Jina Jipya La Sayuni
1Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza,
kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia,
mpaka haki yake itakapoangaza kama mapambazuko,
wokovu wake kama mwanga wa moto.
262:2 Isa 1:26; Za 67:2; Ufu 3:12; Mwa 32:28; Ufu 2:7; Es 4:14; Za 50:12Mataifa wataona haki yako,
nao wafalme wote wataona utukufu wako;
wewe utaitwa kwa jina jipya
lile ambalo kinywa cha Bwana kitatamka.
362:3 Zek 9:16; 1The 2:19; Isa 28:5Utakuwa taji ya fahari mkononi mwa Bwana,
taji ya kifalme mkononi mwa Mungu wako.
462:4 Law 26:43; 1Pet 2:10; Hos 2:19; Yer 3:14; Sef 3:17; Mal 3:12; Isa 6:12; 54:6Hawatakuita tena Aliyeachwa,
wala nchi yako kuiita Ukiwa.
Bali utaitwa Hefsiba,62:4 Hefsiba maana yake Yeye ninayemfurahia.
nayo nchi yako itaitwa Beula,62:4 Beula maana yake Aliyeolewa.
kwa maana Bwana atakufurahia,
nayo nchi yako itaolewa.
562:5 Kum 28:63; Wim 3:11; Isa 65:19; Yer 31:12; Sef 3:17Kama vile kijana aoavyo mwanamwali,
ndivyo wanao62:5 Au: wajenzi wako. watakavyokuoa wewe;
kama bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi wake,
ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.
662:6 Eze 3:17; Ebr 13:17; Isa 52:8; Za 132:4Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, ee Yerusalemu,
hawatanyamaza mchana wala usiku.
Ninyi wenye kumwita Bwana,
msitulie,
762:7 Mt 15:21-28; Sef 3:20; Lk 18:1-8; Isa 60:18; Kum 26:19msimwache apumzike hadi atakapoufanya imara Yerusalemu
na kuufanya uwe sifa ya dunia.
862:8 Kum 28:30-33; Yer 5:17; Mwa 22:16; Isa 14:25; 49:18Bwana ameapa kwa mkono wake wa kuume
na kwa mkono wake wenye nguvu:
“Kamwe sitawapa tena adui zenu
nafaka zenu kama chakula chao;
kamwe wageni hawatakunywa tena
divai mpya ambayo mmeitaabikia,
9lakini wale waivunao nafaka wataila
na kumsifu Bwana,
nao wale wakusanyao zabibu watainywa divai yake
katika nyua za patakatifu pangu.”
1062:10 Isa 11:10-16; 57:14; Za 24:7; Isa 60:11Piteni, piteni katika malango!
Tengenezeni njia kwa ajili ya watu.
Jengeni, jengeni njia kuu!
Ondoeni mawe.
Inueni bendera kwa ajili ya mataifa.
1162:11 Amo 9:14; Kum 12:7; Yoe 2:26; Isa 1:10Bwana ametoa tangazo
mpaka miisho ya dunia:
“Mwambie Binti Sayuni,
‘Tazama, mwokozi wako anakuja!
Tazama ujira wake uko pamoja naye,
na malipo yake yanafuatana naye!’ ”
1262:12 Za 9:14; Mt 21:5; Isa 35:4; Ufu 22:12; Kum 30:4; Zek 9:9; Isa 40:10Wataitwa Watu Watakatifu,
Waliokombolewa na Bwana;
nawe utaitwa Aliyetafutwa,
Mji Usioachwa Tena.
시온의 영광과 새 이름
1시온의 의가 밝게 비치고 예루살렘의 구원이 횃불처럼 타오를 때까지 내가 잠잠하지 않으며 침묵을 지키지 않을 것이다.
2예루살렘아, 모든 민족이 너의 62:2 또는 ‘공의를’구원을 볼 것이며 세상의 모든 왕들이 너의 영광을 볼 것이다. 너는 여호와께서 주신 새 이름으로 불려질 것이며
3여호와를 위한 아름다운 면류관이 될 것이다.
4사람들이 다시는 너를 버려진 땅이나 황무지라고 부르지 않고 하나님이 기뻐하신다는 뜻으로 ‘헵시바’, 결혼을 했다는 뜻으로 ‘라’ 라 부를 것이다. 이것은 여호와께서 너를 기쁘게 여기실 것이며 그가 너에게 결혼한 남편과 같을 것이기 때문이다.
5젊은 남자가 처녀와 결혼하듯이 62:5 원문에는 ‘네 아들들이’너를 세운 자가 너와 결혼할 것이며 신랑이 신부를 보고 기뻐하듯 네 하나님이 너를 보고 기뻐하실 것이다.
6예루살렘아, 내가 네 성벽 위에 파수꾼을 세웠으니 그들은 밤낮 잠잠하지 않을 것이다. 여호와를 부르는 자들아, 너희는 쉬지 말며
7여호와께서 예루살렘을 복구하여 온 세상이 찬양하는 도시로 만드실 때까지 그를 쉬지 못하시게 하라.
8여호와께서 능력의 팔인 오른손으로 맹세하셨다. “내가 다시는 네 곡식을 네 원수들의 양식으로 주지 않겠다. 네가 수고하여 얻은 포도주를 다시는 외국인들이 마시지 못할 것이며
9곡식을 추수한 자들이 그것을 먹고 나 여호와를 찬양할 것이요 포도를 거둔 자들이 내 성전 뜰에서 포도주를 마실 것이다.”
10예루살렘 사람들아, 성 밖으로 나가서 돌아오는 네 백성을 위해 길을 예비하라. 대로를 닦고 돌을 제거하라. 온 세계가 알 수 있도록 기를 세워라.
11여호와께서 온 세상에 선포하신다. “너희는 예루살렘 주민에게 나 여호와가 그들을 구원하러 간다고 말하며 그들에게 줄 선물을 가지고 간다고 말하라.”
12사람들은 그들을 ‘하나님의 거룩한 백성’, ‘여호와께서 구원하신 백성’ 이라 부를 것이며 예루살렘을 ‘하나님이 사랑하시는 도시’, ‘하나님이 버리지 않은 도시’ 라 부를 것이다.