Mwanzo 13 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mwanzo 13:1-18

Abramu Na Loti Watengana

113:1 Mwa 45:25; 12:9; 11:27Hivyo Abramu akakwea kutoka Misri kwenda Negebu, yeye na mkewe na kila kitu alichokuwa nacho, pia Loti akaenda pamoja naye. 213:2 Mwa 12:5; 26:13; 32:15; Mit 10:22; Ay 1:3; 42:12Wakati huo Abramu alikuwa tajiri sana wa mifugo, fedha na dhahabu.

313:3 Mwa 12:8-9Kutoka Negebu, akapita mahali hadi mahali, hadi akafika Betheli, mahali hapo ambapo mwanzoni alipiga hema lake kati ya Betheli na Ai 413:4 Mwa 12:7; 4:26hapo ambapo alikuwa amejenga madhabahu ya kwanza. Huko Abramu akaliitia jina la Bwana.

513:5 Mwa 11:27Basi Loti, ambaye alikuwa anafuatana na Abramu, alikuwa pia na makundi ya mbuzi, kondoo, ngʼombe na mahema. 613:6 Mwa 12:5; 33:9; 36:7Lakini nchi haikuwatosha kukaa pamoja kwa ajili ya wingi wa mali zao. 713:7 Mwa 26:20-21; 10:18; 15:20; 12:6; 34:30; Hes 20:3; Kut 3:8; Amu 1:4Ukazuka ugomvi kati ya wachunga mifugo wa Abramu na wale wa Loti. Wakati huo, Wakanaani na Waperizi ndio waliokuwa wenyeji wa nchi hiyo.

813:8 Mwa 11:27; 19:9; Mit 15:18; 20:3; Kut 2:14; Hes 16:13; Za 133:1Hivyo Abramu akamwambia Loti, “Pasiwe na ugomvi wowote kati yangu na wewe, wala kati ya wachungaji wangu na wako, kwa kuwa sisi ni ndugu. 913:9 Mwa 20:15; 34:10; 47:6; Yer 40:4Je, nchi yote haiko mbele yako? Tutengane. Kama ukielekea kushoto, nitakwenda kulia; kama ukielekea kulia, mimi nitakwenda kushoto.”

1013:10 1Fal 7:47; 2Nya 4:17; Hes 13:29; 33:48; Mwa 19:22; 2:8-10; 46:7; 14:2, 8Loti akatazama akaona lile bonde lote la Yordani kuwa lilikuwa na maji tele, kama bustani ya Bwana, kama nchi ya Misri, kuelekea Soari. (Hii ilikuwa kabla Bwana hajaharibu Sodoma na Gomora.) 11Hivyo Loti akajichagulia bonde lote la Yordani, akaelekea upande wa mashariki. Watu hao wawili wakatengana: 1213:12 Mwa 10:19; 11:27; 19:17-29; 14:12Abramu akaishi katika nchi ya Kanaani, wakati Loti aliishi miongoni mwa miji ya lile bonde na kupiga mahema yake karibu na Sodoma. 1313:13 Mwa 18:20; 19:4; 19:5; 20:6; 39:9; Isa 1:10; 3:9; Hes 32:23; 1Sam 12:23; 2Sam 12:13; Za 51:4; Eze 16:49-50; 2Pet 2:8Basi watu wa Sodoma walikuwa waovu, wakifanya sana dhambi dhidi ya Bwana.

1413:14 Mwa 28:14; 32:12; 48:16; Kum 3:27; 13:17; Isa 54:3Baada ya Loti kuondoka Bwana akamwambia Abramu, “Ukiwa hapo ulipo, inua macho yako utazame kaskazini na kusini, mashariki na magharibi. 1513:15 Mwa 12:7; Gal 3:16Nchi yote unayoiona nitakupa wewe na uzao wako hata milele. 1613:16 Mwa 12:2; 16:10; 17:20; 21:13-18; 25:16; Hes 23:10Nitaufanya uzao wako uwe mwingi kama mavumbi ya nchi, hivyo kama kuna yeyote awezaye kuhesabu mavumbi, basi uzao wako utahesabika. 1713:17 Mwa 12:7; 15:7; Hes 13:17-25Ondoka, tembea katika marefu na mapana ya nchi, kwa maana ninakupa wewe.”

1813:18 Mwa 8:20; 14:13; 18:1; 23:2, 17, 19; 25:9; 49:30; 50:13; 35:27; Hes 13:22; Yos 10:3, 36; Amu 1:10; 1Sam 30:31; 2Sam 2:1-11; 1Nya 11:1Basi Abramu akaondoa mahema yake, akaenda kuishi karibu na mialoni ya Mamre huko Hebroni, huko akamjengea Bwana madhabahu.

Het Boek

Genesis 13:1-18

Abram en Lot gaan hun eigen weg

1Zo verlieten zij Egypte en trokken weer noordwaarts naar de Negev: Abram, zijn vrouw, Lot en alles wat zij bezaten. 2Abram had veel vee, zilver en goud. 3Zij trokken net zo lang in noordelijke richting tot ze bij hun oude kamp tussen Betel en Ai kwamen. 4Het altaar dat Abram daar had gebouwd, stond er nog en opnieuw aanbad Abram daar de naam van de Here.

5Lot had net als Abram veel vee en tenten voor zichzelf en zijn dienaren. 6Daarom konden zij niet bij elkaar blijven, want het land was niet groot genoeg voor al hun vee. 7De herders van Abram en Lot kregen zelfs onderling ruzie, wat gevaarlijk was vanwege de vijandige Kanaänieten en Perizzieten die daar woonden.

8Abram besprak het probleem met Lot. ‘Het is niet goed dat wij ruzie maken en dat onze herders met elkaar overhoop liggen,’ meende hij. ‘Wij zijn tenslotte familie! 9Laten we daarom uit elkaar gaan, er is hier plaats genoeg. Als jij een stuk grond in het oosten kiest, ga ik naar het westen. Als jij een plaats in het westen kiest, ga ik naar het oosten.’ 10Lot keek goed om zich heen en zag het vruchtbare gebied langs de rivier de Jordaan, met overal genoeg water. Voordat de Here Sodom en Gomorra vernietigde, leek het gebied tot Soar aan toe wel op de hof van Eden of het land Egypte. 11Daarom koos Lot voor de Jordaanstreek in het oosten en trok er met zijn vee en zijn dienaren heen. Hij en Abram gingen uit elkaar. 12Abram bleef in Kanaän en Lot vestigde zich in de steden van de Jordaanstreek in de buurt van de stad Sodom. 13Maar de inwoners van dit gebied waren erg slecht en zondigden tegen de Here.

14-15 Nadat Lot was vertrokken, zei de Here tegen Abram: ‘Kijk zo ver u kunt naar alle kanten, want al dit land zal Ik u en uw nakomelingen geven. 16Ik zal u zoveel nakomelingen geven dat ze, net als het stof van de aarde, niet kunnen worden geteld!

17Doorkruis dit land in alle richtingen, dan zult u zien wat Ik u allemaal ga geven.’ 18Abram sloeg zijn kamp op bij de eikenbossen van Mamre, in de buurt van Hebron en bouwde daar een altaar voor de Here.