehemu za ndani na miguu kwa maji, na kumteketeza yule kondoo dume mzima juu ya madhabahu kuwa sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

22Kisha akaleta kondoo dume mwingine, ndiye kondoo dume kwa ajili ya kuwaweka wakfu, naye Aroni na wanawe wakaweka mikono yao juu ya kichwa chake. 238:23 Law 14:14, 25; 8:23; Rum 12:1; 1Kor 6:20Mose akamchinja yule kondoo dume, akaichukua sehemu ya damu yake na kuipaka juu ya ncha ya sikio la kuume la Aroni, na juu ya kidole gumba cha mkono wake wa kuume na juu ya kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume. 248:24 Ebr 9:18-22Pia Mose akawaleta hao wana wa Aroni mbele, akaipaka sehemu ya hiyo damu kwenye ncha za masikio yao ya kuume, juu ya vidole gumba vya mikono yao ya kuume, na juu ya vidole vikubwa vya miguu yao ya kuume. Kisha akanyunyiza damu pande zote za madhabahu. 258:25 Law 3:3-5; Kut 29:22Akachukua mafuta ya mnyama, mafuta ya mkia, mafuta yote yanayozunguka sehemu za ndani, mafuta yanayofunika ini, figo zote mbili pamoja na mafuta yake, na paja la kulia. 268:26 Law 2:4Kisha kutoka kwenye kikapu cha mikate iliyotengenezwa bila chachu, kilichokuwa mbele za Bwana, akachukua andazi moja, na jingine lililotengenezwa kwa mafuta, na mkate mwembamba; akaviweka hivi vyote juu ya mafungu ya mafuta ya mnyama, na juu ya lile paja la kulia. 278:27 Hes 5:25Akaviweka hivi vyote mikononi mwa Aroni na wanawe, na kuviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa. 288:28 Kut 29:25; Mwa 8:21; Efe 5:2Kisha Mose akavichukua kutoka mikononi mwao na kuviteketeza juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kuwa sadaka ya kuwekwa wakfu, harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. 298:29 Law 7:31-34Kisha akachukua kidari, kilicho fungu la Mose la kondoo dume kwa ajili ya kuwekwa wakfu, na kukiinua mbele za Bwana kama sadaka ya kuinuliwa, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

308:30 Kut 28:1-2; Law 7:36; Kut 30:30; Hes 3:3; 1Pet 1:2Kisha Mose akachukua sehemu ya mafuta ya upako, na sehemu ya damu kutoka kwenye madhabahu, na kuvinyunyiza juu ya Aroni na mavazi yake, na juu ya wanawe na mavazi yao. Kwa hiyo akamweka Aroni na mavazi yake wakfu, pamoja na wanawe na mavazi yao.

318:31 Law 6:16; Kut 29:31; Eze 46:20Kisha Mose akamwambia Aroni na wanawe, “Pika hiyo nyama kwenye ingilio la Hema la Kukutania, na uile hapo pamoja na mkate kutoka kwenye kikapu cha sadaka ya kuweka wakfu, kama nilivyoagiza, nikisema, ‘Aroni na wanawe wataila.’ 32Kisha teketeza nyama na mikate iliyobaki. 338:33 Law 14:8; 15:13, 28; Hes 19:11; Eze 43:25Msitoke kwenye ingilio la Hema la Kukutania kwa muda wa siku saba, mpaka siku zenu za kuwekwa wakfu ziwe zimetimia, kwa kuwa muda wenu wa kuwekwa wakfu utakuwa siku saba. 348:34 Ebr 7:16; Law 18:30; 22:9; Hes 3:7; 9:19; Kum 11:1; 1Fal 2:3; Eze 48:11; 3:7; 1Tim 5:21Lile lililofanyika leo liliagizwa na Bwana ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu. 35Lazima mkae kwenye ingilio la Hema la Kukutania usiku na mchana kwa siku saba, na kufanya lile Bwana analolitaka, ili kwamba msife; kwa kuwa hilo ndilo nililoamriwa.” 36Kwa hiyo Aroni na wanawe wakafanya kila kitu Bwana alichoamuru kupitia kwa Mose.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

利未記 8:1-36

膏立亞倫父子們做祭司

1耶和華對摩西說: 2「你把亞倫父子們帶來,也要帶聖衣、膏油、一頭作贖罪祭的公牛、兩隻公綿羊和一籃無酵餅, 3然後把全體會眾招聚到會幕門前。」 4摩西按照耶和華的指示行事,會眾都聚集在會幕門前。

5摩西告訴會眾:「這是耶和華吩咐我做的事。」 6他把亞倫父子們帶來,用水洗他們。 7摩西亞倫穿上內袍,束上腰帶,穿上外袍,套上以弗得,用精巧的帶子把以弗得繫在亞倫身上, 8然後給他戴上胸牌,把烏陵和土明放在胸牌內, 9再把禮冠戴在他頭上,在禮冠前繫上金牌,即聖冠,都遵照耶和華的吩咐。

10摩西拿膏油抹聖幕和聖幕裡的一切物件,使它們聖潔; 11再用膏油在祭壇上灑七次,又抹祭壇和祭壇上的器具、洗濯盆和盆座,使它們聖潔。 12然後,摩西把膏油倒在亞倫頭上膏立他,使他聖潔。 13摩西又把亞倫的兒子們帶來,給他們穿上內袍,束上腰帶,裹上頭巾,都遵照耶和華的吩咐。

14摩西牽來那頭作贖罪祭的公牛,亞倫父子們把手放在牛頭上。 15摩西宰了牛,用手指蘸一些牛血抹在祭壇的四角上,以潔淨祭壇;把剩下的血倒在祭壇腳旁,使祭壇聖潔。 16他取出遮蓋內臟的脂肪、肝葉、兩個腎臟和腎臟上的脂肪,放在壇上焚燒, 17又照耶和華的吩咐,把公牛的皮、肉和糞便帶到營外燒掉。

18然後,摩西獻上作燔祭的公綿羊,亞倫父子們把手放在羊頭上。 19摩西宰了那隻羊,將羊血灑在祭壇周圍; 20把羊切成塊,焚燒羊頭、肉塊和脂肪; 21用水洗淨羊的內臟和腿,放在壇上焚燒,作蒙耶和華悅納的馨香火祭,都遵照耶和華的吩咐。

22摩西獻上另一隻為授聖職而獻的公綿羊。亞倫父子們把手放在羊頭上。 23摩西宰了羊,將一些羊血抹在亞倫的右耳垂、右手大拇指和右腳大腳趾上。 24他又把亞倫的兒子們帶來,將一些血抹在他們的右耳垂、右手大拇指和右腳大腳趾上,然後把剩下的血都灑在祭壇四周。 25他取下羊的右腿和脂肪,即肥尾巴、遮蓋內臟的脂肪、肝葉、兩個腎臟和腎臟上的脂肪, 26又從放在耶和華面前盛無酵餅的籃子中取一個無酵餅、一個油餅和一個薄餅,放在羊的右腿和脂肪上。 27他把這些放在亞倫父子們的手上,作為搖祭在耶和華面前搖一搖。 28隨後,他從他們手上拿過這些祭物,放在祭壇的燔祭上焚燒,作為授聖職時獻的祭。這是蒙耶和華悅納的馨香火祭。 29摩西又把祭牲的胸肉作為搖祭在耶和華面前搖一搖,這是他授聖職時所應得之份,都遵照耶和華的吩咐。

30摩西拿了一些膏油和壇上的血,灑在亞倫和他的衣服上,也灑在他兒子們和他們的衣服上,使亞倫父子們和他們的衣服聖潔。

31摩西亞倫父子們說:「你們要照我的指示在會幕門口煮祭肉吃,也要吃籃子裡為授聖職而獻的餅。 32吃剩的肉和餅,你們要燒掉。 33你們的聖職禮為期七天,這七天之內,你們不可走出會幕門口。 34今天所做的這一切都是耶和華吩咐的,是為你們贖罪。 35七天之內,你們必須日夜待在會幕門口,要遵守耶和華的吩咐,免得你們死亡。這是耶和華對我的吩咐。」 36於是,亞倫父子們遵行了耶和華藉摩西吩咐的一切。