Isaya 2 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 2:1-22

Mlima Wa Bwana

(Mika 4:1-3)

12:1 Isa 1:1Hili ndilo aliloliona Isaya mwana wa Amozi kuhusu Yuda na Yerusalemu:

22:2 Dan 2:35; 11:45; Yoe 3:17; Mdo 2:17; Isa 11:9; 65:9; Zek 14:10; Yer 16:19Katika siku za mwisho

mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa

kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote,

utainuliwa juu ya vilima,

na mataifa yote yatamiminika huko.

32:3 Zek 8:21; Lk 24:47; Yn 4:22; Isa 33:22; 45:23; Yer 3:17; Kum 33:19Mataifa mengi yatakuja na kusema,

“Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana,

kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.

Atatufundisha njia zake,

ili tuweze kuenenda katika mapito yake.”

Sheria itatoka Sayuni,

neno la Bwana litatoka Yerusalemu.

42:4 Hos 2:18; Yer 30:11; Za 96:13; 51:4; 46:9; Yoe 3:10; Mwa 49:10; Zek 9:10Atahukumu kati ya mataifa

na ataamua migogoro ya mataifa mengi.

Watafua panga zao ziwe majembe,

na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi.

Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine,

wala hawatajifunza vita tena.

52:5 Isa 60:19-20; 1Yn 1:5-7; Isa 58:1; 60:1Njooni, enyi nyumba ya Yakobo,

tutembeeni katika nuru ya Bwana.

Siku Ya Bwana

62:6 Kum 18:10, 14; 31:17; Yer 12:7; 2Nya 16:7; Isa 44:25; 2Fal 16:7; Kum 31:17Umewatelekeza watu wako,

nyumba ya Yakobo.

Wamejaa ushirikina utokao Mashariki,

wanapiga ramli kama Wafilisti

na wanashikana mikono na wapagani.

72:7 Mwa 41:43; Kum 17:16; Mik 5:10; Za 17:14; Isa 31:1; Kum 17:17Nchi yao imejaa fedha na dhahabu,

hakuna mwisho wa hazina zao.

Nchi yao imejaa farasi,

hakuna mwisho wa magari yao.

82:8 Isa 10:9-11; 17:8; 44:17; Ufu 9:20; 2Nya 32:19; Mik 5:13; Isa 44:17; Za 135:15Nchi yao imejaa sanamu,

wanasujudia kazi za mikono yao,

vitu vile vidole vyao vimevitengeneza.

92:9 Za 62:9; Isa 13:11; 5:15; 2:11, 17; Hes 4:5; Neh 4:5Kwa hiyo mwanadamu atashushwa

na binadamu atanyenyekezwa:

usiwasamehe.

102:10 Ufu 6:15-16; Nah 3:11; Za 145:12; Isa 2:19; 2The 1:9Ingieni kwenye miamba,

jificheni ardhini

kutokana na utisho wa Bwana

na utukufu wa enzi yake!

112:11 Isa 24:21-23; 37:23; 10:12; 5:15; Eze 31:10; Oba 1:8; Neh 9:29; Ay 40:11; Za 46:10; Hab 2:5Macho ya mtu mwenye majivuno yatanyenyekezwa

na kiburi cha wanadamu kitashushwa,

Bwana peke yake ndiye atakayetukuzwa siku hiyo.

122:12 Za 76:12; 59:12; Eze 7:7; Ay 40:11; Isa 13:6-9; 34:8; Yer 30:7; Mao 1:12; 2Sam 22:28; Yoe 1:15; Amo 5:18Bwana Mwenye Nguvu Zote anayo siku aliyoiweka akiba

kwa wote wenye kujivuna na wenye kiburi,

kwa wote wanaojikweza

(nao watanyenyekezwa),

132:13 Amu 9:15; Isa 10:33, 34; 29:17; Eze 27:5; Za 22:12; Zek 11:2kwa mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu sana,

na mialoni yote ya Bashani,

142:14 Isa 30:25; 40:4kwa milima yote mirefu

na vilima vyote vilivyoinuka,

152:15 Isa 25:2, 12; 30:25; 32:14; 33:18; Sef 1:16kwa kila mnara ulio mrefu sana

na kila ukuta wenye ngome,

162:16 Mwa 10:4; 1Fal 10:22; 9:26kwa kila meli ya biashara,2:16 Au: ya Tarshishi (ona pia 1Fal 10:22; 22:48; 2Nya 9:21; 20:36; Isa 60:9.)

na kila chombo cha baharini cha fahari.

172:17 2Sam 22:28; Ay 40:112:17 Nah 3:13; Ebr 10:31; Kum 2:25; Isa 11:10, 15Majivuno ya mwanadamu yatashushwa,

na kiburi cha wanadamu kitanyenyekezwa,

Bwana peke yake ndiye atatukuzwa siku hiyo,

182:18 Kum 9:21; Mik 5:13; Eze 36:25; Isa 21:9; Yer 10:11; 1Sam 5:2nazo sanamu zitatoweka kabisa.

192:19 Hos 10:8; Nah 1:3-6; Ay 9:6; 30:9; Ebr 12:26; Hab 3:6; Amu 6:2; Isa 7:19; 14:16; Ay 30:6; Lk 23:30; Ufu 6:15Watu watakimbilia kwenye mapango ndani ya miamba,

na kwenye mahandaki ardhini

kutokana na utisho wa Bwana

na utukufu wa enzi yake,

ainukapo kuitikisa dunia.

202:20 Law 11:19; Eze 36:25; 7:19-20; 14:6; Ufu 9:20; Isa 2:11; Ay 22:24Siku ile, watu watawatupia

panya na popo

sanamu zao za fedha na za dhahabu,

walizozitengeneza ili waziabudu.

212:21 Kut 33:22; Za 145:12; Isa 33:10; 2:19Watakimbilia kwenye mapango miambani

na kwenye nyufa za miamba

kutokana na utisho wa Bwana

na utukufu wa enzi yake,

ainukapo kuitikisa dunia.

222:22 Mit 23:4; Yer 17:5; Yak 4:14; Ay 12:19; Za 119:8-9; Isa 51:12; 40:15; Za 18:42; 118:6, 8; 146:3Acheni kumtumainia mwanadamu,

ambaye hana kitu ila pumzi katika pua zake.

Yeye ana thamani gani?

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以赛亚书 2:1-22

主必统治万邦

1亚摩斯的儿子以赛亚看到以下有关犹大耶路撒冷的异象。

2在末后的日子,耶和华殿所在的山必耸立,

高过群山,超过万岭,

万族都要涌向它。

3众民都必来,说:

“来吧!让我们登耶和华的山,

雅各之上帝的殿。

祂必将祂的路指示给我们,

使我们走祂的道。”

因为训诲必出于锡安

耶和华的话语必来自耶路撒冷

4祂必在各国施行审判,

为列邦平息纷争。

他们必将刀剑打成犁头,

把矛枪制成镰刀。

国与国不再刀兵相见,

人们不用再学习战事。

5雅各家啊,来吧!

让我们走在耶和华的光中。

耶和华审判的日子

6耶和华啊,你离弃了你的子民——雅各的后裔,

因为他们当中充满了东方的恶俗,

非利士人一样占卜,

跟外族人同流合污。

7他们境内金银遍地,

财宝无穷;

他们境内马匹充裕,

战车无数。

8他们境内偶像林立,

他们跪拜自己用手所造的物品,

跪拜自己用指头所造之物。

9他们必遭羞辱和贬抑。

耶和华啊,

求你不要赦免他们。

10要躲进岩穴,藏入地洞,

逃避耶和华的愤怒和威荣!

11到那日,狂妄的人将被挫败,

骄傲的人将遭贬抑;

唯独耶和华将受尊崇。

12因为万军之耶和华已定了日子,

要惩罚一切骄傲狂妄和自高自大的人,

使他们沦为卑贱;

13祂必毁灭黎巴嫩高大的香柏树和巴珊的橡树,

14毁灭一切崇山峻岭,

15毁灭高耸的城楼和坚固的城墙,

16毁灭他施的商船和一切华美的船只。

17到那日,狂妄的人必被挫败,

骄傲的人必遭贬抑,

唯独耶和华受尊崇。

18偶像必被彻底铲除。

19耶和华使大地震动的时候,

众人躲进岩穴,藏入地洞,

逃避祂的愤怒和威荣。

20到那日,众人必把造来敬拜的金银偶像丢给田鼠和蝙蝠。

21耶和华使大地震动的时候,

众人必躲进山洞和岩缝,

逃避祂的愤怒和威荣。

22不要再倚靠世人,

他们的生命不过是一口气,

他们有什么值得称道的呢?