Kumbukumbu 19 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Kumbukumbu 19:1-21

Miji Ya Makimbilio

(Hesabu 35:9-34; Yoshua 20:1-9)

119:1 Kum 6:10-11; 12:29Wakati Bwana Mungu wenu atakapokuwa amewaangamiza mataifa ambayo nchi yao anawapa ninyi, wakati mtakapokuwa mmewafukuza na kuishi katika miji yao na nyumba zao, 219:2 Yos 20:2ndipo mtenge miji mitatu iliyopo katikati ya nchi kwa ajili yenu, katika nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kuimiliki. 3Jengeni barabara katika miji hiyo na kuigawa mara tatu, nchi anayowapa Bwana Mungu wenu kama urithi, ili kwamba yeyote amuuaye mtu aweze kukimbilia humo.

4Hii ndiyo kanuni kuhusu mtu amuuaye mwingine na kukimbilia humo kuokoa maisha yake, yaani, yeye amuuaye jirani yake bila kukusudia, wala hakumchukia kabla ya hapo. 5Kwa mfano, mtu aweza kwenda msituni na jirani yake kukata miti, naye anapozungusha shoka kuangusha mti, shoka linaweza kuchomoka kutoka kwenye mpini na kumpiga jirani yake na kumuua. Yule mtu anaweza kukimbilia katika mmojawapo ya miji hii na kuokoa maisha yake. 619:6 Hes 35:12Kama sivyo, mlipiza kisasi cha damu anaweza kumfuatilia kwa hasira kali, naye akamkamata na kumuua kama umbali ni mrefu sana hata ingawa hastahili kifo, kwa sababu amemuua jirani yake bila kukusudia. 7Hii ndiyo sababu nimewaagiza ninyi kutenga miji mitatu ya makimbilio kwa ajili yenu.

819:8 Kut 34:24; Mwa 15:18; Kum 11:24Kama Bwana Mungu wenu akipanua nchi yenu, kama alivyoahidi kwa kiapo kwa baba zenu na kuwapa nchi yote aliyowaahidi, 919:9 Kum 6:5; Yos 20:7-8kwa sababu mmefuata kwa uangalifu sheria zote ninazowaamuru leo, kumpenda Bwana Mungu wenu na kuenenda siku zote katika njia zake, ndipo mtenge miji mingine, mitatu zaidi. 1019:10 Mit 6:17; Yer 7:6; 26:15; Kum 21:1-9; Hes 35:33Fanyeni hivi ili damu isiyo na hatia isimwagwe katika nchi yenu, ambayo Bwana Mungu wenu anawapa kama urithi wenu, ili kwamba msije mkawa na hatia ya kumwaga damu.

1119:11 Kut 21:12; Hes 35:16; 1Yn 3:15; Mit 28:17; 29:10Lakini kama mtu anamchukia ndugu yake, akamvizia, akamshambulia na kumuua, kisha akakimbilia katika mmojawapo ya miji hii, 12wazee wa mji wake watatuma ujumbe kwake, kumleta kutoka mji ule na kumkabidhi mlipiza kisasi cha damu kumuua. 1319:13 Kum 7:2; 21:9; 1Fal 2:31Msimwonee huruma. Lazima mwondoe katika Israeli hatia ya umwagaji damu isiyo na hatia ili kwamba mpate kufanikiwa.

1419:14 Kum 27:17; Ay 24:2; Za 16:6; Mit 15:25; 22:28; 23:10; Isa 1:23; Hos 5:10Usisogeze jiwe la mpaka wa jirani yako ambao uliwekwa na wale waliokutangulia katika urithi upokeao katika nchi Bwana Mungu wako anayowapa kuimiliki.

Mashahidi

1519:15 Kum 17:6; Mt 18:16; 26:60; 2Kor 3:1; Yn 8:17; 1Tim 5:19; Ebr 10:28Shahidi mmoja hatoshi kumtia hatiani mtu kwa uhalifu au kosa lolote ambalo anaweza kuwa amelitenda. Lazima shauri lolote lithibitishwe kwa ushuhuda wa mashahidi wawili au watatu.

1619:16 Kut 23:1; Mit 6:19; Za 27:12; 1Fal 21:13Kama shahidi mwenye nia ya kumdhuru mwingine akisimama kumshtaki mtu kwa uhalifu, 1719:17 Kut 21:6; Kum 17:6watu wawili wanaohusika katika mabishano lazima wasimame mbele za Bwana na mbele ya makuhani na waamuzi ambao wako kazini wakati huo. 1819:18 Kut 23:7Waamuzi lazima wafanye uchunguzi kwa makini na shahidi akionekana kuwa ni mwongo, akitoa ushuhuda wa uongo dhidi ya ndugu yake, 1919:19 Mit 19:5-10; 1Kor 5:13; Dan 6:24basi mtende kama alivyotaka kumtendea ndugu yake. Ni lazima mwondoe uovu miongoni mwenu. 2019:20 Kum 13:11; 17:13; 13:13; 21:21Watu watakaosalia watasikia hili na kuogopa, uovu kama huo kamwe hautatendeka tena miongoni mwenu. 2119:21 Kut 21:24; Mt 5:38Msionyeshe huruma, uhai kwa uhai, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu.

King James Version

Deuteronomy 19:1-21

1When the LORD thy God hath cut off the nations, whose land the LORD thy God giveth thee, and thou succeedest them, and dwellest in their cities, and in their houses;19.1 succeedest: Heb. inheritest, or, possessest 2Thou shalt separate three cities for thee in the midst of thy land, which the LORD thy God giveth thee to possess it. 3Thou shalt prepare thee a way, and divide the coasts of thy land, which the LORD thy God giveth thee to inherit, into three parts, that every slayer may flee thither.

4¶ And this is the case of the slayer, which shall flee thither, that he may live: Whoso killeth his neighbour ignorantly, whom he hated not in time past;19.4 in…: Heb. from yesterday the third day 5As when a man goeth into the wood with his neighbour to hew wood, and his hand fetcheth a stroke with the axe to cut down the tree, and the head slippeth from the helve, and lighteth upon his neighbour, that he die; he shall flee unto one of those cities, and live:19.5 head: Heb. iron19.5 helve: Heb. wood19.5 lighteth…: Heb. findeth 6Lest the avenger of the blood pursue the slayer, while his heart is hot, and overtake him, because the way is long, and slay him; whereas he was not worthy of death, inasmuch as he hated him not in time past.19.6 slay…: Heb. smite him in life19.6 in…: Heb. from yesterday the third day 7Wherefore I command thee, saying, Thou shalt separate three cities for thee. 8And if the LORD thy God enlarge thy coast, as he hath sworn unto thy fathers, and give thee all the land which he promised to give unto thy fathers; 9If thou shalt keep all these commandments to do them, which I command thee this day, to love the LORD thy God, and to walk ever in his ways; then shalt thou add three cities more for thee, beside these three: 10That innocent blood be not shed in thy land, which the LORD thy God giveth thee for an inheritance, and so blood be upon thee.

11¶ But if any man hate his neighbour, and lie in wait for him, and rise up against him, and smite him mortally that he die, and fleeth into one of these cities:19.11 mortally: Heb. in life 12Then the elders of his city shall send and fetch him thence, and deliver him into the hand of the avenger of blood, that he may die. 13Thine eye shall not pity him, but thou shalt put away the guilt of innocent blood from Israel, that it may go well with thee.

14¶ Thou shalt not remove thy neighbour’s landmark, which they of old time have set in thine inheritance, which thou shalt inherit in the land that the LORD thy God giveth thee to possess it.

15¶ One witness shall not rise up against a man for any iniquity, or for any sin, in any sin that he sinneth: at the mouth of two witnesses, or at the mouth of three witnesses, shall the matter be established.

16¶ If a false witness rise up against any man to testify against him that which is wrong;19.16 that…: or, falling away 17Then both the men, between whom the controversy is, shall stand before the LORD, before the priests and the judges, which shall be in those days; 18And the judges shall make diligent inquisition: and, behold, if the witness be a false witness, and hath testified falsely against his brother; 19Then shall ye do unto him, as he had thought to have done unto his brother: so shalt thou put the evil away from among you. 20And those which remain shall hear, and fear, and shall henceforth commit no more any such evil among you. 21And thine eye shall not pity; but life shall go for life, eye for eye, tooth for tooth, hand for hand, foot for foot.