Ayubu 36 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 36:1-33

Elihu Atukuza Wema Wa Mungu

1Elihu akaendelea kusema:

2“Nivumilie kidogo zaidi nami nitakuonyesha

kwamba yako mengi zaidi ya kusemwa kwa ajili ya Mungu.

336:3 Ay 4:17; 8:3Ninayapata maarifa yangu kutoka mbali,

nami nitamhesabia haki Muumba wangu.

436:4 Ay 6:28; 13:6; 37:5, 16, 23; 32:17Uwe na hakika kwamba maneno yangu si ya uongo;

mmoja aliye mkamilifu katika maarifa yuko pamoja na wewe.

536:5 Za 31:22; 69:33; Hes 23:19; Rum 11:29“Mungu ni mwenye nguvu, lakini hamdharau mwanadamu;

ni mwenye nguvu, naye ni thabiti katika shauri lake.

636:6 Ay 8:22; 4:10Hawaachi waovu waendelee kuishi,

bali huwapa walioteswa haki yao.

736:7 Za 34:15; 113:8; Mt 6:18; Isa 22:23Yeye haondoi macho yake kwa wenye haki;

huwaketisha penye viti vya enzi pamoja na wafalme

na kuwatukuza milele.

836:8 2Sam 3:34; 2Fal 23:33Lakini ikiwa watu wamefungwa kwenye minyororo,

wakiwa wameshikiliwa na kamba za mateso,

936:9 Ay 15:25huwaonyesha yale waliyoyatenda,

kwamba wametenda dhambi kwa majivuno.

1036:10 Ay 33:16; 2Fal 17:13; Ay 5:17Huwafanya wao kusikia maonyo,

na huwaagiza kutubu uovu wao.

1136:11 Kut 28:1; Hag 1:12; Isa 1; 19Kama wakitii na kumtumikia,

wataishi siku zao zilizobaki katika mafanikio,

na miaka yao katika utoshelevu.

1236:12 Law 26:38; Ay 15:22; 4:21; Efe 4:18Lakini wasiposikiliza,

wataangamia kwa upanga,

nao watakufa pasipo maarifa.

1336:13 Ay 15:12; Rum 2:5; Ay 5:2; 4:17; Amo 4:11“Wasiomcha Mungu moyoni mwao huficha chuki;

hata anapowafunga, hawamwombi msaada.

1436:14 Kum 23:17Wanakufa wangali vijana,

miongoni mwa wanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu.

1536:15 Ay 5:15; 2Kor 12:10; Ay 33:16; 34:33Bali wao wanaoteseka huwaokoa katika mateso yao,

na kuzungumza nao katika dhiki zao.

1636:16 Hos 2:14; Za 23:5; 78:19“Yeye anakubembeleza utoke katika mataya ya dhiki,

ili kukuweka mahali palipo na nafasi mbali na kizuizi,

hadi kwenye meza yako ya faraja iliyojaa vyakula vizuri.

1736:17 Ay 20:29; 22:11Lakini sasa umelemewa na hukumu kwa ajili ya uovu;

hukumu na haki vimekukamata.

1836:18 Kut 23:8; Amo 5:12; Ay 34:33Uwe mwangalifu ili yeyote asikushawishi kwa utajiri;

usipotoshwe kwa fungu kubwa la rushwa.

1936:19 Za 49:6; Yer 9:23Je, utajiri wako hata nguvu zako nyingi

vinaweza kukusaidia usiingie kwenye dhiki?

2036:20 Ay 34:20-25Usiutamani usiku uje,

ili uwaburute watu mbali na nyumba zao.

2136:21 Ay 34:33; Za 66:18; Ebr 11:25Jihadhari usigeukie uovu,

ambao unaupenda zaidi kuliko mateso.

2236:22 Isa 40:13; Rum 11:34“Mungu ametukuzwa katika nguvu zake.

Ni nani aliye mwalimu kama yeye?

2336:23 Ay 34:10, 13; Rum 11:33; Mwa 18:25; Kum 32:4Ni nani aliyemwelekeza katika njia zake,

au kumwambia, ‘Wewe umetenda yasiyo sawa’?

2436:24 1Nya 16:24; Za 35:27; 59:16; Ufu 15:3Kumbuka kuzitukuza kazi zake,

ambazo watu wamezisifu katika wimbo.

2536:25 Rum 1:20Wanadamu wote wameiona;

watu wanaikazia macho kwa mbali.

2636:26 1Kor 13:12; Mwa 21:33; Ebr 1:12Tazama jinsi Mungu alivyo mkuu,

kupita ufahamu wetu!

Hesabu ya miaka yake haitafutiki.

2736:27 2Sam 1:21; Za 147:8“Yeye huvuta juu matone ya maji,

ayachujayo kama mvua kutoka kwenye vijito;

2836:28 Ay 22:11; Mt 5:45mawingu huangusha chini maji yake,

nayo mvua nyingi huwanyeshea wanadamu.

2936:29 Mit 8:28; Isa 40:22Ni nani ajuaye jinsi ayatandazavyo mawingu,

jinsi angurumavyo kutoka hemani mwake.

3036:30 Kut 19:16; Yer 10:13; Hab 3:11; Isa 51:10; Za 18:12, 14; 97:4Tazama jinsi anavyotandaza umeme wa radi kumzunguka,

naye huvifunika vilindi vya bahari.

3136:31 1Fal 17:1; Amo 4:7-8; Isa 30:23; Mdo 14:17Hivi ndivyo atawalavyo mataifa,

na kuwapa chakula kwa wingi.

3236:32 Ay 28:24; Za 18:14Huujaza mkono wake kwa umeme wa radi,

na kuuagiza kulenga shabaha yake.

33Ngurumo zake hutangaza dhoruba inayokuja;

hata mifugo hujulisha kukaribia kwake.36:33 Au: hutangaza kuja kwake.

King James Version

Job 36:1-33

1Elihu also proceeded, and said, 2Suffer me a little, and I will shew thee that I have yet to speak on God’s behalf.36.2 I have…: Heb. there are yet words for God 3I will fetch my knowledge from afar, and will ascribe righteousness to my Maker. 4For truly my words shall not be false: he that is perfect in knowledge is with thee.

5Behold, God is mighty, and despiseth not any: he is mighty in strength and wisdom.36.5 wisdom: Heb. heart 6He preserveth not the life of the wicked: but giveth right to the poor.36.6 poor: or, afflicted 7He withdraweth not his eyes from the righteous: but with kings are they on the throne; yea, he doth establish them for ever, and they are exalted. 8And if they be bound in fetters, and be holden in cords of affliction; 9Then he sheweth them their work, and their transgressions that they have exceeded. 10He openeth also their ear to discipline, and commandeth that they return from iniquity. 11If they obey and serve him, they shall spend their days in prosperity, and their years in pleasures. 12But if they obey not, they shall perish by the sword, and they shall die without knowledge.36.12 perish: Heb. pass away 13But the hypocrites in heart heap up wrath: they cry not when he bindeth them. 14They die in youth, and their life is among the unclean.36.14 They…: Heb. Their soul dieth36.14 unclean: or, sodomites

15He delivereth the poor in his affliction, and openeth their ears in oppression.36.15 poor: or, afflicted 16Even so would he have removed thee out of the strait into a broad place, where there is no straitness; and that which should be set on thy table should be full of fatness.36.16 that…: Heb. the rest of thy table 17But thou hast fulfilled the judgment of the wicked: judgment and justice take hold on thee.36.17 take…: or, should uphold thee 18Because there is wrath, beware lest he take thee away with his stroke: then a great ransom cannot deliver thee.36.18 deliver…: Heb. turn thee aside 19Will he esteem thy riches? no, not gold, nor all the forces of strength. 20Desire not the night, when people are cut off in their place. 21Take heed, regard not iniquity: for this hast thou chosen rather than affliction. 22Behold, God exalteth by his power: who teacheth like him? 23Who hath enjoined him his way? or who can say, Thou hast wrought iniquity?

24Remember that thou magnify his work, which men behold. 25Every man may see it; man may behold it afar off. 26Behold, God is great, and we know him not, neither can the number of his years be searched out. 27For he maketh small the drops of water: they pour down rain according to the vapour thereof: 28Which the clouds do drop and distil upon man abundantly. 29Also can any understand the spreadings of the clouds, or the noise of his tabernacle? 30Behold, he spreadeth his light upon it, and covereth the bottom of the sea.36.30 bottom: Heb. roots 31For by them judgeth he the people; he giveth meat in abundance. 32With clouds he covereth the light; and commandeth it not to shine by the cloud that cometh betwixt. 33The noise thereof sheweth concerning it, the cattle also concerning the vapour.36.33 the vapour: Heb. that which goeth up