Mithali 6 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mithali 6:1-35

Maonyo Dhidi Ya Upumbavu

16:1 Mwa 43:9; Ebr 7:22; Ezr 10:27; Mit 17:18Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako,

ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi

kwa ajili ya mwingine,

2kama umetegwa na ulichosema,

umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,

3basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru,

kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako:

Nenda ukajinyenyekeshe kwake;

msihi jirani yako!

46:4 Rut 3:18; Za 132:4Usiruhusu usingizi machoni pako,

usiruhusu kope zako zisinzie.

56:5 Za 91:3; 2Sam 2:18; Isa 13:14; Za 91:3Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji,

kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.

66:6 Mit 6:11Ewe mvivu, mwendee mchwa;

zitafakari njia zake ukapate hekima!

7Kwa maana yeye hana msimamizi,

wala mwangalizi, au mtawala,

86:8 Mit 30:24-25; 10:4lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi

na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.

96:9 Mit 24:30-34; 26:13-16Ewe mvivu, utalala hata lini?

Utaamka lini kutoka usingizi wako?

106:10 Mit 24:33; Mhu 4:5Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,

bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:

116:11 Mit 6:10-11; 20:13; 24:30-34hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi,

na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

12Mtu mbaya sana na mlaghai,

ambaye huzungukazunguka

na maneno ya upotovu,

136:13 Za 35:19; Mit 16:30ambaye anakonyeza kwa jicho lake,

anayetoa ishara kwa miguu yake

na kuashiria kwa vidole vyake,

146:14 Za 36:4; 140:2; Mik 2:1; Isa 32:7ambaye hupanga ubaya

kwa udanganyifu moyoni mwake:

daima huchochea fitina.

15Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula;

ataangamizwa mara, pasipo msaada.

166:16 Mit 3:32; 8:13; 15:8, 9, 26; 16:5Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana,

naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:

176:17 Za 120:2; Mit 12:22; Yer 2:34; Mik 7:2; Hos 4:1-2macho ya kiburi,

ulimi udanganyao,

mikono imwagayo damu isiyo na hatia,

186:18 Mwa 6:5; Ay 15:31; Rum 3:15moyo uwazao mipango miovu,

miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,

196:19 Kum 19:16; Za 27:12; Mit 15:18; Zek 8:17shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo,

na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.

Onyo Dhidi Ya Uasherati

206:20 Mit 3:21; 1:8Mwanangu, zishike amri za baba yako,

wala usiyaache mafundisho ya mama yako.

216:21 Kum 6:8; Mit 3:3Yafunge katika moyo wako daima,

yakaze kuizunguka shingo yako.

226:22 Mit 3:23; 2:11Wakati utembeapo, yatakuongoza;

wakati ulalapo, yatakulinda;

wakati uamkapo, yatazungumza nawe.

236:23 Za 19:8; 10:17Kwa maana amri hizi ni taa,

mafundisho haya ni mwanga

na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,

246:24 Mwa 39:8; Za 55:21yakikulinda na mwanamke aliyepotoka,

kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.

256:25 2Sam 11:2-5; Mt 5:28Moyo wako usitamani uzuri wake

wala macho yake yasikuteke,

266:26 Mit 27:22-23; 29:3; Eze 13:18kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini,

hata ukose kipande cha mkate,

naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.

27Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake

bila nguo zake kuungua?

28Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka

bila miguu yake kuungua?

296:29 Kut 20:14; Mit 2:16-19Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine;

hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.

30Watu hawamdharau mwizi kama akiiba

kukidhi njaa yake wakati ana njaa.

316:31 Kut 22:1-14Pamoja na hayo, kama akikamatwa,

lazima alipe mara saba,

ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.

326:32 Kut 20:14; Mit 7:7; 9:4, 16Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa;

yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.

336:33 Mit 5:9-14Mapigo na aibu ni fungu lake

na aibu yake haitafutika kamwe;

346:34 Hes 5:14; Mwa 34:7kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume,

naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.

356:35 Ay 31:9-11; Wim 8:7Hatakubali fidia yoyote;

atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

箴言 6:1-35

日常警言

1孩子啊,你若為鄰人作保,

為外人擊掌立約;

2你若被自己口中的話套住,

被自己的諾言纏住,

3孩子啊,你已落入鄰人的手中,

你當如此自救:

要謙卑地向他求情。

4勿讓你的眼睛睡覺,

莫叫你的眼皮打盹。

5要救自己脫離困境,

像羚羊掙脫獵人的手,

飛鳥逃脫捕鳥人的手。

6懶惰的人啊,去看看螞蟻,

觀察牠的生活,就會有智慧。

7螞蟻沒有元帥,

沒有官長,

也沒有君王,

8卻在夏季儲備糧食,

在收割時積聚食物。

9懶惰的人啊,你要躺到何時?

要睡到何時才起床?

10再睡一會兒,再打個盹兒,

抱著手躺一會兒,

11貧窮要像盜賊一樣攻擊你,

缺乏要像武士一樣撲向你。

12無賴與惡人滿口詭詐,

13擠眉弄眼,手腳示意,

14心術不正,設下詭計,惹事生非。

15因此,災難必突然臨到,

他們頃刻之間遭到毀滅,

無可挽救。

16耶和華所憎惡的事有六樣,

連祂厭惡的事共有七樣:

17高傲的眼睛,

撒謊的舌頭,

殺害無辜的手,

18圖謀詭計的心,

奔跑作惡的腳,

19撒謊的假證人和在弟兄中挑起爭端的人。

20孩子啊,要遵守你父親的誡命,

不可背棄你母親的訓言。

21你要常常將這些刻在心坎上,

繫在頸項上。

22你行走,它們必引領你;

你躺臥,它們必護衛你;

你醒來,它們必與你交談。

23因為誡命是燈,訓言是光,

管教責備是生命之道,

24能使你遠離邪惡的女人,

避開油嘴滑舌的妓女。

25你的心不要貪戀她的美色,

也不要被她的媚眼所迷惑,

26因為娼妓會使人傾家蕩產6·26 娼妓會使人傾家蕩產」或譯「娼妓的淫資不過是一個餅」。

淫婦會獵殺人寶貴的生命。

27人若將火藏在懷中,

哪能不燒著衣服呢?

28人若行走在火炭上,

哪能不燙傷雙腳呢?

29與別人妻子通姦也是這樣,

凡靠近她的必難逃罪責。

30賊因充饑而偷,

沒有人藐視他;

31但若被抓到,他要償還七倍,

就是傾家蕩產也要償還。

32和有夫之婦通姦的,

實在愚不可及,

他是自尋死路。

33他必挨打,受辱,

他的恥辱永難抹去。

34那丈夫妒火燃燒,

報仇時絕不留情。

35賠他再多財物,他也不會接受;

送他再多禮物,他都不肯甘休。