Kutoka 39 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kutoka 39:1-43

Mavazi Ya Kikuhani

(Kutoka 28:1-14)

139:1 Kut 35:19-23; 28:2; Za 93:5; Eze 43Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Kisibau

239:2 Kut 28:6; Law 8:7Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri. 3Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi. 439:4 Law 24:7; Yos 4:7Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau. 539:5 Isa 11:5; Ufu 1:13Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

639:6 Kut 28:9; Ay 28:16; Isa 49:16; Ufu 1:17Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa. 739:7 Law 24:7; Yos 4:7; Kut 28:12; Yos 4:7; Neh 2:20Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Kifuko Cha Kifuani

(Kutoka 28:15-30)

839:8 Law 8:8; Kut 28:15; Isa 59:17Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa. 9Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja39:9 Shibiri moja ni sawa na sentimita 22. na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili. 1039:10 Kut 28:17; Eze 28:13; Ufu 21:19, 20; Isa 54:12Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi; 1139:11 Ufu 4:3; Isa 54:11; Yer 17:1safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi; 12safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto; 1339:13 Dan 10:6; Ay 28:16; Ufu 21:11katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu. 1439:14 Ufu 21:12Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.

15Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba. 16Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani. 17Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani, 18nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele. 19Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau. 20Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau. 21Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Mavazi Mengine Ya Kikuhani

(Kutoka 28:31-43)

2239:22 Kut 28:31; Law 8:7; 1Sam 2:18; 2Sam 6:14Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji, 23na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike. 24Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho. 2539:25 Kut 28:33Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga. 26Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

2739:27 Kut 28:39, 40; 39:27; Law 8:13; Kut 28:4; Isa 61:10; Rum 3:22; Gal 3:27Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji, 2839:28 Law 6:10; 8:2; Kut 28:39, 42; Eze 44:17, 18na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri. 29Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

3039:30 Isa 23:18; Zek 14:20; Za 93:5; Isa 23:18Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana. 31Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.

Mose Akagua Maskani Ya Mungu

(Kutoka 35:10-19)

3239:32 Kut 25:9; 25:40Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose. 3339:33 Kut 25:8-40; 36:10-16; Ebr 9:1-28Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake; 34kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo,39:34 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. pazia la kufunikia; 3539:35 Kut 30:6; 37:1Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema, 3639:36 Kut 25:23-30; 37:10-16meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho; 3739:37 Kut 25:31-39; 25:6; Ufu 1:13-20; Mt 5:14; Flp 2:15kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa; 3839:38 Kut 31:1-10; 37:25-28; 30:22-32; 37:29; 30:34-38; 36:35madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema; 3939:39 Kut 37:1-8; 38:1-7; 30:18madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake; 4039:40 Kut 27:9-19; 38:9-20; Ufu 3:12mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania; 41na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.

4239:42 Kut 25:9Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose. 4339:43 Kut 25:9; 35:10; Mwa 31:55; Law 9:22-23; Hes 6:23-27; Kum 26:15; 2Sam 6:18; 1Fal 8:14, 55; 1Nya 16:2; 2Nya 30:27Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.

Korean Living Bible

출애굽기 39:1-43

제사장의 예복

1그들은 여호와께서 모세에게 명령하신 대로 청색, 자색, 홍색 실로 제 사장들이 성소에서 섬길 때 입을 아름다운 옷을 만들고 또 아론이 입을 거룩한 옷 도 만들었다.

에봇

2그들은 금실과 청색, 자색, 홍색 실과 가늘게 꼰 베실로 39:2 앞치마 비슷한 제사장의 예복.에봇을 만들었는데

3금을 얇게 두들겨 오려서 실을 만들어 청색, 자색, 홍색 실과 가는 베실에 섞어 그것을 정교하게 짰다.

4그들은 또 에봇의 어깨받이를 만들어 에봇 앞판과 뒷판의 양쪽 끝에 달아 서로 연결하고

5에봇 위에 매는 허리띠는 여호와께서 모세에게 명령하신 대로 에봇을 짤 때와 같은 방법으로 금실과 청색, 자색, 홍색 실과 가늘게 꼰 베실로 정교하게 에봇에 붙여 짰다.

6그리고 그들은 호마노를 깎아 금테에 물리고 인장 반지를 새기듯이 그 위에 야곱의 열두 아들의 이름을 새겨

7여호와께서 모세에게 명령하신 대로 그것을 양쪽 어깨받이에 달아 이스라엘 열두 지파의 상징으로 삼았다.

가슴패

8그들은 또 에봇과 마찬가지로 금실과 청색, 자색, 홍색 실과 가늘게 꼰 베실로 가슴패를 정교하게 짰다.

9그것은 가로 세로가 각각 한 뼘으로 네모가 반듯하고 두 겹으로 되어 있었다.

10그런 다음 그들은 그 가슴패 위에 네 줄의 보석을 물렸다. 첫째 줄에는 홍옥, 황옥, 녹주석;

11둘째 줄에는 홍수정, 청옥, 금강석;

12셋째 줄에는 호박, 백마노, 자수정;

13넷째 줄에는 감람석, 호마노, 벽옥이었다. 이것들은 다 금테에 물렸으며

14이 열두 보석 위에는 이스라엘 열두 지파를 상징하는 야곱의 아들들의 이름이 하나씩 새겨져 있었다.

15그리고 그들은 순금을 노끈처럼 땋아 금사슬을 만들고

16또 금테 둘과 금고리 둘을 만들어 그 고리를 가슴패 위쪽 양끝에 달고

17땋은 그 두 금사슬을 가슴패 윗고리에 연결하였으며

18사슬의 다른 두 끝은 에봇 앞쪽의 두 어깨받이 금테에 매달았다.

19그런 다음 그들은 금고리 두 개를 더 만들어 그 고리가 잘 보이지 않도록 가슴패 양쪽 아래 끝 안쪽에 달았으며

20또 다른 금고리 두 개를 더 만들어 에봇의 양쪽 옆구리 부분인 허리띠 바로 위에 달고

21여호와께서 모세에게 명령하신 대로 청색 끈으로 가슴패 고리를 에봇 고리에 매어 가슴패가 움직이지 않고 허리띠 위쪽 에봇에 부착되어 있도록 하였다.

제사장의 다른 예복

22그들은 에봇 속에 받쳐 입는 겉옷을 전부 청색 실로 짜서 만들었다.

23그 옷은 머리가 들어갈 수 있도록 구멍을 만들고 찢어지지 않게 구멍 둘레를 갑옷 깃처럼 짰다.

24그리고 청색, 자색, 홍색 실과 가는 베실로 그 옷자락의 가장자리에 석류를 만들어 달고

25순금으로 방울을 만들어 그 가장자리로 돌아가며 석류 사이사이에 달아

26여호와께서 모세에게 명령하신 대로 방울과 석류가 하나씩 번갈아 달리게 하였다.

27그들은 또 아론과 그의 아들들을 위하여 고운 모시로 긴 속옷과

28두건과 관과 속바지를 만들고

29가는 베실과 청색, 자색, 홍색 실로 수를 놓아 띠를 만들었는데 이 모든 것은 여호와께서 모세에게 명령하신 대로 만든 것이었다.

30그리고 그들은 순금으로 거룩한 패를 만들어 그 위에 인장 반지를 새기듯이 ‘여호와께 성결’ 이라 새기고

31여호와께서 모세에게 명령하신 대로 그 패를 청색 끈으로 관 앞면에 매었다.

성막의 모든 일이 완성됨

32이렇게 해서 성막의 모든 일이 완성되었다. 이스라엘 백성들은 모든 것을 여호와께서 모세에게 명령하신 그대로 만들어

33모세에게 가져왔다. 그들이 가져온 것은 막과 그 모든 기구, 갈고리, 널빤지, 가로대, 성막 기둥과 그 받침,

34붉게 물들인 숫양의 가죽 덮개, 바닷소의 가죽 덮개, 법궤를 가리는 휘장,

35십계명이 든 법궤와 그 운반채, 법궤의 뚜껑인 39:35 또는 ‘시은좌’속죄소,

36상과 그 모든 기구와 차림빵,

37순금 등대와 그 등잔과 그 모든 기구와 기름,

38향단, 거룩한 의식에 쓸 기름, 향기로운 향, 성막 출입구 휘장,

39놋제단과 놋그물, 그 제단의 운반채와 모든 기구, 넓적한 물통과 그 받침,

40뜰의 포장, 뜰 기둥과 그 밑받침, 뜰의 출입구 막, 뜰의 포장에 쓸 말뚝과 줄, 성막에서 쓰이는 모든 기구,

41그리고 아론과 그의 아들들이 성소에서 제사장 일을 볼 때 입을 거룩한 옷이었다.

42여호와께서 모세에게 명령하신 대로 이스라엘 백성은 모든 일을 완성하였다.

43모세가 그 모든 것을 점검해 보니 그들이 여호와께서 명령하신 그대로 만들었다. 그래서 모세는 그들에게 축복하였다.