Ayubu 37 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 37:1-24

137:1 Za 38:10; Isa 15:5; Yer 4:19; Hab 3:16“Kwa hili moyo wangu unatetemeka,

nao unaruka kutoka mahali pake.

237:2 Za 18:13; 29:3-9Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake,

sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.

337:3 2Sam 22:13; Za 18:14; Ay 36:32; Mt 24:27; Lk 17:24Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote

na kuupeleka hata miisho ya dunia.

437:4 1Sam 2:10; Kut 20:19Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake;

Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari.

Wakati sauti yake ingurumapo tena,

huuachilia umeme wake wa radi.

537:5 Ay 11:7-9Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu;

yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.

637:6 Kum 28:12; Ay 38:22; Mwa 7:4; Ay 36:27Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’

nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’

737:7 Ay 12:14; Za 111:2; 109:27; 104:19-23Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake,

yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.

837:8 Ay 28:26; 38:40; Za 104:22Wanyama hujificha;

hubakia kwenye mapango yao.

937:9 Za 50:3; 147:17Dhoruba hutoka katika chumba chake,

baridi hutoka katika upepo uendao kasi.

1037:10 Ay 38:29-30; Za 147:17Pumzi ya Mungu hutoa barafu,

eneo kubwa la maji huganda.

1137:11 Ay 26:8; 36:30; 28:26Huyasheheneza mawingu kwa maji,

naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.

1237:12 Za 147:16; 148:8; Ay 37:3Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake,

juu ya uso wa dunia yote,

kufanya lolote ayaamuruyo.

1337:13 Kut 9:22-23; 1Sam 12:17; Kut 9:18; 1Fal 18:45Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu,

au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.

1437:14 Ay 32:10; 5:9“Ayubu, sikiliza hili;

nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.

1537:15 Ay 36:30, 32Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu,

na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?

1637:16 Ay 36:29; 5:9; 36:4Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia,

hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?

1737:17 Mdo 27:13Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako

wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,

1837:18 Mwa 1:1, 8; Ay 22:14; Kum 28:23; Za 104:2je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga,

zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?

1937:19 Rum 8:26; Ay 13:18; 9:3“Tuambieni yatupasayo kumwambia;

hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.

20Je, aambiwe kwamba nataka kuongea?

Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?

2137:21 Amu 5:31; Mdo 22:1; 26:13Basi hakuna awezaye kulitazama jua,

jinsi linavyongʼaa angani,

upepo ukishafagia mawingu.

2237:22 Za 19:5; Kut 24:17Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu;

Mungu huja katika utukufu wa kutisha.

2337:23 Ay 5:9; Rum 11:33; Ay 8:3; Yer 25:5; Mao 3:33Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza;

katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.

2437:24 Mik 6:8; Mt 10:28; 11:25; Efe 5:15Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni,

kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

New International Version

Job 37:1-24

1“At this my heart pounds

and leaps from its place.

2Listen! Listen to the roar of his voice,

to the rumbling that comes from his mouth.

3He unleashes his lightning beneath the whole heaven

and sends it to the ends of the earth.

4After that comes the sound of his roar;

he thunders with his majestic voice.

When his voice resounds,

he holds nothing back.

5God’s voice thunders in marvelous ways;

he does great things beyond our understanding.

6He says to the snow, ‘Fall on the earth,’

and to the rain shower, ‘Be a mighty downpour.’

7So that everyone he has made may know his work,

he stops all people from their labor.37:7 Or work, / he fills all people with fear by his power

8The animals take cover;

they remain in their dens.

9The tempest comes out from its chamber,

the cold from the driving winds.

10The breath of God produces ice,

and the broad waters become frozen.

11He loads the clouds with moisture;

he scatters his lightning through them.

12At his direction they swirl around

over the face of the whole earth

to do whatever he commands them.

13He brings the clouds to punish people,

or to water his earth and show his love.

14“Listen to this, Job;

stop and consider God’s wonders.

15Do you know how God controls the clouds

and makes his lightning flash?

16Do you know how the clouds hang poised,

those wonders of him who has perfect knowledge?

17You who swelter in your clothes

when the land lies hushed under the south wind,

18can you join him in spreading out the skies,

hard as a mirror of cast bronze?

19“Tell us what we should say to him;

we cannot draw up our case because of our darkness.

20Should he be told that I want to speak?

Would anyone ask to be swallowed up?

21Now no one can look at the sun,

bright as it is in the skies

after the wind has swept them clean.

22Out of the north he comes in golden splendor;

God comes in awesome majesty.

23The Almighty is beyond our reach and exalted in power;

in his justice and great righteousness, he does not oppress.

24Therefore, people revere him,

for does he not have regard for all the wise in heart?37:24 Or for he does not have regard for any who think they are wise.