Ufunuo 13 – NEN & SZ-PL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ufunuo 13:1-18

113:1 Dan 7:1-6; Ufu 16:13; 12:3; Dan 11:36; Ufu 17:3Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari.

Mnyama Kutoka Baharini

Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru. 213:2 Dan 7:6; 7:5; 7:4; Ufu 16:10Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa. 313:3 Ufu 17:8Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama. 413:4 Kut 15:11Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”

513:5 Dan 11:36; 2The 2:4; Ufu 11:2Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili. 613:6 Ufu 12:12Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni. 713:7 Dan 7:21; Ufu 11:7; 5:9Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa. 813:8 Ufu 3:10; 3:5; 20:12; Mt 25:34Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.

913:9 Ufu 2:7Yeye aliye na sikio na asikie.

1013:10 Yer 15:2; 43:11; Hes 6:12; Ufu 14:12Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka,

atachukuliwa mateka.

Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga,

atauawa kwa upanga.

Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.

Mnyama Kutoka Dunia

1113:11 Ufu 13:1, 2Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka. 1213:12 Ufu 19:20; 20:4Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona. 1313:13 Mt 24:24; 2Fal 1:10; Lk 9:54Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi. 1413:14 2The 2:9, 10; Ufu 12:9Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi. 1513:15 Dan 3:3-6Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa. 1613:16 Ufu 19:5; 14:9Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso, 1713:17 Ufu 14:9; 14:11; 15:2ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.

1813:18 Ufu 17:9; 15:2; 21:17Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.

Słowo Życia

Apokalipsa 13:1-18

Bestia z morza

1Wtedy zobaczyłem dziwną bestię, wyłaniającą się z morza. Miała siedem głów, dziesięć rogów, a na nich—dziesięć koron. Na głowach miała wypisane imiona obrażające Boga. 2Bestia ta przypominała lamparta, ale miała niedźwiedzie łapy i lwią paszczę. Smok przekazał jej całą swoją moc, tron i wielką władzę.

3Jedna z głów bestii została śmiertelnie raniona, ale rana ta została nagle uleczona. Wtedy cały świat podziwiał bestię 4i oddawał cześć smokowi, bo to on obdarzył ją taką potęgą. Ludzie oddawali cześć również samej bestii, mówiąc: „Kto może się z nią równać? Kto może stanąć z nią do walki?”.

5Następnie pozwolono bestii bluźnić przeciwko Bogu i działać przez czterdzieści dwa miesiące. 6Otworzyła więc paszczę i zaczęła obrażać Boga oraz Jego świątynię, i poniżać mieszkańców nieba. 7Pozwolono jej walczyć ze świętymi i pokonać ich. I dostała władzę nad wszystkimi plemionami, ludami, językami i narodami świata. 8A wszyscy ludzie, których imion nie zapisano przed powstaniem świata w księdze życia zabitego Baranka, oddadzą cześć bestii.

9Kto ma uszy do słuchania, niech słucha uważnie:

10Ten, kto ma trafić do więzienia,

zostanie uwięziony;

ten zaś, kto ma zginąć,

zostanie zamordowany.

Czas ten będzie bowiem dla świętych

próbą wytrwałości i wiary.

Bestia z ziemi

11Potem zobaczyłem inną bestię, wyłaniającą się z ziemi. Miała dwa rogi, podobne do rogów Baranka, ale przemawiała jak smok. 12Besta ta sprawowała władzę w imieniu pierwszej bestii, która została uleczona ze śmiertelnej rany, i wzywała całą ziemię i jej mieszkańców do otaczania jej czcią. 13Bestia z ziemi dokonywała niezwykłych cudów—na oczach ludzi zrzucała nawet na ziemię ogień z nieba. 14W ten sposób oszukiwała ich, nakłaniając do oddawania czci pierwszej bestii. Rozkazała im nawet wykonać wielki posąg bestii, która wcześniej została śmiertelnie raniona, ale ożyła. 15Pozwolono jej nawet ożywić ten posąg i sprawić, aby przemówił! Gdy to uczyniła, posąg ten sprawił, że wszyscy, którzy nie chcieli się przed nim pokłonić, zostali skazani na śmierć. 16Rozkazał również, aby wszystkim ludziom—wielkim i małym, biednym i bogatym, niewolnikom i wolnym—na prawej ręce lub na czole umieszczono znak. 17-18Bez tego oznaczenia nie można było niczego sprzedać ani kupić. Znakiem tym było zaś imię bestii lub jej cyfrowy symbol: sześćset sześćdziesiąt sześć. Liczba ta oznacza pewnego człowieka. Aby odkryć jej znaczenie, potrzeba jednak dużej mądrości. Kto ją posiada, niech rozszyfruje liczbę bestii.