Marko 3 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 3:1-35

Mtu Aliyepooza Mkono Aponywa

(Mathayo 12:9-14; Luka 6:6-11)

13:1 Mt 4:23; Mk 1:21Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na huko palikuwa na mtu aliyepooza mkono. 23:2 Mt 12:10; Lk 14:1Wakawa wanamwangalia waone kama atamponya siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki. 3Yesu akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, “Njoo hapa mbele ya watu wote.”

4Kisha Yesu akawauliza, “Je, ni lipi lililo halali siku ya Sabato: Ni kutenda mema au kutenda mabaya? Ni kuokoa maisha au kuua?” Lakini wao wakanyamaza kimya.

53:5 Yn 11:33Yesu akawatazama pande zote kwa hasira, akahuzunika sana kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukaponywa kabisa! 63:6 Mt 22:16; Mk 12:13; Mt 12:14Kisha Mafarisayo wakatoka nje, nao wakaanza kufanya shauri la kumuua Yesu wakiwa na Maherode.

Umati Wa Watu Wamfuata Yesu

73:7 Mt 4:25Yesu pamoja na wanafunzi wake wakaondoka huko wakaenda baharini, nao umati mkubwa wa watu kutoka Galilaya ukamfuata. 83:8 Mt 11:21Waliposikia mambo yote aliyokuwa akiyafanya, umati mkubwa wa watu ukamjia kutoka Uyahudi, Yerusalemu, Idumaya, na ngʼambo ya Yordani, pamoja na wale wa sehemu za karibu na Tiro na Sidoni. 9Kwa sababu ya umati mkubwa wa watu, aliwaambia wanafunzi wake waweke tayari mashua ndogo kwa ajili yake, ili kuwazuia watu kumsonga. 103:10 Mt 4:23; 9:20Kwa kuwa alikuwa amewaponya wagonjwa wengi, wale wenye magonjwa walikuwa wanasukumana ili wapate kumgusa. 113:11 Mt 4:3; Mk 1:23, 24Kila mara pepo wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kupiga kelele wakisema, “Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.” 123:12 Mt 8:4; Mdo 16:17, 18Lakini aliwaonya wasimseme yeye ni nani.

Yesu Achagua Mitume Kumi Na Wawili

(Mathayo 10:1-4; Luka 6:12-16)

133:13 Mt 5:11Yesu akapanda mlimani na kuwaita wale aliowataka, nao wakamjia. 143:14 Mk 6:30Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri 153:15 Mt 10:1na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu. 163:16 Yn 1:42Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro); 173:17 Lk 2Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo); 18Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo, 19na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.

Yesu Na Beelzebuli

(Mathayo 12:22-32; Luka 11:14-23; 12:10)

203:20 Mk 6:31Kisha Yesu aliporudi nyumbani, umati wa watu ukakusanyika tena, kiasi kwamba yeye na wanafunzi wake hawakuweza kula chakula. 213:21 Yn 10:20; Mdo 26:24Ndugu zake walipopata habari wakaja ili kumchukua kwa maana watu walikuwa wakisema, “Amerukwa na akili.”

223:22 Mt 15:1; 12:24; Yn 10:20; Mt 9:34Walimu wa sheria walioteremka kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli!3:22 Beelzebuli kwa Kiyunani ni Beelzebubu, yaani mkuu wa pepo wachafu. Anatoa pepo wachafu kwa kutumia mkuu wa pepo wachafu!”

233:23 Mk 4:2; Mt 4:10Basi Yesu akawaita na kuzungumza nao kwa mifano akasema: “Shetani awezaje kumtoa Shetani? 24Kama ufalme ukigawanyika dhidi yake wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama. 25Nayo nyumba kama ikigawanyika dhidi yake yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama. 26Naye Shetani kama akijipinga mwenyewe na awe amegawanyika, hawezi kusimama bali mwisho wake umewadia. 273:27 Isa 49:24-25Hakuna mtu yeyote awezaye kuingia kwenye nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu. Ndipo ataweza kuteka nyara mali zake. 283:28 Mt 12:31; Lk 12:10; 1Yn 5:16Amin, nawaambia, dhambi zote na makufuru yote ya wanadamu watasamehewa. 293:29 Mt 12:31-32; Lk 12:10Lakini yeyote anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, atakuwa na hatia ya dhambi ya milele.”

303:30 Mk 3:22Yesu alisema hivi kwa sababu walikuwa wanasema, “Ana pepo mchafu.”

Mama Na Ndugu Zake Yesu

(Mathayo 12:46-50; Luka 8:19-21)

313:31 Mt 12:46; Lk 8:19Kisha wakaja ndugu zake Yesu pamoja na mama yake. Wakasimama nje, wakamtuma mtu kumwita. 32Umati wa watu ulikuwa umeketi kumzunguka, nao wakamwambia, “Mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”

33Akawauliza, “Mama yangu na ndugu zangu ni nani?”

34Kisha akawatazama wale watu waliokuwa wameketi kumzunguka pande zote, akasema, “Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu. 35Mtu yeyote anayetenda mapenzi ya Mungu, huyo ndiye ndugu yangu, na dada yangu na mama yangu.”

Knijga O Kristu

Marko 3:1-35

Isus iscjeljuje u subotu

(Mt 12:9-14; Lk 6:6-11)

1Isus ponovno ode u tamošnju sinagogu. Ondje je bio neki čovjek usahnule ruke. 2Isusovi neprijatelji budno su pazili hoće li mu iscijeliti ruku u subotu da ga mogu optužiti. 3Isus reče čovjeku usahnule ruke: “Ustani i dođi ovamo na sredinu!”

4Zatim ih upita: “Je li subotom dopušteno činiti dobro ili zlo, život spasiti ili pogubiti?” Šutjeli su. 5Srdito ih pogleda duboko ožalošćen tvrdoćom njihovih srca te reče čovjeku: “Ispruži ruku!” On ju ispruži, a ruka mu postane zdrava. 6Farizeji se smjesta odu dogovoriti s herodovcima da ga smaknu.

Mnoštvo slijedi Isusa

(Mt 4:23-25; 12:15-16; Lk 6:17-19)

7Isus i njegovi učenici odu na jezero, a za njima krene veliko mnoštvo iz cijele Galileje, Judeje, 8Jeruzalema, Idumeje, s istočne strane Jordana, čak i iz okolice Tira i Sidona. Vijest o čudima koje je činio nadaleko se pročula, pa su ga dolazili osobno vidjeti.

9Isus reče učenicima da mu dovezu čamac koji će biti spreman ako se mnoštvo previše natisne oko njega. 10Toga je dana mnoge iscijelio pa je na njega nahrupilo golemo mnoštvo bolesnika pokušavajući ga dotaknuti. 11Kad bi ga vidjeli ljudi opsjednuti nečistim duhom, pali bi pred njim ničice i vikali: “Ti si Božji Sin!” 12A on im je oštro zabranjivao da ga očituju.

Isus izabira dvanaestoricu apostola

(Mt 10:1-4; Lk 6:12-16; Djela 1:13)

13Zatim ode u goru i pozove one koje je izabrao da mu se ondje pridruže te oni dođu. 14Od njih odabere dvanaestoricu da ga prate i imenuje ih apostolima. Njih je poslao da propovijedau 15i da imaju vlast istjerivati zloduhe. 16Evo imena Dvanaestorice što ih je izabrao:

Šimun (kojemu je nadjenuo ime Petar),

17Jakov i Ivan (Zebedejevi sinovi, kojima je Isus dao nadimak Boanerges, to jest “Sinovi groma”),

18Andrija,

Filip,

Bartolomej,

Matej,

Toma,

Jakov (Alfejev sin),

Tadej,

Šimun (član političke stranke koja se zalagala za nasilno svrgavanje rimske vlasti) i

19Juda Iškariotski (koji ga je poslije izdao).

Isus i knez zloduha

(Mt 12:22-29; Lk 11:14-23; 12:10)

20Kad se vratio u dom gdje je boravio, opet je nagrnulo toliko mnoštvo da nisu stigli ni jesti. 21Kad su za to čuli njegovi, dođu ga odvesti jer su govorili da je izvan sebe. 22Ali pismoznanci što su došli iz Jeruzalema rekoše da ga je opsjeo Beelzebub, poglavica zlih duhova, pa da uz njegovu pomoć izgoni zloduhe.

23Isus dozove ljude i počne im govoriti u prispodobama: “Kako može Sotona izgoniti Sotonu? 24Kraljevstvo koje je u sebi podvojeno propast će. 25Dom u kojemu vlada nesloga ne može opstati. 26Ako se dakle Sotona bori sam protiv sebe, kako će se onda održati? Ne bi uspio u tome. 27Ne možete ući u kuću snažnog čovjeka i opljačkati ga a da ga najprije ne svežete. Tek tada ga možete orobiti.

28Zaista vam kažem da se svaki ljudski grijeh može oprostiti, pa čak i hula. 29Ali hula na Svetoga Duha nikad se ne može oprostiti. To je vječni grijeh.”

30To im reče jer su govorili da ima nečistog duha.

Prava Isusova obitelj

(Mt 12:46-50; Lk 8:19-21)

31Stigli su onamo njegova majka i braća, stajali vani te mu po nekim ljudima poručili da iziđe razgovarati s njima. 32Oko njega je sjedilo mnoštvo kad mu rekoše: “Vani su ti majka, braća i sestre, žele te vidjeti.”

33On im odgovori: “Tko mi je majka? Tko su mi braća?” 34Pogleda ljude koji su sjedili u krugu oko njega, pa reče: “Ovo su mi majka i braća! 35Zaista, tko god čini Božju volju, taj mi je i brat, i sestra i majka.”