Mwanzo 36 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 36:1-43

Wazao Wa Esau

(1 Nyakati 1:34-42)

136:1 Mwa 2:4; 25:30Hivi ndivyo vizazi vya Esau (yaani Edomu).

236:2 Mwa 26:34; 28:8-9Esau akaoa wake kutoka miongoni mwa wanawake wa Kanaani: Ada binti wa Eloni Mhiti, Oholibama binti wa Ana, mjukuu wa kike wa Sibeoni Mhivi, 3pia akaoa Basemathi binti wa Ishmaeli, dada yake Nebayothi.

436:4 1Nya 1:35Ada akamzalia Esau Elifazi, Basemathi akamzaa Reueli, 536:5 1Nya 1:35Oholibama akamzaa Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wana wa Esau waliozaliwa kwake huko Kanaani.

636:6 Mwa 12:5; 1Nya 1:35Esau akawachukua wake zake, watoto wake wa kiume na wa kike na wote wa nyumbani mwake, mifugo yake pamoja na wanyama wake wengine wote na mali yake yote ambayo alikuwa ameipata akiwa Kanaani, akahamia katika nchi iliyo mbali na Yakobo ndugu yake. 736:7 Mwa 13:6; 27:39Mali zao zilikuwa nyingi sana kiasi kwamba haikuwa rahisi wao kuishi pamoja, nchi waliyokuwa wakiishi isingewatosha wote kwa ajili ya mifugo yao. 836:8 Kum 2:4Kwa hiyo Esau (ambaye ni Edomu) aliishi katika nchi ya kilima huko Seiri.

936:9 Mwa 2:4Hawa ndio wazao wa Esau, baba wa Waedomu, katika nchi ya kilima cha Seiri.

1036:10 Mwa 36:3Haya ndiyo majina ya wana wa Esau:

Elifazi, mwana wa Esau ambaye mkewe Ada alimzalia; na Reueli, mwana wa Esau ambaye mkewe Basemathi alimzalia.

1136:11 1Nya 1:45Wana wa Elifazi ni:

Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi.

1236:12 Kut 17:8, 16; 1Sam 15:2Elifazi mwana wa Esau alikuwa pia na suria aliyeitwa Timna, ambaye alimzalia Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Ada mke wa Esau.

1336:13 Mwa 36:3Wana wa Reueli ni:

Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio waliokuwa wajukuu wa Basemathi mkewe Esau.

1436:14 Mwa 36:2Wana wa Oholibama binti Ana, mkewe Esau, aliyekuwa mjukuu wa Sibeoni, aliomzalia Esau ni:

Yeushi, Yalamu na Kora.

1536:15 Mwa 36:19-40; Kut 15:15Hawa ndio waliokuwa wakuu miongoni mwa wazao wa Esau:

Wakuu wa wana wa Elifazi, mzaliwa wa kwanza wa Esau ni:

Temani, Omari, Sefo, Kenazi, 1636:16 Mwa 32:3Kora, Gatamu na Amaleki. Hawa ndio waliokuwa wakuu waliotoka kwa Elifazi huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Ada.

1736:17 1Nya 1:37Wakuu wa wana wa Reueli, mwana wa Esau ni:

Nahathi, Zera, Shama na Miza. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa Reueli huko Edomu, waliokuwa wajukuu wa kiume wa Basemathi mkewe Esau.

1836:18 Mwa 36:2Wakuu wa wana wa Esau ambao mkewe Oholibama alimzalia ni:

Yeushi, Yalamu na Kora. Hawa ndio wakuu waliotoka kwa mke wa Esau, Oholibama binti Ana.

1936:19 1Nya 1:35Hawa ndio waliokuwa wana wa Esau (ndiye Edomu), na hawa ndio waliokuwa wakuu wao.

2036:20 Mwa 14:6Hawa ndio walikuwa wana wa Seiri, Mhori, waliokuwa wakiishi katika nchi ile:

Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, 2136:21 Mwa 36:30Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio wana wa Seiri huko Edomu waliokuwa wakuu kwa Wahori.

22Wana wa Lotani walikuwa:

Hori na Homamu. Timna alikuwa dada yake Lotani.

23Wana wa Shobali walikuwa:

Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo na Onamu.

2436:24 Mwa 36:2Wana wa Sibeoni walikuwa:

Aiya na Ana. Huyu Ana ndiye aligundua chemchemi ya maji moto jangwani alipokuwa akichunga punda za Sibeoni baba yake.

2536:25 Mwa 36:2Watoto wa Ana walikuwa:

Dishoni na Oholibama binti wa Ana.

26Wana wa Dishoni walikuwa:

Hemdani, Eshbani, Ithrani na Kerani.

27Wana wa Eseri walikuwa:

Bilhani, Zaavani na Akani.

28Wana wa Dishani walikuwa:

Usi na Arani.

2936:29 Mwa 36:20Hawa ndio waliokuwa wakuu wa Wahori:

Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, 3036:30 Mwa 36:21Dishoni, Eseri na Dishani. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Wahori, kufuatana na makundi yao, katika nchi ya Seiri.

Watawala Wa Edomu

(1 Nyakati 1:43-54)

3136:31 Mwa 17:6Wafuatao ni wafalme waliotawala Edomu kabla ya mfalme yeyote wa Israeli kutawala:

32Bela mwana wa Beori alikuwa mfalme wa Edomu. Mji wake uliitwa Dinhaba.

3336:33 Isa 34:6Bela alipofariki, Yobabu mwana wa Zera kutoka Bosra akawa mfalme baada yake.

3436:34 Yer 49:7Yobabu alipofariki, Hushamu kutoka nchi ya Watemani akawa mfalme baada yake.

3536:35 Rut 1:1, 6; Mwa 19:37Hushamu alipofariki, Hadadi mwana wa Bedadi, aliyeshinda Midiani katika nchi ya Moabu, akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Avithi.

36Hadadi alipofariki, Samla kutoka Masreka akawa mfalme baada yake.

3736:37 Mwa 26:22Samla alipofariki, Shauli kutoka Rehobothi ngʼambo ya Mto Frati akawa mfalme baada yake.

38Shauli alipofariki, Baal-Hanani mwana wa Akbori akawa mfalme baada yake.

39Baal-Hanani mwana wa Akbori alipofariki, Hadadi akawa mfalme baada yake. Mji wake uliitwa Pau, na mkewe aliitwa Mehetabeli binti Matredi, binti Me-Zahabu.

4036:40 Mwa 36:15Hawa ndio wakuu waliotokana na Esau, kwa majina, kufuatana na koo zao na nchi zao:

Timna, Alva, Yethethi, 41Oholibama, Ela, Pinoni, 42Kenazi, Temani, Mibsari, 4336:43 Mwa 36:9Magdieli na Iramu. Hawa ndio walikuwa wakuu wa Edomu, kufuatana na makazi yao katika nchi waliyoimiliki.

Huyu ndiye alikuwa Esau, baba wa Waedomu.

Persian Contemporary Bible

پيدايش 36:1-43

نسل عيسو

(اول تواريخ 1‏:34‏-42)

1اسامی زنان و فرزندان عيسو كه او را ادوم نيز می‌گفتند از اين قرار است:

2‏-3عيسو با سه دختر كنعانی ازدواج كرد: عاده (دختر ايلون حيتّی)، اهوليبامه (دختر عنا، نوه صبعون حّوی) و بسمه (دختر اسماعيل و خواهر نبايوت.)

4عاده، اليفاز را برای عيسو زاييد و بسمه رعوئيل را. 5اهوليبامه، يعوش و يعلام و قورح را زاييد. همهٔ پسران عيسو در سرزمين كنعان متولد شدند.

6‏-8عيسو، زنان و پسران و دختران و همهٔ اهل بيت و تمامی حيوانات و دارايی خود را كه در سرزمين كنعان به دست آورده بود، برداشت و از نزد برادرش يعقوب به كوه سعير رفت، زيرا هر دو گله‌ها و رمه‌های فراوان داشتند و زمين آنقدر بزرگ نبود كه در يكجا با هم زندگی كنند.

9‏-12اسامی ادومی‌ها يعنی نوادگان عيسو، كه از زنان او عاده و بسمه در كوهستان سعير متولد شدند، از اين قرار است:

فرزندان اليفاز پسر عاده: تيمان، اومار، صفوا، جعتام، قناز و عماليق (كه مادرش تمناع كنيز اليفاز بود). 13عيسو نوه‌های ديگری هم داشت كه فرزندان رعوئيل پسر بسمه بودند؛ اسامی آنها از اين قرار است: نحت، زارح، شمه و مزه.

14اهوليبامه، زن عيسو (دختر عنا و نوهٔ صبعون) سه پسر برای عيسو زاييد به نامهای يعوش، يعلام و قورح.

15‏-16نوه‌های عيسو سران اين قبايل شدند: تيمان، اومار، صفوا، قناز، قورح، جعتام و عماليق. قبايل نامبرده فرزندان اليفاز پسر ارشد عيسو و همسرش عاده بودند.

17سران اين قبايل فرزندان رعوئيل پسر عيسو از همسرش بسمه بودند: نحت، زارح، شمه و مزه.

18‏-19سران اين قبايل پسران عيسو از همسرش اهوليبامه بودند: يعوش، يعلام و قورح.

20‏-21قبايلی كه از نسل سعير حوری، يكی از خانواده‌های ساكن سرزمين سعير، به وجود آمدند عبارتند از: لوطان، شوبال، صبعون، عنا، ديشون، ايصر و ديشان.

22‏-28حوری و هومام فرزندان لوطان بودند. لوطان خواهری داشت به نام تمناع. فرزندان شوبال: علوان، مناحت، عيبال، شفو و اونام. فرزندان صبعون: ايّه و عنا (عنا همان پسری بود كه موقع چرانيدن الاغهای پدرش چشمه‌های آب گرم را در صحرا يافت). فرزندان عنا: ديشون و اهوليبامه. فرزندان ديشون: حمدان، اشبان، يتران و كران. فرزندان ايصر: بلهان، زعوان و عقان. فرزندان ديشان: عوص و اران.

29‏-30اسامی سران قبايل حوری كه در سرزمين سعير بودند عبارتند از: لوطان، شوبال، صبعون، عنا، ديشون، ايصر و ديشان.

پادشاهان ادوم

(اول تواريخ 1‏:43‏-54)

31‏-39پيش از اين كه در اسرائيل پادشاهی روی كار آيد، در سرزمين ادوم اين پادشاهان يكی پس از ديگری به سلطنت رسيدند:

بالع، پسر بعور اهل دينهابه واقع در ادوم.

يوباب، پسر زارح از شهر بصره.

حوشام، از سرزمين تيمانی‌ها.

حداد، پسر بداد. او لشكر مديانی‌ها را در سرزمين موآب شكست داد. نام شهر او عويت بود.

سمله، از اهالی مسريقه.

شائول، اهل رحوبوت كه در كنار رودخانه‌ای واقع بود.

بعل حانان، پسر عكبور.

حداد، از اهالی فاعو كه نام زنش مهيطب‌ئيل دختر مطرد و نوهٔ ميذهب بود.

40‏-43اين قبايل از عيسو به وجود آمدند: تمناع، علوه، يتيت، اهوليبامه، ايله، فينون، قناز، تيمان، مبصار، مجدی‌ئيل و عيرام. همهٔ اينها ادومی بودند و هر يک نام خود را بر ناحيه‌ای كه در آن ساكن بودند نهادند.