Ezekieli 30 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 30:1-26

Maombolezo Kwa Ajili Ya Misri

1Neno la Bwana likanijia kusema: 230:2 Isa 13:6; Yak 5:1“Mwanadamu, toa unabii na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Ombolezeni ninyi na mseme,

“Ole wa siku ile!”

330:3 Oba 1:15; Yoe 2:11; Eze 32:7; 34:12; 7:7; Yoe 1:15Kwa kuwa siku ile imekaribia,

siku ya Bwana imekaribia,

siku ya mawingu,

siku ya maangamizi kwa mataifa.

430:4 Eze 29:19; Yer 50:15; 25:19; Dan 11:43; Mwa 10:6; Eze 29:10Upanga utakuja dhidi ya Misri,

nayo maumivu makuu yataijia Ethiopia.

Mauaji yatakapoangukia Misri,

utajiri wake utachukuliwa

na misingi yake itabomolewa.

530:5 Eze 27:10; Yer 25:20; 2Nya 9:14; Nah 3:9Kushi30:5 Kushi ndiyo Ethiopia. na Putu, Ludi na Arabia yote, Libya30:5 Libya ndiyo Kubu. na watu wa nchi ya Agano watauawa kwa upanga pamoja na Misri.

630:6 Eze 29:10“ ‘Hili ndilo Bwana asemalo:

“ ‘Wale walioungana na Misri wataanguka

na kiburi cha nguvu zake kitashindwa.

Kutoka Migdoli hadi Aswani,

watauawa ndani yake kwa upanga,

asema Bwana Mwenyezi.

730:7 Eze 29:12“ ‘Hizo nchi zitakua ukiwa

miongoni mwa nchi zilizo ukiwa,

nayo miji yao itakuwa magofu

miongoni mwa miji iliyo magofu.

830:8 Yer 49:27; Eze 39:6; Nah 1:6; Eze 29:9Ndipo watakapojua kwamba mimi ndimi Bwana,

nitakapoiwasha Misri moto

na wote wamsaidiao watapondwa.

930:9 Kum 31:6; Mt 10:28; Eze 24:3; 44:630:9 Mwa 10:6; Isa 18:1-2; 23:5; Eze 32:9-10; Sef 2:12“ ‘Siku hiyo wajumbe watatoka kwangu kwa merikebu, ili kuwatia hofu Ethiopia, wakiwa katika hali yao ya kuridhika. Maumivu makali yatawapata siku ya maangamizi ya Misri, kwa kuwa hakika itakuja.

1030:10 Yer 39:1; Eze 29:19“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Nitakomesha makundi ya wajeuri ya Misri

kwa mkono wa Nebukadneza mfalme wa Babeli.

1130:11 Eze 28:7; 29:19Yeye na jeshi lake, taifa lililo katili kuliko mataifa yote,

litaletwa ili kuangamiza nchi.

Watafuta panga zao dhidi ya Misri

na kuijaza nchi kwa waliouawa.

1230:12 Isa 19:6; Yer 46:8; Eze 29:9; 19:7Nitakausha vijito vya Naili

na nitaiuza nchi kwa watu waovu,

kwa mkono wa wageni,

nitaifanya nchi ukiwa na kila kitu

kilichomo ndani yake.

Mimi Bwana nimenena haya.

1330:13 Yer 43:12; Isa 19:13; Eze 6:6; Zek 10:11“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Nitaangamiza sanamu

na kukomesha vinyago katika Memfisi30:13 Kiebrania ni Nofu.

Hapatakuwepo tena na mkuu katika nchi ya Misri,

nami nitaeneza hofu katika nchi nzima.

1430:14 Eze 29:14; Hes 13:22; Za 78:12; Yer 46:25Nitaifanya Pathrosi30:14 Pathrosi ni Misri ya Juu. kuwa ukiwa

na kuitia moto Soani,

nami nitaipiga kwa adhabu Thebesi30:14 Thebesi kwa Kiebrania ni No (au No-Amoni), mji katika Misri.

15Nitaimwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiumu,30:15 Kiebrania ni Sini.

ngome ya Misri,

nami nitakatilia mbali

makundi ya wajeuri wa Thebesi.

1630:16 Yos 7:15; Isa 19:13Nitaitia moto nchi ya Misri;

Pelusiumu itagaagaa kwa maumivu makuu.

Thebesi itachukuliwa na tufani,

Memfisi itakuwa katika taabu daima.

1730:17 Mwa 41:45Wanaume vijana wa Oni30:17 Yaani Heliopoli (Mji wa Jua). na wa Pi-Besethi30:17 Yaani Bubasti.

wataanguka kwa upanga

nayo hiyo miji itatekwa.

1830:18 Law 26:13; Isa 9:4; Yer 2:16; 43:7Huko Tahpanhesi mchana utatiwa giza

nitakapovunja kongwa la Misri;

hapo kiburi cha nguvu zake kitakoma.

Atafunikwa na mawingu

na vijiji vyake vitatekwa.

1930:19 Eze 28:22Kwa hiyo nitaipiga Misri kwa adhabu,

nao watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’ ”

2030:20 Eze 26:1; 29:17; 32:1Katika mwaka wa kumi na moja, mwezi wa kwanza, siku ya saba, neno la Bwana likanijia kusema: 2130:21 Yer 48:25; 44:30; 30:13; 46:11“Mwanadamu, nimevunja mkono wa Farao mfalme wa Misri. Haukufungwa ili upone au kuwekewa kipande cha ubao ili upate nguvu za kuweza kuchukua upanga. 2230:22 Mwa 15:18; Yer 46:25; Za 37:17; Zek 11:17Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume na Farao mfalme wa Misri. Nitavunja mikono yake yote miwili, ule mkono ulio mzima pia na ule uliovunjika na kuufanya upanga uanguke toka mkononi mwake. 2330:23 Eze 29:12Nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote. 2430:24 Zek 10:6-12; 12:5; Eze 21:14; Sef 2:12; Yer 51:52Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli na kuutia upanga wangu mkononi mwake, lakini nitavunja mikono ya Farao, naye atalia kwa huzuni mbele yake kama mtu aliyetiwa jeraha la kumfisha. 2530:25 Kut 7:5; Za 9:16; 59:13; 1Nya 21:12; Isa 10:5; Eze 29:19Nitaitia nguvu mikono ya mfalme wa Babeli, lakini mikono ya Farao italegea. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, nitakapoutia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babeli, naye ataunyoosha dhidi ya Misri. 2630:26 Eze 29:12Nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi mbalimbali. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以西結書 30:1-26

為埃及唱哀歌

1耶和華對我說: 2「人子啊,你要說預言,這樣宣告主耶和華的話,

『哀號吧!你們要為那日悲傷。

3因為日子近了,耶和華的日子近了,

那是烏雲密佈的日子,

列國淪亡的時候。

4必有刀劍攻擊埃及

埃及必屍橫遍野,

古實必痛苦不堪。

敵人要擄掠埃及的財富,

摧毀她的根基。

5古實路德阿拉伯利比亞以及她的其他盟友都必與她一同死於刀下。』

6「耶和華說,

埃及的盟友都要覆滅,

埃及的傲氣必蕩然無存,

密奪色弗尼的居民都要喪身刀下。

這是主耶和華說的。

7埃及要變成荒地中的荒地,

她的城邑要淪為廢墟中的廢墟。

8我要點火燒埃及

埃及的所有盟友都要滅亡。

那時,他們就知道我是耶和華。

9「『在那日,我要差遣使者乘船出去驚嚇安逸的古實人,在埃及遭難的日子,他們必痛苦不堪。看啊,這日子快到了。』

10「主耶和華說,

『我要藉巴比倫尼布甲尼撒的手消滅埃及的百姓。

11他和追隨他的都是萬民中最殘暴的人。

我要差他們去毀滅埃及

大肆殺戮,

使埃及屍骨遍野。

12我要使尼羅河乾涸,

把土地賣給惡人,

我要藉外族人的手使地和地上的一切都荒廢,

這是我耶和華說的。』

13「主耶和華說,

『我要毀滅偶像,

剷除挪弗的神像。

埃及再沒有君王,

國內到處充滿恐懼。

14我要使巴特羅荒廢,

放火焚燒瑣安

審判底比斯

15把我的烈怒傾倒在埃及的堡壘——

消滅底比斯的百姓。

16我要放火燒埃及

要受痛苦的折磨,

底比斯要被攻破,

挪弗終日惶恐不已,

17亞文比伯實的壯丁必死於刀下,

眾城都要遭受擄掠。

18我粉碎埃及勢力的那天,

答比匿日月無光,

她的銳氣全消。

烏雲要籠罩她,

她城邑的居民要被擄去。

19我必這樣審判埃及

他們就知道我是耶和華。』」

20第十一年一月七日,耶和華對我說: 21「人子啊,我打斷了埃及王法老的臂膀,沒有人替他敷藥包紮,以致他無力拿刀。 22主耶和華說,『我要與埃及王法老為敵,我要把他那強壯的臂膀和曾經受傷的臂膀一起打斷,使刀從他手中掉落。 23我要把埃及人驅散到列國,分散到列邦。 24我要使巴比倫王的臂膀強壯有力,把我的刀交在他手中。我要打斷法老的臂膀,使法老在他面前像受了致命傷的人一樣呻吟。 25我要使巴比倫王的臂膀強壯有力,而法老的雙臂必軟弱無力。我要把我的刀交在巴比倫王手中,讓他揮刀攻擊埃及。那時他們就知道我是耶和華。 26我要把埃及人驅散到列國,分散到列邦,這樣他們就知道我是耶和華。』」