Hagai 1 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hagai 1:1-15

Wito Wa Kuijenga Nyumba Ya Bwana

11:1 Ezr 4:24; 5:1-3; 2:2; 3:2; 1Nya 3:19; 6:15; Mt 1:12-13Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua1:1 Yoshua kwa Kiebrania ni Yeshua, maana yake ni Yehova ni wokovu. mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:

21:2 Isa 13:4; 29:13Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’ ”

31:3 Ezr 5:1Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai: 41:4 2Sam 7:2; Yer 33:12“Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”

51:5 Mao 3:40; Hag 2:15-18Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu. 61:6 Law 26:20; Isa 5:10; 9:20; 55:2; Amo 4:8; Hag 2:16; Zek 8:10Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”

7Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu. 81:8 Ay 22:3; Yer 13:11; 1Nya 14:1; Za 132:13-14; Kut 29:43Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana. 91:9 Kum 28:38; Isa 5:10; Neh 13:11; Za 103:16; Eze 22:21“Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe. 101:10 Kum 28:24; Mwa 27:28; 1Fal 17:1; 2Nya 6:26; Yer 3:3; Law 26:19; Yoe 1:18-19Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake. 111:11 Kum 11:26; 28:22; Rut 1:1; 1Fal 17:1; Hag 2:17; Isa 5:6; 7:25; Hes 18:12Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”

121:12 Isa 1:9; 50:10; 55:11; Mt 28:20; Kum 31:12; Hag 2:2; Ezr 5:2; Mhu 12:13; Ay 36:11Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.

131:13 Hes 14:9; 27:21; 2Nya 15:2; 36:15; Mwa 26:3; Rum 8:31; Isa 41:10; Mt 28:20Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana. 141:14 Ezr 5:2; Za 110:3; 2Nya 36:22; Hag 2:21; 1Nya 6:15; 1Kor 15:58Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao, 151:15 Hag 2:10, 20; Ezr 4:24katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.

Korean Living Bible

학개 1:1-15

성전을 지으라는 여호와의 명령

1페르시아의 다리우스황제 2년 6월 일에 여호와께서 예언자 학개를 통하여 스 알디엘의 아들인 유다 총독 스룹바벨과 여호사닥의 아들인 대제사장 여호수아에게 말씀하셨다.

2“전능한 나 여호와가 말한다. 이 백성들이 성전을 건축할 때가 아직 되지 않았다고 말하고 있다.

3여호와께서 다시 예언자 학개를 통하여 말씀하셨다.

4“내 성전은 황폐한 채로 있는데 너희는 호화 주택에 살고 있느냐?

5그러므로 전능한 나 여호와가 말한다. 너희는 자기 소행을 잘 살펴보아라.

6너희가 많이 심었으나 적게 거두었으며 너희가 먹어도 배부르지 않고 마셔도 흡족하지 않으며 입어도 따뜻하지 않고 품삯을 받아도 구멍 뚫린 지갑에 넣는 격이 되었다.

7“전능한 나 여호와가 말한다. 너희는 자기 소행을 잘 살펴보아라.

8너희는 산에 올라가서 목재를 가져다가 성전을 건축하라. 그러면 내가 그것으로 기뻐하고 영광을 얻을 것이다. 이것은 나 여호와의 말이다.

9너희가 많은 수확을 기대했으나 얻은 것은 적었으며 너희가 수확한 것을 집으로 가져갔으나 내가 그것을 날려 버렸다. 그 이유가 무엇이냐? 이것은 내 집이 황폐한데도 너희가 자기 집안 일에만 급급하였기 때문이다.

10그래서 너희 때문에 하늘이 이슬을 내리지 않고 땅에서 농산물이 나지 않게 되었으며

11또 내가 가뭄이 들게 하였으므로 들과 산과 곡식과 새 포도주와 기름과 땅의 모든 농산물과 사람과 짐승과 애써 수고한 모든 것이 피해를 입게 되었다.”

백성들의 순종

12그때 스알디엘의 아들 스룹바벨과 여호사닥의 아들인 대제사장 여호수아와 남은 모든 백성이 예언자 학개가 전한 여호와의 말씀에 순종하였다. 이것은 그들의 하나님 여호와께서 학개를 보내셨기 때문이었다. 그래서 백성들은 여호와를 두려워하였다.

13그때 학개는 “내가 너희와 함께한다” 는 여호와의 말씀을 백성들에게 전하였다.

14여호와께서 스알디엘의 아들인 유다 총독 스룹바벨과 여호사닥의 아들인 대제사장 여호수아와 그리고 남아 있는 모든 백성의 마음을 감동시키시므로 그들이 자기들의 하나님, 전능하신 여호와의 성전을 재건하기 시작했는데

15그때는 다리우스황제 2년 6월 24일이었다.