Ufunuo 19 – NEN & BDS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 19:1-21

Shangwe Huko Mbinguni

119:1 Ufu 11:15; 7:10; 4:11Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema:

“Haleluya!

Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,

219:2 Kum 32:43; Ufu 6:10kwa maana hukumu zake

ni za kweli na za haki.

Amemhukumu yule kahaba mkuu

aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake.

Mungu amemlipiza kisasi

kwa ajili ya damu ya watumishi wake.”

319:3 Isa 34:10; Ufu 14:11Wakasema tena kwa nguvu:

“Haleluya!

Moshi wake huyo kahaba unapanda juu

milele na milele.”

419:4 Ufu 4:4-6; 5:14Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu:

“Amen, Haleluya!”

519:5 Za 134:1; Ufu 11:18Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema:

“Msifuni Mungu wetu,

ninyi watumishi wake wote,

ninyi nyote mnaomcha,

wadogo kwa wakubwa!”

619:6 Ufu 11:15Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipiga kelele wakisema:

“Haleluya!

Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala.

719:7 Mt 25:10; Efe 5:32; Ufu 21:2, 9Tufurahi, tushangilie

na kumpa utukufu!

Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia

na bibi arusi wake amejiweka tayari.

819:8 Ufu 15:4; 19:14; 15:6; Isa 61:10; Eze 44:17; Zek 3:4Akapewa kitani safi, nyeupe

inayongʼaa, ili avae.”

(Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.)

919:9 Ufu 1:19; Lk 14:15; Ufu 21:5; 22:6Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’ ” Naye akaongeza kusema, “Haya ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”

1019:10 Ufu 22:8; Mdo 10:25, 26; Ufu 22:9; 12:17Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”

Aliyepanda Farasi Mweupe

1119:11 Ufu 6:2; 3:14; Kut 15:3Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita. 1219:12 Ufu 1:14; 6:2; 2:17Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe. 1319:13 Isa 63:2, 3; Yn 1:1Amevaa joho lililochoviwa katika damu, na Jina lake ni “Neno la Mungu.” 1419:14 Ufu 19:8; 3:4; 17:14Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri. 1519:15 Ufu 1:16; 12:5; 14:20; Isa 11:4; 2The 2:8; Za 2:9Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi. 1619:16 Ufu 17:14; 19:12; 1Tim 6:15Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili:

Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.

Mnyama Na Majeshi Yake Yashindwa

1719:17 Ufu 8:13; Eze 39:17Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu, 1819:18 Eze 39:18-20ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa.”

1919:19 Ufu 16:14, 16Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake. 2019:20 Ufu 16:13; 13:12; Dan 7:11; Ufu 21:8; 14:19Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. 21Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao.

La Bible du Semeur

Apocalypse 19:1-21

Sept paroles de louange

1Après cela, j’entendis dans le ciel comme la voix puissante d’une foule immense qui disait :

Alléluia !

Loué soit Dieu !

Car à lui appartiennent

le salut et la gloire

et la puissance.

2Ses jugements sont vrais et justes

car il a condamné

la grande prostituée

qui corrompait la terre

par ses débauches,

et il lui a fait rendre compte

du sang des serviteurs de Dieu

répandu par sa main.

3Une seconde fois, ils dirent :

Alléluia !

Loué soit Dieu !

Car la fumée

de la ville embrasée

s’élève pour l’éternité !

4Alors les vingt-quatre représentants du peuple de Dieu et les quatre êtres vivants se prosternèrent devant le Dieu qui siège sur le trône, et l’adorèrent en disant :

Amen ! Loué soit Dieu !

5Et du trône partit une voix.

Louez notre Dieu, disait-elle, vous tous ses serviteurs et vous qui le craignez, petits et grands.

Les noces de l’Agneau et de sa fiancée

6Et j’entendis comme la voix d’une foule immense, semblable au bruit de grandes eaux et au grondement violent du tonnerre. Elle disait :

Alléluia !

Loué soit Dieu !

Car le Seigneur,

notre Dieu tout-puissant,

est entré dans son règne.

7Réjouissons-nous,

exultons d’allégresse

et apportons-lui notre hommage.

Voici bientôt

les noces de l’Agneau.

Sa fiancée s’est préparée.

8Et il lui a été donné

de s’habiller

d’un lin pur éclatant.

Ce lin représente le statut des membres du peuple saint déclarés justes19.8 Autre traduction : les actes justes des membres du peuple saint..

Les paroles authentiques de Dieu

9L’ange me dit alors : Ecris : Heureux les invités au festin des noces de l’Agneau.

Et il ajouta : Ce sont là les paroles authentiques de Dieu.

10Alors je me prosternai à ses pieds pour l’adorer, mais il me dit : Ne fais pas cela ! Je suis ton compagnon de service et celui de tes frères qui sont attachés à la vérité dont Jésus est le témoin. Adore Dieu ! Car le témoignage rendu par Jésus est ce qui inspire la prophétie de ce livre.

L’aboutissement de l’histoire du salut, en sept visions

Première vision : le cavalier sur un cheval blanc

11Là-dessus, je vis le ciel ouvert et voici, il y avait un cheval blanc. Son cavalier s’appelle « Fidèle et Véritable ». Il juge avec équité, il combat pour la justice. 12Ses yeux flamboient comme une flamme ardente. Sa tête est couronnée de nombreux diadèmes19.12 Emblèmes de la domination universelle (comparer v. 16).. Il porte un nom gravé qu’il est seul à connaître. 13Il est vêtu d’un manteau trempé de sang. Il s’appelle La Parole de Dieu19.13 Voir Jn 1.1.. 14Les armées célestes, vêtues de lin blanc et pur, le suivent sur des chevaux blancs. 15De sa bouche sort une épée aiguisée pour frapper les peuples et il les dirigera avec un sceptre de fer19.15 Voir Ap 2.27 ; 12.5.. Il va aussi écraser lui-même le raisin dans le pressoir à vin de l’ardente colère du Dieu tout-puissant. 16Sur son manteau et sur sa cuisse est inscrit un titre : « Roi des rois et Seigneur des seigneurs ».

Deuxième vision : le grand festin des charognards

17Puis je vis un ange, debout dans le soleil, qui cria d’une voix forte à tous les oiseaux qui volent au zénith dans le ciel : Venez, rassemblez-vous pour le grand festin de Dieu 18afin de dévorer la chair des rois, des chefs d’armées, des guerriers, la chair des chevaux et de leurs cavaliers, la chair de tous les hommes, libres et esclaves, petits et grands.

Troisième vision : la capture de la bête et du faux prophète

19Je vis la bête et les rois de la terre. Ils avaient rassemblé leurs armées pour combattre le Cavalier et son armée. 20La bête fut capturée et, avec elle, le faux prophète qui avait accompli des signes impressionnants pour le compte de la bête. Par ces signes, il avait trompé les hommes qui portaient la marque de la bête et qui avaient adoré son image. Ils furent tous deux jetés vifs dans l’étang ardent de feu et de soufre. 21Les autres hommes furent tués par l’épée qui sort de la bouche du Cavalier. Et tous les oiseaux se rassasièrent de leur chair.