Nahumu 1 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Nahumu 1:1-15

11:1 Isa 13:1; 19:1; Yer 23:33-34; 50:18; Mwa 10:11; Nah 2:8; 3:7Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.

Hasira Ya Mungu Dhidi Ya Ninawi

21:2 Kut 20:5; Mwa 4:24; Kum 32:41; 7:10; Za 94:1Bwana ni mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi;

Bwana hulipiza kisasi na amejaa ghadhabu.

Bwana hulipiza kisasi juu ya watesi wake,

naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.

31:3 Neh 9:17; Kut 34:7; 19:16; Za 103:8; Mik 7:18; 2Sam 22:10; Za 50:3; 104:3Bwana si mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu,

Bwana hataacha kuadhibu wenye hatia.

Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani,

na mawingu ni vumbi la miguu yake.

41:4 2Sam 22:16; Kut 14:22; Isa 33:9; Yos 3:15, 16Anakemea bahari na kuikausha,

anafanya mito yote kukauka.

Bashani na Karmeli zinanyauka

na maua ya Lebanoni hukauka.

51:5 Kut 19:18; Ay 9:6; 2Sam 22:8; Yoe 2:10; Eze 38:20; Mik 1:4Milima hutikisika mbele yake

na vilima huyeyuka.

Nchi hutetemeka mbele yake,

dunia na wote waishio ndani yake.

61:6 Za 130:3; Eze 22:14; Isa 5:24-25; 42:25; Yer 10:10; 1Fal 19:11Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu?

Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali?

Ghadhabu yake imemiminwa kama moto,

na miamba inapasuka mbele zake.

71:7 Yer 33:11; 17:17; Za 22:9; 1:6; 2Tim 2:19Bwana ni Mwema,

kimbilio wakati wa taabu.

Huwatunza wale wanaomtegemea,

81:8 Isa 8:7; Amo 8:8; Dan 9:26lakini kwa mafuriko makubwa,

ataangamiza Ninawi;

atafuatilia adui zake hadi gizani.

91:9 Hos 7:15Shauri baya lolote wapangalo dhidi ya Bwana

yeye atalikomesha;

taabu haitatokea mara ya pili.

101:10 2Sam 23:6; Isa 49:26; 5:24; Mal 4:1Watasongwa katikati ya miiba

na kulewa kwa mvinyo wao.

Watateketezwa kama mabua makavu.

11Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja,

ambaye anapanga shauri baya

dhidi ya Bwana

na kushauri uovu.

121:12 Isa 10:34; 54:6-8; Mao 3:31-32Hili ndilo asemalo Bwana:

“Ingawa wana muungano nao ni wengi sana,

watakatiliwa mbali na kuangamia.

Ingawa nimekutesa wewe, ee Yuda,

sitakutesa tena.

131:13 Isa 9:4; Ay 12:18; Za 107:14Sasa nitavunja nira zao kutoka shingo yako,

nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”

141:14 Isa 14:22; Mik 5:13; Yer 28:8; Eze 32:22-23Hii ndiyo amri Bwana aliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi:

“Hutakuwa na wazao

watakaoendeleza jina lako.

Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha

ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu.

Nitaandaa kaburi lako,

kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”

151:15 Isa 40:9; Rum 10:15; Isa 52:7; Mdo 10:36; Law 23:2-4Tazama, huko juu milimani,

miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema,

ambaye anatangaza amani!

Ee Yuda, sherehekea sikukuu zako,

nawe utimize nadhiri zako.

Waovu hawatakuvamia tena;

wataangamizwa kabisa.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Nahúm 1:1-15

1Profecía acerca de Nínive. Libro de la visión que tuvo Nahúm de Elcós.

Manifestación del Señor

2El Señor es un Dios celoso y vengador.

¡Señor de la venganza, Señor de la ira!

El Señor se venga de sus adversarios;

es implacable con sus enemigos.

3El Señor es lento para la ira,

imponente en su fuerza.

El Señor no deja a nadie sin castigo.

Camina en el huracán y en la tormenta;

las nubes son el polvo de sus pies.

4Increpa al mar y lo seca;

hace que todos los ríos se evaporen.

Los montes Basán y Carmelo pierden su lozanía;

el verdor del Líbano se marchita.

5Ante él tiemblan las montañas

y se desmoronan las colinas.

Ante él se agita la tierra,

el mundo y cuanto en él habita.

6¿Quién podrá enfrentarse a su indignación?

¿Quién resistirá el ardor de su ira?

Su furor se derrama como fuego;

ante él se resquebrajan las rocas.

Destrucción de Nínive

7Bueno es el Señor;

es refugio en el día de la angustia,

y protector de los que en él confían.

8Pero destruirá a Nínive1:8 a Nínive. Lit. el lugar de ella.

con una inundación arrasadora;

¡aun en las tinieblas perseguirá a sus enemigos!

9¿Qué tramáis contra el Señor?

¡Él desbaratará vuestros planes!

¡La calamidad no se repetirá!

10Serán consumidos como paja seca,

como espinos enmarañados,

como borrachos ahogados en vino.

11Tú, Nínive, engendraste

al que trama el mal contra el Señor,

al infame consejero.

Liberación del opresor

12Así dice el Señor:

«Aunque los asirios sean fuertes y numerosos,

serán arrancados y morirán.

Y a ti, Judá, aunque te he afligido,

no volveré a afligirte.

13Voy a quebrar el yugo que te oprime,

voy a romper tus ataduras».

14Pero acerca de ti, Nínive,

el Señor ha decretado:

«No tendrás más hijos que perpetúen tu nombre;

extirparé de la casa de tus dioses

las imágenes talladas y los ídolos fundidos.

Te voy a preparar una tumba,

porque eres una infame».

Anuncio de la victoria sobre Nínive

15¡Mirad! Ya se acerca por los montes

el que anuncia las buenas nuevas de victoria,

el que proclama la paz.

¡Celebra tus peregrinaciones, Judá!

¡Paga tus votos!

Porque no volverán a invadirte los malvados,

pues han sido destruidos por completo.