Mwanzo 40 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 40:1-23

Mnyweshaji Na Mwokaji

1Baada ya muda, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, wakamkosea bwana wao, mfalme wa Misri. 240:2 Mit 16:14; Es 2:21Farao akawakasirikia hawa maafisa wake wawili, mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu, 340:3 Mwa 37:36; 39:20akawaweka chini ya ulinzi katika nyumba ya mkuu wa kikosi cha ulinzi katika gereza lile lile alimofungwa Yosefu. 440:4 Mwa 37:36; 42:17Mkuu wa kikosi cha ulinzi akawakabidhi kwa Yosefu, naye akawahudumia.

Walipokuwa wamekaa chini ya ulinzi kwa muda, 5kila mmoja wa hao wawili waliokuwa wamewekwa gerezani, yaani mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri, waliota ndoto usiku mmoja, na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.

6Yosefu alipowajia asubuhi yake, akawaona kwamba walikuwa na huzuni. 7Ndipo Yosefu akawauliza maafisa hao wa Farao waliokuwa chini ya ulinzi pamoja naye nyumbani mwa bwana wake, akasema, “Mbona nyuso zenu zimejaa huzuni leo?”

840:8 Mwa 41:8, 15; Kum 29:29Wakamjibu, “Sisi sote tuliota ndoto, lakini hapakuwa na mtu yeyote wa kuzifasiri.”

Ndipo Yosefu akawaambia, “Je, kufasiri ndoto si kazi ya Mungu? Niambieni ndoto zenu.”

9Basi mkuu wa wanyweshaji akamweleza Yosefu ndoto yake. Akamwambia, “Katika ndoto yangu niliona mzabibu mbele yangu, 1040:10 Isa 27:6; Hos 14:7nao mzabibu ulikuwa na matawi matatu. Mara tu ulipoanza kuchipua, maua yalichanua na vishada vyake vikawa zabibu zilizoiva. 11Kikombe cha Farao kilikuwa mkononi mwangu, nikazitwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe cha Farao, na nikaweka kikombe mkononi mwake.”

1240:12 Dan 2:36Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Matawi matatu ni siku tatu. 1340:13 Yos 1:11Katika siku hizi tatu, Farao atakutoa gerezani na kukuweka tena kwenye nafasi yako, nawe utaweka kikombe cha Farao mikononi mwake, kama vile ulivyokuwa unafanya ulipokuwa mnyweshaji wake. 1440:14 1Sam 25:31; 1The 2:7Lakini wakati mambo yatakapokuwia mazuri, unikumbuke, unifanyie wema, useme mema juu yangu kwa Farao ili niondoke huku gerezani. 15Kwa maana nilichukuliwa kwa nguvu kutoka nchi ya Waebrania, na hata hapa nilipo sikufanya lolote linalostahili niwekwe gerezani.”

1640:16 Amo 8:1-2Yule mwokaji mkuu alipoona kuwa Yosefu amefasiri ikiwa na maana nzuri, akamwambia Yosefu, “Mimi pia niliota ndoto: Kichwani mwangu kulikuwepo vikapu vitatu vya mikate. 17Katika kikapu cha juu kulikuwa na aina zote za vyakula vilivyookwa kwa ajili ya Farao, lakini ndege walikuwa wakivila kutoka kwenye kikapu nilichokuwa nimebeba kichwani.”

1840:18 Mwa 40:12Yosefu akamwambia, “Hii ndiyo maana yake: Vikapu vitatu ni siku tatu. 1940:19 Kum 21:22-23; 1Sam 17:44Katika siku hizi tatu, Farao atakata kichwa chako na kukutundika juu ya mti. Nao ndege watakula nyama ya mwili wako.”

20Mnamo siku ya tatu, ilikuwa kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Farao, naye akawaandalia maafisa wake wote karamu. Akawatoa gerezani mnyweshaji mkuu na mwokaji mkuu, akawaweka mbele ya maafisa wake: 2140:21 2Fal 25:27; Yer 52:31Ndipo akamrudisha mnyweshaji mkuu kwenye nafasi yake, ili aweke kikombe mikononi mwa Farao tena, 22lakini akamwangika yule mwokaji mkuu, sawasawa na jinsi Yosefu alivyowaambia katika tafsiri yake.

2340:23 Mhu 1:11Pamoja na hayo, mnyweshaji mkuu hakumkumbuka Yosefu, bali alimsahau.

Persian Contemporary Bible

پيدايش 40:1‏-23

يوسف خواب زندانيان را تعبير می‌كند

1‏-3مدتی پس از زندانی شدن يوسف، فرعون رئيس نانوايان و رئيس ساقيان خود را به زندان انداخت، زيرا خشم او را برانگيخته بودند. آنها را به زندان فوطيفار، رئيس محافظان دربار كه يوسف در آنجا بود انداختند. 4آنها مدت درازی در زندان ماندند و فوطيفار يوسف را به خدمت آنها گماشت. 5يک شب هر دو آنها خواب ديدند. 6صبح روز بعد، يوسف ديد كه آنها ناراحت هستند. 7پس، از آنها پرسيد: «چرا امروز غمگين هستيد؟»

8گفتند: «ديشب ما هر دو خواب ديديم و كسی نيست كه آن را تعبير كند.»

يوسف گفت: «تعبير كردن خوابها كار خداست. به من بگوييد چه خوابهايی ديده‌ايد؟»

9‏-10اول رئيس ساقيان خوابی را كه ديده بود، چنين تعريف كرد: «ديشب در خواب درخت انگوری را ديدم كه سه شاخه داشت. ناگاه شاخه‌ها شكفتند و خوشه‌های زيادی انگور رسيده دادند. 11من جام شراب فرعون را در دست داشتم، پس خوشه‌های انگور را چيده، در جام فشردم و به او دادم تا بنوشد.»

12يوسف گفت: «تعبير خواب تو اين است: منظور از سه شاخه، سه روز است. 13تا سه روز ديگر فرعون تو را از زندان آزاد كرده، دوباره ساقی خود خواهد ساخت. 14پس خواهش می‌كنم وقتی دوباره مورد لطف او قرار گرفتی، مرا به ياد آور و سرگذشتم را برای فرعون شرح بده و از او خواهش كن تا مرا از اين زندان آزاد كند. 15زيرا مرا كه عبرانی هستم از وطنم دزديده، به اينجا آورده‌اند. حالا هم بدون آنكه مرتكب جرمی شده باشم، مرا در زندان انداخته‌اند.»

16وقتی رئيس نانوايان ديد كه تعبير خواب دوستش خير بود، او نيز خواب خود را برای يوسف بيان كرده، گفت: «در خواب ديدم كه سه سبد پر از نان روی سر خود دارم. 17در سبد بالايی چندين نوع نان برای فرعون گذاشته بودم، اما پرندگان آمده آنها را خوردند.»

18‏-19يوسف به او گفت: «مقصود از سه سبد، سه روز است. سه روز ديگر فرعون سرت را از تنت جدا كرده، بدنت را به دار می‌آويزد و پرندگان آمده گوشت بدنت را خواهند خورد.»

20سه روز بعد، جشن تولد فرعون بود و به همين مناسبت ضيافتی برای مقامات مملكتی ترتيب داد. او فرستاد تا رئيس ساقيان و رئيس نانوايان را از زندان به حضورش آورند. 21سپس رئيس ساقيان را به كار سابقش گمارد، 22ولی رئيس نانوايان را به دار آويخت، همانطور كه يوسف گفته بود. 23اما رئيس ساقيان يوسف را به ياد نياورد.