Ufunuo 18 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 18:1-24

Kuanguka Kwa Babeli

118:1 Ufu 17:1; 10:1; Eze 43:2Baada ya haya nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, akiwa na mamlaka makuu na dunia ikamulikiwa na mngʼao wake. 218:2 Ufu 18:4; Yer 51:37Naye akalia kwa nguvu kwa sauti kubwa, akisema:

“Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu!

Umekuwa makao ya mashetani

na makazi ya kila pepo mchafu,

makazi ya kila ndege na kila mnyama achukizaye.

318:3 Ufu 14:8; 17:2; Eze 27:9-25Kwa maana mataifa yote yamekunywa

mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.

Nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi nao,

nao wafanyabiashara wa dunia

wametajirika kutokana na wingi wa utajiri wake.”

418:4 Isa 48:20; 2Kor 6:17Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema:

“Tokeni katikati yake, enyi watu wangu,

ili msije mkashiriki dhambi zake,

ili msije mkapatwa na pigo lake lolote;

518:5 2Nya 28:9; Ezr 9:6; Ufu 16:19kwa kuwa dhambi zake zimelundikana hadi mbinguni,

naye Mungu ameukumbuka uhalifu wake.

618:6 Za 137:8; Yer 50:15-29; Ufu 14:10; 17:10Mtendee kama yeye alivyotenda;

umlipe mara mbili kwa ajili ya yale aliyotenda.

Katika kikombe chake mchanganyie

mara mbili ya kile alichochanganya.

718:7 Eze 28:2-8; Za 10:6; Sef 2:15Mpatie mateso na huzuni nyingi sawa na

utukufu na anasa alizojipatia.

Kwa kuwa moyoni mwake hujivuna, akisema,

‘Mimi ninatawala kama malkia;

mimi si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.’

818:8 Isa 9:14; 47:9Kwa hiyo mapigo yatampata kwa siku moja:

mauti, maombolezo na njaa.

Naye atateketezwa kwa moto,

kwa maana Bwana Mungu amhukumuye ana nguvu.

918:9 Ufu 14:8, 11; 19:13; Yer 51:8; Eze 26:17-18“Wafalme wa dunia waliozini naye na kushiriki anasa zake watakapoona moshi wa kuungua kwake, watamlilia na kumwombolezea. 1018:10 Ufu 18:15, 17; 18:16-19; 17:12Kwa hofu kubwa ya mateso yake, watasimama mbali na kulia na wakisema:

“ ‘Ole! Ole, ee mji mkubwa,

ee Babeli mji wenye nguvu!

Hukumu yako imekuja katika saa moja!’

1118:11 Eze 27:27; 27:31; 18:15, 19“Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumwomboleza kwa sababu hakuna anunuaye bidhaa zao tena: 1218:12 Eze 27:12-22Bidhaa za dhahabu, za fedha, za vito vya thamani na vya lulu, kitani safi, nguo za rangi ya zambarau, hariri, nguo nyekundu, aina zote za miti ya udi, na vifaa vyote vya pembe za ndovu, vifaa vyote vya miti yenye thamani kuliko yote, shaba, chuma na marmar, 1318:13 Eze 27:13; 1Tim 1:10bidhaa za mdalasini, vikolezi, za uvumba, manemane, na uvumba wenye harufu nzuri, za divai, na mafuta ya zeituni, za unga mzuri na ngano; ngʼombe na kondoo; farasi na magari; na miili na roho za wanadamu.

14“Watasema, ‘Yale matunda ambayo roho yako iliyatamani yamekoma. Utajiri wako wote na fahari yako vimetoweka, wala haviwezi kupatikana tena kamwe!’ 1518:15 Ufu 18:3, 10, 17; Eze 27:31Wale wafanyabiashara waliotajirika kwa bidhaa hizo kutoka kwake watasimama mbali naye kwa hofu kubwa ya mateso yanayompata. Watalia na kuomboleza wakipiga kelele wakisema:

1618:16 Ufu 17:4; 18:10, 19“ ‘Ole! Ole, ee mji mkubwa,

uliyekuwa umevikwa mavazi ya kitani safi,

ya rangi ya zambarau na nyekundu,

ukimetameta kwa dhahabu,

vito vya thamani na lulu!

1718:17 Ufu 17:16; Eze 27:28-30Katika muda wa saa moja utajiri wote mkubwa

kama huu umeangamia!’

“Kila nahodha, na wote wasafirio kwa meli, na wote wapatao kipato chao kutokana na bahari, watasimama mbali. 1818:18 Eze 27:32; Ufu 13:4Watakapouona moshi wa kuungua kwake watalia wakisema, ‘Je, kulipata kuwako mji mkubwa kama huu?’ 1918:19 Eze 27:30; Ufu 17:16Nao watajirushia mavumbi vichwani mwao, huku wakilia na kuomboleza, wakisema:

“ ‘Ole! Ole, ee mji mkubwa,

mji ambao wote wenye meli baharini

walitajirika kupitia kwa mali zake!

Katika saa moja tu ameangamizwa!

2018:20 Yer 51:48; Ufu 12:12; 19:2Furahia kwa ajili yake, ee mbingu!

Furahini watakatifu, mitume na manabii!

Mungu amemhukumu

kwa vile alivyowatendea ninyi.’ ”

2118:21 Ufu 5:2; Yer 51:63Kisha malaika mmoja mwenye nguvu akainua jiwe kubwa kama la kusagia akalitupa baharini akisema:

“Hivyo ndivyo mji mkubwa Babeli

utakavyotupwa chini kwa nguvu

wala hautaonekana tena.

2218:22 Isa 24:8; Eze 26:13; Yer 25:10Nyimbo za wapiga vinubi na waimbaji,

wapiga filimbi na wapiga tarumbeta

kamwe hazitasikika tena ndani yako.

Ndani yako kamwe hataonekana tena fundi

mwenye ujuzi wa aina yoyote.

Wala sauti ya jiwe la kusagia

kamwe haitasikika tena.

2318:23 Yer 16:9; 25:10; Isa 23:8; Nah 3:4Mwanga wa taa

hautaangaza ndani yako tena.

Sauti ya bwana arusi na bibi arusi

kamwe haitasikika ndani yako tena.

Wafanyabiashara wako walikuwa watu maarufu wa dunia.

Mataifa yote yalipotoshwa kwa uchawi wako.

2418:24 Ufu 16:6; 17:6; Yer 51:49Ndani yake ilionekana damu ya manabii na ya watakatifu

na wote waliouawa duniani.”

La Bible du Semeur

Apocalypse 18:1-24

Deuxième parole : la chute de Babylone18.0 Voir les prophéties de l’Ancien Testament sur la chute de Babylone (Es 3 ; 21 ; 47 ; Jr 50) et de Tyr (Ez 26 ; 27).

1Après cela, je vis un autre ange descendre du ciel. Il détenait un grand pouvoir, et toute la terre fut illuminée du rayonnement de sa gloire. 2Il cria d’une voix forte :

Elle est tombée, elle est tombée,

la grande Babylone18.2 Es 21.9..

Et elle est devenue

un antre de démons,

repaire de tous les esprits impurs,

repaire de tous les oiseaux impurs18.2 Voir Es 13.21. Certains manuscrits insèrent : repaire de toutes les bêtes impures.,

et détestables.

3Car tous les peuples

ont bu le vin

de sa prostitution furieuse.

Les rois de la terre, avec elle,

se sont livrés à la débauche,

et les commerçants de la terre

ont fait fortune

grâce à son luxe

démesuré.

Troisième parole : le châtiment de Babylone

4Puis j’entendis encore une autre voix venant du ciel qui disait :

Sortez du milieu d’elle, membres de mon peuple18.4 Jr 51.45., afin de ne pas participer à ses péchés et de ne pas être frappés avec elle des fléaux qui vont l’atteindre. 5Car ses péchés se sont amoncelés jusqu’au ciel, et Dieu s’est souvenu de toutes ses actions injustes. 6Traitez-la comme elle a traité les autres, payez-la au double de ses méfaits. Et, dans la coupe où elle donnait à boire aux autres, versez-lui une mixture deux fois plus forte. 7Autant elle a vécu dans la splendeur et le luxe, autant donnez-lui de tourments et de malheurs. « Je trône ici en reine, se disait-elle, je ne suis pas veuve, non jamais je ne connaîtrai le deuil ! »

8Voilà pourquoi, en un seul jour, elle verra tous les fléaux fondre sur elle : épidémie, deuil et famine. Elle-même sera consumée par le feu, car le Dieu qui a prononcé la sentence sur elle est un puissant Seigneur.

Quatrième, cinquième et sixième paroles : lamentations sur la ruine de Babylone

9Alors les rois de la terre qui ont partagé sa vie de débauche et de luxe pleureront et se lamenteront sur elle, en voyant monter la fumée de la ville embrasée. 10Ils se tiendront à bonne distance, de peur d’être atteints par ses tourments : « Malheur ! Malheur ! gémiront-ils, la grande ville, ô Babylone, ville puissante ! Une heure a suffi pour l’exécution de ton jugement ! »

11Les marchands de la terre, eux aussi, pleurent et mènent deuil sur elle, car il n’y a plus personne pour acheter leurs marchandises : 12leurs cargaisons d’or, d’argent, de pierres précieuses et de perles, leurs étoffes de fin lin, de pourpre, de soie et d’écarlate, leurs bois aromatiques et leurs bibelots d’ivoire, tous les objets en bois précieux, en bronze, en fer et en marbre, 13la cannelle et autres épices, les parfums, la myrrhe et l’encens, le vin et l’huile, la farine et le froment, les ovins et bovins, les chevaux et les chariots, les corps et les âmes d’hommes.

14– Les objets de tes passions ont fui bien loin de toi. Raffinements et splendeurs sont perdus pour toi ! Plus jamais on ne les retrouvera !

15Les marchands qui s’étaient enrichis par leur commerce avec elle se tiendront à bonne distance, de peur d’être atteints par ses tourments. Ils pleureront et mèneront deuil. 16Ils diront :

Quel malheur ! Quel malheur ! La grande ville qui se drapait de fin lin, de pourpre et d’écarlate, parée de bijoux d’or, de pierres précieuses et de perles ! 17En une heure, tant de richesses ont été réduites à néant !

Tous les capitaines des bateaux et leur personnel, les marins et tous ceux qui vivent du trafic sur mer, se tenaient aussi à bonne distance 18et se répandaient en cris à la vue de la fumée qui montait de la ville embrasée, disant : Quelle ville pouvait rivaliser avec la grande cité ?

19Ils se jetaient de la poussière sur la tête18.19 Geste symbolique du deuil et de la consternation dans l’Ancien Testament (voir Ez 27.30)., ils criaient, pleuraient et se lamentaient :

Malheur ! Malheur ! La grande ville, dont la prospérité avait enrichi tous les armateurs des mers ! En une heure, elle a été réduite à néant !

20Réjouis-toi de sa ruine, ciel ! Et vous, membres du peuple saint, apôtres et prophètes, réjouissez-vous ! Car en la jugeant, Dieu vous a fait justice.

Septième parole : plus de trace de la grande cité mondaine

21Alors un ange puissant prit une pierre semblable à une grosse meule et la jeta dans la mer en disant :

Ainsi, avec la même violence, sera précipitée Babylone, la grande ville, et on ne la retrouvera plus18.21 Voir Jr 51.64. !

22Ah ! Babylone ! On n’entendra plus chez toi la musique des harpistes et des chanteurs ! Ni flûte, ni trompette ne résonnera plus dans tes murs ! On n’y verra plus d’artisan d’aucun métier ! Le bruit de la meule s’y taira pour toujours. 23La lumière de la lampe n’y brillera plus. Le jeune époux et sa femme ne s’y feront plus entendre. Tout cela arrivera parce que tes marchands étaient les puissants de la terre, parce qu’avec tes sortilèges, tu as trompé tous les peuples, 24et que chez toi on a vu couler le sang des prophètes et des membres du peuple saint, ainsi que de tous ceux qu’on a égorgés sur la terre.