Kumbukumbu 20 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 20:1-20

Kwenda Vitani

120:1 Za 20:7; Isa 31:1; Hes 14:9; Kum 3:22; 1Sam 17:45; Isa 41:10; 2Nya 32:7-8; Hes 23:21; Kum 31:6, 8; 2Nya 13:12; 32:7, 8Mtakapokwenda vitani kupigana na adui zenu na mkaona farasi na magari ya vita na jeshi kubwa kuliko lenu, msiwaogope, kwa sababu Bwana Mungu wenu aliyewatoa kutoka Misri, atakuwa pamoja nanyi. 2Wakati mtakapokaribia kwenda vitani, kuhani atakuja mbele na kuhutubia jeshi. 320:3 1Sam 17:32; Ay 23:16; Za 22:14; Isa 7:4; 35:4; Yer 51:46Atasema: “Sikia, ee Israeli, leo unakwenda vitani kupigana na adui zako. Usife moyo wala usiogope, usitishwe wala usitiwe hofu mbele yao. 420:4 2Nya 20:14-22; Kut 14:14; 1Nya 5:22; Neh 4:20; Amu 12:3; 15:18; Za 44:7; 144:10; Kum 1:30Kwa kuwa Bwana Mungu wenu ndiye huenda pamoja nanyi kuwapigania dhidi ya adui zenu na kuwapatia ushindi.”

520:5 Neh 12:27Maafisa wataliambia jeshi: “Je, kuna yeyote aliyejenga nyumba mpya ambayo haijawekwa wakfu? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akaiweka wakfu. 620:6 Yer 31:5; Eze 28:26; Mik 1:6; 1Kor 9:7Je, kuna yeyote aliyepanda shamba la mizabibu na hajaanza kulifurahia? Yeye na arudi nyumbani, au sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akalifurahia. 720:7 Kum 24:5; Mit 5:18Je, kuna yeyote aliyeposa mwanamke na hajamwoa? Yeye na arudi nyumbani, ama sivyo anaweza kufa vitani na mtu mwingine akamwoa.” 820:8 Amu 7:3Kisha maafisa wataongeza haya, “Je, kuna mtu anayeogopa ama kufa moyo? Yeye na arudi nyumbani ili ndugu zake nao wasije wakafa moyo pia.” 9Wakati maafisa watakapomaliza kuzungumza na jeshi, watawateua wakuu wa vikosi.

1020:10 Kum 2:26; Lk 14:31-32; 2Sam 20:18-20Wakati mtakapokwenda kushambulia mji, wapeni watu wake masharti ya amani. 1120:11 2Fal 6:22; 1Fal 9:21; 1Nya 22:2; Isa 31:7Wakikubali na kuwafungulia malango yao, watu wake wote watawatumikia kwa kufanya kazi ngumu na watawatumikia. 12Ikiwa watakataa kufanya mapatano ya amani na wakiwaingiza katika vita, basi mtauzunguka mji huo kwa vita. 1320:13 Hes 31:7Wakati Bwana Mungu wenu atakapouweka mji huo mkononi mwenu, waueni kwa upanga wanaume wote waliomo ndani yake. 1420:14 Yos 8:2; 22:8; Hes 31:11; 31:53Kwa upande wa wanawake, watoto, mifugo na kila kitu kingine chochote ndani ya huo mji, mnaweza kuvichukua kama nyara kwa ajili yenu. Nanyi mnaweza kuzitumia hizo nyara ambazo Bwana Mungu wenu amewapa kutoka kwa adui zenu. 1520:15 Yos 9:9Hivi ndivyo mtakavyofanya kwa miji yote ambayo iko mbali nanyi, ambayo haimilikiwi na mataifa ya karibu.

1620:16 Kut 23:31-33; Hes 21:2-3; Kum 7:2; Yos 6:21; 10:1; 11:14Hata hivyo, katika miji ya mataifa ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi, msiache kitu chochote hai kinachopumua. 17Waangamizeni kabisa Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi, kama Bwana Mungu wenu alivyowaamuru. 1820:18 Kut 34:16; 10:7; 23:33; Kum 12:30-31; Yos 23:12-13; 1Kor 15:33; 2Fal 21:3, 15; Za 106:34-41; Hos 8:11La sivyo, watawafundisha kufuata mambo yote ya machukizo wanayofanya wakiabudu miungu yao, nanyi mtatenda dhambi dhidi ya Bwana Mungu wenu.

19Wakati mtakapouzunguka mji kwa vita kwa muda mrefu, mkipigana dhidi yake ili kuuteka, msiharibu miti yake kwa kuikata kwa shoka, kwa sababu mtaweza kula matunda yake. Hivyo msiikate. Je, miti hiyo ya mashambani ni watu, hata muizingire? 20Hata hivyo, mnaweza kuikata miti ambayo sio miti ya matunda na kuitumia kujenga ngome, mpaka mji ulio katika vita na ninyi utakapoanguka.

King James Version

Deuteronomy 20:1-20

1When thou goest out to battle against thine enemies, and seest horses, and chariots, and a people more than thou, be not afraid of them: for the LORD thy God is with thee, which brought thee up out of the land of Egypt. 2And it shall be, when ye are come nigh unto the battle, that the priest shall approach and speak unto the people, 3And shall say unto them, Hear, O Israel, ye approach this day unto battle against your enemies: let not your hearts faint, fear not, and do not tremble, neither be ye terrified because of them;20.3 faint: Heb. be tender20.3 tremble: Heb. make haste 4For the LORD your God is he that goeth with you, to fight for you against your enemies, to save you.

5¶ And the officers shall speak unto the people, saying, What man is there that hath built a new house, and hath not dedicated it? let him go and return to his house, lest he die in the battle, and another man dedicate it. 6And what man is he that hath planted a vineyard, and hath not yet eaten of it? let him also go and return unto his house, lest he die in the battle, and another man eat of it.20.6 eaten…: Heb. made it common 7And what man is there that hath betrothed a wife, and hath not taken her? let him go and return unto his house, lest he die in the battle, and another man take her. 8And the officers shall speak further unto the people, and they shall say, What man is there that is fearful and fainthearted? let him go and return unto his house, lest his brethren’s heart faint as well as his heart.20.8 faint: Heb. melt 9And it shall be, when the officers have made an end of speaking unto the people, that they shall make captains of the armies to lead the people.20.9 to lead…: Heb. to be in the head of the people

10¶ When thou comest nigh unto a city to fight against it, then proclaim peace unto it. 11And it shall be, if it make thee answer of peace, and open unto thee, then it shall be, that all the people that is found therein shall be tributaries unto thee, and they shall serve thee. 12And if it will make no peace with thee, but will make war against thee, then thou shalt besiege it: 13And when the LORD thy God hath delivered it into thine hands, thou shalt smite every male thereof with the edge of the sword: 14But the women, and the little ones, and the cattle, and all that is in the city, even all the spoil thereof, shalt thou take unto thyself; and thou shalt eat the spoil of thine enemies, which the LORD thy God hath given thee.20.14 take: Heb. spoil 15Thus shalt thou do unto all the cities which are very far off from thee, which are not of the cities of these nations. 16But of the cities of these people, which the LORD thy God doth give thee for an inheritance, thou shalt save alive nothing that breatheth: 17But thou shalt utterly destroy them; namely, the Hittites, and the Amorites, the Canaanites, and the Perizzites, the Hivites, and the Jebusites; as the LORD thy God hath commanded thee: 18That they teach you not to do after all their abominations, which they have done unto their gods; so should ye sin against the LORD your God.

19¶ When thou shalt besiege a city a long time, in making war against it to take it, thou shalt not destroy the trees thereof by forcing an axe against them: for thou mayest eat of them, and thou shalt not cut them down (for the tree of the field is man’s life) to employ them in the siege:20.19 for the…: or, for, O man, the tree of the field is to be employed in the siege20.19 to employ…: Heb. to go from before thee 20Only the trees which thou knowest that they be not trees for meat, thou shalt destroy and cut them down; and thou shalt build bulwarks against the city that maketh war with thee, until it be subdued.20.20 it…: Heb. it come down