Isaya 62 – Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu) NEN

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 62:1-12

Jina Jipya La Sayuni

1Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza,

kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia,

mpaka haki yake itakapoangaza kama mapambazuko,

wokovu wake kama mwanga wa moto.

262:2 Isa 1:26; Za 67:2; Ufu 3:12; Mwa 32:28; Ufu 2:7; Es 4:14; Za 50:12Mataifa wataona haki yako,

nao wafalme wote wataona utukufu wako;

wewe utaitwa kwa jina jipya

lile ambalo kinywa cha Bwana kitatamka.

362:3 Zek 9:16; 1The 2:19; Isa 28:5Utakuwa taji ya fahari mkononi mwa Bwana,

taji ya kifalme mkononi mwa Mungu wako.

462:4 Law 26:43; 1Pet 2:10; Hos 2:19; Yer 3:14; Sef 3:17; Mal 3:12; Isa 6:12; 54:6Hawatakuita tena Aliyeachwa,

wala nchi yako kuiita Ukiwa.

Bali utaitwa Hefsiba,62:4 Hefsiba maana yake Yeye ninayemfurahia.

nayo nchi yako itaitwa Beula,62:4 Beula maana yake Aliyeolewa.

kwa maana Bwana atakufurahia,

nayo nchi yako itaolewa.

562:5 Kum 28:63; Wim 3:11; Isa 65:19; Yer 31:12; Sef 3:17Kama vile kijana aoavyo mwanamwali,

ndivyo wanao62:5 Au: wajenzi wako. watakavyokuoa wewe;

kama bwana arusi amfurahiavyo bibi arusi wake,

ndivyo Mungu wako atakavyokufurahia wewe.

662:6 Eze 3:17; Ebr 13:17; Isa 52:8; Za 132:4Nimeweka walinzi juu ya kuta zako, ee Yerusalemu,

hawatanyamaza mchana wala usiku.

Ninyi wenye kumwita Bwana,

msitulie,

762:7 Mt 15:21-28; Sef 3:20; Lk 18:1-8; Isa 60:18; Kum 26:19msimwache apumzike hadi atakapoufanya imara Yerusalemu

na kuufanya uwe sifa ya dunia.

862:8 Kum 28:30-33; Yer 5:17; Mwa 22:16; Isa 14:25; 49:18Bwana ameapa kwa mkono wake wa kuume

na kwa mkono wake wenye nguvu:

“Kamwe sitawapa tena adui zenu

nafaka zenu kama chakula chao;

kamwe wageni hawatakunywa tena

divai mpya ambayo mmeitaabikia,

9lakini wale waivunao nafaka wataila

na kumsifu Bwana,

nao wale wakusanyao zabibu watainywa divai yake

katika nyua za patakatifu pangu.”

1062:10 Isa 11:10-16; 57:14; Za 24:7; Isa 60:11Piteni, piteni katika malango!

Tengenezeni njia kwa ajili ya watu.

Jengeni, jengeni njia kuu!

Ondoeni mawe.

Inueni bendera kwa ajili ya mataifa.

1162:11 Amo 9:14; Kum 12:7; Yoe 2:26; Isa 1:10Bwana ametoa tangazo

mpaka miisho ya dunia:

“Mwambie Binti Sayuni,

‘Tazama, mwokozi wako anakuja!

Tazama ujira wake uko pamoja naye,

na malipo yake yanafuatana naye!’ ”

1262:12 Za 9:14; Mt 21:5; Isa 35:4; Ufu 22:12; Kum 30:4; Zek 9:9; Isa 40:10Wataitwa Watu Watakatifu,

Waliokombolewa na Bwana;

nawe utaitwa Aliyetafutwa,

Mji Usioachwa Tena.