Matendo 6 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Matendo 6:1-15

Mateso Na Kuenea Kwa Injili

(6:1–9:31)

Saba Wachaguliwa Kuhudumu

16:1 Mdo 2:21; 4:35; 9:29, 39-41; 1Tim 5:3Basi ikawa katika siku hizo, wakati idadi ya wanafunzi ilipokuwa ikiongezeka sana, palitokea manungʼuniko kati ya Wayahudi wa Kiyunani, dhidi ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahaulika katika mgawanyo wa chakula wa kila siku. 26:2 Mdo 11:26; Ebr 4:12; Kut 18:17Wale mitume kumi na wawili wakakusanya wanafunzi wote pamoja wakasema, “Haitakuwa vyema sisi kuacha huduma ya neno la Mungu ili kuhudumu mezani. 36:3 Mdo 1:14-16; Lk 1:15; Kut 18:21; Neh 13:13; 1Tim 3:7, 8Kwa hiyo ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, watu wenye sifa njema, waliojawa na Roho Mtakatifu na hekima, ambao tunaweza kuwakabidhi kazi hii, 46:4 Mdo 2:42nasi tutatumia muda wetu kuomba na huduma ya neno.”

56:5 Mdo 11:19; 22:20; 8:5-40; 21:8; Lk 1:15Yale waliyosema yakawapendeza watu wote, nao wakamchagua Stefano (mtu aliyejawa na imani na Roho Mtakatifu) pamoja na Filipo, Prokoro, Nikanori, Timoni, Parmena na Nikolao, mwongofu kutoka Antiokia. 66:6 Mdo 13:3; 2Tim 1:6; Hes 27; 18; Mk 5:23Wakawaleta watu hawa mbele ya mitume, nao wakawaombea na kuwawekea mikono juu yao.

76:7 Mdo 12:24; 19:20Neno la Mungu likazidi kuenea. Idadi ya wanafunzi ikazidi kuongezeka sana katika Yerusalemu hata makuhani wengi wakaitii ile imani.

Kukamatwa Kwa Stefano

86:8 Yn 4:48Stefano, akiwa amejaa neema na nguvu za Mungu, alifanya ishara na miujiza mikubwa miongoni mwa watu. 96:9 Mt 27:32; 22:3; 23:34; 2:9Hata hivyo, ukainuka upinzani wa watu wa Sinagogi la Watu Huru (kama lilivyokuwa linaitwa), la Wayahudi wa Kirene na wa Iskanderia, na wengine kutoka Kilikia na Asia. Watu hawa wakaanza kupingana na Stefano. 106:10 Lk 21:15; Mdo 5:39Lakini hawakuweza kushindana na hekima yake wala huyo Roho ambaye alisema kwake.

116:11 2Fal 21:10; Mt 26:59-61Ndipo kwa siri wakawashawishi watu fulani waseme, “Tumemsikia Stefano akisema maneno ya kufuru dhidi ya Mose na dhidi ya Mungu.”

Stefano Afikishwa Mbele Ya Baraza

126:12 Mt 5:22Wakawachochea watu, wazee na walimu wa Sheria, nao wakamkamata Stefano wakamfikisha mbele ya baraza. 136:13 Mt 24:15; Mdo 7:48Wakaweka mashahidi wa uongo ambao walishuhudia wakisema, “Mtu huyu kamwe haachi kusema dhidi ya mahali hapa patakatifu na dhidi ya Sheria. 146:14 Mdo 26:3; 28:17Kwa maana tumemsikia akisema kwamba Yesu wa Nazareti atapaharibu mahali patakatifu na kubadili desturi zote tulizopewa na Mose.”

156:15 Mt 5:22Watu wote waliokuwa wameketi katika baraza wakimkazia macho Stefano, wakaona uso wake unangʼaa kama uso wa malaika.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

使徒行傳 6:1-15

選立執事

1那時,門徒的人數與日俱增。當中有些講希臘話的猶太人埋怨講希伯來話的猶太人,說對方在日常分配食物的事上怠慢了他們的寡婦。 2於是,十二使徒召集所有的門徒,對他們說:「我們不應該忽略傳上帝的道,去管理膳食。 3弟兄姊妹,請從你們中間選出七位聲譽良好、被聖靈充滿、有智慧的人來負責膳食, 4而我們要專心祈禱和傳道。」

5大家一致同意,便選出充滿信心、被聖靈充滿的司提凡,此外還有腓利伯羅哥羅尼迦挪提門巴米拿,以及曾信過猶太教、來自安提阿的外族人尼哥拉6大家將這七個人帶到使徒面前。使徒把手按在他們身上,為他們禱告。

7上帝的道興旺起來,耶路撒冷的門徒大大增多,連許多祭司也皈信了。

司提凡被捕

8司提凡得到極大的恩典和能力,在百姓中間行了驚人的神蹟奇事。 9但有些來自古利奈亞歷山大基利迦亞細亞、屬於「自由人6·9 自由人」指的是原為奴隸,後來獲得自由的人。會堂」的猶太人聯合起來與司提凡辯論。 10他們無法駁倒司提凡,因為他靠著智慧和聖靈說話。

11於是,他們暗中唆使一些人誣告司提凡說:「我們聽見他說褻瀆摩西和上帝的話!」 12又煽動百姓、長老和律法教師抓住司提凡,把他押到公會。 13他們還派人作偽證說:「司提凡常常講侮辱聖地6·13 聖地」指「聖殿」。和律法的話。 14我們聽見他說那個拿撒勒人耶穌要毀壞聖殿,還要摒棄摩西傳給我們的規矩。」 15在場的人都盯著司提凡,只見他的容貌好像天使一樣。