Ezekieli 35 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 35:1-15

Unabii Dhidi Ya Edomu

1Neno la Bwana likanijia kusema: 235:2 Mwa 14:6; Kum 2:5; Yer 49:7-8; Amo 1:11“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake 335:3 Yer 6:12; Eze 34:10; 25:12-14; Oba 1:10na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika. 435:4 Yer 49:10; 44:2Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

535:5 Za 137:7; Eze 21:29; Za 63:10; Oba 1:13“ ‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake, 635:6 Isa 63:2-6; 34:3kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia. 735:7 Yer 46:19; 49:17Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda. 835:8 Eze 31:12Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote. 935:9 Isa 34:5-6; Yer 49:13-17; Oba 1:10Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

1035:10 Za 83:12; Eze 36:2-5“ ‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko, 1135:11 Eze 25:14; Oba 1:15; Mt 7:2; Isa 26:9; Za 9:16kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu. 1235:12 Yer 50:7; Za 9:16Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.” 1335:13 Dan 11:36; Yer 49:16Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia. 1435:14 Yer 51:48Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa. 1535:15 Mit 17:5; Eze 36:5; Oba 1:12; Mao 4:4-21; Yer 50:11-13; Isa 34:5-6; Eze 32:29Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’ ”

New International Version – UK

Ezekiel 35:1-15

A prophecy against Edom

1The word of the Lord came to me: 2‘Son of man, set your face against Mount Seir; prophesy against it 3and say: “This is what the Sovereign Lord says: I am against you, Mount Seir, and I will stretch out my hand against you and make you a desolate waste. 4I will turn your towns into ruins and you will be desolate. Then you will know that I am the Lord.

5‘ “Because you harboured an ancient hostility and delivered the Israelites over to the sword at the time of their calamity, the time their punishment reached its climax, 6therefore as surely as I live, declares the Sovereign Lord, I will give you over to bloodshed and it will pursue you. Since you did not hate bloodshed, bloodshed will pursue you. 7I will make Mount Seir a desolate waste and cut off from it all who come and go. 8I will fill your mountains with the slain; those killed by the sword will fall on your hills and in your valleys and in all your ravines. 9I will make you desolate for ever; your towns will not be inhabited. Then you will know that I am the Lord.

10‘ “Because you have said, ‘These two nations and countries will be ours and we will take possession of them,’ even though I the Lord was there, 11therefore as surely as I live, declares the Sovereign Lord, I will treat you in accordance with the anger and jealousy you showed in your hatred of them and I will make myself known among them when I judge you. 12Then you will know that I the Lord have heard all the contemptible things you have said against the mountains of Israel. You said, ‘They have been laid waste and have been given over to us to devour.’ 13You boasted against me and spoke against me without restraint, and I heard it. 14This is what the Sovereign Lord says: while the whole earth rejoices, I will make you desolate. 15Because you rejoiced when the inheritance of Israel became desolate, that is how I will treat you. You will be desolate, Mount Seir, you and all of Edom. Then they will know that I am the Lord.” ’