Waebrania 5 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waebrania 5:1-14

15:1 Ebr 2:17; 8:3; 9:9-27Kwa maana kila kuhani mkuu anayechaguliwa miongoni mwa wanadamu anawekwa kuwawakilisha kwa mambo yanayomhusu Mungu, ili apate kutoa matoleo na dhabihu kwa ajili ya dhambi. 25:2 Ebr 2:18; 4:15; 7:28Kwa kuwa yeye mwenyewe ni dhaifu, aweza kuwachukulia kwa upole wale wasiojua na kupotoka. 35:3 Law 4:3; 9:7; 16:6; 15:16, 17; Ebr 7:27; 9:7Hii ndiyo sababu inampasa kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi zake mwenyewe na vivyo hivyo kwa ajili ya dhambi za watu. 45:4 Kut 28:1; Hes 14:40; 18:7; 2Nya 26:18; 1Nya 23:13; Yn 3:27Hakuna anayejitwalia heshima hii mwenyewe; ni lazima aitwe na Mungu, kama vile Aroni alivyoitwa. 55:5 Yn 8:54; Ebr 2:17; 1:5; 1:1; Za 2:7; Mdo 13:33Pia Kristo hakujitwalia utukufu yeye mwenyewe wa kuwa Kuhani Mkuu, bali Mungu alimwambia,

“Wewe ni Mwanangu;

leo mimi nimekuzaa.”

65:6 Ebr 5:10; 6:20; 7:2-22; 7:17, 21; Mwa 14:18; Za 110:4Pia mahali pengine asema,

“Wewe ni kuhani milele,

kwa mfano wa Melkizedeki.”

75:7 Lk 22:41-44; 23:46; Mt 27:46; Za 22:24; Mk 14:36Katika siku za maisha ya Yesu hapa duniani, alimtolea maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, yeye awezaye kumwokoa na mauti, naye Mungu akamsikia kwa sababu ya kutii kwake kwa unyenyekevu. 85:8 Ebr 1:2; 3:6; Flp 2:8Ingawa alikuwa Mwana, alijifunza utiifu kutokana na mateso aliyoyapata, 95:9 Ebr 2:10; 11:40; Isa 45:17; Yn 17:1, 5na akiisha kukamilishwa, akawa chanzo cha wokovu wa milele kwa wote wanaomtii. 105:10 Ebr 5:6; 6:20; 2:17Naye amewekwa na Mungu kuwa Kuhani Mkuu kwa mfano wa Melkizedeki.

Wito Wa Kukua Kiroho

115:11 Yn 16:12; 2Pet 3:16; Mt 13:15Tunayo mengi ya kusema kuhusu habari ya ukuhani huu, lakini ni vigumu kuyaeleza, kwa sababu ninyi ni wazito wa kuelewa. 125:12 Ebr 6:1; 1Kor 3:2; 1Pet 2:2Kwa hakika, ingawa mpaka wakati huu ingewapasa kuwa walimu, bado mnahitaji mtu wa kuwafundisha tena hatua za awali za kweli ya Neno la Mungu. Mnahitaji maziwa, wala si chakula kigumu! 135:13 1Kor 13:11; 14:20; Efe 4:14; 1Pet 2:2Kwa maana yeyote aishiye kwa kunywa maziwa bado yeye ni mtoto mchanga, hana ujuzi katika mafundisho kuhusu neno la haki. 145:14 1Kor 2:6; Isa 7:15; 1Kor 2:14, 15Lakini chakula kigumu ni kwa ajili ya watu wazima, ambao kwa kujizoeza wamejifunza kupambanua kati ya mema na mabaya.

King James Version

Hebrews 5:1-14

1For every high priest taken from among men is ordained for men in things pertaining to God, that he may offer both gifts and sacrifices for sins: 2Who can have compassion on the ignorant, and on them that are out of the way; for that he himself also is compassed with infirmity. 3And by reason hereof he ought, as for the people, so also for himself, to offer for sins. 4And no man taketh this honour unto himself, but he that is called of God, as was Aaron. 5So also Christ glorified not himself to be made an high priest; but he that said unto him, Thou art my Son, to day have I begotten thee. 6As he saith also in another place, Thou art a priest for ever after the order of Melchisedec. 7Who in the days of his flesh, when he had offered up prayers and supplications with strong crying and tears unto him that was able to save him from death, and was heard in that he feared; 8Though he were a Son, yet learned he obedience by the things which he suffered; 9And being made perfect, he became the author of eternal salvation unto all them that obey him; 10Called of God an high priest after the order of Melchisedec.

11Of whom we have many things to say, and hard to be uttered, seeing ye are dull of hearing. 12For when for the time ye ought to be teachers, ye have need that one teach you again which be the first principles of the oracles of God; and are become such as have need of milk, and not of strong meat. 13For every one that useth milk is unskilful in the word of righteousness: for he is a babe. 14But strong meat belongeth to them that are of full age, even those who by reason of use have their senses exercised to discern both good and evil.