Waebrania 6 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Waebrania 6:1-20

Hatari Ya Kuanguka

16:1 Flp 3:12, 13, 14; Ebr 5:12; 9:14Kwa hiyo, tukiachana na mafundisho yale ya awali kuhusu Kristo na tukisonga mbele ili tufikie utimilifu, sio kuweka tena msingi wa mafundisho ya kuzitubia kazi zisizo na uhai na imani katika Mungu, 26:2 Yn 3:25; Mdo 6:6; 2:24; 17:18, 22mafundisho kuhusu aina za ubatizo, kuwekea watu mikono, ufufuo wa wafu, na hukumu ya milele. 36:3 Mdo 18:21; 1Kor 4:19Mungu akitujalia tutafanya hivyo.

46:4 Ebr 10:22; Efe 2:8; Gal 3:2; Mt 12:31, 32; 2Pet 2:20, 21; 1Yn 5:16; Yn 4:10; 6:32Kwa kuwa ni vigumu kwa wale ambao wakati fulani walishapata nuru, ambao walishaonja kipawa cha mbinguni, ambao wamekwisha kushiriki katika Roho Mtakatifu, 56:5 Ebr 2:5; 4:12; Za 34:8ambao wameonja uzuri wa Neno la Mungu na nguvu za wakati ujao, 66:6 2Pet 2:21; 1Yn 5:16; Mt 4:3; Ebr 10:29kisha wakianguka, kuwarejesha tena katika toba. Kwa kuwa wanamsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili na kumdhalilisha hadharani, nayo ikawa hasara kwao.

76:7 Za 65:10; Mwa 1:11, 12Ardhi ile ipokeayo mvua inyeshayo juu yake mara kwa mara hutoa mazao yanayowanufaisha wale ambao kwa ajili yao yalimwa, nayo nchi hiyo hupokea baraka kutoka kwa Mungu. 86:8 Mwa 3:17, 18; Isa 5:6; 27:4Lakini ardhi ikizaa miiba na mibaruti, haina thamani na iko hatarini ya kulaaniwa. Mwisho wake ni kuchomwa moto.

96:9 1Kor 10:14Ingawa tunasema hivi, ndugu zangu wapendwa, kwa upande wenu tuna hakika ya mambo mema zaidi, mambo yale yahusuyo wokovu. 106:10 Mt 10:40, 42; 1The 1:3Mungu si mdhalimu: yeye hataisahau kazi yenu na upendo ule mlioonyesha kwa ajili yake katika kuwahudumia watakatifu na hata sasa mnaendelea kuwahudumia. 116:11 Ebr 3:6, 14; Kol 2:2; Flp 1:6Nasi twataka kila mmoja wenu aonyeshe bidii iyo hiyo ili mpate kujua uhakika kamili wa lile tumaini mpaka mwisho, 126:12 Ebr 13:7; 10:36; 2The 1:4; Yak 1:3; Ufu 13:10; 14:12ili msije mkawa wavivu, bali mpate kuwaiga wale ambao kwa imani na saburi hurithi zile ahadi.

Uhakika Wa Ahadi Ya Mungu

136:13 Mwa 22:16, 17; Lk 1:73; Za 105:9Mungu alipompa Abrahamu ahadi yake, kwa kuwa hakuwepo mwingine aliyekuwa mkuu kuliko yeye ambaye angeweza kuapa kwa jina lake, aliapa kwa nafsi yake, 146:14 Mwa 22:17akisema, “Hakika nitakubariki na kukupa wazao wengi.” 156:15 Mwa 21:5Abrahamu naye, baada ya kungoja kwa saburi, alipokea kile kilichoahidiwa.

166:16 Kut 22:10Wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuwaliko, nacho kiapo hicho huthibitisha kile kilichosemwa na hivyo humaliza mabishano yote. 176:17 Ebr 6:18; Za 110:4; Rum 4:16; Ebr 11:9; Rum 11:29Mungu alipotaka kuonyesha kwa udhahiri zaidi ile asili ya kutokubadilika kwa ahadi yake kwa warithi wa ahadi, aliithitibisha kwa kiapo. 186:18 Hes 23:19; Tit 1:2; Ebr 3:6Mungu alifanya hivyo ili kwa vitu viwili visivyobadilika, yaani ahadi yake na kiapo chake, ambavyo kwavyo Mungu hawezi kusema uongo, sisi ambao tumemkimbilia ili tulishike lile tumaini lililowekwa mbele yetu tuwe na faraja thabiti. 196:19 Law 16:2; Ebr 9:2, 3, 7Tunalo tumaini hili kama nanga ya roho iliyo imara na thabiti. Tumaini hili huingia katika sehemu takatifu iliyopo nyuma ya pazia, 206:20 Ebr 4:14; 2:17; 5:6mahali ambapo Yesu mtangulizi wetu aliingia kwa niaba yetu. Yeye amekuwa Kuhani Mkuu milele, kwa mfano wa Melkizedeki.

King James Version

Hebrews 6:1-20

1Therefore leaving the principles of the doctrine of Christ, let us go on unto perfection; not laying again the foundation of repentance from dead works, and of faith toward God, 2Of the doctrine of baptisms, and of laying on of hands, and of resurrection of the dead, and of eternal judgment. 3And this will we do, if God permit. 4For it is impossible for those who were once enlightened, and have tasted of the heavenly gift, and were made partakers of the Holy Ghost, 5And have tasted the good word of God, and the powers of the world to come, 6If they shall fall away, to renew them again unto repentance; seeing they crucify to themselves the Son of God afresh, and put him to an open shame. 7For the earth which drinketh in the rain that cometh oft upon it, and bringeth forth herbs meet for them by whom it is dressed, receiveth blessing from God: 8But that which beareth thorns and briers is rejected, and is nigh unto cursing; whose end is to be burned. 9But, beloved, we are persuaded better things of you, and things that accompany salvation, though we thus speak. 10For God is not unrighteous to forget your work and labour of love, which ye have shewed toward his name, in that ye have ministered to the saints, and do minister. 11And we desire that every one of you do shew the same diligence to the full assurance of hope unto the end: 12That ye be not slothful, but followers of them who through faith and patience inherit the promises. 13For when God made promise to Abraham, because he could swear by no greater, he sware by himself, 14Saying, Surely blessing I will bless thee, and multiplying I will multiply thee. 15And so, after he had patiently endured, he obtained the promise. 16For men verily swear by the greater: and an oath for confirmation is to them an end of all strife. 17Wherein God, willing more abundantly to shew unto the heirs of promise the immutability of his counsel, confirmed it by an oath: 18That by two immutable things, in which it was impossible for God to lie, we might have a strong consolation, who have fled for refuge to lay hold upon the hope set before us: 19Which hope we have as an anchor of the soul, both sure and stedfast, and which entereth into that within the veil; 20Whither the forerunner is for us entered, even Jesus, made an high priest for ever after the order of Melchisedec.