Danieli 8 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Danieli 8:1-27

Maono Ya Danieli Ya Kondoo Dume Na Beberu

18:1 Dan 5:1Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Mfalme Belshaza, mimi Danieli, nilipata maono, baada ya maono ambayo yalikuwa yamenitokea mbeleni. 28:2 Mwa 10:22; Es 2:8; Ezr 4:9Katika maono yangu, nilijiona nikiwa ndani ya ngome ya Shushani katika jimbo la Elamu. Katika maono nilikuwa kando ya Mto Ulai.8:2 Mto Ulai ni mfereji uliokuwa kati ya Shushani na Elymaisi; sasa unaitwa Mto Karuni. 38:3 Dan 10:5; Ufu 13:11Nikatazama juu, na hapo mbele yangu kulikuwa na kondoo dume mwenye pembe mbili, akiwa amesimama kando ya mto, nazo pembe zake zilikuwa ndefu. Pembe moja ilikuwa ndefu kuliko hiyo nyingine, lakini iliendelea kukua baadaye. 48:4 Dan 11:3, 16; Isa 41:3Nikamtazama yule kondoo dume alivyokuwa akishambulia kuelekea magharibi, kaskazini na kusini. Hakuna mnyama yeyote aliyeweza kusimama dhidi yake, wala hakuna aliyeweza kuokoa kutoka nguvu zake. Alifanya kama atakavyo, naye akawa mkuu.

5Nilipokuwa ninatafakari hili, ghafula beberu mwenye pembe moja kubwa sana katikati ya macho yake alikuja kutoka magharibi, akiruka kasi juu ya dunia yote bila kugusa ardhi. 6Alikuja akimwelekea yule kondoo dume mwenye pembe mbili niliyemwona akisimama kando ya mto, akamshambulia kwa hasira nyingi. 78:7 Dan 7:7; 11:11Nikamwona akimshambulia yule kondoo dume kwa hasira nyingi, akimpiga yule kondoo dume na kuvunja pembe zake mbili. Yule kondoo dume hakuwa na nguvu za kumzuia yule beberu, hivyo akamwangusha yule kondoo dume chini na kumkanyaga, wala hakuna aliyeweza kumwokoa yule kondoo dume kutoka nguvu za huyo beberu. 88:8 2Nya 26:16-21; Dan 5:20; 7:2; Ufu 7:1Yule beberu akawa mkubwa sana, lakini katika kilele cha nguvu zake ile pembe yake ndefu ilivunjika, na mahali pake pakaota pembe nne kubwa kuelekea pande nne za dunia.

98:9 Eze 20:6; Dan 11:16; Za 48:2; Dan 7:8Kutoka mojawapo ya zile pembe nne palitokea pembe ndogo ukaongezeka nguvu kuelekea kusini, na kuelekea mashariki, na kuelekea Nchi ya Kupendeza. 108:10 Isa 14:13; Ufu 8:10; 12:4; Dan 7:7Pembe hiyo ikaendelea kukua hadi kufikia jeshi la mbinguni, nayo ikalitupa baadhi ya jeshi la vitu vya angani hapa chini duniani, na kulikanyaga. 118:11 Dan 11:36-37; Eze 46:13-14; Dan 12:11; 11:31Pembe hiyo ikajikweza ili iwe kama Mkuu wa hilo jeshi; ikamwondolea dhabihu ya kila siku, napo mahali pake patakatifu pakashushwa chini. 12Kwa sababu ya uasi, jeshi la watakatifu na dhabihu za kila siku vikatiwa mikononi mwake. Ikafanikiwa katika kila kitu ilichofanya, nayo kweli ikatupwa chini.

138:13 Kum 33:2; Dan 4:23; 12:6; Lk 21:24; Isa 28:18; Ufu 11:2Kisha nikamsikia mtakatifu mmoja akizungumza na mtakatifu mwingine, akamwambia, “Je, itachukua muda gani maono haya yatimie: maono kuhusu dhabihu ya kila siku, uasi unaosababisha ukiwa, kutwaliwa kwa mahali patakatifu, na jeshi litakalokanyagwa chini ya nyayo?”

148:14 Dan 12:11-12Akaniambia, “Itachukua siku 2,300. Ndipo mahali patakatifu patawekwa wakfu tena.”

Tafsiri Ya Maono

158:15 Eze 2:1; Dan 10:16-18Mimi Danieli nilipokuwa ninaangalia maono na kujaribu kuelewa, mbele yangu alisimama mmoja aliyefanana na mwanadamu. 168:16 Dan 9:21; Lk 1:19; Dan 7:16Kisha nikasikia sauti ya mwanadamu kutoka Mto Ulai ikiita, “Gabrieli, mwambie mtu huyu maana ya maono haya.”

178:17 Eze 44:4; Ufu 1:17; Hab 2:3; Eze 1:28; Dan 2:46Alipokuwa akikaribia pale nilipokuwa nimesimama, niliogopa, nikaanguka kifudifudi. Akaniambia, “Mwana wa mwanadamu, fahamu kuwa maono haya yanahusu siku za mwisho.”

188:18 Dan 10:9; Eze 2:2; Zek 4:1Alipokuwa akinena nami, nilikuwa katika usingizi mzito, huku nimelala kifudifudi. Ndipo aliponigusa na kunisimamisha wima.

198:19 Isa 10:25; Za 102:13Akaniambia, “Nitakuambia yale yatakayotokea baadaye wakati wa ghadhabu, kwa sababu maono haya yanahusu wakati wa mwisho ulioamriwa. 208:20 Eze 27:10Kondoo dume mwenye pembe mbili ambaye ulimwona anawakilisha wafalme wa Umedi na Uajemi. 218:21 Dan 10:20; 11:2Yule beberu mwenye nywele nyingi ni mfalme wa Uyunani, nayo ile pembe ndefu katikati ya macho yake ni mfalme wa kwanza. 22Zile pembe nne zilizoota badala ya ile pembe iliyovunjika zinawakilisha falme nne ambazo zitatokea kutoka taifa lake, lakini hakuna hata mmoja utakaokuwa na nguvu kama ule uliovunjika.

23“Katika sehemu ya mwisho ya utawala wao, wakati waasi watakapokuwa waovu kabisa, atainuka mfalme mwenye uso mkali, aliye stadi wa hila. 248:24 Dan 7:25; 2:34; 11:21; Ay 34:7Atakuwa na nguvu nyingi, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe. Atasababisha uharibifu wa kutisha, na atafanikiwa kwa chochote anachofanya. Atawaangamiza watu maarufu na watu watakatifu. 258:25 Dan 11:36; 11:21; Ay 34:20Atasababisha udanganyifu ustawi, naye atajihesabu mwenyewe kuwa bora. Wakati wajisikiapo kuwa wako salama, atawaangamiza wengi, na kushindana na Mkuu wa wakuu. Lakini ataangamizwa, isipokuwa si kwa uwezo wa mwanadamu.

268:26 Isa 8:16; Ufu 10:4; Dan 10:14; Eze 12:27; Isa 29:11; Ufu 22:10“Maono kuhusu jioni na asubuhi ambayo umepewa ni kweli, lakini yatie muhuri maono haya, kwa maana yanahusu wakati mrefu ujao.”

278:27 Dan 2:47-48; Isa 21:3; Dan 7:28; 10:8; 4:19Mimi Danieli nilikuwa nimechoka sana, na nikalala nikiwa mgonjwa kwa siku kadhaa. Ndipo nikaamka, nikaenda kwenye shughuli za mfalme. Nilifadhaishwa na maono hayo, nami sikuweza kuyaelewa.

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

但以理书 8:1-27

公绵羊和公山羊的异象

1在看见先前的异象之后,我但以理伯沙撒王执政第三年又看见一个异象。 2我在异象中看见自己在以拦省的书珊城,又看见自己站在乌莱河畔。 3我举目观看,见一只长着长角的公绵羊站在河边,其中一角比另一角长,较长的角是后长出来的。 4我看见这公绵羊向西方、北方和南方顶撞,没有兽能抵挡它,或逃脱它的威力。它随心所欲,狂妄自大。

5我正沉思的时候,忽然从西面出现一只公山羊,穿越大地,脚不沾地。它双眼之间有一个大角。 6这公山羊来到我之前看见的那只站在河边的双角公绵羊那里,愤怒地向它顶去。 7我看见公山羊愤怒地顶向公绵羊,攻击它,折断了它的双角。公绵羊无力抵挡,被撞倒在地,践踏在脚下,无人能救它脱离公山羊的威力。 8公山羊极其狂妄自大。但正值鼎盛之时,它的大角突然折断,在原处又长出四个奇特的角,朝着天的四方。 9其中一个角又长出一个小角,向南方、东方和佳美之地8:9 佳美之地”指以色列,下同11:1641扩张势力。 10它逐渐强大,高及天军,将一些天军和星宿抛到地上,用脚践踏。 11它狂妄自大,要与天军的统帅比高,它废除日常献给祂的祭,毁坏祂的圣所。 12因为反叛的缘故,天军和日常所献的祭都交给了它。它将真理抛在地上,它所行的无不顺利。

13接着,我听见一位圣者在说话,另一位圣者问他:“异象中出现的有关日常所献的祭,毁灭性的反叛和践踏圣所及天军的事要持续多久呢?” 14他对我说:“两千三百个昼夜。之后,圣所才会洁净。”

解释异象

15但以理看见这异象,正想明白它的意思,忽然有一个外貌像人的站在我面前。 16我听见有人声从乌莱河两岸之间呼喊:“加百列啊,要让此人明白这异象。” 17于是,他朝我站的地方走来,当他走来的时候,我吓得俯伏在地。他对我说:“人子啊,你要明白,这异象是关于末后的时期。” 18他和我说话的时候,我伏在地上昏睡过去,他便轻拍我,扶我起来, 19对我说:“我要告诉你将来上帝发烈怒时所发生的事,因为这异象是关于那定好的末后时期。 20你看见的那只有两角的公绵羊指玛代波斯的诸王。 21公山羊指希腊王,在它双眼之间的大角指第一个王。 22大角折断后,从原处长出四个角表示四个国必从这国兴起,但都不及这国强大。 23在四国的末期,人们恶贯满盈的时候,必有一个面貌凶恶、诡计多端的王兴起。 24他势力强大,却不是靠自己的力量。他必带来可怕的毁灭,而且凡事亨通,他必毁灭强者和圣民。 25他利用诡计和骗术得逞,心高气傲,乘人不备突然毁灭许多人,甚至要攻击万君之君,然而他终必被击垮,但并非被人的手击垮。 26异象中所说的两千三百个昼夜是真的。但你要保密,不可告诉别人,因为这指的是遥远的将来。”

27但以理精疲力尽,病了几天。后来我起来照常办理王的事务,但我对这异象感到惊奇不已,不明白它的意思。