Marko 2 – NEN & CRO

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Marko 2:1-28

Yesu Amponya Mtu Aliyepooza

(Mathayo 9:1-8; Luka 5:17-26)

12:1 Mt 9:4Baada ya siku kadhaa Yesu alirudi Kapernaumu, watu wakasikia kwamba amerudi nyumbani. 22:2 Mk 1:45; 2:13Hivyo watu wengi wakakusanyika kiasi kwamba hapakubaki nafasi yoyote hata mlangoni! Naye akawahubiria Neno. 32:3 Mt 4:24Ndipo baadhi ya watu wakaja wakamletea Yesu mtu aliyepooza, akiwa amebebwa na watu wanne. 4Kwa kuwa walikuwa hawawezi kumfikisha kwa Yesu kwa ajili ya umati wa watu, walitoboa tundu kwenye paa mahali pale alipokuwa Yesu, wakamshusha yule aliyepooza kwa kitanda alichokuwa amelalia. 52:5 Lk 7:48Yesu alipoiona imani yao, alimwambia yule mtu aliyepooza, “Mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”

6Basi baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa wameketi huko wakawaza mioyoni mwao, 72:7 Isa 43:25“Kwa nini mtu huyu anasema hivi? Huyu anakufuru! Ni nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”

82:8 Mt 9:4Mara moja Yesu akatambua rohoni mwake kile walichokuwa wanawaza mioyoni mwao, naye akawaambia, “Kwa nini mnawaza hivyo mioyoni mwenu? 9Je, ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia huyu aliyepooza, ‘Umesamehewa dhambi zako,’ au kusema, ‘Inuka, uchukue mkeka wako, uende’? 102:10 Mt 8:20Lakini ili mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi…” Yesu akamwambia yule aliyepooza, 11“Nakuambia, inuka, chukua mkeka wako, uende nyumbani kwako.” 122:12 Mt 9:8; 9:33Yule mtu aliyekuwa amepooza akasimama, akachukua mkeka wake, akatembea machoni pao wote! Jambo hili likawashangaza wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, “Hatujapata kuona jambo kama hili kamwe!”

Yesu Amwita Lawi

(Mathayo 9:9-13; Luka 5:27-32)

132:13 Lk 5:15; Yn 6:2Yesu akaenda tena kandokando ya Bahari ya Galilaya. Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye akaanza kuwafundisha. 142:14 Mt 4:19Alipokuwa akitembea, akamwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi forodhani mahali pa kutoza ushuru, akamwambia, “Nifuate.” Lawi akaondoka, akamfuata Yesu.

152:15 Mt 9:10Yesu alipokuwa akila chakula nyumbani mwa Lawi, watoza ushuru wengi pamoja na “wenye dhambi” walikuwa wakila pamoja naye na wanafunzi wake, kwa maana kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakimfuata. 162:16 Mdo 23:9; 9:11Baadhi ya walimu wa sheria waliokuwa Mafarisayo walipomwona akila pamoja na watoza ushuru na “wenye dhambi,” wakawauliza wanafunzi wake: “Mbona Yesu anakula pamoja na watoza ushuru na ‘wenye dhambi’?”

172:17 Lk 19:10; 1Tim 1:15Yesu aliposikia haya akawaambia, “Watu wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio wagonjwa. Sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.”

Yesu Aulizwa Kuhusu Kufunga

(Mathayo 9:14-17; Luka 5:33-39)

182:18 Mt 6:16-18; Mdo 1; Mt 9Basi wanafunzi wa Yohana pamoja na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Baadhi ya watu wakamjia Yesu na kumuuliza, “Mbona wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga lakini wanafunzi wako hawafungi?”

19Yesu akawajibu, “Wageni wa bwana arusi wawezaje kufunga wakati angali pamoja nao? Wakati bwana arusi bado yuko pamoja nao, hawawezi kufunga. 202:20 Lk 17:22Lakini wakati utafika ambapo bwana arusi ataondolewa kwao. Siku hiyo ndipo watakapofunga.

21“Hakuna mtu ashoneaye kiraka cha nguo mpya kwenye nguo iliyochakaa. Akifanya hivyo, kile kiraka kipya kitachanika kutoka ile nguo iliyochakaa, nayo itachanika zaidi. 222:22 Lk 5:33-38Wala hakuna mtu awekaye divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Akifanya hivyo, ile divai mpya itavipasua hivyo viriba, nayo hiyo divai itamwagika na viriba vitaharibika. Lakini divai mpya huwekwa kwenye viriba vipya.”

Bwana Wa Sabato

(Mathayo 12:1-8; Luka 6:1-5)

232:23 Kum 23:25; Mt 12:1; Lk 6:1Siku moja ya Sabato, Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wakipita katikati ya mashamba ya nafaka. Walipokuwa wakitembea, wanafunzi wake wakaanza kuvunja masuke. 242:24 Mt 12:2Mafarisayo wakamwambia, “Tazama, mbona wanafanya jambo lisilo halali kufanywa siku ya Sabato?”

25Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma kamwe alivyofanya Daudi wakati yeye na wenzake walikuwa na njaa, wakahitaji chakula? 262:26 1Nya 24:6; 2Sam 8:17; Law 24:5-9; 1Sam 21:1-6Daudi aliingia katika nyumba ya Mungu, wakati Abiathari alikuwa kuhani mkuu, akaila ile mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ni halali kuliwa na makuhani peke yao. Naye pia akawapa wenzake.”

272:27 Kut 23:12; Kum 5:14; Kol 2:16Kisha Yesu akawaambia, “Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, lakini si mwanadamu kwa ajili ya Sabato. 282:28 Mt 8:20Hivyo, Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”

Knijga O Kristu

Marko 2:1-28

Isus iscjeljuje uzetog čovjeka

(Mt 9:1-8; Lk 5:17-26)

1Nekoliko dana nakon toga vrati se u Kafarnaum, a vijest o njegovu dolasku brzo se pročuje gradom. 2U kući u kojoj je boravio okupilo se toliko ljudi da više nije bilo mjesta ni za koga, čak ni pred vratima. A on im je propovijedao Riječ. 3Uto dođu četvorica noseći uzetog čovjeka na nosilima. 4Kako nisu mogli kroz mnoštvo doći do Isusa, načine rupu u glinenom krovu nad njegovom glavom i spuste bolesnika na nosilima ravno pred Isusa. 5Kad Isus vidje njihovu vjeru, reče bolesniku: “Sinko, oprošteni su ti grijesi!”

6Ali neki židovski vjerski vođe koji su ondje sjedili rekoše u sebi: 7“Kako ovaj može tako govoriti! On huli! Tko može opraštati grijehe osim jedinoga Boga!”

8Isus duhom prozre njihove misli pa ih upita: “Zašto to smatrate hulom? 9Što je lakše reći uzetom čovjeku: ‘Grijesi su ti oprošteni’ ili ‘Ustani, uzmi svoja nosila i idi’? 10Dokazat ću vam da ja, Sin Čovječji, imam vlast na zemlji opraštati grijehe.” Okrene se zatim prema uzetome i reče: 11“Zapovijedam ti: ustani, uzmi nosila i idi kući!”

12Čovjek smjesta ustane, uzme nosila i iziđe naočigled mnoštvu. Svi su se divili i slavili Boga govoreći: “Takvo što još nikad nismo vidjeli!”

Isus poziva Levija

(Mt 9:9-13; Lk 5:27-32)

13Isus ponovno ode na obalu jezera. Poučavao je mnoštvo koje se okupilo oko njega. 14Prolazeći tuda, opazi Levija, Alfejeva sina, kako ubire porez te ga pozove: “Pođi sa mnom!” Levi ustane i pođe za njim.

15Dok je Isus poslije bio u kući za stolom, došli su brojni ubirači poreza i grešnici i pridružili se njemu i njegovim učenicima. Mnogo takvih bilo je među onima koji su išli za Isusom. 16No kad neki pismoznanci, farizeji, ugledaju Isusa kako jede s tim ozloglašenim ljudima, kazaše njegovim učenicima: “Zašto vaš učitelj jede s ubiračima poreza i drugim grešnicima?”

17Kad je Isus to čuo, reče im: “Ne treba liječnik zdravima, nego bolesnima. Nisam došao zvati pravednike, već grešnike.”

Rasprava o postu

(Mt 9:14-17; Lk 5:33-39)

18Ivanovi učenici i farizeji povremeno su postili. Jednoga dana neki ljudi dođu Isusu i upitaju ga: “Zašto Ivanovi učenici i farizeji poste, a tvoji učenici ne poste?”

19Isus im odgovori: “Mogu li uzvanici na svadbenoj večeri postiti dok su s mladoženjom? Ne mogu postiti dok je mladoženja s njima. 20Ali doći će dani kada će im ugrabiti mladoženju. Tada će postiti.

21Nitko ne krpa rupe na staroj odjeći zakrpom od još nesmočena platna. Zakrpa bi se skupila, razvukla tkaninu i napravila još veću rupu. 22Nitko ne ulijeva novo vino u stare mjehove jer bi se raspuknuli. Vino bi se prolilo, a mjehovi uništili. Novo se vino lijeva u nove mjehove.”

Rasprava o suboti

(Mt 12:1-8; Lk 6:1-5)

23Jedne su subote Isus i njegovi učenici prolazili poljem usjeva. Učenici počnu putem trgati klasje. 24Farizeji rekoše Isusu: “Zašto čine ono što je subotom zabranjeno? Zakonom je zabranjeno skupljati usjev subotom!”

25Ali Isus im odgovori: “Niste li nikada u Pismu čitali o tomu što je učinio kralj David kad su on i njegovi pratioci u nevolji ogladnjeli? 26Ušao je u Dom Božji 2:26 U Hram. Vidjeti 1 Samuelova 21:1-6. (u to je doba veliki svećenik bio Ebijatar) i jeo prineseni kruh koji je dopušteno jesti samo svećenicima te ga je dao jesti i svojim pratiocima. 27Subota je stvorena radi čovjeka, a ne čovjek radi subote. 28Ja, Sin Čovječji, gospodar sam čak i subote.”