Kutoka 38 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 38:1-31

Madhabahu Ya Sadaka Ya Kuteketezwa

(Kutoka 27:1-8)

138:1 Kut 27:1; 2Nya 29:23, 24; Za 51:15-19; Isa 61:8; Eze 44:11; 45:17; Ebr 9:14; 13:10Akatengeneza madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa mbao za mti wa mshita, kimo chake dhiraa tatu;38:1 Dhiraa 3 ni sawa na mita 1.35. nayo ilikuwa mraba, urefu wake dhiraa tano, na upana wa dhiraa tano38:1 Dhiraa 5 ni sawa na mita 2.25. 238:2 2Nya 1:5; 1Fal 7:45Akatengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili zile pembe na madhabahu zikawa zimeungana, akafunika madhabahu kwa shaba. 338:3 Kut 31:9; 35:16Akatengeneza vyombo vyake vyote kwa shaba: vyungu vyake vya kuondolea majivu, masepetu, mabakuli ya kunyunyizia, uma za nyama na vyombo vya kuchukulia moto. 4Akatengeneza wavu wa shaba chini ya ukingo wa madhabahu ili ufikie nusu ya kimo cha madhabahu. 5Akasubu pete za shaba za kushikilia ile mipiko kwa ajili ya zile pembe nne za huo wavu wa shaba. 6Akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuifunika kwa shaba. 7Akaiingiza ile mipiko kwenye zile pete, ili iwe pande mbili za madhabahu kwa ajili ya kuibeba. Akaitengeneza madhabahu yenye uvungu ndani yake akitumia mbao.

Sinia La Kunawia

(Kutoka 30:18)

838:8 Kut 30:18; 40:7; Kum 23:17; 1Sam 2:22; 1Fal 14:24; 2Fal 16:17; 2Nya 4:2; Za 26:6; Zek 13:1; Eze 36:25; 2Kor 7:1; Ebr 10:22; 1Yn 5:6Akatengeneza sinia la shaba lenye kitako cha shaba kutoka kwa vioo vya shaba vilivyotolewa na wanawake waliohudumu pale ingilio la Hema la Kukutania.

Ua Wa Hema La Kukutania

(Kutoka 27:9-19)

938:9 Kut 27:9; Za 84:2; 92:13Kisha akatengeneza ua. Upande wa kusini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja,38:9 Dhiraa 100 ni sawa na mita 45. na ulikuwa na mapazia ya kitani iliyosokotwa vizuri, 10pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 11Upande wa kaskazini ulikuwa na urefu wa dhiraa mia moja, pamoja na nguzo ishirini na vitako vya shaba ishirini, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo.

12Upande wa mwisho wa magharibi ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini38:12 Dhiraa 50 ni sawa na mita 22.5. na ulikuwa na mapazia, na nguzo kumi na vitako vyake kumi, pamoja na kulabu na tepe za fedha juu ya hizo nguzo. 13Upande wa mwisho wa mashariki jua linakochomoza, pia ulikuwa na upana wa dhiraa hamsini. 14Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano38:14 Dhiraa 15 ni sawa na mita 6.75. yalikuwa upande mmoja wa ingilio, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 15Mapazia yenye urefu wa dhiraa kumi na tano yalikuwa upande mwingine wa ingilio la ua, pamoja na nguzo tatu na vitako vitatu. 16Mapazia yote yaliyozunguka ua yalikuwa ya kitani iliyosokotwa vizuri. 17Vitako vya nguzo vilikuwa vya shaba. Kulabu na tepe juu ya nguzo zilikuwa za fedha, na ncha zake zilifunikwa kwa fedha. Kwa hiyo nguzo zote za ua zilikuwa na tepe za fedha.

1838:18 2Nya 3:14Pazia la ingilio la ua lilikuwa la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu pamoja na kitani iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi. Pazia hilo lilikuwa na urefu wa dhiraa ishirini kama zile za kwenye ua, na kimo chake kilikuwa dhiraa tano, 19likiwa na nguzo nne na vitako vinne vya shaba. Kulabu zake na tepe zake zilikuwa za fedha, na ncha zake zilikuwa zimefunikwa kwa fedha. 2038:20 Kut 35:18; 38:20; 27:10; 2Nya 3:9; Ezr 9:8; Isa 22:23; Efe 2:21, 22Vigingi vyote vya maskani na vya ua ulioizunguka vilikuwa vya shaba.

Vifaa Vilivyotumika

2138:21 Hes 1:50-53; 8:24; 9:15; 10:11; 17:7; 1Nya 23:32; 2Nya 24:6; Mdo 7:44; Ufu 15:5; Hes 4:28-33Ifuatayo ni orodha ya vifaa vilivyotumika kwa ajili ya ujenzi wa maskani, maskani ya Ushuhuda, ambavyo vilitayarishwa na Walawi kama alivyoagiza Mose, chini ya usimamizi wa Ithamari, mwana wa kuhani Aroni. 2238:22 Kut 31:2(Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda, alifanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose, 2338:23 Kut 31:6akiwa pamoja na Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, fundi stadi wa kutia nakshi, kubuni michoro, mtarizi kwa rangi ya buluu, ya zambarau, nyekundu na kitani safi.) 2438:24 Kut 30:12-16; 12:37; Hes 3:47Jumla ya dhahabu iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa kwa ajili ya kazi ya mahali patakatifu ilikuwa na uzito wa talanta 29 na shekeli 730,38:24 Talanta 29 na shekeli 730 ni sawa na tani moja. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.

2538:25 Kut 12:37; 30:12Fedha iliyopatikana kutokana na jumuiya ya watu waliohesabiwa ilikuwa yenye uzito wa talanta mia moja na shekeli 1,775,38:25 Talanta 100 na shekeli 1,775 za fedha ni sawa na tani 3.4. kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. 2638:26 Kut 30:12-16; 12:36-37; Hes 1:46Kila mtu alitoa beka moja, ambayo ni sawa na nusu shekeli ya fedha, kwa kazi ya mahali patakatifu, kutoka kwa kila mtu aliyekuwa amehesabiwa mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi, ambao jumla yao walikuwa wanaume 603,550. 2738:27 Kut 26:19Talanta hizo 100 za fedha zilitumika kusubu vile vitako mia moja kwa ajili ya mahali patakatifu na pazia: vitako mia moja kwa talanta mia, yaani, talanta moja kwa kila kitako. 28Akatumia zile shekeli hizo 1,775 kutengeneza kulabu za nguzo, kufunika ncha za nguzo na kutengeneza vitanzi vyake.

29Shaba iliyopatikana kutokana na sadaka ya kuinuliwa ilikuwa na uzito wa talanta 70 na shekeli 2,400.38:29 Talanta 70 na shekeli 2,400 ni sawa na tani 2.4. 30Akaitumia hiyo shaba kutengeneza vitako vya ingilio la Hema la Kukutania, madhabahu ya shaba pamoja na ule wavu wake na vyombo vyake vyote, 3138:31 Kut 27:19; 2Nya 3:9; Ezr 9:8; Isa 22:23; Efe 2:21, 22vile vitako vya ule ua uliozunguka na vile vya ingilio, na vigingi vyote vya Maskani pamoja na ule ua uliozunguka.

Korean Living Bible

출애굽기 38:1-31

번제단

1그는 아카시아나무로 제물을 태워 바칠 제단을 만들었다. 그것은 가로 세로가 각각 2.3미터로 네모가 반듯하고 높이는 1.4미터였다.

2그리고 제단 네 모퉁이에 뿔이 하나씩 나오도록 만들고 그 제단을 놋으로 쌌다.

3그런 다음 그는 그 단의 모든 기구, 곧 재를 담는 통과 부삽과 피를 담는 그릇과 고기 갈고리와 불 옮기는 그릇을 다 놋으로 만들었으며

4또 단에 쓸 놋그물을 만들어 단의 아래 언저리 밑에 놓아 그것이 단의 절반 높이로 올라오게 하고

5그 놋그물 네 모퉁이에 운반채를 꿸 고리 네 개를 만들었다.

6그리고 운반채는 아카시아나무로 만들어 놋으로 싸고

7그것을 단의 양쪽 고리에 꿰어 단을 운반할 수 있게 하였으며 그 단은 널빤지로 속이 비게 만들었다.

8그는 또 회막 입구에서 섬기는 여자들이 바친 놋거울로 넓적한 물통과 그 받침을 만들었다.

성막 뜰

9다음으로 그는 성막 뜰을 위해 고운 모시 포장을 만들었는데 뜰 남쪽을 위해서 포장의 길이를 45미터로 하고

1020개의 기둥을 만들었다. 그리고 그 기둥 받침은 놋으로 만들고 기둥의 갈고리와 가로대는 은으로 만들었다.

11또 맞은편인 북쪽을 위해서도 이와 똑같이 만들고

12서쪽을 위해서는 포장 길이를 22.5미터로 하였으며 10개의 기둥과 받침을 만들고 기둥의 갈고리와 가로대를 은으로 만들었다.

13그리고 출입구를 낼 뜰 동쪽 길이도 22.5미터가 되게 하였다.

14-15출입구 양쪽을 위해 각각 3개의 기둥 과 받침을 만들고 거기에 칠 6.8미터 길이의 포장을 만들었다.

16이와 같이 뜰 사면의 포장은 모두 고운 모시로 만들었으며

17기둥 받침은 놋으로 만들고 기둥의 갈고리와 가로대와 기둥머리 덮개는 은으로 만들었으며 뜰의 모든 기둥에는 은가로대를 꿸 수 있게 하였다.

18그리고 청색, 자색, 홍색 실과 가늘게 꼰 베실로 수놓아 짜서 뜰의 출입구 막을 만들었으며 그 길이는 9미터, 높이는 뜰의 포장과 마찬가지로 2.3미터로 하였다.

19또 출입구 막을 달 수 있도록 4개의 기둥과 기둥 받침과 기둥머리 덮개, 그리고 가로대와 갈고리를 만들었는데 그 기둥 받침은 놋이며 갈고리와 기둥머리 덮개와 가로대는 은이었다.

20그리고 성막 말뚝과 뜰 사면의 포장 말뚝은 다 놋으로 만들었다.

성막을 만드는 데 쓰인 재료

21법궤를 안치할 성막을 세우는 데 쓴 재료의 품목은 모세의 명령을 받아 제사장 아론의 아들인 이다말이 계산하였으며

22유다 지파 사람 훌의 손자이며 우리의 아들인 브사렐은 여호와께서 모세에게 명령하신 모든 것을 만들었다. 그리고

23그의 조력자인 단 지파 사람 아히사막의 아들 오홀리압은 재능이 있어서 조각하고 정교한 일을 하며 청색, 자색, 홍색 실과 가늘게 꼰 베실로 수놓는 일을 하였다.

24성소를 짓고 그 모든 기구를 만드는 데 사용된 금은 38:24 히 ‘성소의 세겔대로 29달란트와 730세겔’약 톤이었다.

25그리고 인구 조사를 받은 백성들이 바친 은은 38:25 히 ‘성소의 세겔대로 100달란트와 1,775세겔’약 3,420킬로그램이었다.

2620세 이상 인구 조사를 받은 사람이 전부 603,550명이므로 인당 38:26 히 ‘성소의 세겔대로 은 한 베가 곧 반 세겔’약 6그램씩 낸 셈이었다.

27그 중에서 38:27 히 ‘은 100달란트’은 3,400킬로그램으로 성막 벽이 될 기둥과 지성소 앞의 휘장 기둥에 받칠 밑받침 100개를 만들었으며 그 밑받침 하나에는 은 34킬로그램씩 들었다.

28그리고 나머지 은 20킬로그램으로 기둥 갈고리와 기둥머리와 기둥 가로대를 만들었다.

29그 밖에 백성들이 바친 놋은 38:29 히 ‘70달란트와 2,400세겔’약 2,400킬로그램인데

30이것으로 성막 출입구 기둥 받침, 놋제단과 놋그물과 그 모든 기구,

31뜰 사면의 기둥 받침과 뜰 출입구 기둥 받침, 그리고 성막의 말뚝과 뜰 사면의 모든 말뚝을 만들었다.