Amosi 7 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Amosi 7:1-17

Maono Ya Kwanza: Nzige

17:1 Amo 8:1; Za 78:46; Yer 51:14; Yoe 1:4Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua. 27:2 Kut 10:15; Eze 11:13; Isa 37:4; Amo 4:9Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “Bwana Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”

37:3 Kut 32:14; Yon 3:10; Kum 32:36; Za 106:45; 1Nya 21:15; Hos 11:8; Yoe 2:14; Yak 5:16; Yer 18:8; 26:19Kwa hiyo Bwana akaghairi.

Kisha Bwana akasema, “Hili halitatokea.”

Maono Ya Pili: Moto

47:4 Isa 66:16; Yoe 1:19; Kum 32:22Hili ndilo Bwana Mwenyezi alilonionyesha katika maono: Bwana Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi. 57:5 Yoe 2:17Ndipo nikalia, “Bwana Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!”

67:6 Kut 32:14; Yer 18:8; 42:10; Za 102:17; Yon 3:10; Eze 9:8Kwa hiyo Bwana akaghairi.

Bwana Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.”

Maono Ya Tatu: Timazi

7Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake. 87:8 Isa 28:17; Mao 2:8; 2Fal 21:13; Eze 7:2-9; Yer 1:11-13; 15:6; Mik 7:18Naye Bwana akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?”

Nikamjibu, “Uzi wa timazi.”

Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena.

97:9 Law 26:31; Mwa 26:23; 2Fal 14:23; 1Fal 13:34; 2Fal 15:9-10; Isa 63:18; Hos 10:8“Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa,

na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa;

kwa upanga wangu nitainuka

dhidi ya nyumba ya Yeroboamu.”

Amosi Na Amazia

107:10 1Fal 12:32; Yos 7:2; 2Fal 14:23-24; Yer 38:4; 26:8-11Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote. 117:11 Amo 5:27; Yer 36:16Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema:

“ ‘Yeroboamu atakufa kwa upanga,

na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni,

mbali na nchi yao.’ ”

127:12 Mt 8:34; 1Sam 9:9Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako. 137:13 Yer 20:2; 36:5; Amo 2:12; Mdo 4:18; Yos 7:2; 1Fal 12:29Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.”

147:14 1Sam 10:5; Zek 13:5; 2Fal 2:5; 4:38; Isa 9:10; 1Fal 10:27Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu. 157:15 Mwa 37:5; 2Sam 7:8; Yer 7:1-2; 26:12; Eze 2:3-4; Isa 6:9Lakini Bwana akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’ 167:16 Isa 30:10; Eze 20:46; Mik 2:6; Yer 22:2Sasa basi, sikieni neno la Bwana. Ninyi mnasema,

“ ‘Usitabiri dhidi ya Israeli,

na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’

177:17 Hos 4:13; 9:3; Eze 4:13; Yer 28:12; 29:21; Mao 5:11; Amo 5:27; 2:12-13; 2Fal 17:6“Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana:

“ ‘Mke wako atakuwa kahaba mjini,

nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga.

Shamba lako litapimwa na kugawanywa,

na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani.

Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni,

mbali na nchi yao.’ ”

New International Reader’s Version

Amos 7:1-17

Amos Has Visions of Locusts, Fire and a Plumb Line

1The Lord and King gave me a vision. He was bringing large numbers of locusts on the land. The king’s share had already been harvested. Now the later crops were coming up. 2The locusts stripped the land clean. Then I cried out, “Lord and King, forgive Israel! How can Jacob’s people continue? They are such a weak nation!”

3So the Lord had pity on them.

“I will let them continue for now,” he said.

4The Lord and King gave me a second vision. He was using fire to punish his people. It dried up the deep waters. It burned the land up. 5Then I cried out, “Lord and King, please stop! How can Jacob’s people continue? They are such a weak nation!”

6So the Lord had pity on them.

“I will let them continue for now,” the Lord and King said.

7Then the Lord gave me a third vision. He was standing by a wall. It had been built very straight, all the way up and down. He was holding a plumb line. 8The Lord asked me, “What do you see, Amos?”

“A plumb line,” I replied.

Then the Lord said, “Look at what I am doing. I am hanging a plumb line next to my people Israel. It will show how crooked they are. I will no longer spare them.

9“The high places where Isaac’s people worship other gods will be destroyed.

The other places of worship in Israel will also be torn down.

I will use my sword to attack Jeroboam’s royal family.”

Amaziah Tells Amos to Stop Prophesying

10Amaziah was priest of Bethel. He sent a message to Jeroboam, the king of Israel. He said, “Amos is making evil plans against you right here in Israel. The people in the land can’t stand to listen to what he’s saying. 11Amos is telling them,

“ ‘Jeroboam will be killed by a sword.

The people of Israel will be taken away as prisoners.

They will be carried off from their own land.’ ”

12Then Amaziah said to Amos, “Get out of Israel, you prophet! Go back to the land of Judah. Earn your living there. Do your prophesying there. 13Don’t prophesy here at Bethel anymore. This is where the king worships. The main temple in the kingdom is located here.”

14Amos answered Amaziah, “I was not a prophet. I wasn’t even the son of a prophet. I was a shepherd. I also took care of sycamore-fig trees. 15But the Lord took me away from taking care of the flock. He said to me, ‘Go. Prophesy to my people Israel.’ 16Now then, listen to the Lord’s message. You say,

“ ‘Don’t prophesy against Israel.

Stop preaching against the people of Isaac.’

17“But the Lord says,

“ ‘Your wife will become a prostitute

in the city of Bethel.

Your sons and daughters will be killed by swords.

Your land will be measured and divided up.

And you yourself will die in another country.

The people of Israel will surely be taken away as prisoners.

They will be carried off from their own land.’ ”