2 Wathesalonike 2 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wathesalonike 2:1-17

Yule Mtu Wa Kuasi

12:1 Mk 13:27; 1The 4:15-17Ndugu, kuhusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanyika kwetu pamoja mbele zake, tunawasihi, 22:2 2The 3:17; 1Kor 1:8msiyumbishwe kwa urahisi wala msitiwe wasiwasi na roho wala neno au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu, isemayo kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwako. 32:3 Mk 13:5; Dan 8:25; Ufu 13:5, 6Mtu yeyote na asiwadanganye kwa namna yoyote kwa maana siku ile haitakuja mpaka uasi utokee kwanza, na yule mtu wa kuasi adhihirishwe, yule ambaye amehukumiwa kuangamizwa kabisa. 42:4 1Kor 8:5; Isa 14:13, 14; Eze 28:2Yeye atapingana na kujitukuza juu ya kila kitu kiitwacho Mungu au kinachoabudiwa, ili kujiweka juu katika Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.

52:5 1The 3:4Je, hamkumbuki ya kwamba nilipokuwa pamoja nanyi niliwaambia mambo haya? 62:6 2The 2:7Nanyi sasa mnajua kinachomzuia, ili apate kudhihirishwa wakati wake utakapowadia. 72:7 2The 2:6Maana ile nguvu ya siri ya uasi tayari inatenda kazi, lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapoondolewa. 82:8 Isa 11:4; Ufu 2:16Hapo ndipo yule mwasi atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamteketeza kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kabisa kwa utukufu wa kuja kwake. 92:9 Mt 24:24; Ufu 13:13Kuja kwa yule mwasi kutaonekana kana kwamba ni kutenda kazi kwake Shetani ambaye hutumia nguvu zote, ishara, maajabu ya uongo, 102:10 1Kor 1:18na kila aina ya uovu kwa wale wanaoangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli wapate kuokolewa. 112:11 Rum 1:28Kwa sababu hii, Mungu ameruhusu watawaliwe na nguvu ya udanganyifu, ili waendelee kuamini uongo, 122:12 Rum 1:32na wahukumiwe wote ambao hawakuiamini ile kweli, bali wamefurahia uovu.

Simameni Imara

132:13 Efe 1:4; 1The 5:9; 1Pet 1:2Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho kwa kuiamini kweli. 142:14 Rum 8:28; 11:29; 1The 1:5Kwa kusudi hili Mungu aliwaita kwa njia ya kuhubiri kwetu Injili, ili mpate kushiriki katika utukufu wa Bwana Yesu Kristo. 152:15 1Kor 16:13; 11:2Hivyo basi, ndugu wapendwa, simameni imara na myashike sana yale mafundisho tuliyowapa ikiwa ni kwa maneno ya kinywa au kwa barua.

162:16 Yn 3:16Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema, 172:17 1The 3:2; 2The 3:3awafariji mioyo yenu na kuwaimarisha katika kila neno na tendo jema.

New International Version – UK

2 Thessalonians 2:1-17

The man of lawlessness

1Concerning the coming of our Lord Jesus Christ and our being gathered to him, we ask you, brothers and sisters, 2not to become easily unsettled or alarmed by the teaching allegedly from us – whether by a prophecy or by word of mouth or by letter – asserting that the day of the Lord has already come. 3Don’t let anyone deceive you in any way, for that day will not come until the rebellion occurs and the man of lawlessness2:3 Some manuscripts sin is revealed, the man doomed to destruction. 4He will oppose and will exalt himself over everything that is called God or is worshipped, so that he sets himself up in God’s temple, proclaiming himself to be God.

5Don’t you remember that when I was with you I used to tell you these things? 6And now you know what is holding him back, so that he may be revealed at the proper time. 7For the secret power of lawlessness is already at work; but the one who now holds it back will continue to do so till he is taken out of the way. 8And then the lawless one will be revealed, whom the Lord Jesus will overthrow with the breath of his mouth and destroy by the splendour of his coming. 9The coming of the lawless one will be in accordance with how Satan works. He will use all sorts of displays of power through signs and wonders that serve the lie, 10and all the ways that wickedness deceives those who are perishing. They perish because they refused to love the truth and so be saved. 11For this reason God sends them a powerful delusion so that they will believe the lie 12and so that all will be condemned who have not believed the truth but have delighted in wickedness.

Stand firm

13But we ought always to thank God for you, brothers and sisters loved by the Lord, because God chose you as firstfruits2:13 Some manuscripts because from the beginning God chose you to be saved through the sanctifying work of the Spirit and through belief in the truth. 14He called you to this through our gospel, that you might share in the glory of our Lord Jesus Christ.

15So then, brothers and sisters, stand firm and hold fast to the teachings2:15 Or traditions we passed on to you, whether by word of mouth or by letter.

16May our Lord Jesus Christ himself and God our Father, who loved us and by his grace gave us eternal encouragement and good hope, 17encourage your hearts and strengthen you in every good deed and word.