Mathayo 5 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Mathayo 5:1-48

Mahubiri Ya Yesu Kwenye Mlima

(Mathayo 5–7)

Sifa Za Aliyebarikiwa

(Luka 6:20-23)

15:1 Mk 3:13, 20; Lk 6:20-49Basi Yesu alipoona makutano, alipanda mlimani akaketi chini, nao wanafunzi wake wakamjia. 2Ndipo akaanza kuwafundisha, akisema:

35:3 Mt 5:10, 19; 25:34; Isa 57:15“Heri walio maskini wa roho,

maana Ufalme wa Mbinguni ni wao.

45:4 Isa 61:2-3; Ufu 7:17Heri wale wanaohuzunika,

maana hao watafarijiwa.

55:5 Za 37:11; Rum 4:13Heri walio wapole,

maana hao watairithi nchi.

65:6 Isa 55:1-2Heri wenye njaa na kiu ya haki,

maana hao watatoshelezwa.

75:7 Yak 2:13; Za 41:1; Mt 6:14; Mk 11:24Heri wenye huruma,

maana hao watapata rehema.

85:8 Za 24:3-4; 73:1; 17:15; Ebr 12:14Heri walio na moyo safi,

maana hao watamwona Mungu.

95:9 Mt 5:44, 45; Rum 8:14Heri walio wapatanishi,

maana hao wataitwa wana wa Mungu.

105:10 1Pet 3:14Heri wanaoteswa kwa sababu ya haki,

maana Ufalme wa Mbinguni ni wao.

115:11 Isa 51:7; 1Pet 4:14“Heri ninyi watu watakapowashutumu, na kuwatesa na kunena dhidi yenu mabaya ya aina zote kwa uongo kwa ajili yangu. 125:12 Za 9:2; 2Nya 36:16; 2Kor 6:10Furahini na kushangilia kwa maana thawabu yenu ni kubwa mbinguni, kwa kuwa hivyo ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwa kabla yenu.

Chumvi Na Nuru

(Marko 9:50; Luka 14:34-35)

135:13 Mk 9:50; Lk 14:34-35“Ninyi ni chumvi ya ulimwengu. Lakini chumvi ikipoteza ladha yake, yawezaje kurudishiwa ladha yake tena? Haifai tena kwa kitu chochote, ila kutupwa nje ikanyagwe na watu.

145:14 Yn 8:12“Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji uliojengwa kilimani hauwezi kufichika. 155:15 Mk 4:21; Lk 11:33Wala watu hawawashi taa na kuifunika kwa bakuli. Badala yake, huiweka kwenye kinara chake, nayo hutoa mwanga kwa kila mtu aliyemo ndani ya ile nyumba. 165:16 Efe 5:8-9; 1Pet 2:12Vivyo hivyo, nuru yenu iangaze mbele ya watu, ili wapate kuona matendo yenu mema wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.

Kutimiza Sheria

175:17 Rum 3:31; 10:4; Gal 1:24“Msidhani kwamba nimekuja kufuta Sheria au Manabii; sikuja kuondoa bali kutimiza. 185:18 Za 119:89; Mk 13:31Kwa maana, amin nawaambia, mpaka mbingu na dunia zitakapopita, hakuna hata herufi moja ndogo wala nukta itakayopotea kwa namna yoyote kutoka kwenye Sheria, mpaka kila kitu kiwe kimetimia. 195:19 Yak 2:10; 1Kor 15:9Kwa hiyo, yeyote atakayevunja mojawapo ya amri ndogo kuliko zote ya amri hizi, naye akawafundisha wengine kufanya hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni, lakini yeyote azitendaye na kuzifundisha hizi amri ataitwa mkuu katika Ufalme wa Mbinguni. 205:20 Rum 9:31; 10:3Kwa maana nawaambia, haki yenu isipozidi haki ya Mafarisayo na walimu wa sheria, kamwe hamtaingia katika Ufalme wa Mbinguni.

Kuhusu Hasira

(Luka 12:57-59)

215:21 Kut 21:12; 5:17; Law 24:17“Mmesikia walivyoambiwa watu wa zamani kwamba, ‘Usiue. Yeyote atakayeua atapaswa hukumu.’ 225:22 1Yn 3:22; Yn 11:47; Mdo 6:12; Lk 16:24; Yak 3:6Lakini mimi nawaambia kwamba, yeyote atakayemkasirikia ndugu yake, atapaswa hukumu. Tena, yeyote atakayemwambia ndugu yake, ‘Raka,’5:22 Raka ni neno la Kiaramu ambalo maana yake ni dharau au dhihaka ya hali ya juu. atapaswa kujibu kwa Baraza la Wayahudi.5:22 Baraza la Wayahudi lilikuwa kundi kuu kabisa la utawala wa Wayahudi lililoundwa na wazee 70 pamoja na kuhani mkuu. Lakini yeyote atakayesema ‘Wewe mpumbavu!’ atapaswa hukumu ya moto wa jehanamu.

235:23 Mt 8:4; 23:19; Mk 11:25“Kwa hiyo, kama unatoa sadaka yako madhabahuni, ukakumbuka kuwa ndugu yako ana kitu dhidi yako, 245:24 Ay 42:8; 18:19; 1Tim 2:8; 1Pet 3:7iache sadaka yako hapo mbele ya madhabahu. Enda kwanza ukapatane na ndugu yako; kisha urudi na ukatoe sadaka yako.

255:25 Mt 18:35; Lk 12:58-59“Patana na mshtaki wako upesi wakati uwapo njiani pamoja naye kwenda mahakamani, ili mshtaki wako asije akakutia mikononi mwa hakimu, naye hakimu akakutia mikononi mwa askari, nawe ukatupwa gerezani. 26Amin, nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.

Kuhusu Uzinzi

275:27 Kut 20:14; Kum 5:18“Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Usizini.’ 285:28 Mit 6:25; 2Pet 2:14Lakini mimi nawaambia kwamba, yeyote amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake. 295:29 Rum 14:21; 1Kor 8:13Jicho lako la kuume likikusababisha kutenda dhambi, lingʼoe ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kupoteza kiungo kimoja cha mwili wako kuliko mwili wako mzima ukatupwa jehanamu. 305:30 Mt 5:29Kama mkono wako wa kuume ukikusababisha kutenda dhambi, ukate, uutupe mbali. Ni afadhali kwako kupoteza kiungo kimoja cha mwili wako kuliko mwili wako mzima utupwe jehanamu.

Kuhusu Talaka

(Mathayo 19:9; Marko 10:11-12; Luka 16:18)

315:31 Kum 24:1-4“Pia ilinenwa kwamba, ‘Mtu yeyote amwachaye mkewe sharti ampe hati ya talaka.’ 325:32 Lk 16:18Lakini mimi nawaambia, yeyote amwachaye mkewe isipokuwa kwa kosa la uasherati, amfanya mkewe kuwa mzinzi. Na yeyote amwoaye yule mwanamke aliyeachwa, anazini.

Kuhusu Kuapa

335:33 Law 19:12; Hes 30:2; Mt 23:16-22“Tena mmesikia walivyoambiwa watu wa zamani kwamba, ‘Usiape kwa uongo, bali timiza kiapo kile ulichofanya kwa Bwana.’ 345:34 Yak 5:12; Isa 66:1; Mt 23:22Lakini mimi nawaambia, msiape kabisa: iwe kwa mbingu, kwa kuwa ni kiti cha enzi cha Mungu; 355:35 Za 48:2au kwa dunia, kwa kuwa ndipo mahali pake pa kuwekea miguu; au kwa Yerusalemu, kwa kuwa ndio mji wa Mfalme Mkuu. 36Nanyi msiape kwa vichwa vyenu, kwa kuwa hamwezi kuufanya hata unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi. 375:37 Yak 5:12; Efe 6:16; 1Yn 3:12‘Ndiyo’ yenu iwe ‘Ndiyo,’ na ‘Hapana’ yenu iwe ‘Hapana.’ Lolote zaidi ya hili latoka kwa yule mwovu.

Kuhusu Kulipiza Kisasi

(Luka 6:29-30)

385:38 Law 24:20; Kum 19:21“Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Jicho kwa jicho na jino kwa jino.’ 395:39 1Kor 6:7; 1Pet 3:9Lakini mimi nawaambia, msishindane na mtu mwovu. Lakini kama mtu akikupiga kwenye shavu la kuume, mgeuzie na la pili pia. 405:40 1Kor 6:7Kama mtu akitaka kukushtaki na kuchukua joho lako, mwachie achukue na koti pia. 415:41 Mt 27:32; Mk 15:21Kama mtu akikulazimisha kwenda maili moja, nenda naye maili mbili. 425:42 Kum 15:8; Lk 16:30Mpe yeye akuombaye, wala usimgeuzie kisogo yeye atakaye kukukopa.

Upendo Kwa Adui

(Luka 6:27-28, 32-36)

435:43 Law 19:18; Gal 5:14; Kum 23:6; Za 139:21-22“Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Mpende jirani yako na umchukie adui yako.’ 445:44 Yn 15:20; Rum 8:35Lakini ninawaambia: Wapendeni adui zenu na waombeeni wanaowatesa ninyi, 455:45 Lk 6:35; Rum 8:14; Ay 25:3ili mpate kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa maana yeye huwaangazia jua lake watu waovu na watu wema, naye huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki. 465:46 Lk 6:32Kama mkiwapenda tu wale wanaowapenda, mtapata thawabu gani? Je, hata watoza ushuru hawafanyi hivyo? 47Nanyi kama mkiwasalimu ndugu zenu tu, je, mnafanya nini zaidi ya wengine? Je, hata watu wasiomjua Mungu, hawafanyi hivyo? 485:48 Law 19:2; 1Pet 1:16Kwa hiyo kuweni wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

马太福音 5:1-48

八福

1耶稣看见这些人群,就上了山,刚坐下,门徒便走到祂跟前, 2祂就开口教导他们,说:

3“心灵贫穷的人有福了,

因为天国是他们的。

4哀痛的人有福了,

因为他们必得安慰。

5谦和的人有福了,

因为他们必承受土地。

6爱慕公义如饥似渴的人有福了,

因为他们必得饱足。

7心存怜悯的人有福了,

因为他们必蒙上帝的怜悯。

8心灵纯洁的人有福了,

因为他们必看见上帝。

9使人和睦的人有福了,

因为他们必被称为上帝的儿女。

10为义受迫害的人有福了,

因为天国是他们的。

11“人们因为我的缘故侮辱、迫害、肆意毁谤你们,你们就有福了。 12要欢喜快乐,因为你们在天上有很大的奖赏。他们也曾这样迫害以前的先知。

盐和光

13“你们是世上的盐。如果盐失去咸味,怎能使它再变咸呢?它将毫无用处,只有被丢在外面任人践踏。 14你们是世上的光,如同建在山上的城一样无法隐藏。 15人点亮了灯,不会把它放在斗底下,而是放在灯台上,好照亮全家。 16同样,你们的光也应当照在人面前,好让他们看见你们的好行为,便赞美你们天上的父。

成全律法

17“不要以为我是来废除律法和先知书,我不是来废除,乃是来成全。 18我实在告诉你们,就是到天地都消失了,律法的一点一划都不会废除,全都要成就。 19所以,谁违背这些诫命中最小的一条,并教导别人违背,谁在天国将被称为最小的。但谁遵守这些诫命,并教导别人遵守,谁在天国将被称为大的。 20我告诉你们,除非你们的义胜过律法教师和法利赛人的义,否则断不能进天国。

论仇恨

21“你们听过吩咐古人的话,‘不可杀人,杀人的要受审判。’ 22但我告诉你们,凡无缘无故5:22 有古卷无“无缘无故”。向弟兄发怒的,要受审判;凡骂弟兄是白痴的,要受公会5:22 公会”是当时犹太人的最高司法机构,处理宗教、道德和伦理等事务。的审判;凡骂弟兄是笨蛋的,难逃地狱的火。

23“所以,你在祭坛前献祭的时候,要是想起有弟兄和你有过节, 24就该把祭物留在祭坛前,先去跟他和好,然后再来献祭。

25“趁着你和告你的人还在去法庭的路上,你要赶紧与对方和解。不然,他会把你交给审判官,审判官会把你交给差役关进监牢。 26我实在告诉你,要是有一分钱没有还清,你绝不能从那里出来。

论通奸

27“你们听过这样的话,‘不可通奸。’ 28但我告诉你们,凡看见妇女就动淫念的,他在心里已经犯了通奸罪。 29如果你的右眼使你犯罪,就把它剜掉!宁可失去身体的一部分,也比整个人下地狱好。 30如果你的右手使你犯罪,就把它砍掉!宁可失去身体的一部分,也比整个人下地狱好。

论休妻

31“还有话说,‘人若休妻,必须给她休书’。 32但我告诉你们,除非是妻子不贞,否则,休妻就是使妻子犯通奸罪,娶被休女子的人也犯了通奸罪。

论起誓

33“你们也听过吩咐古人的话,‘不可违背誓言,总要向主遵守所起的誓。’ 34但我告诉你们,不可起誓。不可指着天起誓,因为天是上帝的宝座。 35不可指着地起誓,因为地是上帝的脚凳。不可指着圣城耶路撒冷起誓,因为那是大君王的城。 36也不可指着自己的头起誓,因为你不能使一根头发变黑或变白。 37你们说话,是就说是,不是就说不是,多说的便是来自那恶者5:37 那恶者即魔鬼,又名撒旦。

论爱仇敌

38“你们听过这样的话,‘以眼还眼,以牙还牙。’ 39但我告诉你们,不要跟恶人作对。有人打你的右脸,连左脸也转过来让他打。 40有人想控告你,要夺取你的内衣,连外衣也给他。 41有人强迫你走一里路,你就跟他走二里路。 42有求你的,就给他;有向你借的,不可拒绝他。

43“你们听过这样的话,‘要爱邻居,恨仇敌。’ 44但我告诉你们,要爱仇敌,为迫害你们的人祷告。 45这样,你们才是天父的孩子。因为祂让阳光照好人也照坏人,降雨给义人也给恶人。 46如果你们只爱那些爱你们的人,有什么值得嘉奖的呢?就是税吏也会这样做。 47如果你们只问候自己的弟兄,有什么特别呢?就是外族人也会这样做。 48所以,你们要纯全,正如你们的天父是纯全的。