Ayubu 35 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ayubu 35:1-16

Elihu Analaumu Mtu Kujiona Kuwa Mwenye Haki

1Ndipo Elihu akasema:

235:2 Ay 33:32; 2:9; 32:2“Je, unadhani hili ni haki?

Wewe unasema, ‘Nina haki mbele za Mungu.’

335:3 Ay 21:15; 34:9Bado unamuuliza, ‘Ni faida gani nimepata,

na imenifaidi nini kwa kutokutenda dhambi?’

4“Ningependa nikujibu wewe

pamoja na marafiki zako walio pamoja nawe.

535:5 Kum 10:14; Mwa 15:5; Ay 22:12; Za 19:1-4Tazama juu mbinguni ukaone;

yaangalie mawingu yaliyo juu sana juu yako.

635:6 Ay 7:20; Mit 8:36Je, ukitenda dhambi, inamdhuruje Mungu?

Kama dhambi zako zikiwa nyingi,

hilo linamfanyia nini Mungu?

735:7 Rum 11:35; Mit 9:12; 1Kor 4:7; Lk 17:10Kama wewe ni mwadilifu, unampa nini,

au yeye anapokea nini mkononi kwako?

835:8 Eze 18:24; 18:5-9; Zek 7:9-10Uovu wako unamdhuru tu mtu mwingine kama wewe,

nayo haki yako inawafaa wanadamu tu.

935:9 Kut 2:23; Ay 5:15; 12:19; Lk 18:3-7“Wanadamu hulia kwa kulemewa na mateso;

huomba msaada kutoka mkono wenye nguvu.

1035:10 Ay 4:17; Isa 51:13; Za 77:6; Mdo 16:25; 1Pet 4:19Lakini hakuna asemaye, ‘Yuko wapi Mungu Muumba wangu,

yeye anifanyaye niimbe usiku,

1135:11 Za 94:12; Lk 12:24; Ay 32:8yeye atufundishaye sisi zaidi kuliko wanyama wa dunia,

na kutufanya wenye hekima kuliko ndege wa angani?’

1235:12 1Sam 8:18; Mit 1:1Yeye hajibu wakati watu waliapo

kwa sababu ya kiburi cha watu waovu.

1335:13 Kum 1:45; 1Sam 8:18; Ay 15:31; Mit 15:8Naam, Mungu hasikilizi maombi yao ya ubatili;

Mwenyezi hayazingatii.

1435:14 Ay 9:11; Yer 11:11Si zaidi sana kwamba hatakusikiliza

wewe usemapo humwoni,

tena ya kwamba shauri lako liko mbele zake

na wewe lazima umngojee,

15pia zaidi, kwamba hasira yake kamwe haiadhibu

wala haangalii uovu hata kidogo?

1635:16 Ay 34:35-37; 1Kor 4:20Hivyo Ayubu hufumbua kinywa chake kwa maneno yasiyo na maana;

anaongea maneno mengi bila maarifa.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

约伯记 35:1-16

1以利户又说:

2“你在上帝面前自以为义,

你认为这合理吗?

3你还说,‘这与我何干?

我不犯罪又有何益处?’

4我要答复你和你的朋友。

5要抬头观看诸天,

瞻望头顶的穹苍。

6你若犯罪,与上帝何妨?

你若罪恶累累,对祂有何影响?

7你若为人公义,与祂何益?

祂从你手上能得什么好处?

8你的罪恶只能伤害你的同类,

你的公义只能令世人受益。

9“人们因饱受压迫而呼求,

因强权者的压制而求救。

10但无人问,‘创造我的上帝在哪里?

祂使人夜间欢唱,

11使我们比地上的走兽聪明,

比天上的飞鸟有智慧。’

12他们因恶人的嚣张而呼求,

上帝却不回答。

13上帝必不垂听虚妄的呼求,

全能者必不理会。

14更何况你说你看不见祂,

你的案子已呈上,在等祂裁决。

15你还说祂没有发怒降罚,

也不理会罪恶。

16约伯啊,这尽是虚言,

是一大堆无知的话。”