Ayubu 38 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 38:1-41

Sehemu Ya Nne: Mungu Anazungumza

(Ayubu 38–41)

Bwana Anamjibu Ayubu

138:1 1Sam 2:10; Eze 1:4; Kut 19:16-18; Ay 11:5; 40:6; Isa 21:1Kisha Bwana akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema:

238:2 Mk 10:38; 1Tim 1:7“Nani huyu atiaye mashauri yangu giza

kwa maneno yasiyo na maarifa?

338:3 Ay 40:7; 42:4; Mk 11:29; 1Fal 18:46Jikaze kama mwanaume;

nitakuuliza swali,

nawe unijibu.

438:4 Mwa 1:1; Mit 8:29; Za 104:5“Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia?

Niambie, kama unafahamu.

538:5 Za 102:25; Yer 31:37Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake?

Hakika wewe unajua!

Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake?

638:6 Mit 8:25; Ay 26:7Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini,

au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni,

738:7 Mwa 1:16; Za 19:1-4; 148:2-3; 1Fal 22:19; Kum 16:15wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja,

na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha?

838:8 Za 33:7; Yer 5:22; Mwa 1:9-10“Ni nani aliyeifungia bahari milango

ilipopasuka kutoka tumbo,

938:9 Mwa 1:2nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake,

na kuyafungia katika giza nene,

1038:10 Za 33:7; Neh 3:3; Isa 40:12; Ay 7:12nilipoamuru mipaka yake,

na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake,

1138:11 Za 65:7; 89:9; 104:6-9niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi;

hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’?

1238:12 Za 57:8; 74:16; Amo 5:8“Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke,

au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake,

13yapate kushika miisho ya dunia,

na kuwakungʼuta waovu waliomo?

1438:14 Kut 28:11Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri;

sura yake hukaa kama ile ya vazi.

1538:15 Kum 28:29; Ay 15:22; Mwa 17:14; Za 10:15Waovu huzuiliwa nuru yao,

nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa.

1638:16 Mwa 1:7; Ay 9:8“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari?

Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?

1738:17 Za 9:13; Mt 16:18Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti?

Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?

1838:18 Ay 28:24; Isa 40:12; Ay 38:4Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia?

Niambie kama unajua haya yote.

1938:19 Mwa 1:4; Ay 28:3; Za 139:11-12“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi?

Nako maskani mwa giza ni wapi?

2038:20 Ay 24:13Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake?

Unajua njia za kufika maskani mwake?

2138:21 Ay 15:7Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa!

Kwani umeishi miaka mingi!

2238:22 Ay 37:6; Kum 28:12; Za 105:32; 147:17“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji,

au kuona ghala za mvua ya mawe,

2338:23 Za 27:5; Isa 28:17; Eze 13:13; Ufu 16:21; Kut 9:18; Za 9:13ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu,

na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?

2438:24 Ay 28:24; 27:21; Yer 10:13; 51:16Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa,

au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?

2538:25 Ay 28:26Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi

na njia ya umeme wa radi,

2638:26 Ay 36:27; Za 84:6; 107:35; Isa 41:18ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu,

jangwa lisilo na yeyote ndani yake,

2738:27 Ay 28:26; 37:13; Za 104:14ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa,

na majani yaanze kumea ndani yake?

2838:28 2Sam 1:21; Yer 14:22Je, mvua ina baba?

Ni nani baba azaaye matone ya umande?

2938:29 Za 147:16-17Barafu inatoka tumbo la nani?

Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,

3038:30 Ay 37:10wakati maji yawapo magumu kama jiwe,

wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?

3138:31 Ay 9:9; Amo 5:8“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia?

Waweza kulegeza kamba za Orioni?

3238:32 2Fal 23:5; Isa 13:10; 40:26; 45:12; Yer 19:13; Mwa 1:16Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake,

au kuongoza Dubu na watoto wake?

3338:33 Za 148:6; Yer 31:38Je, unajua sheria zinazotawala mbingu?

Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?

3438:34 Ay 5:10; 22:11“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni,

na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?

3538:35 Ay 36:32Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake?

Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?

3638:36 Ay 34:32; Yak 1:5; Za 51:6; Mhu 2:26Ni nani aliyeujalia moyo hekima

au kuzipa akili ufahamu?

3738:37 Yos 3:16; Ay 22:11Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu?

Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni

3838:38 Law 26:19wakati mavumbi yawapo magumu,

na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?

3938:39 Mwa 49:9; Za 104:21“Je, utamwindia simba jike mawindo,

na kuwashibisha simba wenye njaa

4038:40 Ay 37:8; Mwa 49:9wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao,

au wakivizia kichakani?

4138:41 Mwa 8:7; Lk 12:24; Za 147:9; Mt 6:26Ni nani ampaye kunguru chakula

wakati makinda yake yanamlilia Mungu,

yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?

New International Version

Job 38:1-41

The Lord Speaks

1Then the Lord spoke to Job out of the storm. He said:

2“Who is this that obscures my plans

with words without knowledge?

3Brace yourself like a man;

I will question you,

and you shall answer me.

4“Where were you when I laid the earth’s foundation?

Tell me, if you understand.

5Who marked off its dimensions? Surely you know!

Who stretched a measuring line across it?

6On what were its footings set,

or who laid its cornerstone—

7while the morning stars sang together

and all the angels38:7 Hebrew the sons of God shouted for joy?

8“Who shut up the sea behind doors

when it burst forth from the womb,

9when I made the clouds its garment

and wrapped it in thick darkness,

10when I fixed limits for it

and set its doors and bars in place,

11when I said, ‘This far you may come and no farther;

here is where your proud waves halt’?

12“Have you ever given orders to the morning,

or shown the dawn its place,

13that it might take the earth by the edges

and shake the wicked out of it?

14The earth takes shape like clay under a seal;

its features stand out like those of a garment.

15The wicked are denied their light,

and their upraised arm is broken.

16“Have you journeyed to the springs of the sea

or walked in the recesses of the deep?

17Have the gates of death been shown to you?

Have you seen the gates of the deepest darkness?

18Have you comprehended the vast expanses of the earth?

Tell me, if you know all this.

19“What is the way to the abode of light?

And where does darkness reside?

20Can you take them to their places?

Do you know the paths to their dwellings?

21Surely you know, for you were already born!

You have lived so many years!

22“Have you entered the storehouses of the snow

or seen the storehouses of the hail,

23which I reserve for times of trouble,

for days of war and battle?

24What is the way to the place where the lightning is dispersed,

or the place where the east winds are scattered over the earth?

25Who cuts a channel for the torrents of rain,

and a path for the thunderstorm,

26to water a land where no one lives,

an uninhabited desert,

27to satisfy a desolate wasteland

and make it sprout with grass?

28Does the rain have a father?

Who fathers the drops of dew?

29From whose womb comes the ice?

Who gives birth to the frost from the heavens

30when the waters become hard as stone,

when the surface of the deep is frozen?

31“Can you bind the chains38:31 Septuagint; Hebrew beauty of the Pleiades?

Can you loosen Orion’s belt?

32Can you bring forth the constellations in their seasons38:32 Or the morning star in its season

or lead out the Bear38:32 Or out Leo with its cubs?

33Do you know the laws of the heavens?

Can you set up God’s38:33 Or their dominion over the earth?

34“Can you raise your voice to the clouds

and cover yourself with a flood of water?

35Do you send the lightning bolts on their way?

Do they report to you, ‘Here we are’?

36Who gives the ibis wisdom38:36 That is, wisdom about the flooding of the Nile

or gives the rooster understanding?38:36 That is, understanding of when to crow; the meaning of the Hebrew for this verse is uncertain.

37Who has the wisdom to count the clouds?

Who can tip over the water jars of the heavens

38when the dust becomes hard

and the clods of earth stick together?

39“Do you hunt the prey for the lioness

and satisfy the hunger of the lions

40when they crouch in their dens

or lie in wait in a thicket?

41Who provides food for the raven

when its young cry out to God

and wander about for lack of food?