Waebrania 7 – NEN & HHH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waebrania 7:1-28

Kuhani Melkizedeki

17:1 Za 76:2; Mk 5:7; Ebr 7:6; Mwa 14:18-20Kwa kuwa huyu Melkizedeki alikuwa mfalme wa Salemu na kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana. Alipokutana na Abrahamu akirudi kutoka kuwashinda hao wafalme, Melkizedeki alimbariki, 2naye Abrahamu alimpa sehemu ya kumi7:2 Sehemu ya kumi mahali pengine huitwa fungu la kumi au zaka; sehemu ya kumi ya pato hutolewa kwa Mungu. ya kila kitu. Kwanza, jina hilo Melkizedeki maana yake ni “mfalme wa haki.” Na pia “mfalme wa Salemu” maana yake ni “mfalme wa amani.” 37:3 Ebr 7:6; Mt 4:3; Za 110:4Hana Baba wala mama, hana ukoo, hana mwanzo wala mwisho wa siku zake. Kama Mwana wa Mungu, yeye adumu akiwa kuhani milele.

47:4 Mwa 14:20; Mdo 2:29Tazama jinsi alivyokuwa mkuu: Hata Abrahamu, baba yetu mkuu, alimpa sehemu ya kumi ya nyara zake. 57:5 Hes 18:21, 26Basi sheria inawaagiza wana wa Lawi ambao hufanyika makuhani kupokea sehemu ya kumi kutoka kwa watu ambao ni ndugu zao, ingawa ndugu zao ni wazao wa Abrahamu. 67:6 Mwa 14:19, 20; Rum 4:13Huyu Melkizedeki, ingawa hakufuatia ukoo wake kutoka kwa Lawi, lakini alipokea sehemu ya kumi kutoka kwa Abrahamu na kumbariki yeye aliyekuwa na zile ahadi. 7Wala hakuna shaka kwamba mdogo hubarikiwa na aliye mkuu kumliko yeye. 87:8 Ebr 5:6; 6:20Kwa upande mmoja, sehemu ya kumi hupokelewa na wale ambao hupatikana na kufa; lakini kwa upande mwingine hupokelewa na yeye ambaye hushuhudiwa kuwa yu hai. 9Mtu anaweza hata kusema kwamba Lawi, ambaye hupokea sehemu ya kumi, alitoa hiyo sehemu ya kumi kupitia kwa Abrahamu, 10kwa sababu Melkizedeki alipokutana na Abrahamu, Lawi alikuwa bado katika viuno vya baba yake wa zamani.7:10 Yaani, alikuwa hajazaliwa.

Yesu Mfano Wa Melkizedeki

117:11 Ebr 7:18-19; 8:7; 10:1; 7:17; 5:6; Gal 2:21Kama ukamilifu ungeweza kupatikana kwa njia ya ukuhani wa Walawi (kwa kuwa katika msingi huo, sheria ilitolewa kwa watu), kwa nini basi imekuwepo haja ya kuja kuhani mwingine: kuhani kwa mfano wa Melkizedeki, wala si kwa mfano wa Aroni? 12Kwa kuwa yanapotokea mabadiliko ya ukuhani, pia lazima yawepo mabadiliko ya sheria. 137:13 Ebr 7:11, 14Yeye ambaye mambo haya yanasemwa alikuwa wa kabila lingine, na hakuna mtu wa kabila hilo aliyewahi kuhudumu katika madhabahu. 147:14 Isa 11:1; Mt 1:3; 2:6; Lk 3:33; Ufu 5:5Kwa maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika uzao wa Yuda, tena kuhusu kabila hilo Mose hakusema lolote kwa habari za makuhani. 15Tena hayo tuliyosema yako wazi zaidi kama akitokea kuhani mwingine kama Melkizedeki, 16yeye ambaye amefanyika kuhani si kwa misingi ya sheria kama ilivyokuwa kwa baba zake, bali kwa misingi ya uwezo wa uzima usioharibika. 177:17 Za 110:4; Ebr 7:21; 5:6, 10; 6:20Kwa maana imeshuhudiwa kwamba:

“Wewe ni kuhani milele,

kwa mfano wa Melkizedeki.”

187:18 Rum 8:3; Gal 4:9Kwa upande mmoja, ile amri ya mwanzo isiyofaa na dhaifu imebatilishwa 197:19 Ebr 7:11; 9:9; 10:1; Rum 3:20; 7:7, 8; Gal 3:21; Yak 4:8(kwa maana sheria haikufanya kitu chochote kuwa kikamilifu). Kwa upande mwingine, tumeletewa tumaini lililo bora zaidi ambalo linatuleta karibu na Mungu.

20Nalo tumaini hilo halikutolewa pasipo kiapo! Wengine walikuwa makuhani pasipo kiapo chochote, 217:21 Za 110:4; Hes 23:19; 1Sam 15:29; Mal 3:6; Rum 1:29; Ebr 5:6lakini Yesu alifanywa kuhani kwa kiapo wakati Mungu alimwambia:

Bwana ameapa

naye hatabadilisha mawazo yake:

‘Wewe ni kuhani milele.’ ”

227:22 Ebr 8:6; 9:15; 12:24; Lk 22:20Kwa ajili ya kiapo hiki, Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi.

23Basi pamekuwepo na makuhani wengi wa aina hiyo, kwa kuwa kifo kiliwazuia kuendelea na huduma yao ya ukuhani. 247:24 Ebr 7:28Lakini kwa sababu Yesu anaishi milele, anao ukuhani wa kudumu. 257:25 Rum 11:14; 8:34; Ebr 7:19; 1Tim 2:5; 1Yn 2:1Kwa hiyo anaweza kuwaokoa kabisa wale wanaomjia Mungu kupitia kwake, kwa sababu yeye adumu daima kuomba kwa ajili yao.

267:26 Ebr 4:15; 8:1; Efe 1:20; 4:10; 2Kor 5:21Kwa kuwa ilitupasa tuwe na Kuhani Mkuu wa namna hii, yaani, aliye mtakatifu, asiye na lawama, asiye na dosari, aliyetengwa na wenye dhambi na kuinuliwa juu ya mbingu. 277:27 Ebr 5:1, 3; Rum 6:10; Ebr 9:12, 26, 28; 10:10; 1Pet 3:18; Efe 5:2Yeye hahitaji kutoa dhabihu siku kwa siku kwa ajili ya dhambi, kwanza kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe, kisha kwa ajili ya dhambi za watu kama wale makuhani wakuu wengine. Yeye alitoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zao mara moja tu, alipojitoa mwenyewe. 287:28 Ebr 5:2; 1:2; 2:10Kwa kuwa sheria huwaweka makuhani wakuu watu ambao ni dhaifu; lakini lile neno la kiapo, lililokuja baada ya sheria, lilimweka Mwana, ambaye amefanywa kuwa mkamilifu milele.

Habrit Hakhadasha/Haderekh

האיגרת אל-העברים 7:1-28

1אותו מלכי־צדק היה מלך העיר שלם וכהן לאל עליון. כשחזר אברהם מהקרב שבו ניצח מלכים רבים, יצא מלכי־צדק לקבל את פניו וברך אותו, 2ואילו אברהם העניק לו מעשר מכל השלל שלקח. מלכי־צדק פירושו: מלך הצדקה, אך הוא גם מלך השלום, שכן שלם פירושו שלום. 3אין לנו כל מסמך שמעיד על ייחוסו של מלכי־צדק; לא אב ולא אם, וגם לא ידוע לנו דבר על לידתו ועל מותו. חייו דומים לחיי בן־האלוהים וכהונתו עומדת לנצח.

4הבה נבחן את גדולתו של מלכי־צדק:

א) אפילו אברהם אבינו העניק לו מעשר משללו. 5אילו היה מלכי־צדק כהן משבט לוי, היה אברהם חייב לתת לו מעשר, כפי שבמרוצת הזמן ציוותה התורה על בני־ישראל לפרנס את הכוהנים שהקדישו את חייהם לעבודת אלוהים.

6מלכי־צדק לא השתייך למשפחת בני־לוי, ובכל זאת נתן לו אברהם מעשר.

ב) מלכי־צדק ברך את אברהם – שלו ניתנה הבטחת ה׳ – 7וכפי שאנו יודעים, גדול מי שמברך ממקבל הברכה.

ג) 8בכהונת הלויים היו מקבלי המעשר אנשים של בשר ודם, אשר מתו בבוא העת, ואילו על מלכי־צדק אנו קוראים כאילו הוא חי לעולם.

ד) 9אפשר אף לומר שלוי עצמו – אבי שבט הכוהנים, ומי שבדרך כלל מקבל מעשר מאחרים – נתן מעשר למלכי־צדק באמצעות המעשר של אברהם. 10כיצד יתכן הדבר? אמנם לוי טרם נולד, אולם בהיותו זרע אברהם הוא היה בחלציו כשיצא מלכי־צדק לקראת אברהם.

ה) 11אילו כהונת הלווים, שמשמשת יסוד לתורה, יכלה להושיע אותנו, מדוע שלח אלוהים את המשיח ככהן במעמד מלכי־צדק? מדוע לא במעמד אהרון, שהייתה דרגתם של כל שאר הכוהנים? 12התשובה היא: כיוון שאם יש שינוי בכהונה, צריך לשנות גם את התורה.

13‏-14כולנו יודעים שישוע המשיח לא השתייך לשבט לוי, אלא לשבט יהודה אשר אנשיו מעולם לא עסקו בתפקידי כהונה, שכן משה מעולם לא מינה אותם לכך. 15אם כן, אנו יכולים לראות בבירור ששיטתו של אלוהים השתנתה: המשיח, שהוא הכהן הגדול בדרגת מלכי־צדק, 16לא נתמנה לתפקידו על־פי הישן שמחייב השתייכות לשבט לוי, כי אם על־פי הכוח של חיים נצחיים, 17ועדות לכך אנו מוצאים בתהלים: ”אתה כוהן לעולם, על דברתי מלכי־צדק“.

18השיטה הישנה, לפיה עבר תפקיד הכהונה בירושה מאב לבן, נתבטלה, משום שהוכיחה את עצמה כחלשה ובלתי־יעילה. 19התורה לא תיקנה את טבע האדם ולא הושיעה איש. מאידך, אלוהים העניק לנו תקווה טובה יותר: ישוע המשיח שמאפשר לנו להתקרב אל אלוהים. 20אלוהים נשבע שהמשיח יהיה כהן לנצח, אף כי מעולם לא נשבע לכוהנים אחרים. 21רק למשיח אמר אלוהים: ”נשבע ה׳ ולא יינחם: ’אתה כהן לעולם, על דברתי מלכי־צדק‘. “ 22בזכות שבועה זאת, המשיח הוא ערובה חיה לברית טובה יותר.

23הכוהנים הקודמים היו רבים במספר, מפני שמותם מנע מהם להמשיך בתפקידם לנצח. 24ואילו המשיח מחזיק בכהונתו לנצח, מפני שלחייו אין סוף. 25מסיבה זאת יכול המשיח להושיע את כל מי שבא אל אלוהים באמצעותו, ומאחר שהוא חי לנצח, תמיד יסנגר עלינו לפני אלוהים.

26אם כן, המשיח הוא כהן גדול המתאים בדיוק לצרכינו: קדוש, חסר־דופי, מושלם, טהור ונבדל מחוטאים. כן, זהו משיחנו שקיבל מקום כבוד בשמים. 27הוא אינו צריך להקריב מדי יום קורבנות עבור חטאיו וחטאי העם – כמנהג הכוהנים האחרים – שכן המשיח הקריב קורבן אחד לתמיד: המשיח הקריב את עצמו. 28התורה מינתה אנשים חלשים כמונו לשרת ככוהניה הגדולים, ואילו שבועת ה׳, שניתנה לאחר מתן התורה, מינתה את בן־אלוהים המושלם לכוהן נצחי.