Ezekieli 34 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 34:1-31

Wachungaji Na Kondoo

1Neno la Bwana likanijia kusema: 234:2 Mik 3:11; Yud 12; Yer 3:15; Isa 40:11; Za 78:70-72; Yn 21:15-17“Mwanadamu, tabiri juu ya wachungaji wa Israeli, tabiri na uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ole wa wachungaji wa Israeli ambao hujitunza wenyewe tu! Je, haiwapasi wachungaji kutunza kundi la kondoo? 334:3 Amo 6:4; Zek 11:5; Eze 22:27; Isa 56:11Mnakula mafuta ya wanyama, mnavaa mavazi ya sufu na kuchinja kondoo walionona, lakini hamlitunzi kundi. 434:4 Law 25:43; Mik 3:3; 2Tim 2:24; Mdo 9:36; Isa 3:7; Zek 11:15-17Hamkuwatia nguvu walio dhaifu wala hamkuwaganga wenye maradhi wala kuwafunga waliojeruhiwa. Hamkuwarudisha waliotangatanga wala kuwatafuta wale waliopotea. Badala yake mmewatawala kwa ukali na kwa ukatili. 534:5 Hes 27:17; Isa 56:9; Mdo 20:29Hivyo walitawanyika kwa sababu hapakuwepo mchungaji, nao walipotawanyika, wakawa chakula cha wanyama wa mwitu wote. 634:6 Yer 50:6; Law 26:33; Za 95:10; Yer 10:21; 2Nya 18:16; Za 142:4; Hos 7:13; Mt 9:36; 18:12-13Kondoo wangu walitawanyika, wakatangatanga kwenye milima yote na kwenye kila kilima kirefu. Kondoo wangu walitawanyika juu ya uso wa dunia yote bila kuwa na yeyote wa kuwaulizia wala wa kuwatafuta.

7“ ‘Kwa hiyo, ninyi wachungaji, lisikieni neno la Bwana: 834:8 2Nya 18:16; 1Pet 2:25; Yer 50:6; Za 95:10; Yer 10:21; Hos 7:13; Za 42:4; Mt 18:12-13Kwa hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa sababu kondoo zangu wamekosa mchungaji na hivyo wametekwa nyara na kuwa chakula cha wanyama wote wa mwituni na kwa sababu wachungaji wangu, hawakuwatafuta kondoo zangu, bali wachungaji wamejitunza wenyewe, nao hawakuwalisha kondoo zangu, 934:9 Amu 2:14; Isa 59:6; Yud 12kwa hiyo enyi wachungaji, sikieni neno la Bwana: 1034:10 Yer 21:13; Za 72:14; Yer 23:2; Zek 10:3; 1Sam 2:29-30Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume na wachungaji nami nitawadai kondoo zangu mikononi mwao. Nitawafukuza kutoka kwenye kuchunga kundi langu, ili wachungaji wasiendelee kujitunza wenyewe. Nitaokoa kondoo zangu kutoka kwenye vinywa vyao, nao kondoo hawatakuwa tena chakula chao.

1134:11 Za 119:176“ ‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi mwenyewe nitawaulizia kondoo wangu na kuwatafuta. 1234:12 Zek 10:3; Lk 19:10; Eze 30:3; 32:7; Mdo 2:19-21; Isa 40:11Kama vile mchungaji atafutavyo kundi lake lililotawanyika wakati akiwa pamoja nalo, hivyo ndivyo nitakavyowatafuta kondoo wangu. Nitawaokoa kutoka mahali pote walipokuwa wametawanyikia katika siku ya mawingu na giza nene. 1334:13 Mwa 48:21; Yer 23:3, 8; 50:19; Kum 30:4; Eze 11:17Nitawatoa katika mataifa na kuwakusanya kutoka nchi mbalimbali, nami nitawaleta katika nchi yao wenyewe. Nitawalisha kwenye milima ya Israeli, katika mabonde na mahali pote panapokalika katika nchi. 1434:14 Eze 20:40; 37:22; Za 23:2; 37:3; Isa 65:10; Amo 9:14; Eze 36:29-30Nitawachunga kwenye malisho mazuri na miinuko ya mlima wa Israeli patakuwa mahali pao pa malisho. Huko watajipumzisha kwa amani katika nchi ya malisho mazuri, nao watajilisha huko katika malisho tele katika milima ya Israeli. 1534:15 Sef 3:13; Mik 5:4; Za 23:1-2; Yer 33:12Mimi mwenyewe nitawachunga kondoo zangu na kuwafanya wapumzike, asema Bwana Mwenyezi. 1634:16 Isa 61:1-2; Mik 4:6; Sef 3:19; Yer 31:8; Lk 5:32; Mt 2:17; 15:24Nitawaulizia kondoo waliopotea na kuwaleta waliotangatanga. Nitawafunga waliojeruhiwa na kuwatia nguvu walio dhaifu lakini wale waliojikinai na wenye nguvu nitawaangamiza. Nitalichunga kundi kwa haki.

1734:17 Mt 25:32-33; Eze 20:37“ ‘Kwa habari yenu, enyi kundi langu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo, kati ya kondoo dume na mbuzi. 1834:18 Mwa 30:15; Eze 32:2Je, haiwatoshi ninyi kujilisha kwenye malisho mazuri? Je, ni lazima ninyi kuyakanyaga pia malisho yenu yaliyobaki kwa miguu yenu? Je, haiwatoshi ninyi kunywa maji safi? Je, ni lazima kuyachafua maji mengine kwa miguu yenu? 19Je, ni lazima kundi langu wajilishe kwa yale mliyoyakanyaga na kunywa maji mliyoyachafua kwa miguu yenu?

2034:20 Eze 34:17“ ‘Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi awaambialo: Tazama, mimi mwenyewe nitahukumu kati ya kondoo wanono na waliokonda. 2134:21 Kum 33:17Kwa sababu mmewapiga kikumbo na kuwapiga kwa pembe zenu kondoo wote walio dhaifu mpaka wakawafukuza, 2234:22 Za 72:12-14; Yer 23:2-3; Eze 20:37-38nitaliokoa kundi langu na hawatatekwa nyara tena. Nitahukumu kati ya kondoo na kondoo. 2334:23 Ebr 13:20; Isa 40:11; Eze 37:24; Isa 31:4; Mik 5:4Nitaweka juu yao mchungaji mmoja, mtumishi wangu Daudi, naye atawachunga, atawachunga na kuwa mchungaji wao. 2434:24 Eze 36:28; Yer 33:14; 30:4; Yn 10:16; Kut 29:45; Za 89:49; Isa 53:4; Ufu 7:17Mimi Bwana nitakuwa Mungu wao, naye mtumishi wangu Daudi atakuwa mkuu miongoni mwao. Mimi Bwana nimenena.

2534:25 Law 26:6; 25:18; Hos 2:18; Yer 23:6; Isa 11:6-9; Hes 25:12; Eze 16:62“ ‘Nitafanya nao Agano la amani na kuwaondoa wanyama wa mwitu kutoka nchi yao ili kondoo wangu waweze kupumzika nyikani na msituni kwa salama. 2634:26 Mwa 12:2; Za 68:9; Yoe 2:23; Kum 28:12; 11:13-15Nitawabariki wao pamoja na maeneo yanayozunguka kilima changu. Nitawanyeshea mvua kwa majira yake, kutakuwepo mvua za baraka. 2734:27 Yer 2:20; Law 26:13; Yer 30:8; Eze 20:42; Yer 25:14; Za 72:16; Ay 14:9Miti ya shambani itatoa matunda yake na ardhi itatoa mazao yake, watu watakaa salama katika nchi yao. Watajua kuwa Mimi ndimi Bwana, nitakapovunja vifungo vya nira zao na kuwaokoa kutoka mikono ya wale waliowafanya watumwa. 2834:28 Hos 11:11; Zek 14:11; Amo 9:15; Yer 30:10; 32:37; Eze 28:26; 39:26Hawatatekwa tena nyara na mataifa, wala wanyama pori hawatawala tena. Wataishi kwa salama, wala hakuna yeyote atakayewatia hofu. 2934:29 Isa 4:2; Yoe 2:19; Eze 36:15, 29; Za 137:3Nitawapa nchi yenye sifa kutokana na mazao yake, hawatapatwa na njaa katika nchi tena wala hawatadharauliwa na mataifa. 3034:30 Eze 14:11; 37:27; 2Tim 1:12Ndipo watakapojua kuwa Mimi, Bwana, Mungu wao, niko pamoja nao, na kwamba wao, nyumba ya Israeli, ni watu wangu, asema Bwana Mwenyezi. 3134:31 Za 100:3; Yer 23:1; Za 28:9Ninyi ni kondoo wangu, kondoo wa malisho yangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu, asema Bwana Mwenyezi.’ ”

New International Version – UK

Ezekiel 34:1-31

The Lord will be Israel’s shepherd

1The word of the Lord came to me: 2‘Son of man, prophesy against the shepherds of Israel; prophesy and say to them: “This is what the Sovereign Lord says: woe to you shepherds of Israel who only take care of yourselves! Should not shepherds take care of the flock? 3You eat the curds, clothe yourselves with the wool and slaughter the choice animals, but you do not take care of the flock. 4You have not strengthened the weak or healed those who are ill or bound up the injured. You have not brought back the strays or searched for the lost. You have ruled them harshly and brutally. 5So they were scattered because there was no shepherd, and when they were scattered they became food for all the wild animals. 6My sheep wandered over all the mountains and on every high hill. They were scattered over the whole earth, and no-one searched or looked for them.

7‘ “Therefore, you shepherds, hear the word of the Lord: 8as surely as I live, declares the Sovereign Lord, because my flock lacks a shepherd and so has been plundered and has become food for all the wild animals, and because my shepherds did not search for my flock but cared for themselves rather than for my flock, 9therefore, you shepherds, hear the word of the Lord: 10this is what the Sovereign Lord says: I am against the shepherds and will hold them accountable for my flock. I will remove them from tending the flock so that the shepherds can no longer feed themselves. I will rescue my flock from their mouths, and it will no longer be food for them.

11‘ “For this is what the Sovereign Lord says: I myself will search for my sheep and look after them. 12As a shepherd looks after his scattered flock when he is with them, so will I look after my sheep. I will rescue them from all the places where they were scattered on a day of clouds and darkness. 13I will bring them out from the nations and gather them from the countries, and I will bring them into their own land. I will pasture them on the mountains of Israel, in the ravines and in all the settlements in the land. 14I will tend them in a good pasture, and the mountain heights of Israel will be their grazing land. There they will lie down in good grazing land, and there they will feed in a rich pasture on the mountains of Israel. 15I myself will tend my sheep and make them lie down, declares the Sovereign Lord. 16I will search for the lost and bring back the strays. I will bind up the injured and strengthen the weak, but the sleek and the strong I will destroy. I will shepherd the flock with justice.

17‘ “As for you, my flock, this is what the Sovereign Lord says: I will judge between one sheep and another, and between rams and goats. 18Is it not enough for you to feed on the good pasture? Must you also trample the rest of your pasture with your feet? Is it not enough for you to drink clear water? Must you also muddy the rest with your feet? 19Must my flock feed on what you have trampled and drink what you have muddied with your feet?

20‘ “Therefore this is what the Sovereign Lord says to them: see, I myself will judge between the fat sheep and the lean sheep. 21Because you shove with flank and shoulder, butting all the weak sheep with your horns until you have driven them away, 22I will save my flock, and they will no longer be plundered. I will judge between one sheep and another. 23I will place over them one shepherd, my servant David, and he will tend them; he will tend them and be their shepherd. 24I the Lord will be their God, and my servant David will be prince among them. I the Lord have spoken.

25‘ “I will make a covenant of peace with them and rid the land of savage beasts so that they may live in the wilderness and sleep in the forests in safety. 26I will make them and the places surrounding my hill a blessing.34:26 Or I will cause them and the places surrounding my hill to be named in blessings (see Gen. 48:20); or I will cause them and the places surrounding my hill to be seen as blessed I will send down showers in season; there will be showers of blessing. 27The trees will yield their fruit and the ground will yield its crops; the people will be secure in their land. They will know that I am the Lord, when I break the bars of their yoke and rescue them from the hands of those who enslaved them. 28They will no longer be plundered by the nations, nor will wild animals devour them. They will live in safety, and no-one will make them afraid. 29I will provide for them a land renowned for its crops, and they will no longer be victims of famine in the land or bear the scorn of the nations. 30Then they will know that I, the Lord their God, am with them and that they, the Israelites, are my people, declares the Sovereign Lord. 31You are my sheep, the sheep of my pasture, and I am your God, declares the Sovereign Lord.” ’