Ayubu 37 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 37:1-24

137:1 Za 38:10; Isa 15:5; Yer 4:19; Hab 3:16“Kwa hili moyo wangu unatetemeka,

nao unaruka kutoka mahali pake.

237:2 Za 18:13; 29:3-9Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake,

sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.

337:3 2Sam 22:13; Za 18:14; Ay 36:32; Mt 24:27; Lk 17:24Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote

na kuupeleka hata miisho ya dunia.

437:4 1Sam 2:10; Kut 20:19Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake;

Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari.

Wakati sauti yake ingurumapo tena,

huuachilia umeme wake wa radi.

537:5 Ay 11:7-9Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu;

yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.

637:6 Kum 28:12; Ay 38:22; Mwa 7:4; Ay 36:27Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’

nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’

737:7 Ay 12:14; Za 111:2; 109:27; 104:19-23Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake,

yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.

837:8 Ay 28:26; 38:40; Za 104:22Wanyama hujificha;

hubakia kwenye mapango yao.

937:9 Za 50:3; 147:17Dhoruba hutoka katika chumba chake,

baridi hutoka katika upepo uendao kasi.

1037:10 Ay 38:29-30; Za 147:17Pumzi ya Mungu hutoa barafu,

eneo kubwa la maji huganda.

1137:11 Ay 26:8; 36:30; 28:26Huyasheheneza mawingu kwa maji,

naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.

1237:12 Za 147:16; 148:8; Ay 37:3Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake,

juu ya uso wa dunia yote,

kufanya lolote ayaamuruyo.

1337:13 Kut 9:22-23; 1Sam 12:17; Kut 9:18; 1Fal 18:45Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu,

au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.

1437:14 Ay 32:10; 5:9“Ayubu, sikiliza hili;

nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.

1537:15 Ay 36:30, 32Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu,

na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?

1637:16 Ay 36:29; 5:9; 36:4Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia,

hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?

1737:17 Mdo 27:13Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako

wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,

1837:18 Mwa 1:1, 8; Ay 22:14; Kum 28:23; Za 104:2je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga,

zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?

1937:19 Rum 8:26; Ay 13:18; 9:3“Tuambieni yatupasayo kumwambia;

hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.

20Je, aambiwe kwamba nataka kuongea?

Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?

2137:21 Amu 5:31; Mdo 22:1; 26:13Basi hakuna awezaye kulitazama jua,

jinsi linavyongʼaa angani,

upepo ukishafagia mawingu.

2237:22 Za 19:5; Kut 24:17Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu;

Mungu huja katika utukufu wa kutisha.

2337:23 Ay 5:9; Rum 11:33; Ay 8:3; Yer 25:5; Mao 3:33Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza;

katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.

2437:24 Mik 6:8; Mt 10:28; 11:25; Efe 5:15Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni,

kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

King James Version

Job 37:1-24

1At this also my heart trembleth, and is moved out of his place. 2Hear attentively the noise of his voice, and the sound that goeth out of his mouth.37.2 Hear…: Heb. Hear in hearing 3He directeth it under the whole heaven, and his lightning unto the ends of the earth.37.3 lightning: Heb. light37.3 ends: Heb. wings 4After it a voice roareth: he thundereth with the voice of his excellency; and he will not stay them when his voice is heard. 5God thundereth marvellously with his voice; great things doeth he, which we cannot comprehend.

6For he saith to the snow, Be thou on the earth; likewise to the small rain, and to the great rain of his strength.37.6 likewise…: Heb. and to the shower of rain, and to the showers of rain of his strength 7He sealeth up the hand of every man; that all men may know his work. 8Then the beasts go into dens, and remain in their places. 9Out of the south cometh the whirlwind: and cold out of the north.37.9 south: Heb. chamber37.9 north: Heb. scattering winds 10By the breath of God frost is given: and the breadth of the waters is straitened. 11Also by watering he wearieth the thick cloud: he scattereth his bright cloud:37.11 his…: Heb. the cloud of his light 12And it is turned round about by his counsels: that they may do whatsoever he commandeth them upon the face of the world in the earth. 13He causeth it to come, whether for correction, or for his land, or for mercy.37.13 correction: Heb. a rod

14Hearken unto this, O Job: stand still, and consider the wondrous works of God. 15Dost thou know when God disposed them, and caused the light of his cloud to shine? 16Dost thou know the balancings of the clouds, the wondrous works of him which is perfect in knowledge? 17How thy garments are warm, when he quieteth the earth by the south wind? 18Hast thou with him spread out the sky, which is strong, and as a molten looking glass? 19Teach us what we shall say unto him; for we cannot order our speech by reason of darkness. 20Shall it be told him that I speak? if a man speak, surely he shall be swallowed up.

21And now men see not the bright light which is in the clouds: but the wind passeth, and cleanseth them. 22Fair weather cometh out of the north: with God is terrible majesty.37.22 Fair…: Heb. Gold 23Touching the Almighty, we cannot find him out: he is excellent in power, and in judgment, and in plenty of justice: he will not afflict. 24Men do therefore fear him: he respecteth not any that are wise of heart.