Nahumu 3 – NEN & NASV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nahumu 3:1-19

Ole Wa Ninawi

13:1 Eze 22:2; Mik 3:10; Za 12:2Ole wa mji umwagao damu,

uliojaa uongo,

umejaa nyara,

usiokosa kuwa na vitu vya kuteka nyara.

23:2 Isa 34:3; Yer 47:3Kelele za mijeledi,

vishindo vya magurudumu,

farasi waendao mbio

na mshtuo wa magari ya vita!

3Wapanda farasi wanaenda mbio,

panga zinameremeta,

na mikuki inangʼaa!

Majeruhi wengi,

malundo ya maiti,

idadi kubwa ya miili isiyohesabika,

watu wanajikwaa juu ya mizoga:

43:4 Isa 47:9; 23:17; 2The 2:9, 10; Dan 2:2; Ufu 9:20, 21; Eze 16:25-29yote haya kwa sababu ya wingi wa tamaa za kahaba,

anayeshawishi, bibi wa mambo ya uchawi,

anayewatia utumwani mataifa kwa ukahaba wake

na pia jamaa za watu kwa ulozi wake.

53:5 Nah 2:13; Isa 47:2-3; 20:4; Yer 13:22Bwana Mwenye Nguvu Zote anasema,

“Mimi ni kinyume na ninyi.

Nitafunika uso wako kwa gauni lako.

Nitaonyesha mataifa uchi wako

na falme aibu yako.

63:6 Kut 29:14; Ay 9:31; 1Sam 2:30; Yer 51:37; Isa 14:16Nitakutupia uchafu,

nitakufanyia dharau

na kukufanya kioja.

73:7 Isa 13:14; 31:9; Nah 1:1; Ay 3:14; Yer 51:37Wote wanaokuona watakukimbia na kusema,

‘Ninawi ipo katika kuangamia:

ni nani atakayeomboleza kwa ajili yake?’

Nitampata wapi yeyote wa kukufariji?”

83:8 Amo 6:2; Yer 46:25; Isa 19:6-9Je, wewe ni bora kuliko No-Amoni,

uliopo katika Mto Naili,

uliozungukwa na maji?

Mto ulikuwa kinga yake,

nayo maji yalikuwa ukuta wake.

93:9 Mwa 10:6; 2Nya 12:3; Eze 27:10; 30:5Kushi3:9 Kushi ni Ethiopia. na Misri walikuwa nguvu zake zisizo na mpaka;

Putu na Libia walikuwa miongoni mwa wale walioungana naye.

103:10 Isa 20:4; 2Fal 8:12; Isa 13:16; Hos 13:16; Ay 6:26-27; Eze 24:6; Yer 40:1; Yoe 3:3; Oba 1:11Hata hivyo alichukuliwa mateka

na kwenda uhamishoni.

Watoto wake wachanga walivunjwa vunjwa vipande

kwenye mwanzo wa kila barabara.

Kura zilipigwa kwa watu wake wenye heshima,

na watu wake wote wakuu walifungwa kwa minyororo.

113:11 Isa 49:26; 2:10Wewe pia utalewa;

utakwenda mafichoni

na kutafuta kimbilio kutoka kwa adui.

123:12 Wim 2:13; Ufu 6:13; Isa 28:4Ngome zako zote ni kama mitini

yenye matunda yake ya kwanza yaliyoiva;

wakati inapotikiswa,

tini huanguka kwenye kinywa chake alaye.

133:13 Isa 19:16; 45:2; Yer 50:37; Nah 2:6Tazama vikosi vyako:

wote ni wanawake!

Malango ya nchi yako

yamekuwa wazi kwa adui zako;

moto umeteketeza mapingo yake.

143:14 2Nya 32:4; Nah 2:1Teka maji kwa ajili ya kuzingirwa kwako,

imarisha ulinzi wako,

Ufanyie udongo wa mfinyanzi kazi,

yakanyage matope,

karabati tanuru la kuchomea matofali!

153:15 Isa 27:1; 2Sam 2:26; Yer 51:14; Yoe 1:4Huko moto utakuteketeza,

huko upanga utakuangusha chini

na kama vile panzi, watakumaliza.

Ongezeka kama panzi,

ongezeka kama nzige!

163:16 Kut 10:13Umeongeza idadi ya wafanyabiashara wako

mpaka wamekuwa wengi kuliko nyota za angani,

lakini kama nzige wanaacha nchi tupu

kisha huruka na kwenda zake.

173:17 Ufu 9:7; Yer 51:17Walinzi wako ni kama nzige,

maafisa wako ni kama makundi ya nzige

watuao kwenye kuta wakati wa siku ya baridi:

lakini wakati jua linapotokea wanaruka kwenda zao,

na hakuna ajuaye waendako.

183:18 Za 76:5-6; Yer 25:27; 50:18; Eze 31:3; Isa 56:10; 1Fal 22:17Ee mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wanasinzia;

wakuu wako wanalala chini mavumbini kupumzika.

Watu wako wametawanyika juu ya milima

bila kuwa na mtu yeyote wa kuwakusanya.

193:19 Yer 30:13; Mik 1:9; Ay 27:23; Mao 2:15; Sef 2:15; Isa 14:8; 37:18Hakuna kitu kinachoweza kuponya jeraha lako;

jeraha lako ni la kukuua.

Kila anayesikia habari zako,

hupiga makofi kwa kuanguka kwako,

kwa kuwa ni nani ambaye hajaguswa

na ukatili wako usio na mwisho?

New Amharic Standard Version

ናሆም 3:1-19

ለነነዌ

1ለደም ከተማ ወዮላት!

ሐሰት፣ ዘረፋም ሞልቶባታል፤

ብዝበዛዋ ተግዞ አያልቅም።

2የጅራፍ ድምፅ፣

የመንኰራኵር ኳኳቴ፣

የፈጣን ፈረስ ኰቴ፣

የሠረገሎች ድምፅ ተሰምቷል።

3ፈረሰኛው ይጋልባል፤

ሰይፍ ይንቦገቦጋል፤

ጦር ያብረቀርቃል።

የሞተው ብዙ ነው፤

ሬሳ በሬሳ ሆኗል፤

ስፍር ቍጥር የለውም፤

መተላለፊያ አልተገኘም።

4ይህ ሁሉ የሆነው ቅጥ ባጣች፣

አሳሳችና መተተኛ በሆነች ዘማዊት ምክንያት ነው፤

እርሷም በዝሙቷ አሕዛብን፣

በጥንቈላዋም ሕዝቦችን ባሪያ ያደረገች ናት።

5የሰራዊት ጌታ እግዚአብሔር እንዲህ ይላል፤

“እኔ በጠላትነት ተነሥቼብሻለሁ፤

ቀሚስሽን እስከ ፊትሽ እገልበዋለሁ፤

ዕርቃንሽን ለአሕዛብ፣

ኀፍረትሽንም ለነገሥታት አሳያለሁ።

6ቈሻሻ እደፋብሻለሁ፤

እንቅሻለሁ፤

ማላገጫም አደርግሻለሁ።

7የሚያዩሽ ሁሉ ከአንቺ እየሸሹ፣

‘ነነዌ ፈራርሳለች፤ ማን ያለቅስላታል?’ ይላሉ፤

የሚያጽናናሽንስ ከወዴት አገኛለሁ?”

8አንቺ በአባይ ወንዝ አጠገብ ካለችው፣

በውሃ ከተከበበችው፣

ከኖእ አሞን3፥8 አንዳንዶች ቴብስ ይላሉ። ትበልጫለሽን?

ወንዙ መከላከያዋ፣

ውሃውም ቅጥሯ ነው።

9ኢትዮጵያና ግብፅ ወሰን የለሽ ኀይሏ ናቸው፤

ፉጥና ሊቢያም ረዳቶቿ ነበሩ።

10ይሁን እንጂ በምርኮ ተወሰደች፤

ተሰድዳም ሄደች።

በየመንገዱ ማእዘን ላይ፣

ሕፃናቷ ተፈጠፈጡ፤

በመሳፍንቷ ላይ ዕጣ ተጣለ፤

ታላላቅ ሰዎቿ ሁሉ በሰንሰለት ታሰሩ።

11አንቺ ደግሞ ትሰክሪአለሽ፤

ትደበቂአለሽ፣

ከጠላትም መሸሸጊያ ትፈልጊአለሽ።

12ምሽጎችሽ ሁሉ ሊበሉ እንደ ደረሱ

የመጀመሪያ በለስ ፍሬ ናቸው፤

በሚወዛወዙበት ጊዜ፣

ፍሬዎቹ በበላተኛው አፍ ውስጥ ይወድቃሉ።

13እነሆ፤ ጭፍሮችሽ፣

ሁሉም ሴቶች ናቸው!

የምድርሽ በሮች፣

ለጠላቶችሽ ወለል ብለው ተከፍተዋል፤

መዝጊያዎቻቸውንም እሳት በልቷቸዋል።

14ለከበባው ውሃ ቅጅ፤

መከላከያሽን አጠናክሪ፤

የሸክላውን ዐፈር ፈልጊ፤

ጭቃውን ርገጪ፤

ጡቡንም ሥሪ።

15በዚያ እሳት ይበላሻል፤

ሰይፍ ይቈርጥሻል፤

እንደ ኵብኵባም ይግጥሻል።

እንደ ኵብኵባ እርቢ፤

እንደ አንበጣም ተባዢ።

16ከሰማይ ከዋክብት እስኪበልጡ ድረስ፣

የነጋዴዎችሽን ቍጥር አበዛሽ፤

ምድሪቱን ግን እንደ አንበጣ ግጠው አሟጠጡ፤

ከዚያም በርረው ሄዱ።

17ጠባቂዎችሽ እንደ አንበጣ፣

መኳንንትሽም በብርድ ቀን

በቅጥር ሥር እንደሚቀመጥ ኵብኵባ ናቸው፤

ፀሓይ ሲወጣ ግን ይበርራሉ፤

የት እንደሚበርሩም አይታወቅም።

18የአሦር ንጉሥ ሆይ፤ እረኞችህ3፥18 ገዦች ማለት ነው። አንቀላፉ፤

መኳንንትህ ዐርፈው ተኙ፤

ሕዝብህ ሰብሳቢ ዐጥተው፣

በተራራ ላይ ተበትነዋል።

19ቍስልህን ሊፈውስ የሚችል የለም፤

ስብራትህም ለሞት የሚያደርስ ነው።

ስለ አንተ የሰማ ሁሉ፣

በውድቀትህ ደስ ብሎት ያጨበጭባል፤

ወሰን የሌለው ጭካኔህ

ያልነካው ማን አለና?