2 Wafalme 9 – NEN & NRT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

2 Wafalme 9:1-37

Yehu Atiwa Mafuta Kuwa Mfalme

19:1 1Sam 10:5; 2Fal 8:28Nabii Elisha akamwita mtu mmoja kutoka kwa wana wa manabii na kumwambia, “Jikaze viuno, uichukue hii chupa ya mafuta, na uende Ramoth-Gileadi. 2Ukifika huko, mtafute Yehu mwana wa Yehoshafati, mwana wa Nimshi. Enda kwake, umtenge na wenzake, na umpeleke katika chumba cha ndani. 39:3 1Fal 19:16Kisha chukua hii chupa na umimine mafuta juu ya kichwa chake, nawe utangaze, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli.’ Kisha ufungue mlango na ukimbie; usikawie!”

4Basi yule kijana nabii akaenda Ramoth-Gileadi. 5Wakati alipofika, akawakuta maafisa wa jeshi wameketi pamoja, akasema, “Nina ujumbe wako, ee jemadari.”

Yehu akauliza, “Kwa yupi miongoni mwetu?”

Akamjibu, “Kwako wewe, jemadari.”

69:6 1Fal 19:16Yehu akainuka na kuingia ndani ya nyumba. Ndipo yule nabii akamimina mafuta juu ya kichwa cha Yehu na kutangaza, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, Mungu wa Israeli: ‘Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya watu wa Bwana, yaani Israeli. 79:7 Mwa 4:24; Kum 32:43Inakupasa uiangamize nyumba ya bwana wako Ahabu, nami nitalipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii na damu ya watumishi wote wa Bwana iliyomwagwa na Yezebeli. 89:8 1Sam 25:22Nyumba yote ya Ahabu itaangamia. Nitamkatilia mbali kila mzaliwa wa kiume wa Ahabu katika Israeli, aliye mtumwa ama aliye huru. 99:9 1Fal 14:10Nitaifanya nyumba ya Ahabu kuwa kama ile nyumba ya Yeroboamu mwana wa Nebati, na kama ile nyumba ya Baasha mwana wa Ahiya. 109:10 1Fal 21:23Kuhusu Yezebeli, mbwa watamla kwenye kiwanja huko Yezreeli, wala hakuna mtu atakayemzika.’ ” Kisha akafungua mlango na kukimbia.

119:11 Yn 10:20; 1Sam 10:11Yehu alipotoka nje na kurudi kwenda kwa maafisa wenzake, mmoja wao akamuuliza, “Je, kila kitu ni salama? Kwa nini huyu mwenye wazimu alikuja kwako?”

Yehu akajibu, “Wewe unamfahamu huyo mtu, na aina ya mambo ambayo yeye husema.”

12Wakasema, “Hiyo siyo kweli! Tuambie.”

Yehu akasema, “Haya ndiyo aliyoniambia: ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakutia mafuta uwe mfalme juu ya Israeli.’ ”

139:13 Mt 21:8; 2Sam 15:10Wakaharakisha kuvua mavazi yao, na kuyatandaza chini ya Yehu ili akanyage juu kwenye ngazi ya nje. Kisha wakapiga tarumbeta na kupaza sauti wakisema, “Yehu ni mfalme!”

Yehu Anamuua Yoramu Na Ahazia

149:14 Kum 4:43; 2Fal 8:28Basi Yehu mwana wa Yehoshafati, mwana wa Nimshi, akafanya shauri baya dhidi ya Yoramu. (Wakati huu, Yoramu na Israeli wote walikuwa wakiilinda Ramoth-Gileadi dhidi ya Hazaeli mfalme wa Aramu, 159:15 2Fal 8:29lakini Mfalme Yoramu alikuwa amerudishwa Yezreeli ili kujiuguza kutokana na majeraha ambayo Waaramu walimtia katika vita na Hazaeli mfalme wa Aramu.) Yehu akasema, “Kama hii ndiyo nia yenu, msimruhusu hata mmoja kutoroka nje ya mji kwenda kupeleka habari huko Yezreeli.” 169:16 2Nya 22:7Ndipo Yehu akaingia katika gari lake la vita na kuendesha kwenda Yezreeli, kwa sababu Yoramu alikuwa amepumzika huko, na Ahazia mfalme wa Yuda alikuwa ameenda kumwona.

179:17 1Sam 14:16Mlinzi aliyesimama juu ya kinara cha Yezreeli alipoona askari wa Yehu wanakuja, akaita akisema, “Naona askari wanakuja.”

Yoramu akaamuru, “Mtwae mpanda farasi umtume akakutane nao na kuuliza, ‘Je, mmekuja kwa amani?’ ”

18Mpanda farasi akaondoka kwenda kukutana na Yehu na kusema, “Hivi ndivyo asemavyo mfalme: ‘Je, mmekuja kwa amani?’ ”

Yehu akamjibu, “Una nini na amani? Unga msafara nyuma yangu.”

Mlinzi akatoa habari, “Mjumbe amewafikia lakini harudi.”

19Basi mfalme akamtuma mpanda farasi wa pili. Wakati alipowafikia akasema, “Hivi ndivyo asemavyo mfalme, ‘Je, mmekuja kwa amani?’ ”

Yehu akajibu, “Una nini na amani? Unga msafara nyuma yangu.”

209:20 2Sam 18:27Yule mlinzi akatoa taarifa akasema, “Mjumbe amewafikia, lakini hata yeye harudi. Uendeshaji ule ni kama wa Yehu mwana wa Nimshi, anaendesha kama mwenye wazimu!”

219:21 1Fal 21:1Yoramu akaagiza, akasema, “Weka tayari gari langu la vita.” Na baada ya gari kuwa tayari, Yoramu mfalme wa Israeli, na Ahazia mfalme wa Yuda, wakaondoka kila mmoja kwenye gari lake ili kukutana na Yehu. Walikutana naye katika shamba lililokuwa mali ya Nabothi, Myezreeli. 229:22 1Fal 18:19Yoramu alipomwona Yehu akauliza, “Je, Yehu, umekuja kwa amani?”

Yehu akajibu, “Kunawezaje kuwa na amani wakati ibada za sanamu na uchawi wa mama yako Yezebeli ungaliko?”

239:23 2Fal 11:14Yoramu akageuka nyuma na kukimbia, akimwambia Ahazia, “Huu ni uhaini, Ahazia!”

249:24 1Fal 22:34Kisha Yehu akatwaa upinde wake na kumchoma Yoramu katikati ya mabega. Mshale ukapenya kwenye moyo wake, naye akaanguka ghafula ndani ya gari lake. 259:25 1Fal 21:19-22Yehu akamwambia Bidkari, mwendeshaji wa gari lake, “Mwinue na umtupe katika shamba lililokuwa mali ya Nabothi, Myezreeli. Kumbuka jinsi mimi na wewe tulivyokuwa tukiendesha pamoja magari yetu nyuma ya Ahabu baba yake, wakati Bwana alipotoa unabii huu kumhusu: 269:26 1Fal 21:19‘Jana niliona damu ya Nabothi na damu ya wanawe, nami kwa hakika nitakufanya uilipe juu ya shamba hili, asema Bwana.’ Sasa basi, mwinue na umtupe juu ya kiwanja, kulingana na neno la Bwana.”

279:27 Amu 1:27; 2Fal 23:29Wakati Ahazia mfalme wa Yuda alipoona kilichotokea, akakimbia kupitia barabara ya Beth-Hagani. Yehu akamkimbiza akipaza sauti na kusema, “Muue naye pia!” Wakamjeruhi katika gari lake kwenye njia ielekeayo Guri karibu na Ibleamu, lakini akatorokea Megido na akafia huko. 289:28 2Fal 23:30Watumishi wake wakambeba kwa gari la vita na kumpeleka Yerusalemu, wakamzika pamoja na baba zake kwenye kaburi lake katika Mji wa Daudi. 299:29 2Fal 8:25(Katika mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu, Ahazia alianza kutawala katika Yuda.)

Yezebeli Auawa

309:30 Yer 4:30; Eze 23:40Kisha Yehu akaenda Yezreeli. Yezebeli aliposikia habari hii, akayapaka macho yake rangi, akatengeneza nywele zake na kutazama nje dirishani. 319:31 1Fal 16:9-10Yehu alipokuwa akiingia langoni, Yezebeli akasema, “Je, umekuja kwa amani, Zimri, wewe muuaji wa bwana wako?”

32Yehu akaangalia juu dirishani na kuita, “Je, ni nani aliye upande wangu? Ni nani?” Matowashi wawili au watatu wakamtazama. 339:33 Za 7:5Yehu akasema, “Mtupeni huyo mwanamke chini!” Kwa hiyo wakamtupa chini, nayo baadhi ya damu yake ikatapanyika ukutani na nyingine juu ya farasi walipokuwa wakimkanyaga kwa miguu yao.

349:34 1Fal 16:31Yehu akaingia ndani, akala na akanywa. Akasema, “Mshughulikieni huyo mwanamke aliyelaaniwa. Mzikeni, kwa sababu alikuwa binti wa mfalme.” 35Lakini walipotoka kwenda kumzika, hawakukuta kitu chochote isipokuwa fuvu la kichwa, miguu yake na mikono. 369:36 Za 68:23; 1Fal 21:23Wakarudi na kumwambia Yehu, ambaye alisema, “Hili ndilo neno la Bwana alilosema kupitia kinywa cha mtumishi wake Eliya Mtishbi, kwamba: Katika kiwanja cha Yezreeli, mbwa wataikula nyama ya Yezebeli. 379:37 Za 83:10; Yer 8:2Maiti ya Yezebeli itakuwa kama mavi shambani katika uwanja wa Yezreeli, kwamba hakutakuwepo mtu atakayeweza kusema, ‘Huyu ndiye Yezebeli.’ ”

New Russian Translation

4 Царств 9:1-37

Помазание Ииуя на царство в Израиле

1Пророк Елисей призвал одного из учеников пророческих и сказал ему:

– Заправь полы плаща под пояс, возьми этот сосуд с маслом и ступай в Рамот Галаадский. 2Когда придешь туда, разыщи там Ииуя, сына Иосафата, внука Нимши. Пойди к нему и уведи его от его друзей во внутреннюю комнату. 3Возьми этот сосуд, полей масло ему на голову и произнеси: «Так говорит Господь: „Я помазываю тебя в цари Израиля“». Потом открой дверь и беги, не задерживайся!

4И молодой человек, пророк, пошел в Рамот Галаадский. 5Когда он пришел туда, он увидел военачальников, сидящих вместе.

– У меня есть весть для тебя, военачальник, – сказал он.

– Для кого из нас? – спросил Ииуй.

– Для тебя, военачальник, – ответил он.

6Ииуй встал и прошел в дом. Пророк возлил масло на голову Ииуя и произнес:

– Так говорит Господь, Бог Израиля: «Я помазываю тебя в цари Господнего народа, Израиля. 7Истреби дом Ахава, твоего господина, чтобы Мне отомстить за кровь Моих слуг пророков и за кровь всех Господних слуг, пролитую Иезавелью. 8Погибнет весь дом Ахава. Я истреблю у Ахава всякого человека мужского пола – и раба, и свободного. 9Я уподоблю дом Ахава дому Иеровоама, сына Навата, и дому Бааши, сына Ахии9:9 См. 3 Цар. 14:10-11; 16:3-4.. 10А Иезавель сожрут псы на участке земли в Изрееле, и никто ее не похоронит».

После этого он открыл дверь и убежал. 11Когда Ииуй вышел к слугам господина, один из них спросил его:

– Все ли благополучно? Зачем к тебе приходил этот сумасшедший?

– Вы сами знаете, что это за человек и что он может сказать, – ответил Ииуй.

12– Неправда! – сказали они. – Расскажи нам.

Ииуй сказал:

– Он сказал мне: «Так говорит Господь: „Я помазываю тебя в цари Израиля“».

13Они заторопились, взяли плащи и постелили их ему прямо на ступеньках. Потом они затрубили в рог и закричали:

– Воцарился Ииуй!

Гибель царей Иорама и Охозии

(2 Пар. 22:7-9)

14Ииуй, сын Иосафата, внук Нимши, составил заговор против Иорама. (Иорам и весь Израиль защищали Рамот Галаадский от Хазаила, царя Арама, 15но царь Иорам9:15 Евр.: «Иегорам», вариант имени Иорам; также в ст. 17 и 21-24. вернулся в Изреель, чтобы оправиться от ран, которые арамеи нанесли ему в битве с царем Арама Хазаилом.) Ииуй сказал:

– Если вы согласны, то не давайте никому выйти из города и рассказать новости в Изрееле.

16Он взошел на колесницу и поехал в Изреель, потому что там отдыхал Иорам, а Охозия, царь Иудеи, пришел его навестить. 17Когда часовой, стоявший на башне в Изрееле, увидел, как приближаются воины Ииуя, он закричал:

– Я вижу воинов.

– Отправь им навстречу всадника, – приказал Иорам. – Пусть спросит: «С миром ли вы?».

18Всадник выехал навстречу Ииую и сказал:

– Царь спрашивает, с миром ли вы?

– Что тебе до мира? – ответил Ииуй. – Поезжай за мной.

И часовой доложил:

– Посланец доехал до них, но назад не возвращается.

19Тогда царь послал второго всадника. Подъехав к ним, он сказал:

– Царь спрашивает, с миром ли вы?

Ииуй ответил:

– Что тебе до мира? Поезжай за мной.

20И часовой доложил:

– Посланец доехал до них, но и он не возвращается назад. А человек, скачущий впереди, похож на Ииуя, сына Нимши, – он скачет, как безумец.

21– Запрягай мою колесницу, – приказал Иорам.

И когда ее запрягли, Иорам, царь Израиля, и Охозия, царь Иудеи, выехали в колесницах навстречу Ииую. Они встретили его у участка земли, который принадлежал Навоту из Изрееля. 22Увидев Ииуя, Иорам спросил:

– Ты с миром, Ииуй?

– Какой мир, – ответил Ииуй, – пока множатся идолопоклонство и чародейство твоей матери Иезавели?

23Иорам повернул назад и обратился в бегство, крича Охозии:

– Измена, Охозия!

24Ииуй натянул лук и поразил Иорама между лопатками. Стрела пронзила ему сердце, и он осел в колеснице. 25Ииуй сказал своему сановнику Бидекару:

– Подними его и брось на поле, что принадлежало Навоту из Изрееля. Помнишь, как мы с тобой ехали в колесницах за его отцом Ахавом, когда Господь изрек о нем такое пророчество: 26«Вчера Я видел кровь Навота и кровь его сыновей, – возвещает Господь, – и непременно взыщу с тебя за нее на этом участке земли». Итак, подними его и брось на тот самый участок по слову Господа9:25-26 См. 3 Цар. 21:19, 24, 29..

Гибель Охозии

27Увидев, что случилось, Охозия, царь Иудеи, бежал по дороге к Бет-Хаггану9:27 Или: «по дороге, которая ведет к садовому дому».. Ииуй гнался за ним, крича:

– Убейте и этого!

Люди ранили Охозию в колеснице на дороге, поднимающейся к Гуру, что близ Ивлеама, но он скрылся в городе Мегиддо, где и умер. 28Слуги отвезли его на колеснице в Иерусалим и похоронили с его предками в его гробнице в Городе Давида. 29(Охозия стал царем Иудеи на одиннадцатом году правления Иорама, сына Ахава.)

Гибель Иезавели

30Ииуй пошел в Изреель. Когда Иезавель услышала об этом, она подвела глаза, уложила волосы и стала смотреть в окно. 31Когда Ииуй вошел в ворота, она спросила:

– С миром ли ты пришел, Зимри, убийца своего господина?9:31 Иезавель намекает здесь на судьбу военачальника Зимри, который убил своего царя Илу и истребил весь царский род, но сам погиб через семь дней (см. 3 Цар. 16:9-20).

32Он поднял взгляд к окну и позвал:

– Кто за меня? Кто?

Из окна выглянули два или три евнуха.

33– Сбросьте ее вниз! – сказал Ииуй.

Они сбросили ее, и кровь ее брызнула на стену и на коней, которые растоптали ее.

34Ииуй зашел, поел и попил. Потом он сказал:

– Разыщите эту проклятую и похороните; она все-таки царская дочь.

35Но когда пошли ее хоронить, не нашли ничего, кроме черепа, ног и кистей рук 36и, вернувшись, доложили Ииую, который сказал:

– Это слово Господа, которое Он изрек через Своего слугу, Илию из Тишбы: «На земле Изрееля псы сожрут тело Иезавели. 37Труп Иезавели будет на участке Изрееля как навоз на поле, так что никто не скажет: „Это Иезавель“»9:33-37 См. ст. 10 и 3 Цар. 21:23..