Mwanzo 28 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 28:1-22

128:1 Mwa 24:3Basi Isaki akamwita Yakobo, akambariki na akamwamuru, akisema, “Usioe mwanamke wa Kikanaani. 2Nenda mara moja mpaka Padan-Aramu, kwenye nyumba ya Bethueli baba wa mama yako. Uchukue mke kati ya binti za Labani ambaye ni ndugu wa mama yako. 328:3 Mwa 17:1; Hes 6:24Mungu Mwenyezi28:3 Mungu Mwenyezi hapa ni jina la Kiebrania, El-Shaddai (yaani Mungu Mwenye utoshelevu wote). na akubariki uwe na uzao uongezeke idadi yako upate kuwa jamii kubwa ya watu. 428:4 Mwa 12:2, 3; 17:8Na akupe wewe na uzao wako baraka aliyopewa Abrahamu, upate kumiliki nchi unayoishi sasa kama mgeni, nchi ambayo Mungu alimpa Abrahamu.” 528:5 Hos 12:12; Mwa 24:29Kisha Isaki akamuaga Yakobo, naye akaenda Padan-Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, ndugu wa Rebeka, aliyekuwa mama wa Yakobo na Esau.

6Sasa Esau akajua kuwa Isaki amembariki Yakobo na kumtuma kwenda Padan-Aramu ili achukue mke huko na kwamba alipombariki alimwamuru akisema, “Usioe mke katika binti za Wakanaani,” 7tena kwamba Yakobo amewatii baba yake na mama yake naye amekwenda Padan-Aramu. 828:8 Mwa 26:35Esau akatambua jinsi ambavyo baba yake Isaki anavyowachukia binti za Wakanaani. 9Ndipo Esau akaenda kwa Ishmaeli, akamwoa Mahalati, ndugu wa Nebayothi na binti wa Ishmaeli mwana wa Abrahamu, kuongezea wale wake wengine aliokuwa nao.

Ndoto Ya Yakobo Huko Betheli

10Yakobo akatoka Beer-Sheba kwenda Harani. 11Alipofika mahali fulani, akalala hapo kwa sababu jua lilikuwa limetua. Akachukua jiwe moja la mahali pale, akaliweka chini ya kichwa chake akajinyoosha akalala usingizi. 1228:12 Yn 1:51Akaota ndoto ambayo aliona ngazi imesimamishwa juu ya ardhi, ncha yake ikiwa imefika mbinguni na malaika wa Mungu wakawa wakipanda na kushuka juu yake. 13Juu yake alisimama Bwana, akasema, “Mimi ni Bwana, Mungu wa baba yako Abrahamu na Mungu wa Isaki. Nchi ambayo umelala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako. 1428:14 Mwa 26:4; 12:3; Gal 3:8Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya nchi, nawe utaenea upande wa magharibi na mashariki, kaskazini na kusini. Kupitia wewe na uzao wako mataifa yote ya duniani yatabarikiwa. 1528:15 Kum 31:6, 8; Law 26:42; Za 105:10Niko pamoja nawe nami nitakulinda kila uendako na nitakurudisha katika nchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapofanya hayo niliyokuahidi.”

1628:16 1Fal 3:15; Yer 31:26Yakobo alipoamka kutoka usingizini, akawaza, “Hakika Bwana yuko mahali hapa, wala mimi sikujua.” 1728:17 Kut 3:5; Yos 5:15Kwa hiyo akaogopa, akasema, “Mahali hapa panatisha kama nini! Bila shaka hapa ndipo nyumba ya Mungu ilipo, hili ni lango la mbinguni.”

18Asubuhi yake na mapema, Yakobo akalichukua lile jiwe aliloliweka chini ya kichwa chake, akalisimamisha kama nguzo na kumimina mafuta juu yake. 1928:19 Yos 16:2; Amu 1:23, 26Mahali pale akapaita Betheli,28:19 Betheli maana yake Nyumba ya Mungu. ingawa mji ule hapo kwanza uliitwa Luzu.

2028:20 Mwa 31:13; Amu 1:23, 26Kisha Yakobo akaweka nadhiri, akisema, “Kama Mungu akiwa pamoja nami na kunilinda katika safari niendayo, akinipa chakula nile na nguo nivae 2128:21 Kum 26:17; Za 48:14; 118:28na nirudi salama nyumbani kwa baba yangu, hapo ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu, 2228:22 Mwa 14:20; Lk 18:12nalo jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu na katika yote utakayonipa nitakutolea wewe sehemu ya kumi.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

创世记 28:1-22

1以撒雅各叫来,给他祝福,又嘱咐他说:“你不要娶迦南的女子为妻。 2马上去巴旦·亚兰,到你外祖父彼土利家,在你舅父拉班的女儿中选一个做妻子。 3愿全能的上帝赐福给你,使你的子孙众多,成为许多民族。 4愿上帝把赐给亚伯拉罕的福气赐给你和你的后代,让你承受你寄居之地为产业,就是上帝赐给亚伯拉罕的地方。” 5以撒雅各前往巴旦·亚兰,去亚兰人彼土利的儿子拉班那里。拉班雅各以扫的舅父。

6以扫看见父亲给雅各祝福,让他到巴旦·亚兰娶妻,叮嘱他不要娶迦南的女子, 7又看见雅各听从父母到巴旦·亚兰去了, 8就知道父亲以撒不喜欢迦南的女子。 9他便到亚伯拉罕的儿子以实玛利那里,娶了以实玛利的女儿、尼拜约的妹妹玛哈拉为妻。他娶玛哈拉以前已经有两个妻子了。

雅各的梦

10雅各离开别示巴,前往哈兰11到了一个地方,太阳已经下山,他便在那里过夜。他枕着一块石头睡觉, 12梦中看见有个梯子立在地上,直通到天上,梯子上有上帝的天使上上下下。 13耶和华站在梯子上28:13 在梯子上”或译“在他旁边”。雅各说:“我是耶和华,是你祖父亚伯拉罕的上帝,也是以撒的上帝。我要把你现在躺卧的地方赐给你和你的后代。 14你的后代必多如地上的尘沙,遍布四方,地上万族必因你和你的后代而蒙福。 15我与你同在,无论你去哪里,我都会保护你,领你返回这片土地。我必实现对你的应许,决不离弃你。”

16雅各一觉醒来,说:“耶和华居然在这里,我却不知道。” 17他就害怕起来,说:“这地方何等可畏!这里是上帝的家,是通天的大门。”

18雅各清早起来,把枕的那块石头立成柱子作记号,在上面浇上油。 19他称那地方为伯特利28:19 伯特利”意思是“上帝的家”。,那地方以前叫路斯20雅各许愿说:“如果上帝与我同在,在路上保护我,供给我衣食, 21带领我平安地回到父亲的家,我就一定敬奉耶和华为我的上帝。 22我立为柱子的这块石头必成为上帝的殿。凡你赐给我的,我必把十分之一献给你。”