Mithali 7 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 7:1-27

Onyo Dhidi Ya Mwanamke Mzinzi

17:1 Mt 1:8Mwanangu, shika maneno yangu

na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.

27:2 Mit 4:4; Law 18:5; Kum 32:10Shika amri zangu nawe utaishi;

linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.

37:3 Kum 6:8; Mit 3:3; Isa 30:8; 2Kor 3:3Yafunge katika vidole vyako;

yaandike katika kibao cha moyo wako.

4Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,”

uite ufahamu jamaa yako;

57:5 Ay 31:9; Mit 2:16watakuepusha na mwanamke mzinzi,

kutokana na mwanamke mpotovu

na maneno yake ya kubembeleza.

6Kwenye dirisha la nyumba yangu

nilitazama nje kupitia upenyo

kwenye mwimo wa dirisha.

77:7 Mit 6:32Niliona miongoni mwa wajinga,

nikagundua miongoni mwa wanaume vijana,

kijana asiye na akili.

8Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake,

akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke

97:9 Ay 24:15wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake,

giza la usiku lilipokuwa likiingia.

107:10 1Tim 2:9Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki,

hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.

117:11 Mit 9:13; 1Tim 5:13(Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi,

miguu yake haitulii nyumbani;

127:12 Mit 8:1-36; 23:26-28mara kwenye barabara za mji,

mara kwenye viwanja vikubwa,

kwenye kila pembe huvizia.)

137:13 Mwa 39:12; Mit 1:20Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu,

na kwa uso usio na haya akamwambia:

147:14 Law 7:11-18“Nina sadaka za amani nyumbani;

leo nimetimiza nadhiri zangu.

15Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki;

nimekutafuta na nimekupata!

167:16 Isa 19:9Nimetandika kitanda changu

kwa kitani za rangi kutoka Misri.

177:17 Amo 6:4; Mwa 37:25Nimetia manukato kitanda changu

kwa manemane, udi na mdalasini.

187:18 Mwa 39:7Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi;

tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!

19Mume wangu hayupo nyumbani;

amekwenda safari ya mbali.

20Amechukua mkoba uliojazwa fedha

na hatakuwepo nyumbani karibuni.”

217:21 Mit 1:8-9; 8:32Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha;

alimshawishi kwa maneno yake laini.

227:22 Ay 18:10Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke

kama fahali aendaye machinjoni,

kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,

237:23 Ay 15:22; 16:13; Mit 6:26; Mhu 9:12mpaka mshale umchome ini lake,

kama ndege anayenaswa kwenye mtego,

bila kujua itamgharimu maisha yake.

247:24 Mit 1:8-9; 8:32Sasa basi wanangu, nisikilizeni;

sikilizeni kwa makini nisemalo.

257:25 Mit 5:7-8Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke,

wala usitangetange katika mapito yake.

267:26 Neh 13:26Aliowaangusha ni wengi;

aliowachinja ni kundi kubwa.

277:27 Amu 16:19; Ufu 22:15Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini,7:27 Kaburini hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol.

ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

箴言 7:1-27

要遠離淫婦

1孩子啊,你要遵從我的吩咐,

把我的誡命珍藏在心中。

2遵守我的誡命,你便存活。

要愛護我的訓言,

如愛護眼中的瞳人。

3要繫在你的指頭上,

刻在你的心版上。

4你要把智慧當作姊妹,

將悟性視為親人。

5她們能使你遠離淫婦,

遠離妓女的甜言蜜語。

6我曾在家裡的窗前,

透過窗櫺往外觀看,

7只見在愚昧的青年人中,

有個無知的青年,

8他穿過靠近淫婦的巷口,

朝她的家門走去,

9趁著日暮黃昏,

藉著夜色昏暗。

10看啊!一個妓女打扮、

心術不正的女子出來迎接他。

11她喧嚷放蕩,不安分守家,

12有時在街上,有時在廣場,

或在各巷口守候。

13她纏著那青年,與他親吻,

厚顏無恥地說:

14「我今天剛獻祭還了願,

家裡有平安祭肉7·14 按猶太律法規定,還願之後所得的祭肉要在第二天吃完。參考利未記7·16

15因此我出來四處尋找你,

終於找到了你!

16我已經鋪好了床,

鋪上了埃及的繡花布,

17又用沒藥、沉香、肉桂薰了床。

18來吧,讓我們通宵暢飲愛情,

讓我們盡情歡愛!

19因為我丈夫不在家,出遠門了。

20他帶著錢囊去了,月底才回來。」

21淫婦花言巧語勾引他,

用諂媚的話語誘惑他。

22那青年立刻隨她而去,

像走向屠宰場的公牛,

又像掉入陷阱的雄鹿,

23直等到利箭射穿他的肝。

他像隻自投網羅的飛鳥,

渾然不知要賠上性命!

24孩子們啊,你們要聽從我的話,

留意我口中的訓言,

25別讓你的心偏向淫婦的道,

步入她的歧途。

26因為她使許多人喪命,

被她殺害的數目眾多。

27她的家是通往陰間的路,

引人墜入死亡的殿。