Maombolezo 2 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Maombolezo 2:1-22

2 Sura hii imetungwa kila beti likianzia, na pia kila mstari katika lile beti, na herufi ya alfabeti ya Kiebrania zikifuatana tangu Aleph (A) hadi Taw (T); zote ni 22. 12:1 Mao 3:44; Za 132:7; 1Nya 28:2; Yer 12:7; Za 99:5; Mt 11:23; 2Sam 1:19Tazama jinsi Bwana alivyomfunika Binti Sayuni

kwa wingu la hasira yake!

Ameitupa chini fahari ya Israeli

kutoka mbinguni mpaka duniani,

hakukumbuka kiti chake cha kuwekea miguu

katika siku ya hasira yake.

22:2 Mao 3:43; Mik 5:11; Isa 25:12; Za 89:39-40; 21:9Bila huruma Bwana ameyameza

makao yote ya Yakobo;

katika ghadhabu yake amebomoa

ngome za Binti Yuda.

Ameuangusha ufalme wake na wakuu wake

chini kwa aibu.

32:3 Za 75:5; 74:11; Isa 42:25; Ay 16:15; Yer 21:4-5Katika hasira kali amevunja

kila pembe2:3 Pembe inawakilisha nguvu; pia 2:17. ya Israeli.

Ameuondoa mkono wake wa kuume

alipokaribia adui.

Amemteketeza Yakobo kama moto uwakao

ule uteketezao kila kitu kinachouzunguka.

42:4 Isa 63:10; Ay 3:23; Mao 3:12-13; Yer 7:20; Eze 24:16; 2Nya 34:21; Eze 20:34Ameupinda upinde wake kama adui,

mkono wake wa kuume uko tayari.

Kama vile adui amewachinja

wote waliokuwa wanapendeza jicho,

amemwaga ghadhabu yake kama moto

juu ya hema la Binti Sayuni.

52:5 Yer 30:14; Ay 13:24; Yer 9:17-20; Isa 29:2; Yer 7:20Bwana ni kama adui;

amemmeza Israeli.

Amemeza majumba yake yote ya kifalme

na kuangamiza ngome zake.

Ameongeza huzuni na maombolezo

kwa ajili ya Binti Yuda.

62:6 Yer 52:13; Sef 3:18; Yer 7:14; Isa 43:28; Mao 4:16; 5:12; Za 80:12; Isa 5:5; 1:8Ameharibu maskani yake kama bustani,

ameharibu mahali pake pa mkutano.

Bwana amemfanya Sayuni kusahau

sikukuu zake zilizoamriwa na Sabato zake;

katika hasira yake kali amewadharau

mfalme na kuhani.

72:7 Eze 7:1-2; Isa 64:10-11; Yer 7:12-14; Law 26:31; Yer 33:4-5; 52:13; Za 78:59-61; Mik 3:12; Yer 7:12-14; Mt 24:2Bwana amekataa madhabahu yake

na kuacha mahali patakatifu pake.

Amemkabidhi adui kuta

za majumba yake ya kifalme;

wamepiga kelele katika nyumba ya Bwana

kama katika siku ya sikukuu iliyoamriwa.

82:8 2Fal 21:13; Isa 34:11; 3:26; Yer 39:8; Za 48:13; Amu 7:7Bwana alikusudia kuangusha

ukuta uliomzunguka Binti Sayuni.

Ameinyoosha kamba ya kupimia

na hakuuzuia mkono wake usiangamize.

Alifanya maboma na kuta ziomboleze,

vyote vikaharibika pamoja.

92:9 Yer 16:13; Amo 8:11-12; Hos 3:4; 2Nya 15:3; Yer 14:14; Isa 45:2; 2Fal 24:15; Kum 28:36; 2Fal 25:7; Za 74:9; Mik 3:6, 7Malango yake yamezama ardhini,

makomeo yake ameyavunja na kuyaharibu.

Mfalme wake na wakuu wake wamepelekwa uhamishoni

miongoni mwa mataifa,

sheria haipo tena,

na manabii wake hawapati tena

maono kutoka kwa Bwana.

102:10 Ay 2:12-13; Isa 3:24, 26; Eze 27:30-31; Isa 15:3; Mao 3:28; 4:5; Isa 47:1-5Wazee wa Binti Sayuni

wanaketi chini kimya,

wamenyunyiza mavumbi kwenye vichwa vyao

na kuvaa nguo za gunia.

Wanawali wa Yerusalemu

wamesujudu hadi ardhini.

112:11 Isa 15:3; Ay 30:27; Za 22:14; Ay 16:13; Mao 3:48-51; Za 119:82; 6:7Macho yangu yamedhoofika kwa kulia,

nina maumivu makali ndani,

moyo wangu umemiminwa ardhini

kwa sababu watu wangu wameangamizwa,

kwa sababu watoto na wanyonyao wanazimia

kwenye barabara za mji.

12Wanawaambia mama zao,

“Wapi mkate na divai?”

wazimiapo kama watu waliojeruhiwa

katika barabara za mji,

maisha yao yadhoofikavyo

mikononi mwa mama zao.

132:13 Isa 37:22; Yer 14:17; 30:12-15; Dan 9:12; 2Fal 19:2; Ay 5:1Ninaweza kusema nini kwa ajili yako?

Nikulinganishe na nini,

ee Binti Yerusalemu?

Nitakufananisha na nini,

ili nipate kukufariji,

ee Bikira Binti Sayuni?

Jeraha lako lina kina kama bahari.

Ni nani awezaye kukuponya?

142:14 Isa 58:1; Yer 8:11; 20:6; Eze 13:3; Yer 28:3; 28:15; Eze 22:28Maono ya manabii wako

yalikuwa ya uongo na yasiyofaa kitu,

hawakuifunua dhambi yako

ili kukuzuilia kwenda utumwani.

Maneno waliyokupa

yalikuwa ya uongo na ya kupotosha.

152:15 Hes 24:20; Eze 25:6; Nah 3:19; Za 45:11; Eze 16:14; Za 48:2; Yer 19:8; 1Fal 9:8Wote wapitiao njia yako

wanakupigia makofi,

wanakudhihaki na kutikisa vichwa vyao

kwa Binti Yerusalemu:

“Huu ndio ule mji ulioitwa

mkamilifu wa uzuri,

furaha ya dunia yote?”

162:16 Za 22:13; 56:2; Ay 16:19; Za 35:25; Eze 36:3; Mao 3:46Adui zako wote wanapanua

vinywa vyao dhidi yako,

wanadhihaki na kusaga meno yao

na kusema, “Tumemmeza.

Hii ndiyo siku tuliyoingojea,

tumeishi na kuiona.”

172:17 Kum 28:15-45; Eze 8:18; Isa 44:26; Mao 1:5; Law 26:16; Za 38:16Bwana amefanya lile alilolipanga;

ametimiza neno lake

aliloliamuru siku za kale.

Amekuangusha bila huruma,

amewaacha adui wakusimange,

ametukuza pembe ya adui yako.

182:18 Za 119:145; Mao 1:16; 3:19; Yer 9:1; 14:7Mioyo ya watu

inamlilia Bwana.

Ee ukuta wa Binti Sayuni,

machozi yako na yatiririke kama mto

usiku na mchana;

usijipe nafuu,

macho yako yasipumzike.

192:19 Mk 13:35; 1Sam 1:15; Za 62:8; Isa 51:20; Neh 3:10; Isa 26:9; Mao 4:1Inuka, lia usiku,

zamu za usiku zianzapo;

mimina moyo wako kama maji

mbele za Bwana.

Mwinulie yeye mikono yako

kwa ajili ya maisha ya watoto wako,

ambao wanazimia kwa njaa

kwenye kila mwanzo wa barabara.

202:20 Kum 28:53; Eze 5:10; Mao 4:10; Yer 23:11-12; 19:9; Za 78:64; Yer 14:15; Kut 32:11; Law 26:29“Tazama, Ee Bwana, ufikirie:

Ni nani ambaye umepata

kumtendea namna hii?

Je, wanawake wakule wazao wao,

watoto waliowalea?

Je, kuhani na nabii auawe

mahali patakatifu pa Bwana?

212:21 Kum 32:25; 2Nya 36:17; Yer 13:14; Zek 11:6“Vijana na wazee hujilaza pamoja

katika mavumbi ya barabarani,

wavulana wangu na wasichana

wameanguka kwa upanga.

Umewaua katika siku ya hasira yako,

umewachinja bila huruma.

222:22 Za 31:13; Yer 6:25; Ay 27:14; Hes 9:13; Yer 20:10“Kama ulivyoita siku ya karamu,

ndivyo ulivyoagiza hofu kuu

dhidi yangu kila upande.

Katika siku ya hasira ya Bwana

hakuna yeyote aliyekwepa au kupona;

wale niliowatunza na kuwalea,

adui yangu amewaangamiza.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

耶利米哀歌 2:1-22

耶和华惩罚耶路撒冷

1主的怒气像乌云一样遮盖锡安2:1 ”希伯来文是“女子”,可能是对锡安的昵称,下同2:4104:22

祂使以色列的荣美从天上坠下。

祂发怒的时候并不顾念自己的脚凳。

2主毫不留情地毁灭雅各一切的住处,

祂在烈怒中夷平犹大的堡垒,

以色列及其首领蒙羞。

3祂发烈怒毁灭以色列全军。

敌人袭来时,祂收回大能的手。

祂像烈焰一样吞噬雅各

4祂抬起右手张弓搭箭,

宛若仇敌,

杀戮一切悦人眼目的人,

将祂的怒火撒向锡安城的帐篷。

5主像敌人一样毁灭以色列

吞噬她的宫殿,夷平她的堡垒,

使犹大人哀哭不止。

6祂摧毁自己的居所,

如同摧毁花园;

祂摧毁自己规定的聚会之处,

使锡安的人民忘记安息日和节期。

祂在烈怒中弃绝所有的君王和祭司。

7主撇弃自己的祭坛,

憎恶自己的圣所,

耶路撒冷的殿墙交给敌人。

他们像过节一样,

在耶和华的殿中喧嚷吵闹。

8耶和华决意拆毁锡安的城墙,

祂拉了准线,

定意毁灭,决不停止。

祂使城墙和壁垒一同悲哀哭泣。

9锡安的城门陷入地中,

主摧毁、砍断她的门闩。

她的君王和首领流落异乡,

律法不复存在,

她的先知得不到从耶和华而来的异象。

10锡安城的长老腰束麻布,

头蒙灰尘,坐在地上,

默然不语;

耶路撒冷的少女垂头至地。

11我哭得眼睛失明,

心如刀割,肝胆欲碎,

因为人民惨遭毁灭,

儿童和婴孩昏倒在街头。

12孩子们问母亲:

“哪里有饼和酒呢?”

他们像受伤的勇士,

昏倒在城中的街头,

在母亲怀中奄奄一息。

13耶路撒冷啊,我该说什么呢?

谁能与你的苦难相比呢?

锡安啊,我用什么话语才能安慰你呢?

你的伤口深如海洋,

谁能医治你呢?

14你的先知所见的异象虚假无用。

他们没有揭露你的罪恶,

以致你被掳。

他们给你的预言虚假谬误。

15路人都拍掌嘲笑你。

他们向耶路撒冷城摇头,

嗤笑道:

“这就是那被誉为完美无瑕、

普世喜悦的城吗?”

16敌人都幸灾乐祸地讥讽你,

他们咬牙切齿地说:

“我们吞灭了她!

这是我们期待已久的日子!

我们终于见到这一天了!”

17耶和华实现了祂的计划,

成就了祂很久以前的应许。

祂毫不留情地毁灭了你,

使你的仇敌幸灾乐祸,

耀武扬威。

18锡安的城墙啊,

你要从心里向主呼求!

你的眼泪要像江河一样昼夜涌流,

不歇不眠。

19你要在夜间起来,

在主面前整夜呼求,

向祂倾心吐意;

你要为饿昏街头的孩童向主举手祷告。

20“耶和华啊,求你看看,

你曾这样对付过谁呢?

母亲岂能吃自己的孩子?

祭司和先知岂能在主的圣所中被杀?

21“老人和小孩陈尸街头,

少男少女都丧身刀下。

你在发怒的日子杀了他们,

毫不留情。

22“你从四面八方召人攻击我,

如同召集人过节。

耶和华发怒的日子,

无人得以逃脱,无人得以幸免。

敌人杀光了我养育的孩子。”