11:1 2Fal 22:1; 2Tim 3:16; 2Pet 1:21; 1Nya 3:14Neno la Bwana lililomjia Sefania mwana wa Kushi, mwana wa Gedalia, mwana wa Amaria, mwana wa Hezekia, wakati wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni mfalme wa Yuda:
Onyo La Maangamizi Yanayokuja
21:2 Mwa 6:7Bwana asema,
“Nitafagia kila kitu
kutoka kwenye uso wa dunia.”
31:3 Yer 4:25; 50:3; Hos 4:3; Eze 14:17“Nitafagilia mbali watu na wanyama;
nitafagilia mbali ndege wa angani
na samaki wa baharini.
Wafanyao maovu watapata tu kokoto,
nami nitamkatilia mbali mwanadamu atoke katika dunia,”
asema Bwana.
Dhidi Ya Yuda
41:4 Yer 6:12; 15:6; Mik 5:13; Sef 2:11; Hos 10:5“Nitaiadhibu Yuda
na wote wakaao Yerusalemu.
Kutoka mahali hapa nitakatilia mbali
kila mabaki ya Baali,
majina ya wapagani na makuhani
waabuduo sanamu:
51:5 Yer 5:7; 8:2; 1Fal 11:33; Law 18:21wale ambao husujudu juu ya mapaa
kuabudu jeshi la vitu vya angani,
wale ambao husujudu na kuapa kwa Bwana
na ambao pia huapa kwa Malkamu,
61:6 Yer 2:13; Isa 9:13; Hos 7:7wale wanaoacha kumfuata Bwana,
wala hawamtafuti Bwana
wala kutaka shauri lake.
71:7 Isa 13:6; 41:1; Eze 7:19; Yoe 3:14; Amo 5:18-20; Yer 46:10Nyamazeni mbele za Bwana Mwenyezi,
kwa maana siku ya Bwana iko karibu.
Bwana ameandaa dhabihu,
amewaweka wakfu wale aliowaalika.
81:8 Isa 24:21; Yer 39:6Katika siku ya dhabihu ya Bwana
nitawaadhibu wakuu
na wana wa mfalme
na wale wote wanaovaa
nguo za kigeni.
91:9 1Sam 5:5; Amo 3:10Katika siku hiyo nitaadhibu wote ambao
hukwepa kukanyaga kizingiti,
ambao hujaza hekalu la miungu yao
kwa dhuluma na udanganyifu.”
101:10 Isa 22:5; Neh 3:13; 2Nya 33:14; Amo 5:16Bwana asema, “Katika siku hiyo
kilio kitapanda juu kutoka lango la Samaki,
maombolezo kutoka mtaa wa pili,
na mshindo mkubwa kutoka vilimani.
111:11 Yak 5:1; Hos 9:6; Ufu 18:11, 12Ombolezeni, ninyi mnaoishi katika eneo la sokoni;
wafanyabiashara wenu wote wameangamizwa,
wote ambao wanafanya biashara ya fedha
wataangamizwa.
121:12 Amo 6:1; Ay 21:15; Za 10:11-13; Yer 48:11; Eze 8:12; 2Fal 21:16; Ay 22:13Wakati huo nitasaka mji wa Yerusalemu kwa taa,
na kuwaadhibu wale ambao
wanakaa katika hali ya kuridhika,
ambao ni kama divai
iliyobaki kwenye machicha,
ambao hudhani, ‘Bwana hatafanya lolote,
jema au baya.’
131:13 2Fal 24:13; Yer 15:13; Mik 6:15; Kum 28:30-39; Mao 5:2; Amo 5:11Utajiri wao utatekwa nyara,
nyumba zao zitabomolewa.
Watajenga nyumba,
lakini hawataishi ndani yake;
watapanda mizabibu
lakini hawatakunywa divai yake.
Siku Kubwa Ya Bwana
141:14 Yer 30:7; Ufu 6:17; Yoe 1:15; 2:1; Mal 4:5; Eze 7:7; Dan 7:13“Siku kubwa ya Bwana iko karibu:
iko karibu na inakuja haraka.
Sikilizeni! Kilio katika siku ya Bwana
kitakuwa kichungu,
hata shujaa atapiga kelele.
151:15 1Sam 2:9; Mk 13:24-25; Yoe 2:2Siku ile ni siku ya ghadhabu,
siku ya fadhaa na dhiki,
siku ya uharibifu na ukiwa,
siku ya giza na utusitusi,
siku ya mawingu na giza nene,
161:16 Yer 4:19; 8:16; Hos 5:8; Amo 3:6; Kum 28:52; Isa 2:15siku ya tarumbeta na mlio wa vita
dhidi ya miji yenye ngome
na dhidi ya minara mirefu.
171:17 Kum 28:52; Isa 59:10; Yer 9:22; Za 79:3; 83:10Nitawaletea watu dhiki,
nao watatembea kama vipofu,
kwa sababu wametenda dhambi
dhidi ya Bwana.
Damu yao itamwagwa kama vumbi
na matumbo yao kama taka.
181:18 Ay 20:20; 40:11; Eze 7:11; 7:19; Kum 29:20; Sef 3:8; Mwa 6:7Fedha yao wala dhahabu yao
hazitaweza kuwaokoa
katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana.
Katika moto wa wivu wake
dunia yote itateketezwa,
kwa maana ataleta mwisho
wa wote wanaoishi katika dunia ghafula.”
1በይሁዳ ንጉሥ በአሞጽ ልጅ በኢዮስያስ ዘመን ወደ ሕዝቅያስ ልጅ፣ ወደ አማርያ ልጅ፣ ወደ ጎዶልያስ ልጅ፣ ወደ ኵሲ ልጅ ወደ ሶፎንያስ የመጣ የእግዚአብሔር ቃል ይህ ነው፤
ስለሚመጣው ጥፋት የተሰጠ ማስጠንቀቂያ
2“ማንኛውንም ነገር፣
ከምድር ገጽ አጠፋለሁ”
ይላል እግዚአብሔር።
3“ሰውንና እንስሳን አጠፋለሁ፤
የሰማይን ወፎች፣
የባሕርንም ዓሦች አጠፋለሁ፤
ሰውን ከምድር ገጽ በማስወግድበት ጊዜ፣
ክፉዎች የፍርስራሽ1፥3 የዕብራይስጡ ቃል ትርጕም በትክክል አይታወቅም። ክምር ይሆናሉ”
ይላል እግዚአብሔር።
በይሁዳ ላይ የተነገረ ጥፋት
4“እጄን በይሁዳ፣
በኢየሩሳሌምም በሚኖሩት ሁሉ ላይ አነሣለሁ፤
የበኣልን ትሩፍ፣
የጣዖታቱንና የአመንዝራ ካህናቱን ስም ሁሉ ከዚህ ስፍራ አጠፋለሁ፤
5የሰማይን ሰራዊት ለማምለክ፣
በሰገነት ላይ ወጥተው የሚሰግዱትን፣
ለእግዚአብሔር እየሰገዱ፣ በስሙም እየማሉ፣
በሚልኮምም1፥5 በዕብራይስጥ ማልካም ይባላል። ደግሞ የሚምሉትን፣
6እግዚአብሔርን ከመከተል ወደ ኋላ የሚመለሱትን፣
እግዚአብሔርን የማይፈልጉትን፣ እንዲረዳቸውም የማይጠይቁትን አጠፋለሁ።”
7በጌታ እግዚአብሔር ፊት ዝም በሉ፤
የእግዚአብሔር ቀን ቀርቧልና።
እግዚአብሔር መሥዋዕት አዘጋጅቷል፤
የጠራቸውንም ቀድሷል።
8በእግዚአብሔር የመሥዋዕት ቀን፣
መሳፍንቱንና የንጉሡን ልጆች፣
እንግዳ ልብስ የሚለብሱትን ሁሉ እቀጣለሁ።
9በዚያን ቀን፣
በመድረኩ ላይ የሚዘልሉትን ሁሉ፣
የአማልክታቸውን ቤት፣
በዐመፅና በማጭበርበር የሚሞሉትን እቀጣለሁ።
10እግዚአብሔር እንዲህ ይላል፤
“በዚያ ቀን ‘ከዓሣ በር’ ጩኸት
በሁለተኛው አደባባይ ዋይታ፣
ከኰረብቶችም ታላቅ ሽብር ይሰማል።
11እናንት በመክቴሽ1፥11 አንዳንዶች በሞርታር ይላሉ። ገበያ የምትኖሩ ዋይ በሉ፤
ነጋዴዎቻችሁ ሁሉ ይደመሰሳሉ፤
በብር የሚነግዱትም ሁሉ ይሞታሉ።
12በዚያ ዘመን ኢየሩሳሌምን በመብራት እፈትሻለሁ፤
ተንደላቅቀው የሚኖሩትን፣
በዝቃጩ ላይ እንደ ቀረ የወይን ጠጅ የሆኑትን፣
‘ክፉም ይሁን መልካም፣
እግዚአብሔር ምንም አያደርግም’ የሚሉትን ቸልተኞች እቀጣለሁ።
13ሀብታቸው ይዘረፋል፤
ቤታቸው ይፈራርሳል፤
ቤቶች ይሠራሉ፤
ነገር ግን አይኖሩባቸውም፤
ወይን ይተክላሉ፤
ጠጁን ግን አይጠጡም።”
ታላቁ የእግዚአብሔር ቀን
14“ታላቁ የእግዚአብሔር ቀን ቅርብ ነው፤
ቅርብ ነው ፈጥኖም ይመጣል፤
በእግዚአብሔር ቀን የሚሰማው ልቅሶ መራራ ነው፤
በዚያ ጦረኛውም ምርር ብሎ ይጮኻል፤
15ያ ቀን የመዓት ቀን፣
የመከራና የጭንቀት ቀን፣
የሁከትና የጥፋት ቀን፣
የጨለማና የጭጋግ ቀን፣
የደመናና የድቅድቅ ጨለማ ቀን ይሆናል፤
16ያ ቀን በተመሸጉ ከተሞችና፣
በረዣዥም ግንቦች ላይ፣
የመለከት ድምፅና የጦርነት ጩኸት የሚሰማበት ቀን ይሆናል።
17“እንደ ዕውር እንዲራመዱ፣
በሰዎች ላይ ጭንቀት አመጣባቸዋለሁ፤
በእግዚአብሔር ላይ ኀጢአትን ሠርተዋልና።
ደማቸው እንደ ትቢያ፣
ሥጋቸውም እንደ ጕድፍ ይጣላል።
18በእግዚአብሔር የቍጣ ቀን፣
ብራቸውም ሆነ ወርቃቸው
ሊያድናቸው አይችልም።”
መላዪቱ ምድር፣
በቅናቱ ትበላለች፤
በምድር በሚኖሩ ሁሉ ላይ፣
ድንገተኛ ፍጻሜ ያመጣባቸዋልና።