Mwanzo 35 – NEN & PCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 35:1-29

Yakobo Arudi Betheli

135:1 Mwa 12:8Kisha Mungu akamwambia Yakobo, “Panda uende Betheli ukakae huko na ukamjengee Mungu madhabahu huko, Yeye aliyekutokea ulipokuwa unamkimbia Esau ndugu yako.”

235:2 Yos 24:15; Kut 19:10, 14Hivyo Yakobo akawaambia watu wa nyumbani mwake pamoja na wote waliokuwa naye, “Iondoeni miungu ya kigeni ile iliyoko katikati yenu, jitakaseni na mkabadilishe nguo zenu. 335:3 Mwa 32:7; Amu 2:15Kisha njooni, twende Betheli, mahali nitakapomjengea Mungu madhabahu, aliyenijibu katika siku ya shida yangu, ambaye amekuwa pamoja nami popote nilipokwenda.” 435:4 Mwa 24:22Kwa hiyo wakampa Yakobo miungu yote ya kigeni waliyokuwa nayo, pamoja na pete zilizokuwa masikioni mwao. Yakobo akavizika chini ya mti wa mwaloni huko Shekemu. 535:5 Kut 15:16Kisha wakaondoka, na hofu ya Mungu ikawapata miji yote iliyowazunguka. Kwa hiyo hakuna aliyewafuatia wana wa Yakobo.

635:6 Mwa 28:19; 10:19Yakobo na watu wote waliokuwa pamoja naye wakafika Luzu (ndio Betheli), katika nchi ya Kanaani. 735:7 Mwa 8:20Huko akajenga madhabahu na akapaita mahali pale El-Betheli,35:7 El-Betheli maana yake Mungu wa Betheli. kwa sababu mahali pale ndipo Mungu alipojifunua kwake alipokuwa akimkimbia ndugu yake.

835:8 Mwa 24:59; 12:8Wakati huu Debora, mlezi wa Rebeka, akafa na akazikwa chini ya mti wa mwaloni ulioko chini ya Betheli. Kwa hiyo pakaitwa Alon-Bakuthi.35:8 Alon-Bakuthi maana yake Mwaloni wa Kilio.

935:9 Mwa 28:13; 32:29Baada ya Yakobo kurudi kutoka Padan-Aramu, Mungu alimtokea tena na kumbariki. 1035:10 Mwa 17:5Mungu akamwambia, “Jina lako ni Yakobo, lakini hutaitwa tena Yakobo, jina lako utakuwa Israeli.” Kwa hiyo akamwita Israeli.

1135:11 Mwa 17:1; 17:6Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu Mwenyezi,35:11 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). ukazae na kuongezeka. Taifa na jamii ya mataifa itatoka kwako, nao wafalme watatoka viunoni mwako. 1235:12 Mwa 28:13; 12:7Nchi niliyowapa Abrahamu na Isaki nakupa wewe pia, nami nitawapa wazao wako baada yako.” 1335:13 Mwa 17:22Kisha Mungu akapanda juu kutoka kwake mahali pale alipozungumza naye.

1435:14 Mwa 28:18; Kut 29:40Yakobo akasimamisha nguzo ya jiwe mahali pale Mungu alipozungumza naye, akamimina sadaka ya kinywaji juu yake, pia akamimina mafuta juu yake. 1535:15 Mwa 12:8Yakobo akapaita mahali pale Mungu alipozungumza naye Betheli.35:15 Betheli maana yake Nyumba ya Mungu.

Vifo Vya Raheli Na Isaki

1635:16 Mwa 48:7Kisha wakaondoka Betheli. Walipokuwa umbali fulani kabla ya kufika Efrathi, Raheli akaanza kusikia uchungu na alipata shida kuu. 1735:17 Kut 1:15; Mwa 30:24Alipokuwa katika shida hii katika kujifungua, mkunga akamwambia, “Usiogope, kwa sababu umempata mwana mwingine.” 1835:18 1Sam 4:21Hapo alipopumua pumzi yake ya mwisho, kwa maana alikuwa akifa, akamwita mwanawe Benoni.35:18 Benoni maana yake Mwana wa huzuni yangu. Lakini babaye akamwita Benyamini.35:18 Benyamini maana yake Mwana wa mkono wangu wa kuume.

1935:19 Mwa 48:7Kwa hiyo Raheli akafa, akazikwa kando ya njia iendayo Efrathi (ndio Bethlehemu). 2035:20 1Sam 10:2; 6:18Juu ya kaburi lake, Yakobo akasimamisha nguzo, ambayo mpaka leo inatambulisha kaburi la Raheli.

21Israeli akaendelea tena na safari yake na kupiga hema mbele mnara wa Ederi. 22Wakati Israeli alipokuwa akiishi katika nchi ile, Reubeni mwanawe alikutana kimwili na suria wa baba yake aitwaye Bilha, naye Israeli akasikia jambo hili.

Yakobo alikuwa na wana kumi na wawili:

23Wana wa Lea walikuwa:

Reubeni mzaliwa wa kwanza wa Yakobo,

Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari na Zabuloni.

2435:24 Mwa 30:24; 35:18Wana wa Raheli walikuwa:

Yosefu na Benyamini.

2535:25 Mwa 30:24Wana waliozaliwa na Bilha mtumishi wa kike wa Raheli walikuwa:

Dani na Naftali.

2635:26 Mwa 37:2Wana waliozaliwa na Zilpa mtumishi wa kike wa Lea walikuwa:

Gadi na Asheri.

Hawa walikuwa wana wa Yakobo, waliozaliwa kwake akiwa Padan-Aramu.

2735:27 Mwa 13:18; Amu 1:10Yakobo akarudi nyumbani kwa baba yake Isaki huko Mamre, karibu na Kiriath-Arba (yaani Hebroni), ambapo walikuwa wameishi Abrahamu na Isaki. 2835:28 Mwa 25:7Isaki aliishi miaka 180. 2935:29 Mwa 15:15; 25:8-9Kisha Isaki akapumua pumzi yake ya mwisho akafa, akakusanywa pamoja na watu wake akiwa mzee wa miaka mingi. Nao wanawe Esau na Yakobo wakamzika.

Persian Contemporary Bible

پيدايش 35:1-29

يعقوب به بيت‌ئيل برمی‌گردد

1خدا به يعقوب فرمود: «حال برخيز و به بيت‌ئيل برو. در آنجا ساكن شو و قربانگاهی بساز و آن خدايی را كه وقتی از دست برادرت عيسو می‌گريختی بر تو ظاهر شد، عبادت نما.»

2آنگاه يعقوب به تمامی اهل خانهٔ خود دستور داد كه بُتهايی را كه با خود آورده بودند، دور بيندازند و غسل بگيرند و لباسهايشان را عوض كنند. 3او به ايشان گفت: «به بيت‌ئيل می‌رويم و من در آنجا برای خدايی كه به هنگام سختی، دعاهايم را اجابت فرمود و هر جا می‌رفتم با من بود، قربانگاهی خواهم ساخت.»

4پس همگی، بُتهای خود و گوشواره‌هايی را كه در گوش داشتند به يعقوب دادند و او آنها را زير درخت بلوطی در شكيم دفن كرد. 5سپس آنها بار ديگر كوچ كردند. و ترس خدا بر تمامی شهرهايی كه يعقوب از آنها عبور می‌كرد قرار گرفت تا به وی حمله نكنند. 6سرانجام به لوز كه همان بيت‌ئيل باشد، واقع در سرزمين كنعان رسيدند. 7يعقوب در آنجا قربانگاهی بنا كرد و آن را قربانگاه «خدای بيت‌ئيل» ناميد (چون هنگام فرار از دست عيسو، در بيت‌ئيل بود كه خدا بر او ظاهر شد.)

8چند روز پس از آن، دبوره دايهٔ پير ربكا مُرد و او را زير درخت بلوطی در درهٔ پايين بيت‌ئيل به خاک سپردند. از آن پس، درخت مذكور را «بلوط گريه» ناميدند.

9پس از آنكه يعقوب از بين‌النهرين وارد بيت‌ئيل شد، خدا بار ديگر بر وی ظاهر شد و او را بركت داد 10و به او فرمود: «بعد از اين ديگر نام تو يعقوب خوانده نشود، بلكه نام تو اسرائيل35‏:10 برای معنی کلمات «يعقوب» و «اسرائيل» نگاه کنيد به 25‏:26 و 32‏:28.‏ خواهد بود. 11من هستم خدای قادر مطلق. بارور و زياد شو! قومهای زياد و پادشاهان بسيار از نسل تو پديد خواهند آمد. 12سرزمينی را كه به ابراهيم و اسحاق دادم، به تو و به نسل تو نيز خواهم داد.» 13سپس خدا از نزد او به آسمان صعود كرد.

14پس از آن، يعقوب در همان جايی كه خدا بر او ظاهر شده بود، ستونی از سنگ بنا كرد و هديهٔ نوشيدنی برای خداوند بر آن ريخت و آن را با روغن زيتون تدهين كرد. 15يعقوب آن محل را بيت‌ئيل (يعنی «خانه خدا») ناميد، زيرا خدا در آنجا با وی سخن گفته بود.

مرگ راحيل و اسحاق

16سپس او و خانواده‌اش بيت‌ئيل را ترک گفتند و به سوی افرات رهسپار شدند. اما هنوز به افرات نرسيده بودند كه دردِ زايمانِ راحيل شروع شد. 17در حالی كه راحيل با سختی وضع حمل می‌نمود، قابله‌اش گفت: «نترس، چون اين بار نيز پسر زاييده‌ای.» 18ولی راحيل در حال مرگ بود. او در حين جان سپردن، پسرش را بن اونی (يعنی «پسر غم من») نام نهاد، ولی بعد پدرش او را بنيامين (يعنی «پسر دست راست من») ناميد.

19پس راحيل وفات يافت و او را در نزديكی راه افرات كه بيت‌لحم هم ناميده می‌شد، دفن كردند. 20يعقوب روی قبرش ستونی از سنگ بنا كرد كه تا به امروز باقی است.

21آنگاه اسرائيل از آنجا كوچ كرد و در آن طرف برج عيدر خيمه زد. 22در همین‌جا بود كه رئوبين با بلهه كنيز پدرش همبستر شد و اسرائيل از اين جريان آگاهی يافت.

23يعقوب دوازده پسر داشت كه اسامی آنها از اين قرار است:

پسران ليه: رئوبين (بزرگترين فرزند يعقوب)، شمعون، لاوی، يهودا، يساكار و زبولون.

24پسران راحيل: يوسف و بنيامين.

25پسران بلهه كنيز راحيل: دان و نفتالی.

26جاد و اشير هم از زلفه، كنيز ليه بودند.

همه پسران يعقوب در بين‌النهرين متولد شدند.

27سرانجام يعقوب نزد پدر خود اسحاق به قريهٔ اربع واقع در مِلک ممری آمد. (آن قريه را حبرون نيز می‌گويند و ابراهيم هم در آنجا زندگی كرده بود.) 28‏-29اسحاق در سن صد و هشتاد سالگی در كمال پيری وفات يافت و به اجداد خويش پيوست و پسرانش عيسو و يعقوب او را دفن كردند.