Ufunuo 14 – NEN & SZ-PL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 14:1-20

Mwana-Kondoo Na Wale 144,000

114:1 Ufu 5:6; Za 2:6; Ufu 7:4; 3:12Kisha nikatazama na hapo mbele yangu alikuwepo Mwana-Kondoo, akiwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale 144,000 wenye Jina la Mwana-Kondoo na Jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao. 214:2 Ufu 1:15; 5:8-9; Eze 1:24; 43:2Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao. 314:3 Ufu 5:9; 4:6; 4:4; 14:1Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao 144,000 waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani. 414:4 2Kor 11:2; Ufu 3:4; Yak 1:18Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo. 514:5 Yn 1:47; Efe 5:27Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote.

Malaika Watatu

614:6 Ufu 8:13; 19:17; 3:10; 13:7Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. 714:7 Za 34:9; Ufu 15:4; 11:13; 8:10Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”

814:8 Isa 21:9; Ufu 17:2-4; 18:3Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, ule uliyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.”

914:9 Ufu 13:14Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye kipaji chake cha uso au kwenye mkono wake, 1014:10 Isa 51:17; Yer 25:15; 51:7yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo. 1114:11 Isa 34:10; Ufu 19:3Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” 1214:12 Ufu 13:10; 1Kor 15:18; 1The 4:16; 1Kor 15:18; 1The 4:16Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Yesu.

1314:13 1Kor 15:18; 1The 4:16; Ufu 2:7; 22:17Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Bwana tangu sasa.”

“Naam,” asema Roho, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”

Kuvuna Mavuno Ya Dunia

1414:14 Dan 7:13; Ufu 1:13; 6:2Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa “kama Mwana wa Adamu” mwenye taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake. 1514:15 Yoe 3:13; Mk 4:29; Yer 51:33Kisha malaika mwingine akaja kutoka hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.” 16Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.

1714:17 Ufu 14:15Malaika mwingine akatoka katika hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali. 1814:18 Ufu 6:9; 8:5; 16:7; 14:15Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.” 1914:19 Ufu 19:15Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu. 2014:20 Yoe 3:13; Ebr 13:12; Ufu 11:8Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi,14:20 Kimo cha hatamu za farasi ni kama mita moja na nusu. kwa umbali wa maili 200.14:20 Maili 200 ni sawa na kilomita 320.

Słowo Życia

Apokalipsa 14:1-20

Baranek i sto cztedzieści cztery tysiące

1Potem zobaczyłem Baranka, stojącego na górze Syjon, a wraz z nim—sto czterdzieści cztery tysiące tych, którzy mają wypisane na czołach Jego imię oraz imię Ojca. 2Usłyszałem też z nieba odgłos podobny do huku wielkiego wodospadu lub potężnego grzmotu. Brzmiał on jak dźwięk muzyki granej przez wielu harfiarzy.

3I usłyszałem nową pieśń, śpiewaną przed tronem Boga, przed czterema istotami i przed starszymi. Nikt oprócz stu czterdziestu czterech tysięcy, uratowanych przez Boga z ziemi, nie mógł nauczyć się tej pieśni. 4Ludzie ci, za życia na ziemi, trzymali się z dala od rozwiązłości seksualnej i są bez skazy—zawsze okazują posłuszeństwo Barankowi. Zostali uratowani z ziemi i są szczególnie cenni dla Boga i Baranka. 5Z ich ust nigdy nie wyszło żadne kłamstwo—są nienaganni!

Trzech aniołów

6Następnie zobaczyłem anioła: leciał środkiem nieba i miał ogłosić mieszkańcom ziemi wieczną dobrą nowinę—miał dotrzeć z nią do każdego narodu, plemienia, języka i ludu. 7Potężnym głosem wołał on: „Nadszedł czas Bożego sądu! Okażcie więc respekt Bogu i oddajcie cześć Temu, który stworzył niebo, lądy, morza i wszystkie źródła wód!”.

8Zaraz po nim pojawił się inny anioł, wołający: „Upadł wielki Babilon, który upajał wszystkie narody świata swoją rozwiązłością!”.

9Za nim pojawił się trzeci anioł. Potężnym głosem wołał on: „Ci, którzy pokłonią się bestii i jej posągowi oraz przyjmą jej znak na rękę lub czoło, 10doświadczą Bożego gniewu i nie będzie dla nich litości! Na oczach świętych aniołów oraz Baranka będą cierpieć w ogniu i siarce. 11Dym z palącego ich ognia będzie się unosił na wieki, będą oni bowiem cierpieć dzień i noc, bez chwili wytchnienia. Taka kara spotka ludzi, którzy oddali cześć bestii i jej posągowi oraz przyjęli znak jej imienia!”.

12Niech te słowa zachęcają świętych do wytrwałości, posłuszeństwa Bożym przykazaniom i zaufania Jezusowi.

13Potem usłyszałem głos z nieba:

—Zapisz te słowa: „Szczęśliwi ci, którzy umierają, wierząc Panu. Duch Święty potwierdza, że odpoczną oni po swojej ciężkiej pracy i otrzymają nagrodę za to, czego dokonali, żyjąc na ziemi”.

Czas żniwa

14Następnie zobaczyłem biały obłok, na którym siedział ktoś, kto wyglądał jak Syn Człowieczy. Na głowie miał złoty wieniec, a w dłoni trzymał ostry sierp.

15Wtedy ze świątyni wyszedł anioł i głośno zawołał do Tego, który siedział na obłoku: „Ziemia dojrzała już do żniwa, zacznij więc zbiory!”. 16Wówczas Ten, który siedział na obłoku, zebrał z niej plon.

17Wtedy wyszedł ze świątyni inny anioł—on również trzymał w ręku ostry sierp. 18Od strony ołtarza nadszedł wtedy następny anioł, mający władzę nad ogniem. Głośno zawołał on do anioła trzymającego sierp: „Zbierz z ziemi grona winorośli, bo już dojrzały i są gotowe na sąd!”. 19Wówczas anioł, który miał w dłoni sierp, zebrał z ziemi grona i wsypał je do wielkiej tłoczni Bożego gniewu. 20Tłocznia ta znajdowała się poza miastem. Gdy wyciśnięto grona, wypłynęła z niej rzeka krwi—miała ona trzysta kilometrów długości i była tak głęboką, że sięgała wędzideł koni.