Waebrania 8 – NEN & HHH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waebrania 8:1-13

Kuhani Mkuu Wa Agano Jipya

18:1 Ebr 2:17; Mk 16:19; Ebr 4:14; Efe 1:20; Kol 3:1Basi jambo tunalotaka kulisema ni hili: Tunaye Kuhani Mkuu ambaye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Aliye Mkuu mbinguni, 28:2 Ebr 9:11, 24; 9:8, 12, 24yeye ahudumuye katika patakatifu, hema la kweli lililowekwa na Bwana, wala si na mwanadamu.

38:3 Ebr 2:17; 5:1; 9:9, 14; Efe 5:2Kila kuhani mkuu huwekwa ili atoe sadaka na dhabihu. Vivyo hivyo, ilikuwa jambo muhimu kwa huyu Kuhani naye awe na kitu cha kutoa. 48:4 Ebr 5:1; 9:9Kama angekuwa duniani, hangekuwa kuhani, kwa sababu tayari wapo watu watoao sadaka kama ilivyoelekezwa na sheria. 58:5 Ebr 9:23; 10:1; 11:7; 12:25; Kol 2:17; Kut 25:40Wanahudumu katika patakatifu palipo mfano na kivuli cha mambo ya mbinguni. Hii ndiyo sababu Mose alionywa alipokaribia kujenga hema, akiambiwa: “Hakikisha kuwa unavitengeneza vitu vyote kwa mfano ulioonyeshwa kule mlimani.” 68:6 Ebr 8:8, 13; Lk 22:20; Gal 3:20; 2Kor 3:6, 8, 9Lakini huduma aliyopewa Yesu ni bora zaidi kuliko yao, kama vile agano ambalo yeye ni mpatanishi wake lilivyo bora zaidi kuliko lile la zamani, nalo limewekwa misingi wa ahadi zilizo bora zaidi.

78:7 Ebr 7:11, 18; 10:1Kwa maana kama hapakuwa na kasoro katika lile agano la kwanza, pasingekuwa na haja ya kutafuta nafasi kwa ajili ya jingine. 88:8 Yer 31:31, 32, 33, 34; Ebr 10:16, 17Lakini Mungu aliona kosa kwa watu, naye akasema:

“Siku zinakuja, asema Bwana,

nitakapofanya agano jipya

na nyumba ya Israeli

na nyumba ya Yuda.

98:9 Kut 19:5-6; 20:1-17Agano langu halitakuwa kama lile

nililofanya na baba zao

nilipowashika mkono

kuwaongoza watoke nchi ya Misri,

kwa sababu hawakuendelea kuwa waaminifu katika agano langu,

nami nikawaacha,

asema Bwana.

108:10 Rum 11:27; 2Kor 3:3; Ebr 10:16; Eze 11:20; Zek 8:8Hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli

baada ya siku zile, asema Bwana.

Nitaziweka sheria zangu katika nia zao

na kuziandika mioyoni mwao.

Nitakuwa Mungu wao,

nao watakuwa watu wangu.

118:11 Isa 54:13; Yn 6:45Mtu hatamfundisha tena jirani yake,

wala mtu kumfundisha ndugu yake akisema, ‘Mjue Bwana,’

kwa sababu wote watanijua mimi,

tangu aliye mdogo kabisa kwao, hadi aliye mkuu sana.

128:12 Ebr 10:17; Yer 31:31-34Kwa sababu nitasamehe uovu wao,

wala sitazikumbuka dhambi zao tena!”

138:13 Ebr 8:6, 8; Lk 22:20; 2Kor 5:17; Rum 10:4Kwa kuliita agano hili “jipya,” Mungu amefanya lile agano la kwanza kuwa kuukuu; nacho kitu kinachoanza kuchakaa na kuwa kikuukuu kiko karibu kutoweka.

Habrit Hakhadasha/Haderekh

האיגרת אל-העברים 8:1-13

1לסיכום דברינו: יש לנו כהן גדול אידיאלי שיושב עתה לימין האלוהים בשמים, 2ומשרת במקדש האמיתי שהוקם על־ידי אלוהים ולא על־ידי אדם.

3מכיוון שכל כהן צריך להקריב מנחות וזבחים, גם המשיח צריך להקריב קורבן כלשהו.

4אילו המשיח היה חי עדיין עלי־אדמות, לא היו מתירים לו לשרת ככהן, משום שהכוהנים כאן עלי־אדמות מקריבים את הקורבנות על־פי חוקי התורה. 5כוהנים אלה משרתים רק את הדגם וההעתק של מה שקיים בשמים, כי לפני שהחל משה לבנות את משכן אלוהים על־פני האדמה, ציווה עליו אלוהים לבנות את המשכן בדיוק לפי הדגם וההעתק שהראה לו על הר סיני. 6אך לכהן הגדול שלנו יש כהונה חשובה הרבה יותר מזו של כוהני הברית־הישנה, שכן הוא מתווך בברית נעלה יותר שמבוססת על הבטחות נפלאות יותר.

7אילו הייתה הברית הראשונה מושלמת, לא היה צורך בברית חדשה. 8אולם העובדה היא שאלוהים עצמו הביע אי־שביעות רצונו מהברית הראשונה באמירתו:8‏.8 ח 8 ירמיהו לא 31‏-34

”הנה ימים באים, נאם ה׳,

וכרתי את בית ישראל

ואת בית־יהודה ברית חדשה.

9לא כברית אשר כרתי את אבותם

ביום החזיקי בידם להוצאם מארץ מצרים,

אשר המה הפרו את בריתי

ואנכי בעלתי (בחלתי) בם נאם ה׳.

10כי זאת הברית אשר אכרת את בית־ישראל

אחרי הימים ההם, נאם ה׳:

נתתי את תורתי בקרבם ועל לבם אכתבנה,

והייתי להם לאלוהים והמה יהיו לי לעם;

11ולא ילמדו עוד איש את רעהו

ואיש את אחיו לאמור:

דעו את ה׳, כי כולם ידעו אותי

למקטנם ועד גדולם נאם ה׳.

12כי אסלח לעוונם ולחטאתם לא אזכר עוד.“

13בהגדרתו ”ברית חדשה“ הוא קבע את התיישנות הברית הראשונה, ואם הברית הראשונה ישנה, הרי שהיא חולפת.